Hamna alio vamia ilikua propaganda za nyerere kujustify vita yake ya kumsaidia rafiki yake pan afrcanist obote kwa kuumiza watanzania hamna tulicho pata kwenye hiyo vita kabisa.Kwahiyo mtu akija kwako kutaka kuchukua ardhi yako utamchekea??utakua mpuuzi wa namna gani.
Huu ndio ukweli na Huwa nasema mara nyingi na alifanya hivi makusudi Ili asipate Changamoto ya kutawala.Nawasalimu wanaJF.
Leo nimeamua niseme ukweli kuhusu nchi yetu hii ya Tanzania.
Katika miaka 24 ya utawala wa Mwalimu Nyerere, alitangaza maadui wakubwa wa watatu wa watanzania:-
1. UJINGA
2. UMASKINI
3. MARADHI
Mwalimu Nyerere hakuwa visionary leader alikuwa mwanaharakati, badala ya kujenga nchi na kuwapatia elimu watanzania alikuwa na misemo tu, kuongea majukwaani tu bila vitendo.
Je, Mwalimu Nyerere kitu gani kilimshinda kujenga shule za msingi kila kijiji kwa miaka yote hiyo 24 badala yake akajenga ofsi za chama kila kijiji?
Je, kitu gani Mwalimu Nyerere kilimshinda kwa miaka 24 kujenga vyuo vya ufundi kila wilaya badala yake alijenga viwanja vya mpira wa miguu?
Lowassa aliweza kujenga shule za secondary kila kata. Je, Mwalimu Nyerere kitu gani kilimshinda kwa miaka 24 kujenga Shule hizo?
Tunaweza kutafuta mchawi wa taifa letu. But kusema kweli Nyerere alitukosea sana watanzania.
Nadhani Mwalimu Nyerere alikuwa na mentality za utawala wa kifalme ambao hauna malengo.
Tunaona mataifa mengi yaliyowekeza kwenye elimu alivyopiga hatua.
Yeye Mwalimu Nyerere hakuwa na nia kabisa ya watanzania wengi kupata elimu. Wakati wa Mwalimu Nyerere kusoma ilikuwa ni bahati na siyo haki ya Mtanzania.
Taifa lisilokuwa na elimu haliwezi kujiendesha vizuri, litabaki kuwa ombaomba tu.
Sisi kama Taifa ni lazima tujue tulipoangukia, tukainuke na kusonga mbele. Bado hatujachelewa.
Tanzania tupo na vijiji na mitaa isiyozidi 20,000. Kwani alishindwa nini kuchukua kila kijiji vijana 10 na kuwapeleka kusoma nchi za nje? Vijana 10 kila kijiji maana yake ni watanzania 200,000 tu.
Yaani angechukuwa wanawake 5 na wanaume 5.
But uwezo alikuwa nao wa kufanya hivyo.
Nitaendelea kueleza machungu yangu haya kwenye uzi huu ili tujue wapi tulipoangukia tukainuke na kusonga mbele...
Ndugu uthibitisho upo mkubwa tu kuonesha Tanzania ni taifa lililojengwa kwenye misingi ambayo siyo ya elimu.Wewe mwenye mada nadhani haumlaumu Nyerere bila uthibitisho,naona unakomaa na swali la alijenga shule za msingi ngapi? Bila shaka kabla ya kuleta mada ya kumlaumu kuhusu elimu,utakuwa umeshafanya utafiti ni shule ngapi alijenga.
Kwa hiyo tulitegemea utuambie kwa miaka 24 aliyokaa madarakani alijenga shule kadhaa...na hawa wa baada yake miaka 38 baada yake wamejenga kadhaa..hapo nasi tuseme ni kweli Nyerere hakufanya kitu.
