Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Ukweli ni upi kuhusu Oscar Kambona?

Na wewe bana....eti imeshakuwa kibweka baada ya kuonyeshwa uhalisia wa Kambona. Sasa wewe unaonyesha ushabiki usio na mantiki. Yaani kusema eti mtu hana ballz ndio kuonyesha uhalisia wake? Na Nyerere wako alivyotumia matusi na ku-condone ngonjera za dhihaka mlizoimbishwa juu ya Kambona, unataka kuniambia hiyo haionyeshi uhalisia wa Nyerere wako? Get real dude. Acha ushabiki usio na akili bwana
 
Na wewe bana....eti imeshakuwa kibweka baada ya kuonyeshwa uhalisia wa Kambona. Sasa wewe unaonyesha ushabiki usio na mantiki. Yaani kusema eti mtu hana ballz ndio kuonyesha uhalisia wake? Na Nyerere wako alivyotumia matusi na ku-condone ngonjera za dhihaka mlizoimbishwa juu ya Kambona, unataka kuniambia hiyo haionyeshi uhalisia wa Nyerere wako? Get real dude. Acha ushabiki usio na akili bwana

Nyani, hivi umesoma public school or private school?

Mimi nimesoma public school na sikuwahi kuimba ngonjera yoyote kuhusu Kambona! au kuna tofauti kubwa sana ya kipindi ulichosoma na nilichosoma mimi?

Kambona nimemsoma kwenye siasa, historia na uraia kama kiongozi mashuhuri na mpigania uhuru wa Tanzania. Hayo ya ngonjera na kuitwa name yalifanywa wapi na nani? Kambona ametaniwa sasa mashuleni kama vile Nyerere na Mwinyi walivyotaniwa big tyme.

Sijui shule uliyosoma ila mimi nilikosoma, mchakamchaka kila asubuhi ziliimbwa nyimbo za kupondea kifimbo cha Mwl na mambo yake kibao, nyimbo za kupondea kashfa za ngono za Mwinyi, nk

Kuna mambo mawili hapa ninapata wasiwasi kuhusu hii argument, labda umepewa habari tofauti kabisa kuhusu Mwl au una chuki binafsi na mzee.
 
Mimi nimesoma public school na sikuwahi kuimba ngonjera yoyote kuhusu Kambona! au kuna tofauti kubwa sana ya kipindi ulichosoma na nilichosoma mimi?

Basi wewe utakuwa ulisoma juzi sana, hizi tuliimbishwa (hatukuimba) mpaka midomo ikakauka!
 
Nyani, hivi umesoma public school or private school?

Mimi nimesoma public school na sikuwahi kuimba ngonjera yoyote kuhusu Kambona! au kuna tofauti kubwa sana ya kipindi ulichosoma na nilichosoma mimi?

Kambona nimemsoma kwenye siasa, historia na uraia kama kiongozi mashuhuri na mpigania uhuru wa Tanzania. Hayo ya ngonjera na kuitwa name yalifanywa wapi na nani? Kambona ametaniwa sasa mashuleni kama vile Nyerere na Mwinyi walivyotaniwa big tyme.

Sijui shule uliyosoma ila mimi nilikosoma, mchakamchaka kila asubuhi ziliimbwa nyimbo za kupondea kifimbo cha Mwl na mambo yake kibao, nyimbo za kupondea kashfa za ngono za Mwinyi, nk

Kuna mambo mawili hapa ninapata wasiwasi kuhusu hii argument, labda umepewa habari tofauti kabisa kuhusu Mwl au una chuki binafsi na mzee.

Wewe Krit, jana si uliniambia kuwa umesoma wakati wa Mwinyi au nimekosea? Mimi nazungumzia watu waliosoma miaka ya mwisho ya sitini na kwenye miaka ya sabini. Na sidhani yaliyosemwa kuhusu Kambona yalikuwa ya utani.

Sina chuki na binafsi na Kifimbo. Hajawahi kunikosea zaidi ya life kuwa ngumu wakati nakua. Nakumbuka washua wangu walikuwa wakinituma kwenda kupanga mstari kwenye duka la ugawaji asubuhi na mapema ili tuwahi unga wa ngano tukapike chapati au mandazi. I hated that and I didn't and I still don't why we (I) to line up to get food. But oh well, it is what it is (or was).

Sasa mimi kusema kwamba watu waliimbishwa ngonjera kuhusu Kambona is based on anecdotal accounts. Unless the people are lying to me, I don't have any other evidence for it didn't happen while I was in school. Hey I'm a '70's baby...but didn't start school till like '83 or '84. By that time Kambona was not even mentioned anywhere. Hata ktk somo la siasa sikuwahi kusikia jina lake. Nimekuja kumsikia mwaka '91 au '92 baada ya introduction ya multi partyism.
 
Mabadiliko ya siasa nchini Tanzania kuanzia mwaka 1967 ndiyo yalisababisha kusimama kwa uchumi wa taifa.

Hili si kweli hata kidogo. Matatizo ya Kiuchumi ya Tanzania hayakutokana na kutangazwa Azimio la Arusha bali hali ya kiuchumi duniani na ukweli sisi tulifanya vizuri ukilinganisha na nchi nyingine. Kwa upande wa Tanzania mambo matatu yalitusumbua sana; Ongezeko la bei ya mafuta la 1970 lilikuwa ni pigo kubwa sana kwenye uchumi wetu na uchumi wa nchi nyingi. Kwa taifa changa hilo lilianza kutuingiza kwenye madeni makubwa. Ukame wa 1974 ukaumiza sana kilimo chetu na kabla hatujatulia tukawa na Vita ya Kagera mwishoni mwa miaka ya sabini na baada ya hapo tukiwa tumeanza kujiandaa, ukaja ukame wa 1984. Ingekuwa sisi Ethiopia tungeimbiwa wimbo wa "We are the World". But we did a lot better as a nation than most countries. Ethiopia (while united with Eritrea), Somalia, Uganda n.k did worse than us na Mwalimu hakuwa Rais wao. So kusema kwa haraka kuwa matatizo yalianzia 1967 (kwa Azimio la Arusha) is a mediocre attempt in trivilializing of history. Matatizo ya kiuchumi ya Tanzania yalikuwa na msingi mkubwa zaidi na Azimio la Arusha was the instrument used to check it, it could have been worse.

Operesheni vijiji vya ujamaa ilisababisha watu kuondolewa kwa nguvu kutoka kwenye makazi yao na mashamba yao, walikusanywa kwenye maeneo mapya yenye wanyama wakali bila nyumba wala chakula. Watanzania hawa walianza maisha mapya kwa kuanza kujenga nyumba kufyeka na kusafisha mapori na kuanza kulima, hali hii ilichukuwa miaka mingi na kipindi hiki ndicho ambacho tatitizo la ukosefu wa chakula lilianza.Wakulima walitoka vijijini kutafuta chakula mijini.

