Ukweli ni upi katika kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA?

Ukweli ni upi katika kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA?

Wewe ndo' unaleta propaganda Kimwaga yuko sahihi.
Laki...
Chuki na uchochezi katika kusema kweli?

Unataka vizazi vijavyo viamini kuwa Waislam walikuwa watu wapumbavu kiasi waliivunja EAMWS wakati wanajenga shule na Chuo Kikuu?

Tuna wajibu wa kueleza ukweli na kupinga proaganda za watu kama Kimwanga.
Unajua kuwa hadi leo historia ya Auschwitz bado inasomeshwa?
 
Laki...
Chuki na uchochezi katika kusema kweli?

Unataka vizazi vijavyo viamini kuwa Waislam walikuwa watu wapumbavu kiasi waliivunja EAMWS wakati wanajenga shule na Chuo Kikuu?

Tuna wajibu wa kueleza ukweli na kupinga proaganda za watu kama Kimwanga.
Unajua kuwa hadi leo historia ya Auschwitz bado inasomeshwa?
Kwani mzee Mohamedi haiwezekani tena kujenga chuo zama hizi?!
 
Ozzanne,
Kwako wewe kuandika historia ya kweli ni kuvunja udugu ila kupotosha historia ni kuunga udugu na kuleta umoja wa kitaifa.

Wala wewe huna haja ya kuniamini ninapoeleza kuwa babu yangu Salum Abdallah ni muasisi wa TANU Tabora na ni muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) akiwa rais 1955 na aliongoza migomo mikubwa mitatu ya wafanyakazi wa reli, 1947, 1949 na 1960.

Ukipenda amini kuwa wala watu hawa hawakupata kuwepo Tanganyika.

Wala sina sababu ya kujidai.

Hawa ni wazee wangu na wala sikuwachagua.

Nimezaliwa wakati wao kwa uchaguzi wa Mungu.

Wala hawa wazee hawakupanga kuwa Nyerere atatoka kwao atakuja Dar es Salaam atamtafuta Abdul Sykes na wataungana na wazalendo wengine kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia hii ndiyo historia ya wazee wangu ambayo ilipotea nami nikaiandika ili isipotee na iwepo hadi siku ya kiama.

Bora wasingeandika kabisa kuliko kuandika historia iliyopotoshwa.

Ikiwa unayo historia ya TANU mfano wa hii yangu iandike isomwe kama dunia inavyosoma yangu.

Nimekusoma ahsante sana.
Hujaandika Waislamu wafanye nini ili kujikwamua kutoka hapo walipo?!
 
Hii nchi hii ina mfumo kristo wallah dhulma dhidi ya Waislam wa tanganyika haitaliacha kanisa salama na wallah tunaumia kwa haya yanayotokea , Allah amjalie sheikh wetu ilunga Pepo ya juu in sha Allah ameacha athari kubwa sn kwa kizazi cha leo maneno yake bado yanaishi japo watu wasema vijana punguzeni jazba wallah hatutapunguza mpk hizza yetu itakaporudi bi idhniLlaah
Jina lako la mwanzo tu tayari limedhihirisha hujui uliandikalo!

Unaitwa Rommy = Romeo jina la kikristo alafu unaliponda kanisa una laana kubwa kubwa wewe na maimani yako eti pepo ya juu kwani kuna pepo ya chini na kati
 
Waislamu ni walalamishi na wanalalamika hadi kwenye secular countries.

Wewe unataka mauislamu yako nenda Saudia au Iran huko utaishi vyema kabisa alafu ndio utajua Tanzanians tuna uvumilivu sana
Statarea,
Umeandika ukiwa umeghadhibika.

Kinachokughadhibisha ni akili yako kukutana na mambo ya kweli lakini hukupata kuyafahamu.

Katika hali kama hii kinachokujia kwanza na haraka ni mshtuko.

Kinachosomeshwa ni historia tu ya watu ambao kwako ni wageni kabisa lakini wamefanya makubwa.

Hili si jambo la kumuudhi yeyote lakini historia hii imevuruga ubongo wako kwani hukudhania kuwa hivi ndivyo ilivyokuwa.

Itakuchukua muda kwa ubongo wako kuukubali ukweli na akili ikasema hii kwa hakika ni kweli.
 
Kinachokusumbua nini lipi kosa langu kumuombea khery mzee wangu said aingie jannahtul firdous au kuna lingine ambalo unalo jina langu lisikuchanganye
Jina lako la mwanzo tu tayari limedhihirisha hujui uliandikalo!