Jambo jingine bayana ni kwamba,hata ukibahatika kupata takwimu ya kutaka kuwatukuza hawa wa baada yake kwamba wamejenga shule za msingi nyingi kila kijiji,lazima utambue vijiji vimeongezeka vingi tu tangu 1985 hadi sasa
Juzi mtoto wa samia kaongoza ujumbe kwenda kwa Museveni, hatujui aliongoza ujumbe kama nani. Nyerere angeongoza kwa style hiyo, hawa kina samia hata hii misitu iliyopo wasingeikuta.Huyu ndio rais aliyeweza kulinda rasilimali zanchi kama leo hii rais ndani ya miaka 2 tu kashauza kila kila kitu tukimpa miaka 20 hii nchi itakuwa sio yetu tena tutarudi kwenye ukoloni
Kabisa kabisa !!Mada yako inahitimisha kuwa Nyerere hakuna alichotufanyia Nchi hii,ameturudisha nyuma sanaa,
Wachangiaji wanakujibu mambo aliyoyafanya kwa Nchi hii,unarudi tena eti tuongelee Elimu tu.
Kuna uwezekano mkubwa hata hapo kwenye elimu,bado elimu iliyotolewa kipindi hicho ilikuwa bora na nzuri kuliko hata sasa
Kumlaumu Mwalimu hakusaidii kitu. Kunakosaidia ni watu kwenda shule na siyo tu kwenda shule ni kupata elimu bora na kuitumia vizuri. Kulalamikalalamika tu hakusaidii kitu mpaka mwisho wa dunia. Ni kama mtu aliyeibiwa pesa kila mara aseme tu ameibiwa na asifanye jitihada za kutafuta pesa zingine, unadhani kulalamika huko kutarejesha pesa zilizoibiwa? Jibu ni hapana. Hivyo, tujifunze kuona matatizo ndiyo, lakini jambo muhimu zaidi ni kutafuta njia za kuyatatua hayo matatizo. Hiyo ndiyo njia ya mafanikio.Nawasalimu wanaJF.
Leo nimeamua niseme ukweli kuhusu nchi yetu hii ya Tanzania.
Katika miaka 24 ya utawala wa Mwalimu Nyerere, alitangaza maadui wakubwa wa watatu wa watanzania:-
1. UJINGA
2. UMASKINI
3. MARADHI
Mwalimu Nyerere hakuwa visionary leader alikuwa mwanaharakati, badala ya kujenga nchi na kuwapatia elimu watanzania alikuwa na misemo tu, kuongea majukwaani tu bila vitendo.
Je, Mwalimu Nyerere kitu gani kilimshinda kujenga shule za msingi kila kijiji kwa miaka yote hiyo 24 badala yake akajenga ofsi za chama kila kijiji?
Je, kitu gani Mwalimu Nyerere kilimshinda kwa miaka 24 kujenga vyuo vya ufundi kila wilaya badala yake alijenga viwanja vya mpira wa miguu?
Lowassa aliweza kujenga shule za secondary kila kata. Je, Mwalimu Nyerere kitu gani kilimshinda kwa miaka 24 kujenga Shule hizo?
Tunaweza kutafuta mchawi wa taifa letu. But kusema kweli Nyerere alitukosea sana watanzania.
Nadhani Mwalimu Nyerere alikuwa na mentality za utawala wa kifalme ambao hauna malengo.
Tunaona mataifa mengi yaliyowekeza kwenye elimu alivyopiga hatua.
Yeye Mwalimu Nyerere hakuwa na nia kabisa ya watanzania wengi kupata elimu. Wakati wa Mwalimu Nyerere kusoma ilikuwa ni bahati na siyo haki ya Mtanzania.
Taifa lisilokuwa na elimu haliwezi kujiendesha vizuri, litabaki kuwa ombaomba tu.
Sisi kama Taifa ni lazima tujue tulipoangukia, tukainuke na kusonga mbele. Bado hatujachelewa.
Tanzania tupo na vijiji na mitaa isiyozidi 20,000. Kwani alishindwa nini kuchukua kila kijiji vijana 10 na kuwapeleka kusoma nchi za nje? Vijana 10 kila kijiji maana yake ni watanzania 200,000 tu.
Yaani angechukuwa wanawake 5 na wanaume 5.
But uwezo alikuwa nao wa kufanya hivyo.
Nitaendelea kueleza machungu yangu haya kwenye uzi huu ili tujue wapi tulipoangukia tukainuke na kusonga mbele...
Asante kwa uchambuzi mzuri..Ndugu uthibitisho upo mkubwa tu kuonesha Tanzania ni taifa lililojengwa kwenye misingi ambayo siyo ya elimu.