Mojawapo ya ukosoaji halali wa Mwalimu na watendaji wake ulikuwa ni utekelezaji wa zoezi la "Operesheni Vijiji vya Ujamaa" ambayo Kawawa alikuwa msimamizi mkuu. Ni kweli kabisa kuwa dhana yake ilikuwa nzuri lakini utekelezaji wake bordered criminal activities. Hilo Mwalimu pia aliliona na mojawapo ya vitu ambavyo alikiri baadaye kuwa didn't go they way he envinsioned them. Badala ya kuisukuma nchi nzima kwenda vijiji vya ujamaa kungekuwa na vijiji vya mazoezi au vya mfano ambavyo vingetumika kushawishi. Hata hivyo, leo hii vijiji vingi vilivyopo vimetokana na zoezi hilo na vinaendelea kufana which vindicates Mwalimu's vision. Leo hii, miradi na mipango mingi inajengwa kutoka vijijini (vilivyoundwa wakati wa operesheni) na imerahisisha upatikanaji wa huduma nyingi muhimu. Utekelezaji was botched? Absolutely, was it a good idea to bring all these Tanzanians in an organized form of living to bring them services and unite them at the basic social level? you betcha!


Tatizo la pili lilikuwa ni kutaifisha mabenki, bima, viwanda nyumba na mashamba ya walioitwa mabwenyenye, makabaila n.k. kutaifisha maana yake ni kuchukua mali ya mtu kwa nguvu bila ya ridhaa yake na bila kumlipa kitu chochote. Matokeo yake mashamba ya mkonge yaligeuka mapori, kwa sababu bei ya mkonge ambao ndio wakati huo ulikuwa ukiingiza fedha nyingi za kigeni iliporomoka. Magonjwa ya ajabu ajabu alianza kushambulia kahawa, nayo mavuno yakapungua kwa kiwango cha kutisha.

Ukosoaji huu una msingi lakini pia una makosa ya kihistoria na kiukweli. Je kulikuwa na ulazima wa kutaifisha njia kuu za uchumi? Mwanzoni lilionekana wazo zuri lakini kwenye utekelezaji it went far than it was necessary. Hilo nalo Mwalimu aliliona na hasa kwenye utaifishaji wa mashamba ya mazao ya biashara. Hatukuwa na uwezo na utaalamu wa kuendesha vyombo hivyo; lakini kwenye makampuni fulani muhimu Mwalimu was absolutely right. Katika Tanzania baada ya Uhuru watu wachache walikuwa na access na ownership ya njia za uchumi na kuacha kikundi cha watu wachache kumilika njia za uchumi wakati wachache ndio wanakuwa omba omba halikuweza kuvumilika.

Leo hii nchi kama Zimbabwe, Namibia, Botswana na Afrika ya Kusini zote zinatambua kwa kiasi kikubwa haja ya kuhakikisha kuwa wale wananchi wa asili wa nchi zao na wenyewe wanapata nafasi katika kumiliki njia za uchumi, nafasi za kibiashara n.k Anayedhania kuwa Waasia na Wazungu waliokuwa wanamiliki makampuni makubwa na ardhi kubwa wangekuwa na ukarimu wa kutoa nafasi kwa watu weusi mtu huyo hajajifunza historia. Watanzania wengi wangeendelea kuwa wahamiaji kwenye ardhi yao huku wakifanya kazi za kubangaiza na kufurahia kile ambacho mabwana wao wanawagaiya.

Leo hii tena Mwalimu anakuwa vindicated na historia. Tumeona jinsi gani ukiuachia ubepari ufanye utakalo inavyosababisha kutoridhika kwa wananchi. Wale wanaokumbuka political economic theories watakumbuka kuwa ubepari huundwa kwanza kabisa na kile tunachosema ni "Ukusanyaji wa Kijima wa Mtaji" (Primitive Accumulation of Capital). Leo wananchi wanapolilia kuona ardhi yao inagawanywa na madini yake yanachotowa kama maji kisimani wanamrudia Mwalimu; wanapoona mabenki yaliyokuwa "yao"yanapewa wageni tena kwa bei chee wanamkumbuka Mwalimu; hata kelele zunazopiga humu kuhusu watawala wetu ni kwa sababu tunatambua kuwa kuna vitu haviendi vinavyopaswa. Watu wasichofahamu ni kila ambacho Mwalimu alikuwa anakisema mwishoni mwa maisha yake "ubepari hauna macho".

Leo hii tunaogopa kutumia neno "ulanguzi" kwa sababu linasikika vibaya, wakati watu wanajua kabisa kuna ulanguzi wa bidhaa mbalimbali nchini. Tunaogopa kuingilia kati uwekezejai kwa sababu 'wawekezaji watakimbia' lakini hadi pale yale ya Delta Nigeria yatakapoanza kutokea Tanzania ndipo tutakapojua Mwalimu siyo tu aliona mbali, bali aliombea pia kuwa siku moja kuna kizazi cha Watanzania ambacho kitakuja na ubunifu wa kuwianisha haki za mtu binafsi na haki za jamii nzima; nafasi sawa kwa wote na uhuru sawa kwa wote. Kwa vile wameacha zile dhana muhimu za Mwalimu, watawala wetu hawana cha kusimamia.


Serikali ilifika wakati ikaliona tatizo lakini ilishindwa kusema ukweli kwa wale wote ambao mali zao zilichukuliwa. Badala yake serikali ilianza kuwaalika kama wawekezaji na siyo tena mabwenyenye.

Bahati mbaya wamebadilisha jina tu; waliorudi ni wale wale na tunatambua kwa matunda ya kazi zao. Kabaila ni nani? Ni mtu yule ambaye anamiliki ardhi kubwa ambayo anatumia kuzalisha mali kwa kuajiri vibarua na kutengeneza pesa kwa kutumia ardhi hiyo. Kina Sinclair siyo mabepari tu, ni makabaila pia! Na sasa hivi tunaogopa kusema hivyo, kwa sababu makabaila kama kina Mkapa ni watanzania wenzetu! Chupa ni tofauti, mvinyo ni ule ule.

Tunaogopa kutumia neno "unyonyaji" wakati wote tunafahamu vizuri ni nini kinaendelea. Watu wanashindwa kuelewa kuwa ubepari asili yake ni manufaa ya watu wachache na adha kwa watu wengi. Leo hii kuna mabepari wakupindukia nchini hadi Bungeni wamelundikana. Msingi wa maisha yao ni faida na faida kwa namna yoyote; kazi yao ni kuchuma wasipopanda, na kucheua wasichotafuna. Madaktari walipotaka nyongeza ya senti chache wakapigwa mkwara wa nguvu lakini mabepari wetu serikali walipojiongezea kipato wakapigiwa makofi! Sasa hivi tunaogopa kuwaita wanyonyaji kwa sababu huko nyuma wanyonyaji walikuwa weupe, sasa hawa weusi wanapotunyonya tena kwa mirija saba saba na kutuacha vimbavu mbavu huku wakiturishia nguo nzuri, Radio nzuri, luninga, na tu barabara kama twa Mwenge, tunajisikia vizuri!

