Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Nyani that is very perceptive of you... nimesheelezea ufraud wa Kambona. Na kwenye swali lako la mwisho the answer is no! The same way sifurahii Nyerere kuitwa Dictator! au wewe unafurahia Nyerere kuitwa Dictator?
 
mzee sisi wengine huwa hatulalamiki mada zinapohamishwa, kuwa merged au kufutwa ila kama ma MoD watashawishika na kuona ni mada muhimu wataiweka kunakosttahili. Nadhani watu hawakutaka kuona ukweli kuhusu Kambona baada ya kuwapa karibu siku nne za kumjenga shujaa wao, manake hadi watu wakaenda kwenye hadithi za familia.. tukakaa wengine tukawaangalia na kusema jamani twende pole pole, hawakutaka.

MKJJ,
Yaani siku nne unaona sawa na miaka 20 na ushee, ambayo Nyerere alitumia kujaza watu ujinga??. Nyerere mwenyewe angekucheka kwa hoja kama hiyo!!!.
 
Nyani that is very perceptive of you... nimesheelezea ufraud wa Kambona. Na kwenye swali lako la mwisho the answer is no! The same way sifurahii Nyerere kuitwa Dictator! au wewe unafurahia Nyerere kuitwa Dictator?

Nyerere was not a dictator the same way Kambona was not a fraud. Agree?....disagree?

Halafu maelezo yako kuhusu ufraud wa Kambona hayajaniridhisha
 
Nyerere was not a dictator the same way Kambona was not a fraud. Agree?....disagree?

Halafu maelezo yako kuhusu ufraud wa Kambona hayajaniridhisha


not necessary.. sasa kuridhika na maelezo yangu sidhani kama naweza kukusaidia kwa hilo. Mtu anaweza kupika chakula kitamu na akakiweka mezani; kama utashiba au utataka zaidi sidhani kama liko ndani ya uwezo wa mpishi.
 
Nyerere was not a dictator the same way Kambona was not a fraud. That's my stance
 
MWK,
Mie Bill Frist na wewe ni Terri Schavo!!! good, lakini wewe ni Ann Coulter.....kazi yako kubwa ni kubadili mada serious kuwa vibweka, ili mradi tu uwe upande mmoja na boo wako, JF Nyerere(MKJJ). Ungekuwa dume ningekufananisha na Rush Limbaugh, maana hiyo spin yako anaiweza huyo bwana.

Mtu yeyote anayemshabikia Nyerere,mie huwa namshangaa........jaribu kukumbuka "Dizim" wakti tukiwa vidudu 1983/84, yaani hata dawa ya mbu na "msasa" ilikuwa dili........nchi ilikuwa imemshinda kabisa,kwa fikra zake sahihi!!!.
 
NN,
MNF usiku huu, watu wanawakandamiza Ravens in Baltimore.........the weather is perfect,kuna baridi kama jahanamu. Wana wa NE ndio tunapenda hiyo hasa kukiwa na snow, go Pats....go Randy Moss!!!.
 
Ha ha Ann Coultier dah wana tu newslater twao tunaitwa Human Events mambo wanayoandika utachoka mwenyewe.

Lakini jamani hamuoni kuwa lingekuwa jambo la busara kama Kambona angeeleza ukweli tu siku ile pale jangwani? After all akina Mtei na wengine wengi walikuwa wanapingana na Mwalimu walikomaa naye mumo kwa mumo na hawakukimbilia ugenini. I guess alijua nini kingemtokea maana naye si alikuwa mmoja wao.
Hili la kusema Kambona ni hero kwa kuwa alikwenda kuwatuliza wanajeshi waliotaka/walio hasi sikubaliani nalo, ile ilikuwa ni kazi yake(kama waziri wao) sasa mtu kufanya kazi yake nayo anapewa uhero? Ndio maana baadhi yetu humu tunamtetea Mkapa kwa kuendesha biashara Ikulu na madudu mengine kisa aliinua uchumi.
Basi nadhani Idi Amin naye ni hero maana aliweza kuongea na wale watekaji(ingawa aliwakaribisha) wakaruhusu baadhi ya abiria na ndege yao wakaondoka salama.
Ila sumu aliyomwaga mwalimu ilikuwa kiboko maana kuna watu wengine wamezaliwa baada ya Kambona kuondoka lakini walikuwa wanajua "madudu" yake yote plus mijina ya ajabu ajabu ambayo ukimuita mwenzio basi kaa tayari tayari kutolewa ngeu.
 
Icadon, huo mfano wa Amin na watekaji mzuri.. mimi sielewi walitaka nani aende kuzungumza na waasi? Leo hii likitokea tatizo Muhimbili au mgomo anayeenda ni Mwakyusa (si mmeona ya botched surgeries?), na likitokea tatizo Elimu ya Juu wa kubanwa ni Msolla. Sasa wameasi wanajeshi na wanatishia serikali iliyoko madarakani, Rais na Makamu wako mahali pa usalama, sasa nani aende kuzungumza na wanajeshi Waziri wa Mawasiliano na Miundo Mbinu?
 
