Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

Kama ile kesi ya MWANA FA NA AY mpaka wakalipwa BIL 2 sijui na tigo ina maana ukitumikaa wimbo bhasi ndo haki ya msanii kulipwa ila likitumiKA BEAT tu bhasi haki ya producer kulipwaa... ngoma ngumu snaa hii 😀 😀 😀
Mkuu huwezi Jua labda hermy B alilipwa na washikaji.

Au aliuza beat na Kila kitu kuhusu hio beat.

Haya mambo huwa yanatokeaga na wasiojiandaa mapema na mikataba yenye kulinda haki zao huishia kulilia tu.

Wasaniii waache njaa njaa wanunue nyimbo na haki hio nyimbo na Kila kitu

Ila yanapotokea mazali kama haya ya ma movie kutumia nyimbo na beat zao wapige pesa.
 
Nafikiri waliingia mgogoro na Prof. Jay baada ya P. Funk kuchukua hela kwa kampuni ya movie iliyotumia beat ya bombo clat ambapo original ni beat ya nikusaidiaje. Profesa alilalamika kuwa hakupewa hata senti
Jamaa aliweka pesa yote mfukoni[emoji28]. Halafu si ilikia milioni mia!
 
Ni balaa boss uwa hawajiulizi familia za kina michael Jackson, Bob marley, tupac kwa nini hadi leo wanafaidika na sanaa za ndugu zao😀😀mjini kuna wahuni ata sio wasanii ila wanawatumia kupiga pesa, bongo kuna majipu mengi wanayachekea kuna WANENE ENTERTAINMENT pia wanawatumia wasanii vibaya nayo yanakubali tu bila kujitambua kama wakina young killer, chin beez, fid q na wengine kibao
Killer alisepa miez sita tuuu,. Alipoona chenga akachora
 
Music publishing ni ishu tata sana. Sio huku kwetu tu bali hata huko kwa walioendelea. Kuna mifano kadhaa ya wanamuziki wakubwa ambao walitangaza kufilisika (bankruptcy) licha ya "kuuza" mamilioni ya kopi za rekodi. Mfano Toni Braxton, TLC n.k. Lakini huo ni mjadala wa siku nyingine.

Typical music production (unless kila kitu mpaka kuimba amefanya mtu mmoja) huwa inahusisha producers, composers, melody makers, session musicians na engineers. Hawa huwa wanakuwa na haki zinazoitwa mechanical rights za huo wimbo. Ukiangalia hapo sijamtaja mtu mmoja, MUIMBAJI/WAIMBAJI. Hawa wanakuwa na haki za uimbaji (singing right) kwenye huo wimbo.

Tafsiri ya rights zilizotajwa hapo juu ni kwamba kwa namna fulani KILA mtu aliyeshiriki kutengeneza huo wimbo (unless kwa sababu fulani amekubali kufanya bure) anatakiwa kulipwa. Analipwaje ndio mjadala ninaouona kwenye huu uzi. Suala la mshiriki kwenye production atalipwaje huwa liko kimkataba, inaweza kuwa malipo ya mara moja au percentage fulani ya publishing (wenzetu wanaitaga points). Kuna watu wamesema kwamba P Funk amepora haki ya watu aliofanya nao kazi ya production. Tutajuaje kama P alishamalizana nao kimalipo na wakaachia rights zao za publishing? Je, hizo haki zao zimesajiliwa kisheria? Hii ishu nitaijadili kidogo huko mbele.

Again, typical music production huwa inasimamiwa Producer. Kwenye music production kumekuwa na tatizo la watu kuchanganya producer na beat maker au session musician. Kwa kawaida huwa inategemewa producer awe pia musician ili awe na uwezo wa kuendesha zoezi zima la production. Lakini SIO lazima yeye apige vyombo au kufanya programming kwenye huo wimbo unaotengenezwa. Kuna mtu kasema "P Funk hajui hata kupiga kinanda", kwanza sio kweli, P Funk anaweza kupiga kinanda, pili ili awe ame-produce wimbo fulani sio lazima personally afanye beat making, yeye anahakikisha kila mhusika ana-play role yake na standard ya production inakuwa per exellent. Producers wengi wakubwa huko duniani huwa hawapigi vyombo wao wenyewe bali hutumia session musician au beat makers mfano Quincy Jones, Dr Dre, P Diddy, Irv Gotti etc.