Unaitwa Rommy = Romeo jina la kikristo alafu unaliponda kanisa una laana kubwa kubwa wewe na maimani yako eti pepo ya juu kwani kuna pepo ya chini na kati
 
Kwani mzee Mohamedi haiwezekani tena kujenfa chuo zama hizi?!
Magnifico,
Katika miaka ya 1970 mwishoni Organization of Islamic Countries (OIC)ilitaka kujenga chuo Tanzania.

Serikali ilikataa kutoa kibali.
OIC wakauhamisha ule mradi chuo kikajengwa Mbale, Uganda.

Katika miaka ya 1990s mwishoni Darul Imaan kutoka Saudi Arabia walitaka kujenga shule ya ufundi Kibaha.

Mradi huu ulipigwa vita na vyombo vya habari kuwa na mradi wa "Waarabu uliokuja kupora ardhi."

Darul Imaan walipoona uadui huu wakasimamisha kazi na ndiyo ukawa mwisho wa hiyo shule.

Aboud Jumbe akailalamikia Darul Imaan kwa hoja kuwa kama Tanzania Bara kuna uadui dhidi ya mradi huo mradi uhamishiwe Zanzibar na akaihakikishia Darul Imaan ushirikiano na serikali.

Mradi ukapelekwa Zanzibar na Zanzibar wakaomba wajenge Chuo Kikuu badala ya shule ya ufundi.

Darul Imaan wakajenga Zanzibar University.

Mwaka wa 2004 nikaalikwa chuoni hapo kutoa mhadhara wa maisha ya Sheikh Hassan bin Ameir.

 
Kinachokusumbua nini lipi kosa langu kumuombea khery mzee wangu said aingie jannahtul firdous au kuna lingine ambalo unalo jina langu lisikuchanganye
Ni Firdausi sio firdous!
Kosa lako ni kulikebehi kanisa na kulitakia mabaya na hayo ndio mafundisho ya dini yako ukiwa umesahau una matumizi ya jina la kanisa (ROMEO)
 
Statarea,
Umeandika ukiwa umeghadhibika.

Kinachokughadhibisha ni akili yako kukutana na mambo ya kweli lakini hukupata kuyafahamu.

Katika hali kama hii kinachokujia kwanza na haraka ni mshtuko.

Kinachosomeshwa ni historia tu ya watu ambao kwako ni wageni kabisa lakini wamefanya makubwa.

Hili si jambo la kumuudhi yeyote lakini historia hii imevuruga ubongo wako kwani hukudhania kuwa hivi ndivyo ilivyokuwa.

Itakuchukua muda kwa ubongo wako kuukubali ukweli na akili ikasema hii kwa hakika ni kweli.
Ungekuwa unasomesha na historia za Wakristo ama kutetea jambo fulani kwa misingi ya Ukristo au kujiweka neutral kwenye historia zako za ajabu ajabu ningekuona wa maana sana!

Ila historia zako huwa zimeegemea upande wa Uislamu, unatumia sababu za kipuuzi sana kuonyesha dini yako ina haki fulani au kunyanyaswa.

Na hii sio wewe tu ama waislamu wa Tanzania wako nayo kuhisi wana haki fulani na hawaipati, walitendewa ubaya n.k ni dunia nzima! Kasoro nchi zinazojitanabisha kuwa ni za Kiislamu.

Mfano hai ni kampeni zinazoendelea Uingereza waislamu wanashawishiana miskitini na kwenye majukwaa yao eti wasimpigie kura Johnson wampigie Jeremy kutokana na misimamo yake juu ya dini.
 
hiyo mihadhara na research unazoenda kuzifanya huko vyuo vya ulaya , UK, German zinafadhiliwa na nani? ni taasisi au mtu binafsi anaekufadhili?
Laki...
Nimekuwekea hapa siku chache zilizopita orodha ya vyuo vikuu nilivyopata kualikwa Ulaya, Marekani na Afrika.

Mimi sijui fedha zao zinakotoka.
 
Hakuna ambaye hakuathirika kwa Ukoloni, tuliuzwa utumwa, tulibebeshwa pembe za ndovu ktk Kigoma hadi Pwani kwa miguu karavani, tulifanyishwa kazi bila ya ujira au ujira mdogo sana kwenye mashamba ya Wakokoni huko Tanga, Zanzibar, Tabora Kigoma na kwingineko.