Mtatoa mifano yote dunia nzima, hata Hitler pia nae ni hero kwa wanazi wenzie!!. Mnyonge mnyongeni lakini haki mpeni, Kambona ana-deserve nafasi yake nzuri tu kwenye historia ya Tanzania.
 
nyerere was a dicator at times....hilo halina ubishi! na vile vile alivuruga uchumi wa nchi.

hakuna kipindi watu walichokuwa wanataabika na njaa kama wakati wa nyerere. wafanyakazi wa serikalini walikuwa na mishahara yao, lakini hakuna cha kukinunua....its such a shame kwa kweli

tunakataa kusema maovu yake kwa kuwa mema yake kwa watanzania ni mengi zaidi ya maovu yake, lakini hakuna mkamilifu, na alitenda mengi maovu, na kama tunataka kusonga mbele...lazima tujue maovu yake pia ili tusiyarudie.

kesi ya kambona ni ngumu kuihukumu kwa kuwa si nyerere si serikali si kambona wametowa ushahidi wa waliyoyasema.

hata kama mwisho amekimbia nchi, lakini sifa yake anastahili ya kugombea uhuru mpaka ukapatikana na akaongoza nchi baada ya uhuru na sio kusifiwa nyerere tu wakati uhuru haukutafutwa na mtu mmoja.

nawakilisha
 
wenzako wamejaribu yamewwashinda. Hivi leo Tanzania kuna chakula cha kutosha? Mwaka jana tulienda kubembeleza chakula ilikuwa ni makosa ya Mwalimu? Umesoma gazeti la Habari Leo la Jana kuwa hali imekuwa ngumu makosa ya Mwalimu? Tunaibiwa Benki Kuu tumlaumu Mwalimu? Leo tumepata viongozi wasanii makosa ya Mwalimu? Mwalimu aliachia madaraka ishirini na mbili iliyopita sawasawa na muda wote aliowatawala Mwalimu je tumefanya vizuri zaidi? Are we more united today than we were 22 years ago? c'mmon now get real!
 
...watu humu mnajiamulia tu ..mtu akishachukua side kwa kuwa yeye ni moderator anafanya analotaka...we are being traped in the same propaganda against kambona in 70s..thATs nit...tunataka legacy za viongozi ziwe kwenye siasa ...hakuna cha balls wala coward...hata legacy ya MALECELA imebaki siasa...pamoja na kuwa ndani ya mjadala kutofautiana kulikowapo....huwezi kutaka watu makini wajadili VIBWEKA ..kwani mara nyingi wengi wetu hata kupita huku kwenye vibweka ni nadra ...na mara nyingi ni kama akili zimechoka kabisa....

lets be serious hamjafanya fair kuiweka hii humu...sio demokrasia hii...

mara nyingi watu wanapenda tu kuhukumu kitu kuita ni OP..hata ile kashafa ya ajira BOT ilipoletwa na mjumbe humu mkaharakisha kuihamishia kwenye porojo..vibweka...wakati sasa imeonekana ni muhimu na PCCB WANAWAHOJI WALE VIJANA ..KUNA TUME....SASA MNATAKIWA MJUE UMUHIMU WA JF NA MJUE NI KIOO ...TUNAJADILI HUMU NA WANAFAIDIKA WENGI ....MNATAKIWA MJUE KWA MWAKA HUU TU MAOVU YOTE MUHIMU ..RICHMOND ..MADINI MIKATABA ets yameanzia humu ...tukamwaga datas ..ndio baadaye wajumbe wenzetu ambao ni wabunge wakayapeleka bungeni....tambueni umuhimu wetu ...hili ndio bunge...mjadala wa kambona utawasaidia na viongozi wengine ambao historia imewaacha makusudi......ni mjadala huu..

acheni kujiamulia tu...TAFADHALI RUDISHENI HII MADA KWENYE SIASA ....NA MSIHAMISHE MADA OVYO...PLEASE!!!
 
yaani in this thread kuna mtu humu ananiboa na vicoment vyake mpaka basi,simtaji jina maana sina balls!
 
Marehemu Sekou Ture alifanya mazungumzo na Rais Nyerere kuhusu kurudi nyumbani kwa Oscar Kambona na Kassim Hanga na Mwalimu alitoa msamaha ili viongozi hao warejee nchini.alitangulia Kassim Hanga lakini Mwalimu alimdhalilisha katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mnazi mmoja kwa kumtukana matusi makubwa na kisha kumrudisha Zanzibar ambako alipotea na hata mwili wake haujaonekana hadi leo.Mwenzake Kambona kuona hivyo akaamua kubaki Uk.
Kassim na Kambona wote wanastahili kuandikwa katika historia kama mashujaa waliopokonywa utu wao na utawala wa kidikteta wa Mwalimu.Ulizeni madingi wa enzi zile.
 