Sasa tuje kwenye ishu tata ya hatimiliki aka publishing. Tofauti na watu wengi wanavyoamini, publishing rights sio automatic. Ni lazima ziwe zimesajiliwa kisheria (registered) ili zilindwe, kama umefanya kazi yoyote ya ubunifu bila kuisajili wakatokea wajanja wakasajili imekula kwako. Jamaa watapiga hela huku wewe ukipiga miayo. Huku kwetu nina uhakika kuanzia wasanii, wapiga vyombo na wengineo walikuwa hawalijui hilo ndio maana watu wengi wakiwemo wasanii wanaamini kwamba akienda studio akalipia kurekodi wimbo automatically unakuwa mali yake. Kitu ambacho sio kweli.

Sijajua mikataba ambayo wasanii wa hapa kwetu (wakiwemo wa WCB) huwa wanaingia na lebo huwa ina-address suala la publishing au hapana. Ambacho nina uhakika nacho ni kwamba wasanii wengi (hasa wa zamani) hawako aware kuhusu ishu ya publishing, na ndio mzozo wa Prof Jay na P Funk ulipoanzia.

Actually ishu ya Prof Jay na P Funk kuhusu beat ya nikusaidiaje haikuanzia kwenye beat hiyo kutumika kwenye movie. Baada ya Prof Jay kurekodi wimbo huo na kuhit, Chameleone akamfuata P akitaka atumie hiyo beat, P akamchaji Chameleone USD 2,000. Prof aliposikia akaja juu na kulalamika kwamba beat yake imeuzwa bila idhini yake. Lakini kiukweli Prof hakuwa ma haki yoyote kwa kuwa Chameleone alitumia beat tu, sio wimbo wote. Wimbo wa Chameleone ukaja kutumika kwenye movie ya Queen of Kitwe iliyotengenezwa na Disney na Chameleone akavuta mpunga. P akakomaa na Disney na kwa kuwa sheria ilikuwa upande wake alalipwa. Again Prof hakuwa na haki kwani wimbo uliotumika ni wa Chameleone na sio wa kwake.

Hitimisho ni kwamba music business is very shady, inatakiwa msanii ajifunze SANA sheria za hatimiliki na ahakikishe haki zake ziko documented na zimesajiliwa kisheria ili zilindwe.
Maelezo mazuri kabisa P funk ndio mwenye haki na beat

Jamaa mmoja katoa mfano mwepesi sana huko juu na unaeleweka.

Yaani "TOYOTA ikikuuzia wewe crown ukaenda tambia mademu au ukaisajili Uber upige Hela huwezi kuwazuia kumuuzia jirani Yako nae crown nae akapige Hela au akat.om.bee mademu.

Still Toyota wanabaki na haki ya ubunifu wa Crown

Gari ni Yako lakini ubunifu ni wao."

Easy tu
 
Ni balaa boss uwa hawajiulizi familia za kina michael Jackson, Bob marley, tupac kwa nini hadi leo wanafaidika na sanaa za ndugu zao😀😀mjini kuna wahuni ata sio wasanii ila wanawatumia kupiga pesa, bongo kuna majipu mengi wanayachekea kuna WANENE ENTERTAINMENT pia wanawatumia wasanii vibaya nayo yanakubali tu bila kujitambua kama wakina young killer, chin beez, fid q na wengine kibao
Tatizo njaa kaka, ukishashiba ndio udaana kupata akili ila njaa ikikupiga unawaza hela ya kula na kumantain jina
 
yaah sema ndo hivyo sijui nani ana mmenage maana bila hivyo atapotea bila kufaidi pesa zakee..sioni akipiga show akati ndo muda wenyewe..!! apate manager kichwa azungukee aisee kuzikusanyaaa amezubaa sanaa...

Management yake ipo vizuri kwenye kutoa kazi ila kitengo cha kumbrand na kumpa promo marioo naona pamelegea kidogo

Niliona kaenda kupiga show kenya lakini sikuona media tour kwenye vipindi vyenye fan base kubwa kama 10 over 10, wakati kenya kashapenya, ilitakiwa akite mizizi maana naskia hata hela ya show kenya, wabongo hulipwa vizuri kuliko home
 
Wakuu kuna wakati ukweli lazima usemwe. Mambo ya kusema mtu aheshimiwe kwa kuwa alikuwa anatengeneza beats nzuri hizo ni heshima za uoga.

P Funk ambaye kiukweli zaidi ya kufanya production ya muziki na kupokea malipo hana jingine kubwa alilolifanyia bongofleva.

Kwa wasiofahamu wasanii wote waliokuwa chini ya bongo records hawana nyimbo au album wanazomiliki vyote anamiliki P Funk.

Ngwea amekufa maskini huku muziki wake unamilikiwa na P Funk mpaka leo anakula hela ya Ngwea.

Ukiona wimbo wa Juma Nature au Feruzi kwenye YouTube, Boomplay au digital platform yoyote usidhani ukisapoti unamsaidia msanii hiyo ni pesa ya Majani. Leo hii ikitokea bahati mbaya Juma Nature hatupo nae watoto wake watarithi nothing utajiri wake wa nyimbo ni mali ya watoto wa Majani kina Paula.