Tukumbuke kuwa kosa lolote baya likifanyika kinachofuata ni kujitakasa kwa toba kwa wale wote ambao serikali iliwapora mali zao. Ni kweli wawekezaji walianza kuja nchini, tunakumbuka walivyochukua benki ya NBC watanzania tulipiga kelele nyingi jinsi walivyoichukua kwa bei ya kutupa. Lakini jambo moja la msingi ni kuwa kibaka akipora mkufu wa dhahabu atauza kwa bei yoyote atakayokuja nayo mnunuzi. Hizi benki hazikuwa zetu tulipora mali za watu na kinachofanyika sasa hivi tunauza kwa staili ile ile ya vibaka. Raisi wetu kila siku ni kiguu na njia akizungukia dunia kutafuta wawekezaji, sawa tunaowapata ndio kama akina buswagi. Bila toba kwa dhambi iliyofanywa na awamu ya kwanza, kwa kukaa na wale wote walioporwa mali zao na kukubali kosa na kuomba msamaha na kukubali kulipa fidia angalau kidogo ni hakika hatasimama kiongozi yeyote katika taifa hili akabadilisha maisha ya watanzania, bila ya kuondoa hii dhuluma taifa la Tanzania lililowafanyia mabwenyenye na makabaila.

Ndugu yangu kuna sheria katika Tanzania na kama kuna mtu anahisi amedhulumiwa afungue kesi. Lakini hata hivyo, kiongozi mzuri ni yule ambaye anakubali makosa ya kihistoria na ambaye haogopi historia yake. Ningekuwa mimi wao, nafahamu kabisa kuwa kuna watu hawakutendewa haki wakati wa utaifishaji; kuna vitu ambavyo inabidi kutengenezwa; lakini katika kutengeneza huko hatutaacha wananchi wetu wawe ombaomba kwenye Taifa leo, au wazamiaji kwenye ardhi yao. Tungetengeneza mpaka pale tu ambapo tunakubaliana na waliodhulumiwa kuwa "ni haki kwa wote". Tungewakaribisha nyumbani Watanzania waliokimbia; tungerudisha makampuni au mashamba ambayo kwa hakika hayakustahili kuwa mikononi mwa serikali, na kwa hakika tungetengeneza kwa kiasi kikubwa pale palipoharibiwa.

Kufanya hivyo kunahitaji uongozi wa kijasiri; siyo ujasiri wa maneno bali ujasiri unaotokana na uthabiti wa vitendo. Bado naamini kabisa kuwa nia ya mwalimu ilikuwa nzuri, naamini maono yake yalikuwa ni mazuri; na ninakubali pia utekelezaji wa baadhi ya maono haya haukuwa sahihi.

Ndugu zangu, sisi tuko kama Marekani. Dhana iliyounda Taifa la Marekani ilianza kwa kutangazaia dunia kuwa "We hold these truths to be self evident; that all people are created equal and endowed by their creator with certain unalieanable rights; among these ar life, liberty and the pursuit of happiness". Wakati wanaandika hilo, Marekani ilikuwa na watumwa kwa mamilioni, wanawake walikuwa hawapigi kura, na wahindi waliishi kama wageni kwenye ardhi yao! Hata hivyo ukweli wa kauli hiyo hapo juu haukundoa ukweli halisi ardhini.

Tangu wakati huo Marekani imejaribu kutengeneza kilichoharibiwa kwa kupigania umoja wa nchi hiyo katika vita vya wenyewe 1860s na baadaye katika kuondoa sheria za kibaguzi na kuwapa wanawake haki ya kupiga kura ya 1920s; kuondoa sheria za Jim Crow miaka ya 1950s na baadaye kupitisha sheria ya Haki za Kiraia ya Mwaka 1964. Hata leo hii Amerika imekuwa ni wazo ambalo linatamaniwa na linaloendelea kuwa halisia. Marekani haijafikia kuwa "mji ung'arao juu ya mlima".

Lakini haiondoi ukweli kuwa wamepiga hatua katika haki za wananchi na raia na licha ya manung'uniko ya hapa na pale Marekani haitarudia utumwa, ubaguzi n.k

Sisi nasi vivyo hivyo, tunaitwa na historia kuwa mji ung'arao pembezoni mwa Afrika. Mji ambao uliweka mwenge juu ya mlima Kilimanjaro kuleta "matumaini pasipo matumaini, upendo penye chuki, na heshima palipojaa dharau". Bahati mbaya mwali wa mwenge ule unazidi kufifia siku kwa siku huku kwa nguvu zetu zote tukiacha misingi ile iliyotuunda kama Taifa na kubakia kuwa waigizaji wa demokrasia!

Siku moja hata hivyo inshallah, atasimama kiongozi katika Taifa letu ambaye atakuwa na ujasiri wa kutengeneza palipobomoka; kujenga pasipojengwa na kulinda vilivyokwishajengwa. Kiongozi huyo yupo na siku moja atakuja. Yawezekana ikawa katika kizazi chetu au kizazi kingine. Tusikate tamaa kwa Taifa letu na tusirudi nyuma kwa aibu! Tusonge mbele enyi wana na mabinti wa Tanzania, tusimame wa moja licha ya tofauti zetu, na pamoja tuongeze juhudi za kuhakikisha kuwa "Taifa huru, la watu sawa, na lenye utu ambalo ni la watu, limetoka kwa watu na ni kwa ajili ya watu litaendelea kuwepo na halitaondoshwa kwenye uso wa dunia!"
 
Basi wewe utakuwa ulisoma juzi sana, hizi tuliimbishwa (hatukuimba) mpaka midomo ikakauka!

Na una hakika kabisa kuwa Nyerere alikuwa responsible katika wewe kuimbishwa hizi ngonjera na akahakikisha kuwa zinaimbwa all over the country from Pemba to Kibondo!

Kama ni kweli basi Nyerere si tu ni kuwa alikuwa na ballz bali pia alikuwa na uwezo alionao MUNGU wa kuwa kila mahali wakati wote.
 
Na una hakika kabisa kuwa Nyerere alikuwa responsible katika wewe kuimbishwa hizi ngonjera na akahakikisha kuwa zinaimbwa all over the country from Pemba to Kibondo!

