Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

Ukweli usemwe: P Funk ndio mtu mnyonyaji zaidi kuwahi tokea kwenye historia ya Bongofleva

Majani anachofanya ni kama kile P Diddy amekifanya kwa wasanii wake, wanamfanya awe rich forever, ndio biashara ya muziki ipo hivyo duniani, ni ya kinyonyaji.

Kilichotakiwa kufanyika awali ilikuwa ni kugawana asilimia za mapato ya wimbo. Producer apate asilimia 50 na mwimbaji apate asilimia 50 kwa kuwa combination yao ndio imetoa wimbo (muziki). Sasa kinachozungumzwa hapa ni kuwa P Funk anamiliki 100% yaani mpaka maneno yaliyoimbwa kwenye nyimbo yeye ndio anayamiliki, hakuna cha mtunzi wala muimbaji.
Mkuu hili unalosema SIO KWELI ukifuatilia mapato ya mirabaha ambapo pesa zimegawanywa kulingana na umiliki wa % katika wimbo husika, hao wasanii wakongwe pia wamepata. Sio kwamba Majani amejimilikisha 100% bali ni 50% kwa nyimbo ambazo aligharamia na aliingia mikataba na hao wasanii
 
P
Bizman na wengine waliokuwa wanasaidia Majani kwenye production, lini uliwahi wasikia wakilalamika!? Je, wakati kazi zinasajiliwa kwenye mamlaka husika hao waliorodheshwa katika production? Ila usisahau hizo ni kazi za Bongo Records. Kama Kuna makubaliano baina ya P Funk na Producers washiriki hayo yanakuwa ni makubaliano yao binafsi.
Pia dunia nzima hakuna professional studio ambayo ina mtu mmoja tu yaani wimbo ufanywe na kukamilishwa na producer pekee. Hapo kuna music engineer, mastering, composer, mixing and dubbing, nk yaani unakuta wimbo mmoja una mikono ya watu hata sita tofauti lakini anayetajwa kama producer huwa ni HEAD OF THE OFFICE.
Ipo hivyo
 
Hivi mkuu naomba unieleweshe, ina maana ukitoka WCB hata ukiwalipa bado nyimbo zinabaki kuwa za kwao?
Kila kona kuna unyonyaji ila mimi kinachonichekesha ni mashabiki wa WCB kutetea yale wanayofanya wcb wakati hao hao walikuwa wanaponda clouds kwa mambo hayo hayo.

Huwezi kupatana vizuri ukiwa na njaa na hawa wasanii uwa wakiwa hawajatoka wana sign mikataba wakiwa wanawaza kuwa na majina na kumiliki magari, wakishapata hivyo na kugundua pesa wanayotengeneza na wanachoambulia ni mbingu na mafuta, basi hapo ndipo wanachanganyikiwa.

Kuhusu kupata pesa ni kweli walipata sana sema walikuwa wanaishi lifestyle flani la movie na usela mavi
Mkuu hili ninaongea nikiwa na uhakika wa 100% ni kuwa pale WCB ukiachana na Mavoko na Konde boy, nyimbo za wasanii wengine wooote waliobaki zinamilikiwa na WCB hao ndio COPYRIGHT HOLDERS, wasanii wamebakiwa na PERFOMANCE RIGHTS ONLY yaani leo Vanny akitoka pale basi hawezi kupata hata 100 endapo wimbo wake utauzwa, nasema HATAPATA HATA MIA WIMBO WAKE UKIUZWA unless otherwise waingie makubaliano mengine leo hii kuhusu hicho kipengele.
 
P

Pia dunia nzima hakuna professional studio ambayo ina mtu mmoja tu yaani wimbo ufanywe na kukamilishwa na producer pekee. Hapo kuna music engineer, mastering, composer, mixing and dubbing, nk yaani unakuta wimbo mmoja una mikono ya watu hata sita tofauti lakini anayetajwa kama producer huwa ni HEAD OF THE OFFICE.
Ipo hivyo
sema ndo hivyo wasanii wanakuwa hawana kitu mfukoni so lazima producer abakie na uhalali wa kumiliki beat... ila kwa msanii kama DIAMOND now hawezi fanya huo ujinga
 
P

Pia dunia nzima hakuna professional studio ambayo ina mtu mmoja tu yaani wimbo ufanywe na kukamilishwa na producer pekee. Hapo kuna music engineer, mastering, composer, mixing and dubbing, nk yaani unakuta wimbo mmoja una mikono ya watu hata sita tofauti lakini anayetajwa kama producer huwa ni HEAD OF THE OFFICE.
Ipo hivyo
Mwisho wa siku beat inakuwa Mali ya producer
Lyrics msaniii

Ova
 
Wakati hao wasanii wanasaini mkataba hawakuona vigezo na masharti?
Ktk issue ya mikataba lazima uwepo upande utakaoumia na hasa kwa msainishwa kutokana na wenye mikataba hupenda kuangalia na kupima upeo wa anayesaini ukionekana mwepesi unapigwa kitu kizito.

Mf;anachozungumza mdau hapa kilifanyika siyo chini ya miaka 15/20 iliyopita sasa unadhani ktk wasanii wetu wa kipindi kile ni yupi angalao alipata wazo la kusema ngoja nimshirikishe mwanasheria ktk huu mkataba?na hata wakisema watake kuuvunja leo lazima zipo chamber zinazowabana either kutoa kiasi cha pesa kuivunja hiyo mikataba unadhani leo afuatwe Ferooz kwamba toa 100Mill umlipe Majani mkataba uvunjwe hiyo pesa anayo?
 
