Ulichoma mtaji mara ngapi mpaka kuja kutoboa kibiashara?

Ulichoma mtaji mara ngapi mpaka kuja kutoboa kibiashara?

Andika business plan , alafu kopa.
Sema hakikisha unasimamia Hesabu wewe, ukiwaachia wafanyakazi utaliwa shoti, wale wasiguse pesa ndo maana wafanyakazi wengi wa serikalini biashara zinawashinda.
Mkuu unagonga kwenye mshono.. mi mwenyewe ni mfanyakazi ila napambana huko nje sema ndio nachezea za uso. Saa nyingine nadhani hata kale ka uhakika kwamba mshahara upo siwezi kufa njaa pengine kananifanya nisiwe serious saana kama inavyotakiwa..?
 
Mtu akikuona leo hii unavyokula bata, maisha mazuri, usafiri mkali na biashara kubwa mjini, anaweza kudhani umefika hapo ulipo kirahisi rahisi tuu. Mimi mwenyewe nilikua nadhani hivyo!

Cha ajabu ni kwamba kila ninapojaribu kutia mguu kwenye biashara nachezea za uso mbaya kabisa najikuta natoka kapa. Mpaka muda huu nimeshajaribu zaidi ya aina 5 tofauti za biashara kuanzia bar, stationary, usafirishaji, kilimo, ufugaji nk na zote hakuna hata moja iliyofanikiwa walau hata kurudisha mtaji!

Nimebaki najiuliza nyie wenzetu mliofanikiwa kutoboa kibiashara je na nyie mwanzo mlichoma mitaji kama sisi? Hebu tupeni akili na sisi tutoboe.

NB: Usije na hoja za "fanya kazi kwa bidii".
Kuna shortcuts huko na kamwe huwezi ambiwa ila kwa mtu anayekuamini sana.
 
Mtu akikuona leo hii unavyokula bata, maisha mazuri, usafiri mkali na biashara kubwa mjini, anaweza kudhani umefika hapo ulipo kirahisi rahisi tuu. Mimi mwenyewe nilikua nadhani hivyo!

Cha ajabu ni kwamba kila ninapojaribu kutia mguu kwenye biashara nachezea za uso mbaya kabisa najikuta natoka kapa. Mpaka muda huu nimeshajaribu zaidi ya aina 5 tofauti za biashara kuanzia bar, stationary, usafirishaji, kilimo, ufugaji nk na zote hakuna hata moja iliyofanikiwa walau hata kurudisha mtaji!

Nimebaki najiuliza nyie wenzetu mliofanikiwa kutoboa kibiashara je na nyie mwanzo mlichoma mitaji kama sisi? Hebu tupeni akili na sisi tutoboe.

NB: Usije na hoja za "fanya kazi kwa bidii".
Mara nyingi sana
 
Mimi ninachoona siyo Kila biashara inanafaa
+Nashauri biashara yako ya kwanza iendane na profession yako(una ujuzi mwingi zaidi hapa) mfano mfamasia afungue famasi etc
+Kingine it takes time aisee......inaonekana Tanzania kuchomoka ni wastani wa miaka mi tatu hivi
+Ukiweza kwepa Kodi kwepa sana ......hizi Kodi sijui malipo ya nn yanakula gharama sana
+Biashara yako iwe chini ya kampuni ...ni rahisi zaidi kudeal na kampuni kuliko jamaa wa mtaani tu.hata serikali inafanya kazi na makampuni
+Hakikisha biashara yako haiweke rehani mtaji wako(Kwa mfano kwenye kukopesha etc)
+Chagua biashara ambayo mteja analipa kwanza ndipo anapata huduma na siyo anapata huduma halafu malipo baadaye



Nawaza hivo tu....
 
Mkuu unagonga kwenye mshono.. mi mwenyewe ni mfanyakazi ila napambana huko nje sema ndio nachezea za uso. Saa nyingine nadhani hata kale ka uhakika kwamba mshahara upo siwezi kufa njaa pengine kananifanya nisiwe serious saana kama inavyotakiwa..?
Yes .
Na kwasababu hiyo kuna uwezekano Kanisa unaowaajiri wanakuibia ndo maana unaona hasara kwasababu husimamii, huna mke? Kama unaye, mfanye kama msimamizi wa mahesabu, awe anazishika yeye, utakuwa umewin . Mbinu hii wanatumia wahindi.
 
Akijaza mzigo akaanza kupata wateja mauzo kwenye droo yanasoma tayari anajibadilisha jina Papaa, Tajiri, Mutu ya watu, Don na mengine ya ujiko mengi.
Anaacha kuongeza mzigo na kutafuta mrija wa pesa zaidi anarukia skirt [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Na sisi Wanamake wa kukuonyesha pesa zinavyotumiwa tunawasubiri na mawig yetu km Joti full kuwindana

Aisee umesema ukweli mtupu.
 
Nilichoma 78 million na madeni juu zaidi ya millioni 30 dadeq mpaka Leo najikongoja biashara sio pow inabidi uwe na moyo wa ziada laa sivyo unaweza kujinyonga[emoji23]
Aisee kwakweli inataka moyo wa chuma kukabiliana na hiyo hali.
 
Acha kabisa mkuu. Nimechoma milioni 80 kwenye dhahabu. Imeniacha mbendembende. Daah...! Bahati mbaya napoteza hela na umri ndio umeenda 40+.

Nimegundua ndio maana wakinga wakishika biashara moja ya duka ni hiyo hiyo hawabadiriki.

Hivi najitafuta kwa upya. Duka nililipukutisha kuingiza kwenye dhahabu. Hivi ndio napambania kulirudishia. Bidhaa sina japo biashara ipo. Hapa ili nirudi sawa natakiwa angalau milioni 40 kwa uchache 20 mpya niitupie humo.

Ila unajua nini? Lazima niyarudie madini yanipe hela.
Achana na madini utachakaa


Hiyo milion 80 yako kama unachimba lazima uwe kichaa !


Na ubaya wa madini yanakupa bonge la hopes ila ndio unakuwa unapotea hivyo.


Kama una chimba acha huo upuuzi komaa na duka

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Kuna bro wangu mmoja nae aliwekeza kwenye bar nadhani alichoma kama 25- 30m au zaidi pale manake ali decorate sana. Siku nimekutana nae namuuliza vip bar inaendeleaje? Jamaa hakua hata na hamu ya kuliongelea hilo suala akaniambia dogo we acha tuu..!
Nilichoma 78 million na madeni juu zaidi ya millioni 30 dadeq mpaka Leo najikongoja biashara sio pow inabidi uwe na moyo wa ziada laa sivyo unaweza kujinyonga[emoji23
 
Back
Top Bottom