Hakuna anayekataa kuwa Kambona hakuchangia upatikanaji wa uhuru hilo halina ubishi ni lazima awekwe kwenye vitabu vya kumbukumbu kama waasisi wa TANU na mmoja wa viongozi wa kwanza Tanganyika huru na Tanzania, lakini hili la kusema apewe ushujaa kisa alitofautiana na mwalimu na akaamua kukimbia nchi hapana, wangapi walitofautiana na mwalimu na walibaki? Alafu tuangalie zile zama za walizotawala kila mtu alikuwa anataka kuwa mtawala, mapinduzi kila kona.
Kosa walilofanya hawa mabwana wawili(RIP) ni kutokutueleza Watanzania nini hasa kilisababisha tofauti zao when they had their chances.
 
wenzako wamejaribu yamewwashinda. Hivi leo Tanzania kuna chakula cha kutosha? Mwaka jana tulienda kubembeleza chakula ilikuwa ni makosa ya Mwalimu? Umesoma gazeti la Habari Leo la Jana kuwa hali imekuwa ngumu makosa ya Mwalimu? Tunaibiwa Benki Kuu tumlaumu Mwalimu? Leo tumepata viongozi wasanii makosa ya Mwalimu? Mwalimu aliachia madaraka ishirini na mbili iliyopita sawasawa na muda wote aliowatawala Mwalimu je tumefanya vizuri zaidi? Are we more united today than we were 22 years ago? c'mmon now get real!

Chakula kipo zaidi ya kile kilichokuwepo enzi za Nyerere wako. Watu siku hizi tunakula sembe tu. Hatuli unga wa nguruwe (yanga). Hatujipangi mistari kwenye maduka ya ugawaji kupata unga wa ngano na sukari. Are we better off today than we were 20 some years ago?
 
Mabadiliko ya siasa nchini Tanzania kuanzia mwaka 1967 ndiyo yalisababisha kusimama kwa uchumi wa taifa. Operesheni vijiji vya ujamaa ilisababisha watu kuondolewa kwa nguvu kutoka kwenye makazi yao na mashamba yao, walikusanywa kwenye maeneo mapya yenye wanyama wakali bila nyumba wala chakula. Watanzania hawa walianza maisha mapya kwa kuanza kujenga nyumba kufyeka na kusafisha mapori na kuanza kulima, hali hii ilichukuwa miaka mingi na kipindi hiki ndicho ambacho tatitizo la ukosefu wa chakula lilianza.Wakulima walitoka vijijini kutafuta chakula mijini.

Tatizo la pili lilikuwa ni kutaifisha mabenki, bima, viwanda nyumba na mashamba ya walioitwa mabwenyenye, makabaila n.k. kutaifisha maana yake ni kuchukua mali ya mtu kwa nguvu bila ya ridhaa yake na bila kumlipa kitu chochote. Matokeo yake mashamba ya mkonge yaligeuka mapori, kwa sababu bei ya mkonge ambao ndio wakati huo ulikuwa ukiingiza fedha nyingi za kigeni iliporomoka. Magonjwa ya ajabu ajabu alianza kushambulia kahawa, nayo mavuno yakapungua kwa kiwango cha kutisha. Serikali ilifika wakati ikaliona tatizo lakini ilishindwa kusema ukweli kwa wale wote ambao mali zao zilichukuliwa. Badala yake serikali ilianza kuwaalika kama wawekezaji na siyo tena mabwenyenye. Tukumbuke kuwa kosa lolote baya likifanyika kinachofuata ni kujitakasa kwa toba kwa wale wote ambao serikali iliwapora mali zao. Ni kweli wawekezaji walianza kuja nchini, tunakumbuka walivyochukua benki ya NBC watanzania tulipiga kelele nyingi jinsi walivyoichukua kwa bei ya kutupa. Lakini jambo moja la msingi ni kuwa kibaka akipora mkufu wa dhahabu atauza kwa bei yoyote atakayokuja nayo mnunuzi. Hizi benki hazikuwa zetu tulipora mali za watu na kinachofanyika sasa hivi tunauza kwa staili ile ile ya vibaka. Raisi wetu kila siku ni kiguu na njia akizungukia dunia kutafuta wawekezaji, sawa tunaowapata ndio kama akina buswagi. Bila toba kwa dhambi iliyofanywa na awamu ya kwanza, kwa kukaa na wale wote walioporwa mali zao na kukubali kosa na kuomba msamaha na kukubali kulipa fidia angalau kidogo ni hakika hatasimama kiongozi yeyote katika taifa hili akabadilisha maisha ya watanzania, bila ya kuondoa hii dhuluma taifa la Tanzania lililowafanyia mabwenyenye na makabaila.
 
Sasa na nyie? mkiweka hii topic wengine tunapotea. Hii topic ni pure politics, wengine ni wanachiacha, hatuwezi kuiona huku. Ndo naishtukia sasa hivi na posts ziko 25 from 9 nilizoziacha jana. Ama kweli JF wakilibebea jambo mbeleko! Haya bwana endeleeni, ngoja sisi tuendelee na Richmond zetu kule.
 
Ilipelekwa kwenye Kibweka baada ya Kambona kuanza kuoneshwa uhalisia wake. Kabla ya hapo ilikuwa ni siasa. Binafsi naamini ni mada muhimu na ingestahili kubaki kwenye siasa but then mimi siyo MoD na yeyote anayetaka kuifuata anaweza kubonyeza mahali fulani kwa urahisi tu.
 
Back
Top Bottom