SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Ugali nikiula hasa dona nausikia kabisa kwa bwana "Abdallah Kichwa wazi" anakuwa kapata stamina 😂😂😂
 
Mimi nilishakataa Biashara ya Wanangu Kulewa, Mihogo na Ugali nilishamuambia Wife siku ukipika ivo vyakula Watoto watengenezee Msosi wao mwingine, Ila mimi sasa siwezi maliza siku tatu sijala ugali nauelewa sana
 
Weka ushahidi wa kisayansi kuhusu kudumaza akili
 
Hapa mtoa mada kaongea kiushabik ila sio kisayansi.
UGALI hapa namaanisha dona na sio sembe dona ilioandaliwa vizuri ina faida mwilini kama ifuatayo.
1. Dona kwa asilimia kubwa ina wanga ambayo huupa mwili nguvu
2. Dona ina kiini tete ile ya njano ambayo inatoa mafuta na protini kwa mbali sana ambayo inasaidia mwili kupata joto na hapa ndio mwili inapopata joto hata kwenye 6 kwa 6 lazima uwe vizuri
3. Dona ina ganda la juu (pumba) ambayo husaidia katika mmeng'enyo wa chakula.
Ukiangalia hapo kwa haraka haraka unaona ukila ugali unapata virutubisho karibia vitatu.

Kitu ambacho hakipo kwenye wali au vyakula vya ngano kwani vyote hivi vina wanga tu.
Hoja ya udumavu wa akili naipinga kama ifuatavyo. Sisi wapogoro na wandamba chakula chetu kikuu ni ubwabwa tunaamini ugali ni uji ukila unakojoa saana yaani sisi asbhi tunaamka na ubwabwa mchana ubwabwa na usik lakini ndio akili yetu ikiwaza zaidi ni kwenda kwenye kigodoro.
Sasa wewe mleta mada tuletee rejea ya watu wanaokula ugali kuwa na udumavu wa akili na wale ambao hawali ugali kuwa vipanga

Ila kati ya vitu nnavyoweza kukubali ni kuwa wanaokula ndizi na viazi mviringo na samaki kwa wingi atleast wanakaukomavu wa akili kuliko wengi
 
Vyakula vya kurutubisha ubongo ni.

1.Ndizi
2.Samaki wa maji baridi.
3.Maziwa
4.Nyama

Kama huamini hilo chunguza jamii zote ambazo watu wao hutumia vyakula hivi kwa wingi kisha utakuja na majibu. Utagundua makabila ya Kilimanjaro
(Wachaga,Wapare,Wameru,Wamasai) hawa wengi wako smart sana upstairs. Hawa intake ya maziwa na nyama ni kubwa sana ila wana ndizi na samaki.

Kanda ya ziwa pia (Wasukuma, Wahaya, Wakerewe) humu nako vipanga ni wengi. Hawa intake ya samaki na ndizi ni kubwa sana ila pia wana nyama na maziwa.

Nyanda za juu (Wanyakyusa)
Hawa intake ya ndizi ni kubwa pamoja na nyama na mchanganyiko wa vyakula vingi asilia ndio maana wengi wana miili mikubwa na brain zipo vizuri.

NB: Nimesema samaki wa maji baridi sababu hata Tanga kuna samaki na Zanzibar ila maajabu hakuna 😂
 
Zanzibar na Pemba hawali ugali je wanatoa vichwa/Vipanga?
Ni akili iliyotumika, ni lazima Rais au makamu wa Rais atokee kisiwani, Ardhi yao haturusiwi kumiliki ila wao wanaweza kumiliki mashamba makubwa uoande wetu, Wana sifa za kupata vyeo / kazi sehemu mbili, n.k.
 
Sera ya jela ni kuwa hawawezi kukupa chochote ambacho kitakufanya wewe ujisikie raha.

Sasa ugali kama ni chakula, umefikaje kule?
 
Ulaya ndio maana unakuta mashamba ya mahindi makubwa na wanalishia mifugo tu
 
Naomba nitajie vyuo vitano ulaya na vitano america ambavyo waafrika wanakimbiza
Ninao ushahidi ila kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu sitoweza kuziweka hapa....ila ukae ukijua kitaaluma we africans tupo vizuri mno kuliko race nyingi tu!
 
Hizo kauli zako zenye kuudharau ugali,ungezisema ukiwa hadharani huku kwetu Zambia ungepigwa na raia kama wanavyompiga mwizi wa simu,ugali huku ni chakula cha heshima sana.
 
Weka ushahidi wa kisayansi kuhusu kudumaza akili
Soma Pia:

SI KWELI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akil


Je, JamiiCheck ni wababaishaji?

This myth has been debunked, verified not to be true kwamba Ugali unadumaza akili

Leo imekuwaje wameachia nyuzi hii ambayo wao wenyewe wamjiridhia kwamba sio Kweli?

Kulikoni huko JamiiCheck JamiiForums ?

Ilipaswa Moderators wauzuie huu uzi.

Huu Uzi Unahatarisha Usalama wa Afya za Watanzania, Huu uzi unalenga kuwadhihaki Watanzania.

Maxence Melo Hawa magaidi ya mitandaoni yadhibitiwe. Unaona hii Imekaaje Mkuu?
 
Reactions: EEX
Siupendi ugali kwa nguvu zangu zote.

Hauna ladha yoyote ile.

Na uzuri wa kujitegemea ni kwamba unafanya mambo mengi vile unavyotaka wewe.

Kwangu sipiki ugali. Nakula ninachotaka mimi kwa pesa zangu mwenyewe.
 
Kumekuwepo na madai kuwa ulaji wa ugali hudumaza akili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?

👇🏿

@JamiiCheck
Hivyo, @JamiiForums imebaini kuwa madai haya hayana ukweli uliojengwa kwa hoja za kisayansi. Ni uzushi usio na uthibitisho wa tafiti au takwimu.

Watanzania, muwaogopeni hawa wakina Uncle bright na magaidi wengine wa mtandaoni, they're bigoted racists twats.

While "it is your right to have your own Opinion, You have no rights to your own facts"

Mjitathmini.

cc Wizara ya Afya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…