Noma sana pia nahisi haya mambo hawafanyagii kwa mkataba tu inakuwa kwa maneno.. labda kama mkifanya album ila kama single tu inakuwa kisela kwa mdomo of which mbeleni yanatokea haya
Mkuu maneno yakitamkwa na mkakubaliana tayari ni mkataba
 
Hii kweli kabisa nilishangaa kumuona chege akipita mtaani kuzungusha kapu la dagaa ...nikajisemea hii laana kabisa...
chege kwani nae kafulia kiasi hichi mkuu??? nasiki kundi lao nature tu ndo bado ana maisha...
 
Sipendi sana kuingilia mada za machawa siku hizi, ila nimona wewe nikujibu.

Kiuhalisia, huyo P Funk ana afadhali kuliko hao WCB.

PF hamiliki Album za wasanii ila anamiliki BEATS. Na ndio maana hujawahi kusikia Msanii analalamika.

Na kiukweli, wasanii wa zamani walipata pesa mnoooo.

Hakuna Msanii ambaye hakupata pesa. Kuna wasanii mpaka walikuwa wanatembea na pesa kwenye but I za gari.

Tatizo kubwa ukiwa msanii WCB ujue Ni Kama unafanya kazi ambayo Ni COMMISSION BASED.

Inatakiwa ufanye kazi halafu, iqe Shows, ngoma mitandaoni au endorsement kila kinachopatikana unakatwa 60% unapewa 40% kwa mkataba wa miaka 10.

Maana yake, unafonzea kila kitu. Miaka 10 kisanii hutakuwa na jipya tena.

Na baada ya kutoka hutakuwa unamiliki nyimbo yoyote Wala digital platform zako.

Kuna vitu watu huwa wanakubali kwasababu ya shida tu.
Huoni kama hiyo 40percent ni kubwa sana maana hujawekeza hata mia zaidi ya sauti yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sema ndo hivyo wasanii wanakuwa hawana kitu mfukoni so lazima producer abakie na uhalali wa kumiliki beat... ila kwa msanii kama DIAMOND now hawezi fanya huo ujinga
Zama tulizopo dunia imefunguka sana,leo hii msanii hata asiyejua ABC za mikataba akishika simu yake akiingia mtandaoni anakutana na habari za wasanii wa nchi nyengine wanaokula shavu kwa kusimamia vizuri kazi zao wenyewe so wanapata idea hawa huwezi kuwaingiza mikataba ya kijinga.

Wakati wa kina Gwair sijui Nature hao kina Ferooz hakukuwa na nyenzo za kuwapa taarifa na elimu nyeti kama sasa leo unakuta msanii ana baba ana elimu kichwani,mjomba sijui mume wa dada wote wanakuwa washauri wake karatasi zinakaa kisheria ila kipindi hiko mikataba wanasaini bar tena usiku wamelewa huku mapajani wamekaliwa na kina Kajala na Sinta na mwenzao Masogange unadhani kuna kitu hapo?sidhani hata kama walikuwa wanasoma wanachokisaini.
 
Zama tulizopo dunia imefunguka sana,leo hii msanii hata asiyejua ABC za mikataba akishika simu yake akiingia mtandaoni anakutana na habari za wasanii wa nchi nyengine wanaokula shavu kwa kusimamia vizuri kazi zao wenyewe so wanapata idea hawa huwezi kuwaingiza mikataba ya kijinga.

Wakati wa kina Gwair sijui Nature hao kina Ferooz hakukuwa na nyenzo za kuwapa taarifa na elimu nyeti kama sasa leo unakuta msanii ana baba ana elimu kichwani,mjomba sijui mume wa dada wote wanakuwa washauri wake ila kipindi hiko mikataba wanasaini bar tena usiku mapajani wamekaliwa na kina Kajala na Sinta unadhani kuna kitu hapo?
Ndio uko sahihi ila unaweza ujue haki zako lakini bado huna wa kukutoa sababu mziki wa Sasa una mambo mengi mpk mtu atoke Kuna branding za kufa mtu ambazo zinahitaji watu wazoefu kwenye field husika.
Ukiwafuata ndio hivyo wanaweka masharti ya kibepari kama hutaki komaa mwenyewe.
 
Huoni kama hiyo 40percent ni kubwa sana maana hujawekeza hata mia zaidi ya sauti yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijaujua hasa msingi wa mabishano yenu but according to quote uliyom-quote mdau hapo juu bado yeye ana hoja.

Assume wewe leo umekuwa msanii chini ya label tajwa hapo juu,leo 2022 ukashikishwa pen na karatasi kwamba kila utakachofanya ukiwa chini ya mkataba tajwa utalipwa let's say 1mill ukija kuachiliwa mateka wewe baada ya huo muda kwanza hiyo million uliyokuwa unapewa 2022 ni sawa na 200K tu na utakutana na damu changa mtaani zinawika mbaya kabisa na zina management nzuri zaidi yako huku baadhi ya haki zako wakibaki nazo waliokuachia mwanzo.

Nadhani ndo hasa msingi wa hii thread kwamba producer au manager akiingia mkataba na msanii ktk kazi zake huyu msanii nae aendelee kupata matunda ya kazi zake hata baada ya yeye kuwa ameshuka kimuziki na ni matokeo tarajiwa ktk fani yoyote.
 
Mtoa Mada,

Hayo ni masuala ya mkataba. Hao wasanii walikuwa wanajua masharti ya P Funk yakoje na walikubali kufanya naye kazi.

Sasa wewe mtaji wako ni sauti tu unataka ule sawa na mtu aliyeenda jiji la New York (jiji la gharama sana kuishi) kusomea Uhandisi wa Sauti na kununua mitambo na kutengeneza urafiki na ma-DJ wampigie nyimbo za studio yake.
 
Back
Top Bottom