Huyu P Funk aliyekuwa anawapiga ngumi na mitama watoto wa kimaskini wakienda kuomba msaada wa kurekodi nyimbo zao.

Kumbuka pale bongo records kwenye utengenezaji wa beats waliusika watu wengi zeze ilitengenezwa na bizimani ila achukui hata sh 10, beat ya mikasi alitengeneza prof ludigo ila achukui hata sh 10 kina Marlon linje walikuwa wanapiga vinanda na vyombo vingine kwenye kutengeneza instrumental za wasanii haki zao za ubunifu anachukua nani kama sio mnyonyaji p Funk?

P Funk tunamuheshimu kwa kutengeneza beats ila zaidi ya production kaufanyia nini huu muziki?
P Funk uwa wakiitwa wasanii walipwe yeye anaenda kuchukua malipo kama nani? Kina Daz Baba wamekuwa vituko mtaani hela zao kwa nini unakula wewe PFunk?

Hii thread haiusiani na tukio lolote bali ukweli usiozungumzwa.
Ingawa threads zako huwa ni za kichawa ila leo nakuunga mkono. Uko sahihi katika hili suala la P Funk. Hawa wakongwe wamenyonya sana wasanii ikiwemo kuwadhalilisha. P Funk ni kweli ana tuhuma za kuwapiga wasanii. Shukrani nyingi kwa kijana wa Tandale kwa kuleta mapinduzi makubwa na kuwapa wasanii heshima wanayostahili. Kwenye huu muziki naweza sema Diamond ni kama NABII.
 
Sipendi sana kuingilia mada za machawa siku hizi, ila nimona wewe nikujibu.

Kiuhalisia, huyo P Funk ana afadhali kuliko hao WCB.

PF hamiliki Album za wasanii ila anamiliki BEATS. Na ndio maana hujawahi kusikia Msanii analalamika.

Na kiukweli, wasanii wa zamani walipata pesa mnoooo.

Hakuna Msanii ambaye hakupata pesa. Kuna wasanii mpaka walikuwa wanatembea na pesa kwenye but I za gari.

Tatizo kubwa ukiwa msanii WCB ujue Ni Kama unafanya kazi ambayo Ni COMMISSION BASED.

Inatakiwa ufanye kazi halafu, iqe Shows, ngoma mitandaoni au endorsement kila kinachopatikana unakatwa 60% unapewa 40% kwa mkataba wa miaka 10.

Maana yake, unafonzea kila kitu. Miaka 10 kisanii hutakuwa na jipya tena.

Na baada ya kutoka hutakuwa unamiliki nyimbo yoyote Wala digital platform zako.

Kuna vitu watu huwa wanakubali kwasababu ya shida tu.
Brother weka taarifa zako vizuri...

Wasanii wote unwaona Nature na wengine ambao album zao walirekodi kwa majani kasoro Prof J wote hakuna album hata moja wanapata hata 50 kwa sasa zote ukiingia copyright utaona Bongorecords na mzigo unaenda huko.

Kuhusu WCB kukata 60/40 aisee mbona hapo wamewasaidia wasanii bro...hivi unamchukua mtu hajulikani unamlea unampa kila kitu kisha wewe kukata 60% useme ananyonywa? Wakati pesa ya kurekodi inatoka hapo kwenye 60,mavazi na video,promo zote kwenye 60. Niambie msanii gani ukimtoa Ali kiba,Nandy(ambao walikua na backup kubwa ya clouds) anaweza kushindana na msanii wa WCB kiuchumi? Usiseme Harmonize maana yeye ametoka huko..leo hii ukisikia Harmonize kaweza kulipa 600M na Ray 800M kuvunja mkataba utasema walikua wananyonywa kama ni hivyo pesa yote hiyo wamepata wapi?

NB:WCB wana udhaifu lakini wana unafuu
 
Baada ya kushinda kesi, Hermy B akawaambia beat atakuwa anawauzia milioni 8, wakakasirika mpaka wakagombana nae kabisa😃😃 wao wanataka wawe wanalipa laki 5 mpaka single milioni
Kwahiyo Msela[Harm B ]hakulambaga kitu
 
Mkuu huwezi Jua labda hermy B alilipwa na washikaji.

Au aliuza beat na Kila kitu kuhusu hio beat.

Haya mambo huwa yanatokeaga na wasiojiandaa mapema na mikataba yenye kulinda haki zao huishia kulilia tu.