Kama ni kweli basi Nyerere si tu ni kuwa alikuwa na ballz bali pia alikuwa na uwezo alionao MUNGU wa kuwa kila mahali wakati wote.

Hata kama hakuwa directly responsible ktk kutoa order lakini ali-condone hizo dhihaka kama hakuzipinga hadharani!!!!
 
Wewe Krit, jana si uliniambia kuwa umesoma wakati wa Mwinyi au nimekosea? Mimi nazungumzia watu waliosoma miaka ya mwisho ya sitini na kwenye miaka ya sabini. Na sidhani yaliyosemwa kuhusu Kambona yalikuwa ya utani.

Sina chuki na binafsi na Kifimbo. Hajawahi kunikosea zaidi ya life kuwa ngumu wakati nakua. Nakumbuka washua wangu walikuwa wakinituma kwenda kupanga mstari kwenye duka la ugawaji asubuhi na mapema ili tuwahi unga wa ngano tukapike chapati au mandazi. I hated that and I didn't and I still don't why we (I) to line up to get food. But oh well, it is what it is (or was).

Sasa mimi kusema kwamba watu waliimbishwa ngonjera kuhusu Kambona is based on anecdotal accounts. Unless the people are lying to me, I don't have any other evidence for it didn't happen while I was in school. Hey I'm a '70's baby...but didn't start school till like '83 or '84. By that time Kambona was not even mentioned anywhere. Hata ktk somo la siasa sikuwahi kusikia jina lake. Nimekuja kumsikia mwaka '91 au '92 baada ya introduction ya multi partyism.

Nyani,

hapa ndipo sana tunakubaliana na kidogo tunatofautiana.

Inaonekana kama vile wote tumesoma kipindi cha Mwinyi na pia kuwa binafsi hatukuimba ngonjera za Kambona. Personal account ni strong kuliko hearsay stories.

Sijui wewe umesomea wapi lakini mimi nimesomea mikoani na nilisoma kwenye historia, siasa, na baadaye lilipoanzishwa somo la uraia kuwa Kambona alikuwa miongoni mwa wapigania uhuru na waanzilishi wa TANU.

Haya ya kuwa the guy alipotea kwenye historia nakukatalia kwa nguvu zote. Kuhusu kupanga foleni kwenye chakula naona kwako hilo ni issue na sijui namna ya kukusaidia zaidi nitakavyomsaidia mtoto fulani leo huko mikoani ambaye hajui kama hata hiyo foleni ya kupata chakula ataipanga.

hali ilikuwa mbaya wakati wa Mwalimu ila kwa sasa ndio inazidi kuwa mbaya zaidi. Ninaenda bongo krismasi hii na napanga kuchukua as many video clips as possible (kutumia digital camera) maana zile ninazotumiwa hazina quality nzuri na you will be surprised of what is going on in your beloved country.

Life nje Dar na mijini inatisha miaka 22 baada ya Nyerere kustaafu na miaka 8 baada ya kifo chake. Zaidi sana mimi naona tu nikubaliane na ile argument yako kuwa waafrika tuna matatizo na wala sio Nyerere au Kambona mwenye uwezo wa kutusaidia!

BTW, sidhani kama ni vyema ukiniita krit ingwa nilifurahia ile conversation about krit
 
Nyani,

hapa ndipo sana tunakubaliana na kidogo tunatofautiana.

Inaonekana kama vile wote tumesoma kipindi cha Mwinyi na pia kuwa binafsi hatukuimba ngonjera za Kambona. Personal account ni strong kuliko hearsay stories.

Sijui wewe umesomea wapi lakini mimi nimesomea mikoani na nilisoma kwenye historia, siasa, na baadaye lilipoanzishwa somo la uraia kuwa Kambona alikuwa miongoni mwa wapigania uhuru na waanzilishi wa TANU.

Haya ya kuwa the guy alipotea kwenye historia nakukatalia kwa nguvu zote. Kuhusu kupanga foleni kwenye chakula naona kwako hilo ni issue na sijui namna ya kukusaidia zaidi nitakavyomsaidia mtoto fulani leo huko mikoani ambaye hajui kama hata hiyo foleni ya kupata chakula ataipanga.

hali ilikuwa mbaya wakati wa Mwalimu ila kwa sasa ndio inazidi kuwa mbaya zaidi. Ninaenda bongo krismasi hii na napanga kuchukua as many video clips as possible (kutumia digital camera) maana zile ninazotumiwa hazina quality nzuri na you will be surprised of what is going on in your beloved country.

Life nje Dar na mijini inatisha miaka 22 baada ya Nyerere kustaafu na miaka 8 baada ya kifo chake. Zaidi sana mimi naona tu nikubaliane na ile argument yako kuwa waafrika tuna matatizo na wala sio Nyerere au Kambona mwenye uwezo wa kutusaidia!

BTW, sidhani kama ni vyema ukiniita krit ingwa nilifurahia ile conversation about krit

Kwanza nisamehe kwa kukuita Krit. It was supposed to be a joke but I botched it. I am sorry. Pili, nakubaliana na wewe mia kwa mia kwamba matatizo yetu yanasababishwa na sisi wenyewe na hao jamaa hawawezi kutusaidia ingawa hii sii hoja inayojadiliwa hapa. Kama umesahau kwa ghafla hoja hapa ni jinsi gani historia itakavyomkumbuka UNSUNG HERO OSCAR KAMBONA!!!

Na kuhusu ugawaji....labda wewe mwenzangu ulizaliwa na kijiko cha fedha mdomoni kwa hiyo huwezi uka-relate adha tulizozipata sisi akina yakhe kule uswahilini. Kwa hilo sikulaumu sana.
 
Kwanza nisamehe kwa kukuita Krit. It was supposed to be a joke but I botched it. I am sorry. Pili, nakubaliana na wewe mia kwa mia kwamba matatizo yetu yanasababishwa na sisi wenyewe na hao jamaa hawawezi kutusaidia ingawa hii sii hoja inayojadiliwa hapa. Kama umesahau kwa ghafla hoja hapa ni jinsi gani historia itakavyomkumbuka UNSUNG HERO OSCAR KAMBONA!!!

Na kuhusu ugawaji....labda wewe mwenzangu ulizaliwa na kijiko cha fedha mdomoni kwa hiyo huwezi uka-relate adha tulizozipata sisi akina yakhe kule uswahilini. Kwa hilo sikulaumu sana.

That's OK,

Nadhani umeamua kwa makusudi kabisa kutojali paragraph mbili ambazo nimeeleza kuwa Kambona nimemsoma Shuleni kuwa alikuwa mpigania uhuru na mwanzilishi wa TANU.

Mawazo yangu binafsi kuhusu Kambona ni kuwa alikuwa mwoga na mbinafsi. The guy without ballz ya ku-stand heat, alianzisha mapinduzi na mambo yalivyogeuka akakimbia na akapotea kabisa alivyopata vipesa?