Tunaona kabisa eti kiongozi wa kisiasa kigezo chake ni kujua kusoma na kuandika tu? Halafu kiongozi huyo ndiye anayetunga sheria!!!!
Huoni limejengwa taifa la namna gani?
Nimetoa mifano mingi tu. Kuna mikoa mingi mno hakukuwa hata na shule moja ya sekondari. Just imagin mkoa mzima hakuna shule ya sekondari.
Pili vijiji vingi tu wananchi walishindwa kusoma elimu ya shule ya msingi kutokana na kukosekana kwa shule. Na wengine walikufa kutokana na umbali wa shule. Yaani kata moja inakuwa na shule moja ya msingi tena iliyojengwa na wakoloni.
Hivi na jambo hili unataka kusifu? Kama mtu ali fail lazima tuseme ili tuweze kujua tulipoangukia.
Matokeo haya tunayoyaona ya vijana kuwa machawa ni ukosefu wa Elimu na mwasisi wa jambo hili ni Mwalimu Nyerere.
Kweli tatizo ni watu wenyewe ulafi umezidi sababu ya kutomjua Mungu na pia Ulimbukeni wa kutaka kuwatambia wengine !!CCM ina kosa gani sasa? Ongeleeni mapungufu ya watu na mtu binafsi, chama kiwe Chadema, CCM, sijui TLP na vingine, swala ni waTanzania tu, ziko hulka za kiTanzania ambazo haijalishi mtu katoka chama gani, swala ni mTanzania tu kwisha, tunafanana hata kama ni chama gani kitaongoza, tena ndiyo tunaweza kuja kuwakumbuka hata hao CCM
Nimeongelea kuna baadhi ya nchi walijenga misingi ya nchi zao katika elimu. Nchi yetu haijajengwa kwenye misingi ya elimu.Asante kwa uchambuzi mzuri..
Hoja yako ni shule za sekondari au shule za msingi kama mada yako ilivyoanza?
Mimi ninaamini,kama ambavyo viongozi wetu wanatuambia siku zote, "Taifa halijengwi siku moja" kama hayo ni ya kweli,basi muasisi nae alifanya sehemu yake,waliofuatia nao wamefanya sehemu yao,maana hatujafika mwisho ndiyo maana hadi leo bado shule zinaendelea kujengwa.
Viongozi kujua kusoma na kuandika,ni jambo tunaloweza kulisahihisha hata kesho tukiamua,halihiitaji kumlaumu mtu aliyeongoza miaka mingi iliyopita.
Kwa ujumla Taifa hili ni letu sote,tukihitaji kulifanya kuwa Taifa bora ni sisi,tukitaka kuendelea hivi tulivyo bado ni maamzi yetu sisi hao hao
Yeye alijitahidi japo kulipambania taifa hili, je wewe umefanya Nini mpaka Sasa? Compare and contrast.Alikaa ikulu kwa zaidi ya miaka 20 ! Bado alishindwa ku organise hata katiba tu?
Kwani unayemlaumu huyo amewahi kuwa Rais wa kwanza wa Tanzania?Yeye alijitahidi japo kulipambania taifa hili, je wewe umefanya Nini mpaka Sasa? Compare and contrast.
Kipindi kile cha uhuru idadi ya watu ilikuwa ni milioni tisa tu ! Sehemu kubwa ya Nchi ilikuwa ni mapori tu !Niambie Nyerere alijenga shule ngapi za msingi?
Chukua Pepsi unywe ndugu. NAKAZIA ππππ¨π¨π¨Nyerere unamuonea bure.
Nyerere amekuta nchi iko so disorganized, magonjwa, ujinga, umaskini wa kutupwa na ukabila
Nyerere alikua na mlima mrefu sana wa kupanda, kwanza kuhakikisha chembechembe za ukabila zinakufa na kuleta umoja, kupambana na ujinga, kuhakikisha watu wanajua hata kusoma na kuandika. Ulitaka awape elimu gani kama hata kusoma na kuandika hawajui? Ulitaka awape elimu ya uraia wakati hata kusoma hawajui?
Mwalimu kakuta pepopunda, surua, polio, kifua kikuu, kifaduro, kwashakoo na magonjwa mengine yametamalaki kwa watanzania, ulitaka awape alimu ya uraia huku akiwaacha wafe?