Kwanza ninaweza kusema Waislamu Waarabu, Wahindi na wengineo walinufaika zaidi na Ukoloni klk sisi Waafrika weusi kwani Waislamu Waarabu na Wahindi walikuwa daraja la pili baada ya Muzungu na sisi weusi tulikuwa daraja la tatu.

Kuna sababu kwa nini miji yote Mikubwa TZ kuna makazi yajulikanayo kama Uzunguni, Uhindini na Uswahilini, na Uswahilini ni kwetu sisi weusi na mweusi haikujalisha kama ulikuwa Muislamu au Mkristo, tulikuwa wote ni daraja la tatu.

Hivyo kusema kwamba Waislamu walionewa wakati wa Ukoloni sijui unamanisha nini na walionewa kwa kulinganisha na nani? Kama kulinganisha na Mwafrika mweusi, hapo nitakupinga.

Umetoa jibu zuri, kusema waislamu walionewa ni uongo mtupu, kuna waislamu walisusa elimu ya mkoloni, na wapo waislamu waliopeleka shule wanao katika mfumo wa kikoloni na wakaja kuwa hadi viongozi wa nchi, kusema waislamu walionewa hakuna mashiko
 
Mohamed Said, inawezekana chuki zako zimetokana na familia ya Sykes kufilisiwa mali zao kipindi Nyerere alipoanza kampeni zake za ujamaa kuanzia mwaka 1964,familia ya sykes ilikumbwa na kimbunga kilichowakumba akina kambona, titi mohamed, kaselabantu etc

Laki...
Ungekuwa unajua ukiandikacho ingekuwa vizuri sana.
Kwa ufahamu wangu hakuna mali yoyote ya Sykes iliyofilisiwa.
 
Mzee said naisi kama nimewahi kukuona masjid idrisa kariakoo mwaka 2009 baada ya swala ya ijumaa, nakumbuka siku hiyo ulisimama na kusema leo ninawaletea historia ya tanganyika kabla ya uhuru nakumbuka siku hiyo waislam wengi walitulia sehem zao wakisubiri kusikia kile ulichowaandalia, sina kumbukumbu vzr ulisema kua miongoni wa wapigania uhuru waliokua hai hadi leo (2009) ni wawili tu ambao wazee sn na hali yao si nzr, nakumbuka ulisema uchunguzi wako ulikuchukua miaka mingi sn kukamilika, historia iliishia kwa Waislam wengi sn msikitini pale kulitokwa na machozi sn nami nikiwemo hii ni baada ya kugundua tumedhulumiwa sn na mbaya zaidi kwenye history babu zetu hawawamo, mzee said kama ni ww kweli basi allah akuifadhi mzee wangu. nakumbuka ilikuwa ndo mara ya kwanza report ile inatolewa na kulikua na wapiga picha wengi na video shooting kibao ulivaa kanzu Nyeupe na kofia yako Nyeupe, Allah kareem mzee wangu ipo siku haqq itajienga na batili in sha Allah na tupo vijana allahmdulilah
Rommy,
Ndiye mimi kaka yangu nilialikwa kuja kuzungumza na Waislam.
 
Nini kiliifanya EAMWS kuhamisha makao yake makuu kutoka Mombasa hadi Dar?

Kama ni Nyerere ndiye aliyeua EAMWS na kuanzisha BAKWATA, je ni yeye mwenyewe aliua EAMWS kule KENYA? Aliwaanzishia baraza gani kule?
Nanren,
Mimi ninaweza nikakujibu kwa yale yaliyotokea Tanzania mwaka wa 1968 ya Kenya siyafamu.

Makao Makuu yalihamia Tanzania kwa ajili ya wingi wa Waislam ukilinganisha na Kenya na Uganda.
 
Ungekuwa unasomesha na historia za Wakristo ama kutetea jambo fulani kwa misingi ya Ukristo au kujiweka neutral kwenye historia zako za ajabu ajabu ningekuona wa maana sana!

Ila historia zako huwa zimeegemea upande wa Uislamu, unatumia sababu za kipuuzi sana kuonyesha dini yako ina haki fulani au kunyanyaswa.