So far naona mie ndio niko bado kwenye hoja ila wale waliotaka hii thread iwe Kambona vs Nyerere ndio walitaka wabadili hii hoja na kuifanya kitu kingine.

Opinion yangu kuhusu Kambona ni kuwa alikuwa hero mwanzoni wakati wa uanzilishi wa TANU (ingawa inaweza kusemwa pia kuwa alikuwa opportunist) ila baadaye ubinafsi wake ukamfanya awe na fikra za kibinafsi zaidi ya watanzania kwa ujumla.

Hata hivyo, for now namruhusu Kambona apumzike salama kaburini.
 
Ok, kama wewe umemsoma Kambona shule ulizoenda basi poa tu. Mimi sikumbuki kumsoma. Na kama maoni yako ni kwamba Kambona ni mwoga, na yenyewe poa. Afterall, ni maoni tu na kila mtu ana ya kwake.
 
Maasi ya 1964 - Kile ambacho Kambona Hakukisema:

Maasi ya wanajeshi ya 1964 ndiyo ambayo inadaiwa yalimpa umaarufu zaidi Kambona. Ilikuwaje? Maasi haya yalianza usiku wa kuamkia Jumatatu ya tarehe 20 Januari, 1964. Yalianza kwa wanajeshi kudai vitu vikubwa viwili kwanza nyongeza ya mishahara na pili kuondolewa kwa maafisa wa kizungu jeshini. Batalioni ya kwanza ya Kolito ya Tanzania Rifles (zamani ikijulikana kama Kings African Rifle) walivamia eneo la silaha la kambi hiyo na kuwaweka kizuizini maofisa wa kizungu na wale Non-Commissioned Officers (NCOs). Kutoka hapo wakazunguka eneo la Ikulu, na pia kushikilia kituo cha radio, uwanja wa ndege, na maeneo mengine nyeti jijini. Baadhi ya Mawaziri inadaiwa waliwekwa kizuizini. Rais Nyerere na Makamu wake Bw. Kawawa walikuwa salama.

Kesho yake Nyerere alijitokeza hadharani. Hata hivyo siku hiyo ya Jumatatu mchana Waziri wa Ulinzi Bw. Oscar Kambona alienda kuzungumza na wanajeshi waasi na alinukulikwa akisema kuwa “nimeweza kuwapatanisha maaskari wazalendo na wageni kwenye Tanzania Rifles na wamenihakikishia kuwa bado ni watii kwa serikali”. Jumanne hali ikawa iko shwari (ndiyo siku Mwalimu alitokea hadharani na kuwahakikishia wananchi kuwa serikali bado ipo madarakani). Maasi ndiyo yalikuwa yameanza tu.

Majadiliano yalikuwa yanaendelea kati ya serikali na viongozi wa wanajeshi hao lakini kwa upande wa serikali wazo kuwa jeshi linaweza kuingia wakati wowote na kuiweka kwenye kabali serikali lilikuwa ni wazo la kutisha. Majadiliano pia hayakuwa yanakwenda vizuri na mwalimu aliyaelezea majadiliano hayo “kama ya mtekaji nyara na mhanga wake”.

Siku ya Ijumaa hata hivyo, majadiliano yalikuwa yanakwama na habari nzito kuwa mpango wa kumpindua Rais ulikuwa mbioni hasa baada ya waasi kuanza kuja na madai zaidi kama “haki ya kuchagua mawaziri watatu” na vitu kama hivyo. Ilikuwa ni Jumamosi ya wiki hiyo ndipo Mwalimu akiona hana jinsi na kwa kusita sita sana aliomba msaada wa Jeshi la Uingereza ambapo usiku wa kuamkika Jumatatu ya tarehe 25 kwa umahiri mkubwa walizunguka Kolito na kuzima maasi hayo.

Ukweli ni kuwa jaribio la kwanza la kuwatuliza maaskari waasi lililofanywa na Kambona halikufanikiwa licha ya yeye kufanya hivyo siyo kwa kujitolea bali kwa kuagizwa na Rais wake. Kambona alichoweza kufanya ni kutuliza muda ule wa Jumatatu ya tarehe 20 lakini hakunyamazisha mipango ya kuipundua serikali. Hata uamuzi wa kuita Jeshi la Uingereza kuiokoa serikali halali ya kiraia ulikuwa ni uamuzi mgumu. (nitawawekea kesho hotuba ya Mwalimu kufuatia kuzimwa kwa maasi hayo). Kambona alishiriki kikamilifu katika kuita Waingereza kuisaidia serikali yake baada ya kushindwa kuondoa tishio la mapinduzi ya kijeshi. Akiwa Waziri wa Ulinzi na mtii kwa serikali yake Kambona alifanya kazi yake kama ilivyopaswa licha ya kutokuwa na matokeo mazuri zaidi ya ilivyotarajiwa.

Lakini maasi yalitokana na nini hasa?

Wiki kama tano hivi kabla ya maasi na siku chache kabla ya maasi kuna mambo yaliyotokea ambayo yanaelezea kidogo kwanini wanajeshi (ingawa si wote) waliamua kuasi. Kwanza kabisa ni uamuzi wa Rais Nyerere kuamua kukomesha zoezi la Uafrikanisho wa utumishi wa umma ambapo watanzania weusi walipewa upendeleo maalumu katika ajira (modern day affirmative action). Kwa mtu ambaye alikuwa anapinga ubaguzi wa rangi Mwalimu aliamua kukomesha zoezi hilo. Kitendo hicho kilitafsiriwa na baadhi ya wanajeshi kuwa mwalimu alikuwa amegeuka ahadi yake kuwa wazungu wataondoka katika uongozi wa jeshi. Hilo likachangiwa na madai ya nyongeza ya mishahara toka kama dola 14.84 kwa mwezi kufikia dola 36.40 kwa mwezi. Hayo yalikuwa yamewauma sana wanajeshi.

Pili, siku chache kabla ya maasi Mwalimu alituma maafisa wa Rifles kama mia tatu hivi kwenda kuleta hali ya amani kufuatia mapinduzi ya Zanzibar (tarehe 12 Januari ile). Ni pale tu walipoondoka hao wengine kwenda kuleta amani Zanzibar hawa waliobakia kama 1600 ndipo walipoasi. Je yawezekana walifikiria kufanya kile kilichotokea Zanzibar?

Ilikuwa ni kutokana na maasi haya ndipo jeshi jipya la Wananchi wa Tanzania lilipoundwa likiwa limeingizwa katika siasa na kuanzisha kile ambacho kilijulikana kama makamisaa wa siasa na wanajeshi wetu walitakiwa kufahamu kabisa sera na itikadi ya chama kile kimoja. Ndiyo maana leo hii kama kuna vyombo ambavyo vinapendwa, kuthaminiwa na kutiiwa na watu wengi ni jeshi letu ambalo kwa hakika ni jeshi la Wananchi wa Tanzania.
 