Mwalimu kakuta Watanzania ni mafukara wa kutupwa, hawana matumaini ya kesho, akaanzisha vijiji angalau wawe pamoja ili iwe rahisi kuwaletea maendeleo kwa sababu walikua so scattered and disorganized, akaanzisha mashamba ya ushirika ama sustainable farming, akahakikisha anapeleka watu shule wakasome waje wampokee ma kubadilisha nchi kina Chenge na wengine, matokeo yake, wamekua wezi.
Nyerere alipigana kuanzisha viwanda, mashamba ya vijiji, na mambo mengine mengi bila kuuza ardhi hata kipande kimoja kwa waarabu wala wazungu.
That man died poor, had nothing kwa kuwapigania Watanzania
Na alivyokua mwema yule bwana, alipotoka madarakani aliangalia nyuma, akaona failures zake na success zake, akakiri kwamba kweli kuna mahala alifeli, na sababu kubwa za failure za mwalimu zilikua nje ya uwezo wake, kumbuka oil crisis and financial crisis za 70s and 80's.
Yule jamaa alipoona he can continue failing, akajipumzikia yeye mwenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote. Angeweza kufia madarakani.
Tukubaliane kwamba CCM ndio ya kulaumiwa, ila kumpa Nyerere zigo la lawama ni kumuonea. Yule bwana aliachia hii nchi miaka zaidi ya 35 iliyopita, hao wengine waliofuata walifanya nini?
Kipindi chake kulikuwa hakuna ufisadi ! Failure ya nchi hii na nchi zote za Africa ni kwa sababu ya UFISADI !! Hata Olusegun Obasanjo alilisema hili mbele ya wakubwa wenzake !!Kwani unayemlaumu huyo amewahi kuwa Rais wa kwanza wa Tanzania?
Tunamuongelea Nyerere kama Rais wa kwanza wa Tanzania. Alijenga raifa la namna gani.
Taifa lilivyo sasa hivi ni failure yake.
Kati yangu na wewe nani anadanganya?Kipindi kile cha uhuru idadi ya watu ilikuwa ni milioni tisa tu ! Sehemu kubwa ya Nchi ilikuwa ni mapori tu !
Shule zilijengwa kila sehemu palipokuwepo watu na zahanati pia zilijengwa kila mahali palipokuwepo watu !
Huduma zote za elimu na afya zilitolewa bure kabisa tena mpaka vitabu madaftari chakula na madawa yalikuwa ni bure !
Tulikuwa pia tukipewa warrants za kusafiria kwenye mabasi na treni kwenda na kurudi popote pale ulipokuwa umepangiwa kusoma !!
Acheni kukaririshwa uongo, Mwalimu alikuwa ni binadamu na alikuwa na baadhi ya mapungufu lakini Mwalimu alikuwa na nia njema kabisa na taifa na wananchi wake ndio maana hakujilimbikizia mali na wala hakuwapendelea familia yake !
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu !!
Niambie nini ilipelekewa mwalimu Nyerere akaandika kitabu cha tujisahihishe kama kulikuwa hakuna ufisadi?Kipindi chake kulikuwa hakuna ufisadi ! Failure ya nchi hii na nchi zote za Africa ni kwa sababu ya UFISADI !! Hata Olusegun Obasanjo alilisema hili mbele ya wakubwa wenzake !!
Hata Mimi naamini hilo ndilo lililokuwa kosa lake kuu ambalo hata huko alipo atakuwa analijutia !! Kama mkapa alivyojutia kuviua Viwanda alivyovikuta !!Hapa naunga mkono 100%. Unafiki ulioje kusema katiba yetu inalinda dikteta lakini huchukuo nafasi yoyote kuzuia hilo, singlehandedly alikuwa na uwezo wa kutupa katiba bora ya muda wote.
Ulikuwepo udokozi sio ufisadi !Niambie nini ilipelekewa mwalimu Nyerere akaandika kitabu cha tujisahihishe kama kulikuwa hakuna ufisadi?
Halafu niambie sababu gani ilisababisha kukawa na azimio la arusha kama ufisadi haukuwepo?