Na hii sio wewe tu ama waislamu wa Tanzania wako nayo kuhisi wana haki fulani na hawaipati, walitendewa ubaya n.k ni dunia nzima! Kasoro nchi zinazojitanabisha kuwa ni za kiislamu.
Mfano hai ni kampeni zinazoendelea Uingereza waislamu wanashawishiana miskitini na kwenye majukwaa yao eti wasimpigie kura Johnson wampigie Jeremy [emoji23][emoji23][emoji23] kutokana na misimamo yake juu ya dini ya Muddy

Statarea,
Inawezekana ni kwa ajili ya labda umri wako, kiwango cha elimu, malezi na mambo mengine mengi tu "exposure," nk. nk.

Nakueleza haya nikiamini mimi nimekupita kwa umri mimi ni mzee kwa hiyo utaniheshimu kwa uzee wangu.

Naamini umefanya kwa kuwa hujui na kama hujui unastahili kusamehewa.
Kwetu sisi Waislam Mtume Muhammad SAW hafanyiwi utani.

Usimtaje Mtume SAW kwa utani.
Hiyo ni kufru kubwa sana ambayo hakuna Muislam yeyote duniani anaweza kustahamili.

Naamini umeelewa na hutorudia tena jambo hili.
Nikejeli mimi unavyopenda lakini weka heshima kwa Mtume Wetu SAW.
 
Statarea,
Inawezekana ni kwa ajili ya labda umri wako, kiwango cha elimu, malezi na mambo mengine mengi tu "exposure," nk. nk.

Nakueleza haya nikiamini mimi nimekupita kwa umri mimi ni mzee kwa hiyo utaniheshimu kwa uzee wangu.

Naamini umefanya kwa kuwa hujui na kama hujui unastahili kusamehewa.
Kwetu sisi Waislam Mtume Muhammad SAW hafanyiwi utani.

Usimtaje Mtume SAW kwa utani.
Hiyo ni kufru kubwa sana ambayo hakuna Muislam yeyote duniani anaweza kustahamili.

Naamini umeelewa na hutorudia tena jambo hili.
Nikejeli mimi unavyopenda lakini weka heshima kwa Mtume Wetu SAW.

Statarea,
Hi si ''historia yangu,'' wala si ''historia ya ajabu ajabu.''

''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism,'' Minerva Press London 1998 sasa ni kitabu kinachotambulika kama ''corrective history,'' na ni kitabu muhimu katika ''political history'' ya Tanganyika.

1574012482532.png

Kitabu kimesahihisha historia rasmi iliyokuwa inatakiwa itambulike.

Publishers hapa nyumbani waliuogopa mswada wangu kwa kuwa ulikuwa unapingana moja kwa moja na historia iliyokuwapo lakini ndiyo watu waliokuwa wanaijua na kuiamini.

Baada ya kutoka kitabu changu wasomi wakataka kujua kama kweli kulikuwa na ''Muslim Struggle,'' Tanganyika iliyopambana na ukoloni wa Waingereza.

Naam kitabu kimeeleza hilo.

Kitabu kimeleta elimu mpya kwa ushahidi usiokuwa na shaka kuwa historia ya Tanganyika ilikuwa imepindishwa kwa kukusudia kutokana na hofu ya Uislam baada ya uhuru kwani kabla ya uhuru Uislam katika kupambana na ukoloni haukuwa tishio.

Hii ndiyo historia mabingwa wa African History duniani, Northwestern University, walinialika nikaizungumze chuoni kwao.

Naam nilizungumza katika Ukumbi wa Eduardo Mondlane, Evanston, Chicago.
Hii sasa si ''historia yangu'' wala si historia ya ''ajabu ajabu.''

Hii ni historia kama ilivyotakiwa iwe,

Nathubutu kusema kuwa histroria ya ajabu ajabu ni hiyo iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni (1981) iliyomkwepa Abdul Sykes, Ally Sykes, Kleist Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Yusuf Badi, Sheikh Rashid Sembe, Zubeir Mtemvu, Yusuf Olotu, Ali Migeyo, Iddi Faizi Mafungo, Paul Bomani, Bilal Rehani Waikela, Omari Suleiman, Rashid Ali Meli, Schneider Abdillah Plantan, Dr. Michael Lugazia, Dr. Luciano Tsere, Dr. Joseph Mutahangarwa, Saadani Abdu Kandoro, Dr. Vedasto Kyaruzi, Bi, Tatu bint Mzee, Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, Oscar Kambona, Bi. Halima Selengia, Bi. Amina Kinabo, Bi. Fatma bint Matola, Bi. Zarula bint Abdulrahman na haya ni majina machache katika orodha ya wapigania uhuru wengi ambayo mimi nimeyarejesha katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
 
Back
Top Bottom