Maasi ya 1964 - Kile ambacho Kambona Hakukisema:

Maasi ya wanajeshi ya 1964 ndiyo ambayo inadaiwa yalimpa umaarufu zaidi Kambona. Ilikuwaje? Maasi haya yalianza usiku wa kuamkia Jumatatu ya tarehe 20 Januari, 1964. Yalianza kwa wanajeshi kudai vitu vikubwa viwili kwanza nyongeza ya mishahara na pili kuondolewa kwa maafisa wa kizungu jeshini. Batalioni ya kwanza ya Kolito ya Tanzania Rifles (zamani ikijulikana kama Kings African Rifle) walivamia eneo la silaha la kambi hiyo na kuwaweka kizuizini maofisa wa kizungu na wale Non-Commissioned Officers (NCOs). Kutoka hapo wakazunguka eneo la Ikulu, na pia kushikilia kituo cha radio, uwanja wa ndege, na maeneo mengine nyeti jijini. Baadhi ya Mawaziri inadaiwa waliwekwa kizuizini. Rais Nyerere na Makamu wake Bw. Kawawa walikuwa salama.

Kesho yake Nyerere alijitokeza hadharani. Hata hivyo siku hiyo ya Jumatatu mchana Waziri wa Ulinzi Bw. Oscar Kambona alienda kuzungumza na wanajeshi waasi na alinukulikwa akisema kuwa “nimeweza kuwapatanisha maaskari wazalendo na wageni kwenye Tanzania Rifles na wamenihakikishia kuwa bado ni watii kwa serikali”. Jumanne hali ikawa iko shwari (ndiyo siku Mwalimu alitokea hadharani na kuwahakikishia wananchi kuwa serikali bado ipo madarakani). Maasi ndiyo yalikuwa yameanza tu.

Majadiliano yalikuwa yanaendelea kati ya serikali na viongozi wa wanajeshi hao lakini kwa upande wa serikali wazo kuwa jeshi linaweza kuingia wakati wowote na kuiweka kwenye kabali serikali lilikuwa ni wazo la kutisha. Majadiliano pia hayakuwa yanakwenda vizuri na mwalimu aliyaelezea majadiliano hayo “kama ya mtekaji nyara na mhanga wake”.

Siku ya Ijumaa hata hivyo, majadiliano yalikuwa yanakwama na habari nzito kuwa mpango wa kumpindua Rais ulikuwa mbioni hasa baada ya waasi kuanza kuja na madai zaidi kama “haki ya kuchagua mawaziri watatu” na vitu kama hivyo. Ilikuwa ni Jumamosi ya wiki hiyo ndipo Mwalimu akiona hana jinsi na kwa kusita sita sana aliomba msaada wa Jeshi la Uingereza ambapo usiku wa kuamkika Jumatatu ya tarehe 25 kwa umahiri mkubwa walizunguka Kolito na kuzima maasi hayo.

Ukweli ni kuwa jaribio la kwanza la kuwatuliza maaskari waasi lililofanywa na Kambona halikufanikiwa licha ya yeye kufanya hivyo siyo kwa kujitolea bali kwa kuagizwa na Rais wake. Kambona alichoweza kufanya ni kutuliza muda ule wa Jumatatu ya tarehe 20 lakini hakunyamazisha mipango ya kuipundua serikali. Hata uamuzi wa kuita Jeshi la Uingereza kuiokoa serikali halali ya kiraia ulikuwa ni uamuzi mgumu. (nitawawekea kesho hotuba ya Mwalimu kufuatia kuzimwa kwa maasi hayo). Kambona alishiriki kikamilifu katika kuita Waingereza kuisaidia serikali yake baada ya kushindwa kuondoa tishio la mapinduzi ya kijeshi. Akiwa Waziri wa Ulinzi na mtii kwa serikali yake Kambona alifanya kazi yake kama ilivyopaswa licha ya kutokuwa na matokeo mazuri zaidi ya ilivyotarajiwa.

Lakini maasi yalitokana na nini hasa?

Wiki kama tano hivi kabla ya maasi na siku chache kabla ya maasi kuna mambo yaliyotokea ambayo yanaelezea kidogo kwanini wanajeshi (ingawa si wote) waliamua kuasi. Kwanza kabisa ni uamuzi wa Rais Nyerere kuamua kukomesha zoezi la Uafrikanisho wa utumishi wa umma ambapo watanzania weusi walipewa upendeleo maalumu katika ajira (modern day affirmative action). Kwa mtu ambaye alikuwa anapinga ubaguzi wa rangi Mwalimu aliamua kukomesha zoezi hilo. Kitendo hicho kilitafsiriwa na baadhi ya wanajeshi kuwa mwalimu alikuwa amegeuka ahadi yake kuwa wazungu wataondoka katika uongozi wa jeshi. Hilo likachangiwa na madai ya nyongeza ya mishahara toka kama dola 14.84 kwa mwezi kufikia dola 36.40 kwa mwezi. Hayo yalikuwa yamewauma sana wanajeshi.

Pili, siku chache kabla ya maasi Mwalimu alituma maafisa wa Rifles kama mia tatu hivi kwenda kuleta hali ya amani kufuatia mapinduzi ya Zanzibar (tarehe 12 Januari ile). Ni pale tu walipoondoka hao wengine kwenda kuleta amani Zanzibar hawa waliobakia kama 1600 ndipo walipoasi. Je yawezekana walifikiria kufanya kile kilichotokea Zanzibar?

Ilikuwa ni kutokana na maasi haya ndipo jeshi jipya la Wananchi wa Tanzania lilipoundwa likiwa limeingizwa katika siasa na kuanzisha kile ambacho kilijulikana kama makamisaa wa siasa na wanajeshi wetu walitakiwa kufahamu kabisa sera na itikadi ya chama kile kimoja. Ndiyo maana leo hii kama kuna vyombo ambavyo vinapendwa, kuthaminiwa na kutiiwa na watu wengi ni jeshi letu ambalo kwa hakika ni jeshi la Wananchi wa Tanzania.

mjj niliangalia mahojiano ya mama maria ile siku ya kumbu kumbu ya mwalimu.TVT.yalikuwa soo sensational....yaani alipoelezea namna alivyofanya siku ile..

