Uliambiwa nini ukiwa Mtoto lakini baada ya kukua ukagundua ni Uongo?

Uliambiwa nini ukiwa Mtoto lakini baada ya kukua ukagundua ni Uongo?

[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] nimejikuta nacheka mwenyewe maana hii mbinu naitumia kila wkt kumtoroka mwanangu
Enzi za kuzungusha antena ndio ilikuwa mbinu yangu kuu ya kumtoroka binti yangu mpendwa, Mungu ni mwema yuko darasa la tatu sasa.
 
niliambiwa na jirani ukimaliza kukojoa tema mate usipotema mama yako anavimba matiti... Mapaka Leo hii Nina miaka 20+ natema mate
 
Nilikuwa mkorofi flani na sili mpaka iwepo soda,

Siku.hiyo sijui ilikuwa haipo au waliamua tu kunikomesha maana niliekewa chakula bila soda ..kuona vile nikakataa kula mama akatoka sebleni na kwenda ndani...aliporudi kaja na chupa ya coca cola nikachukua na kuendelea kula lkn kila nilivyokuwa nakunywa nilikuwa nahisi kama haiko vile nilivyoizoea ila nikakomaa nayo mpaka mwisho.

Miaka zaidi ya 20 baadae ndipo marehemu mama yangu akaniambia kuwa ile haikuwa soda ila aliweka chai ya rangi kwenye chupa ya coca cola mradi tu nile!

Ndio hapo nikajua kuwa hakuna anaweza kunipenda zaidi ya mama aliyenizaa!

Sitasahau...nilimtizama kama ni mpya kwangu siku ile!
 
Eti ukinywa maji ya mchele au kukojea juu ya kichuguu ni dawa ya kuacha kukojoa kitandani,
 
Mvua ikiwa inanyesha na jua linawaka basi fisi anazaa.

Ukikosea, kunja kidole cha mwisho then mzazi atasahau.

Ukila ukavimbiwa unaambiwa uzunguke ghala mara 10 huku ukilipuliza ili chakula kirudi ghalani na kuvimbiwa kunaisha.
 
Nilidanganya mjini kuna gari kubwaaaaaaaa ndefu kutoka mwanza mpaka daisalamu (train)
 
Nakumbuka enzi hizo tunaenda kutafuta kuni mstuni kulikuwa na matunda pori matamu kweli ,ila unaambiwa ukiyala ndani ya msitu simba lazima wakufanye chakula "unaliwa na simba " so ilikuwa lazima mtafute kuni kwanza alafu mnakula mkimaliza nje ya forest . .....

Kumbe nadharia ilikuwa simple [emoji23][emoji23] kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kushindwa kufanya kilichowapeleka msituni mkaishia kula hayo matunda ....
8dcaed8876163a1ec557dd89473871c2.jpg

f8f0eaddeb85166c05cafabd00223fbe.jpg
 
Mama alikuwa akimpata mdogo wangu alikuwa ananidanganya kuwa ameenda kumnunua sokoni!.....Hadi nafika la saba nilikuwa nafikiri kuwa watoto huwa wananunuliwa sokoni!!
Hahahahahahaaaa.

Ingekuwa raha sana kuchagua wenye[emoji196] [emoji196] [emoji196] [emoji196]
 
Nilidanganywa vingi...
Nilikuwa napenda sana kulia lia hovyo pengine kitu kidogo nalia,niliambiwa nkilia usiku ni kuita wachawi na wataondoka na sauti yangu nitakuwa bubu. Nikaacha habari za kujiliza Liza na madeko.

Kingine kula muhindi unaambiwa njoo nikuwekee njia ya kwenda kwenu (wanatamka origin yako huko kwenu)
Nilikuwa naambiwa nikutengenezee njia inayoenda kwa bibi yangu ili nije nipite wakati wa kwenda kumsalimia, hapo nafurahi kweli kweli huku muhindi analiwa tu
 
Mama alikuwa akimpata mdogo wangu alikuwa ananidanganya kuwa ameenda kumnunua sokoni!.....Hadi nafika la saba nilikuwa nafikiri kuwa watoto huwa wananunuliwa sokoni!!
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Mama alinambia hivi "nilikununua hospital, niliona watt weeengi ila nilipofika kwako tuu,ukanichekeaaa nami nikafurahi na kukuchekea pia,nikakuchua ukawa mwanagu mzuuuri hadi Leo"... Looh niliamini eti nimenunuliwa hospital mpaka nipokuja kujua hahahhaha so funny

Ukimchungulia MTU mzima unapofuka macho[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] n.k
Nadhani hii 900 ilimpendeza mama hadi kakununua
 
Back
Top Bottom