Wasaniii waache njaa njaa wanunue nyimbo na haki hio nyimbo na Kila kitu

Ila yanapotokea mazali kama haya ya ma movie kutumia nyimbo na beat zao wapige pesa.
Mkuu umeongea point sana! Mara nyingi watu huwa wanafanya vitu kienyeji halafu ikitokea dili ya hela ndio wanastuka kwamba waliuza game. Kingine kilichochangia ni biashara ya muziki kubadilika, zamani publishing haikuwa big deal kutokana na jinsi muziki ulivyokuwa unauzwa. Lakini siku hizi music publishing is a HUGE business hasa baada ya muziki kuanza kuuzwa digitally. Na ndio maana licha watu kumtukana P Funk, jamaa alishtuka mapema akahakikisha haki zake za publishing zimesajiliwa kisheria na sasa hivi anakula matunda ya jasho lake. Hata Master Jay kwenye interview na Salama alimsifu kwamba jamaa kawaonyesha producers wengine jinsi ya kulinda maslahi ya ubunifu wao.
 
Management yake ipo vizuri kwenye kutoa kazi ila kitengo cha kumbrand na kumpa promo marioo naona pamelegea kidogo

Niliona kaenda kupiga show kenya lakini sikuona media tour kwenye vipindi vyenye fan base kubwa kama 10 over 10, wakati kenya kashapenya, ilitakiwa akite mizizi maana naskia hata hela ya show kenya, wabongo hulipwa vizuri kuliko home
YANI anakwama sana kuhusu show jamaa atashuka umaarufu hajapiga show za maana
 
Hakulamba kitu. Ila hata kina Mwana Fa wenyewe ni kama walichukua nusu ya hiyo hela, nusu nyingine aliichukua wakili wao (Msando) kwa kuwa wao walikuwa wameikatia tamaa kesi na yeye ndio akawekeza akiamini kuwa wanatoboa na kweli wakatoboa.
Kwenye hizo 2b angekuwa producer mwenye akili angekuwa na chake na hapa ndio p funk na Master J utawapenda.
 
Brother weka taarifa zako vizuri...

Wasanii wote unwaona Nature na wengine ambao album zao walirekodi kwa majani kasoro Prof J wote hakuna album hata moja wanapata hata 50 kwa sasa zote ukiingia copyright utaona Bongorecords na mzigo unaenda huko.

Kuhusu WCB kukata 60/40 aisee mbona hapo wamewasaidia wasanii bro...hivi unamchukua mtu hajulikani unamlea unampa kila kitu kisha wewe kukata 60% useme ananyonywa? Wakati pesa ya kurekodi inatoka hapo kwenye 60,mavazi na video,promo zote kwenye 60. Niambie msanii gani ukimtoa Ali kiba,Nandy(ambao walikua na backup kubwa ya clouds) anaweza kushindana na msanii wa WCB kiuchumi? Usiseme Harmonize maana yeye ametoka huko..leo hii ukisikia Harmonize kaweza kulipa 600M na Ray 800M kuvunja mkataba utasema walikua wananyonywa kama ni hivyo pesa yote hiyo wamepata wapi?

NB:WCB wana udhaifu lakini wana unafuu
Watu mnachanganya publishing na management. Hicho ulichokitaja hapo ni mkataba wa management, hauhusiani na publishing. Hiyo biashara ya sijui 40/60 au 30/70 huwa inakuwa kwenye management. Mkataba huwa kwamba kwa mapato fulani au yote yatakayoingia wakati wa mkataba huo wa management, msanii atapata 60% na management itapata 40% or vice versa or whatever the agreement says. Hiyo haihusiani na chochote kuhusu hatimiliki (publishing). Hatimiliki ni kitu kingine kabisa.

Unaposema Juma Nature hapati 50% unataka hiyo hela aipate on what basis? Ninachojua mimi Nature sio msanii wa Bongo Records siku nyingi. Meaning hata yeye akifanya shoo na akatumia nyimbo alizorekodi Bongo Records hatakiwi kumlipa P Funk kwa sababu sio msanii wake kwa sasa.
 
Nadhani hujafahamu mfumo waubepari unayofanya kazi.
Huo ndio ubepari Sasa...na hakunyonyi sababu aha roho mbaya ila sababu ndivyo inavyostahili.
Kwa nini hao wasanii walienda kwake na wasingejisikia huru kwenda kwenye label nyingin?
Kwani yeye hivyo vifaa vya studio aliokota,? Ujuzi je alisomea bure??
 
Mtoa mada jitahidi kujua namna haki zinazofungamana na mziki zipo vipi na ni nani na nani wanaotakiwa kufaidika na muziki fulani utakua umemaliza kila kitu.
P Funk yupo sahihi, Sallam ameghafirika
 
Back
Top Bottom