anasema" usiku wakiwa chumbani na mwalimu wamelala ..mlango uligongwa..anasema yeye machale yakamcheza kwa kuwa siku moja kabla alikuwa ameota ndoto mbaya kuwa mumewe anatafutwa..akamueleza mwalimu kilugha kuwa asiamke kufungua ..akaenda yeye maria kufungua ule mlango..mlangoni alikuwepo ni EMILIO MZENA [nadhani mnamfahamu]..akamuambia amuite mwalimu haraka kwani askari waasi wapo njiani wanakuja ikulu...hapo wakatokomea na mwalimu..[hakutaka kuelezea walikoelekea..ila alicheka sana wakati anaongea hayo hadi machozi yakamtoka...yeye haraka alibadili akavaa baibui [ninja] ...akawatorosha watoto na mama mgaya ..akipita koridoni hakuna aliyemtambua ...hata barabarani alipishana na waasi hawakumtambua [akiwa kwenye landrover private]..she was very courageous...alienda kuwaficha watoto kanisani...asubuhi yake aliongozana na engneer wao..na mmoja wa wapambe wa mwalimu[like mzee mwamindi..if not mistaken]..baada ya maasi kupungua kabla kidogo askari wa uingereza kuingia ..akiwa tena kavalia baibui..wakachukua taxi[motokaa]...wakafanya kazi ya kupiga raking ili kuangalia hali ya amani...mitaani wakipita maeneo ya wenyeji ..ilikuona kama kuna utulivu..."

it was just a nice story ...na its seems yule mama ana story nyingi sana ...na inaelekea alikuwa na role kubwa tu na smart tofauti na watu wengi wanavyofikiri kuwa she was just a house wife...

inahitajika juhudi tafutwe ataengeneze DOCUMENTARY ya nguvu ,itasaidia sana kuhifadhi historia...
 
Mwanakijiji,
jaribu kusema ukweli wote, usichanganye na uongo humo.

1.sema kweli kwamba Nyerere na Kawawa walijificha/walifichwa na Emilius Mzena -- Mkuu wa Usalama wa Taifa.

2.mpe stahiki yake kwamba Kambona alifanya kazi nzuri ya kuwezesha kuvuta muda mpaka majeshi ya Uingereza yakaitwa.

3.Ni vizuri ungeweka msisitizo kwamba Majeshi ya Uingereza yaliitwa kwasababu madai ya waasi yalianza kuwa un-realistic. Suala hapa siyo Kambona kushindwa kazi, ni madai kuwa hayatekelezeki.

4.Mpe sifa zake Kambona kwa ku-risk maisha yake kwa ajili ya nchi yake na Raisi wake. Hata kama huo ulikuwa ni wajibu wake tu, na alipokea maagizo ya Raisi wake, wangapi hukimbia/hugomea maagizo kama hayo?

5.Tanganyika Rifles haikuwa na maafisa 300 mwaka 1964!! Waliotumwa Zanzibar ni FFU na Polisi siyo Tanganyika Rifles.

6.Kambona alifanya kazi nzuri na kubwa wakati wa maasi ya 1964. Kuna uwezekano kabisa utiifu na utumishi wake ktk kipindi kile kigumu na cha mashaka uliiepusha jamhuri yetu changa na UTAWALA WA KIJESHI.

7.Hakuna Ubishi kwamba Nyerere ndiyo Baba wa Taifa letu. Lakini ni vizuri wale walioshirikiana naye nao wakatajwa kuwa walikuwa karibu naye.

NB:
Soma Kitabu cha Maasi ya 1964 utaona kwamba ni Emilius Mzena ndiye aliyemzuga Hingo Ilogi mpaka Nyerere na Kawawa wakaweza kutoroka Ikulu.

Kwa kumbukumbu zangu, Kitabu hicho hakionyeshi kama kulikuwa na mawasiliano kati ya Kambona, na Nyerere aliyekuwa mafichoni.
 
Mwanakijiji,
jaribu kusema ukweli wote, usichanganye na uongo humo.

Hebu tuone ukweli unaouonesha wewe tofauti na nilichoelezea hapo juu.

1.sema kweli kwamba Nyerere na Kawawa walijificha/walifichwa na Emilius Mzena -- Mkuu wa Usalama wa Taifa.

Alifichwa na Usalama wa Taifa; cha ajabu hapo nini ni ukweli kuwa lilikuwa jukumu la Usalama wa Taifa kuhakikisha ulinzi wa Rais. Hata leo wamachinga wakijifanya wanaenda kuandamana kuiteka Ikulu guess what will happen..

2.mpe stahiki yake kwamba Kambona alifanya kazi nzuri ya kuwezesha kuvuta muda mpaka majeshi ya Uingereza yakaitwa.

Alifanya jukumu alilotumwa na alifanya kwa utii kwa rais wake. Uongo hapo ni nini? Kambona alikuwa Walinzi wa Ulinzi wa wakati ule?

3.Ni vizuri ungeweka msisitizo kwamba Majeshi ya Uingereza yaliitwa kwasababu madai ya waasi yalianza kuwa un-realistic. Suala hapa siyo Kambona kushindwa kazi, ni madai kuwa hayatekelezeki.

Ndiyo hilo hilo; kwa sababu wale wanaodai kambona "alituliza waasi" wanashindwa kuelewa kuwa alifanya alichotakiwa kufanya na yeye mwenye alipoona kuwa ujumbe aliotumwa na Mwalimu kuwafikishia waasi hauwaingii kichwani alikubaliana na Mwalimu kuomba majeshi ya Uingereza. Uongo hapo ni nini?


4.Mpe sifa zake Kambona kwa ku-risk maisha yake kwa ajili ya nchi yake na Raisi wake. Hata kama huo ulikuwa ni wajibu wake tu, na alipokea maagizo ya Raisi wake, wangapi hukimbia/hugomea maagizo kama hayo?

Joka Kuu, sasa hilo ni swali jingine kabisa. Kwanza tukubaliane kuwa Kambona alifanya alichofanya kwa maagizo ya Rais wake na akitelekeleza wajibu wake kama Waziri wa Ulinzi. Hata leo hii kikitokea kitu jeshini ni Kapuya atakayekwenda kwanza. Tukishakubaliana hilo basi tujenge hoja kama kweli Kambona alirisk maisha yake. Ukweli ni kuwa hakuwa kwenye hatari ya maisha yake. No sir, he was not in any imminent personal danger. Hakuna hata mahala pamoja kwenye historia panaposema waasi walitishia maisha ya "mjumbe wa serikali" au kuzungumza na serikali.


5.Tanganyika Rifles haikuwa na maafisa 300 mwaka 1964!! Waliotumwa Zanzibar ni FFU na Polisi siyo Tanganyika Rifles.

Hili tutatofautiana; documents nilizoziona mimi zinasema ni maafisa wa jeshi walioenda kule Zanzibar na pia ninafahamu polisi walienda pia. TR ilikuwa na wapiganaji wangapi 1964?

6.Kambona alifanya kazi nzuri na kubwa wakati wa maasi ya 1964. Kuna uwezekano kabisa utiifu na utumishi wake ktk kipindi kile kigumu na cha mashaka uliiepusha jamhuri yetu changa na UTAWALA WA KIJESHI.

Hapa ndipo legend mnapoianzisha na hero creation inapooanza. Kambona hakufanya kitu chochote ambacho hakutakiwa kufanya. Kama Nyerere angesema usiende naye angejiendea basi hicho ni kitendo cha kishujaa; Kama Kambona angeambiwa ukija tutakulipua naye akaenda basi hicho ni kitendo cha kishujaa. Lakini mtu kutekeleza wajibu wake hata kama katika mazingira magumu lazima itambuliwe hivyo. Sasa hii haiondoi ukweli kuwa Kitendo cha Kambona kumtii Nyerere na kufuata maagizo yake kilikuwa ni kitendo cha heshima na cha kuigwa. Maasi hayakutulizwa kwa sababu ya Kambona hilo ni uongo usiothibitika kihistoria. Ukweli ni kuwa maasi yalizimwa baada ya uongozi wa jamhuri yetu kuona kuwa madai ya waasi hayatekelezeki na haiwezekani kuwaridhisha isipokuwa kuwazima kwa nguvu. Maasi yalizimwa sababu ya uamuzi wa kishujaa, wa lazima, na wakutokubembeleza wa Mwalimu Nyerere. The hero was not Kambona, it was Mwalimu.


7.Hakuna Ubishi kwamba Nyerere ndiyo Baba wa Taifa letu. Lakini ni vizuri wale walioshirikiana naye nao wakatajwa kuwa walikuwa karibu naye.

Hili halina mjadala ndugu yangu, tuweke rekodi straight halafu haya mengine yatafuata. Hakuna mahali ambapo nimekataa hata mara moja kuwa Kambona hakuwa karibu na Baba wa TAifa au hakushikiri kwa kiasi kikubwa katika uhuru wa nchi yetu. No sir. NInachosema kumfanya Nyerere ndiye adui, na Kambona the "unsung hero" is mere fabrication of history. Hadi inapofikia 1967 Kambona was a good and dedicated leader and that should be recognized. Until he wento to "self-imposed exile" that is when he turned into a political fraud.


NB:
Soma Kitabu cha Maasi ya 1964 utaona kwamba ni Emilius Mzena ndiye aliyemzuga Hingo Ilogi mpaka Nyerere na Kawawa wakaweza kutoroka Ikulu.

Kwa kumbukumbu zangu, Kitabu hicho hakionyeshi kama kulikuwa na mawasiliano kati ya Kambona, na Nyerere aliyekuwa mafichoni.

Kitabu hiko "hakioneshi" haina maana "hayakuwako". Ndio maana wito wangu wa kufungau makabrasha ya historia yetu bado upo. Na ndio maana nimesema watu walioshiriki bado wapo kwanini wasiohijiwe badala ya kuandika hadithi ya mtu mmoja mwenye hasira, kisasi na maumivu ya moyo na kuifanya kuwa "ni ukweli, ukweli mtupu, na si kingine bali ukweli". Ungana nami kuitisha an open and transparent research on our early history as a republic. Kwanini hilo hamlitaki?
 
Ni vema topiki hii irudishwe Siasa...kwani inahusu siasa, tena siasa kubwa...
 
hoja ya siasa imeletwa kwenye vibweka!
au ndio mkakati unaanzwa wa kuhamisha
hoja nyingine kule siasa ambayo inamrindimo
unaofananafanana na huu wa kwenye hoja hiii?
only time will tell
 
Ni vema topiki hii irudishwe Siasa...kwani inahusu siasa, tena siasa kubwa...


bwana we, labda Kambona hazungumzwi.. inakuwa ni siasa anapozungumzwa Mwalimu na "vibweka" anapozungumzwa Kambona. On the other hand, labda ma MoD walipoona mambo ya Maboli na Magololi basi wakaona vimekwisha nadhani irudishwe tu kule na heading ibadilishwe kidogo iwe "Kambona: Shujaa Aliyesahauliwa?"
 
Ni vema topiki hii irudishwe Siasa...kwani inahusu siasa, tena siasa kubwa...


hapo umenena kaka..haikua haki kuileta kwenye vibweka..kwa sababu hapa wengi wanajitahidi kumwaga details at there best..watu kutupiana vijembe ni kawaida ..lakini kamwe haibadilishi umuhimu wa hii mada kwenye kuweka historia sahihi za viongozi wetu wasioenziwa....

tukumaliza na kambona tutampitiaa na prof abdulrahman babu[ndoto zake za kuwa mgombea mwenza 1995 zilikatishwa na mahakama kusema kuwa alikuwa amehukumia hukumu ya kifo ambayo ilitakiwa kutekelezwa].......wajameni kuna vituko vingi sana vimefanyika.....na nyerere was a smooth operetor..alimtorosha babu na wenzake wasiface deathrow...

kazi aliyofanya kambona kwenye maasi HAIPINGIKI....ukizingatia maaskari wengi walikuwa wakimpenda....kama angekuwa na roho mbaya angeweza kuamua kujitangaza rais....kwa hili watanzania tuna deni kwa spirit yake...ipo siku watu watamfukua wamzike upya kwa itifaki[hii imetokea kwenye nchi nyingi..mnakumbuka hata kenya ,kenyatta aliwafanyia wapiganua uhuru wenzake hivi hivi...matokeo yake tawala zilizofuatia wananchi wakaamua kuwaenzi...kina thom mboya,..ponot..dedan kimathi ets..dedan kimathi hadi leo mwili wake unatafutwa ili azikwe kwa heshima za kijeshi[kumbuka huyu ndie wakati kenyatta akiwa anachuma matunda [work] uingereza na kuwa na bibi wa kizungu pale ..huyu ndie aliyekuwa akiongoza maumau hadi akauliwa..kenyatta hakutaka kumuenzi ..hakutaka aonekane alipigana kumzidi..

hata ukiangalia karume nae alimfukuza okello kwa wivu wa aina hii...

nakamilisha kwa kusema kua viongozi waazilishi wa afrika wote walikuwa na namna iliyofanana ya kukabiliana na tishio la kuibuka kwa umaarufu wa viongozi waandamizi kwenye serikali zao..pia walikuwa na namna inayofanana ya kufunika historia za viongozi wenzao kwenye mapambano kwa lengo la kkutaka nafasi kubwa zaidi kwenye historia za nchi zao.......

changamoto tulionayo sasa ni tofauti..tunao uwazi na haki na uelewa zaidi..marais wa sasa hawawezi tena kumaliza upinzani wa ndani au nje kwa njia hizi ...wanazo njia nyingine kama mnazoziona..lakini ni muendelezo ule ule!!!!!
 
Back
Top Bottom