Mchimba Chumvi
JF-Expert Member
- May 19, 2016
- 2,244
- 5,500
Ilikua inaniuma maza na bibi wanavyoumia.Bwana bwana usiombee kupitia hii hali. (wouldnt wish it even for my worst enemy) jobless corner isikie tuu kwa wenzio maana ikupate mbona utajua maisha yakoje. Tena ombea ikukute wakati huna mchuchu, kama una mchuchu aisee nakwambia ndio utakapo tambua kuwa woman = devil reincarnated.
Mie nilibwagwa na kuambiwa sina mbele wala nyuma kama mche wa sabuni. Mzazi anakusikitikia tena wa mama ndio kabisa unamuona tuu anauzunika, acha kabisa maumivu yake ni balaaa.
All in all mwanawane wewe pambana tuu ndio mapito ya maisha always bliv good is going to happen na muhimu sana angalia sana wale watakao kuwa nae katika wakati huu maana siku neema ikishuka hao ndio wakula nao.
Mungu mwema, yalipita na yaliisha, yamebaki kuwa historia tu kwa sasa.dah tunapita mengi sana pole mkuu
Hawatopata hata hiyo, ufisadi uliopo hapa nchini ni hatariSerikali ya CCM ianze kulipa wasomi wasio na kazi angalau mlo wa siku
itakua mtoto wa kishua wewe sio kwa ubaya lakin , vipato vya tiamaji tiamaji hua mshahara haukutani na mwezi mwingine ukilipwa mshahara leo rumba linaanza next week una survive week mbili nyingine ukisubir mshahara kinachokuokoa ni hicho kibarua unakua unakopesheka kitaa na ndio utumwa unapoanzia ukishika tu fungu linaishia kwa wadeni ili ukope tenaMimi Nina swali,sio kwa ubaya.. huwa inatokana na Nini mtu anafanya kazi miaka mitano,but akipigwa chini miezi miwili tu analia njaa,
Hata akiba ya Kuanza biashara ndogo Huwa hakuna??hata Hela ya kula miezi sita wakati unajitafuta hakuna??
Changamoto inakuga Nini??
Kweli ndugu hapo nimeelewa..so means hata ukilipwa million kumi,nayo itakua ngumu kutunzaMshahara wa 300k 400k hata ukilipwa kwa miaka 10 ukija kusimamishwa mwaka tuu ni vilio na kusaga meno
Hii ni kwasabb mshahara huo ni ngumu mtu kuweka akiba hasa kama ana watu wanao mtegemea
Natokea maisha magumu mkuu,ukitokea Uzi wa kushindana shida nitag nichangie,, sijawahi kuajiriwa ndio maana nimeuliza..itakua mtoto wa kishua wewe sio kwa ubaya lakin , vipato vya tiamaji tiamaji hua mshahara haukutani na mwezi mwingine ukilipwa mshahara leo rumba linaanza next week una survive week mbili nyingine ukisubir mshahara kinachokuokoa ni hicho kibarua unakua unakopesheka kitaa na ndio utumwa unapoanzia ukishika tu fungu linaishia kwa wadeni ili ukope tena
10mil hapo sasa una kuwa umeshaingia uchumi wa daraja la kati chini πKweli ndugu hapo nimeelewa..so means hata ukilipwa million kumi,nayo itakua ngumu kutunza
Natokea maisha magumu mkuu,ukitokea Uzi wa kushindana shida nitag nichangie,, sijawahi kuajiriwa ndio maana nimeuliza..
Hah sikumaliza kuandika Nika press enter,nilitaka Kusema anaelipwa milion kumi,nyumba anapanga suburban neighborhood,watoto shule za gharama,gari Cc2000,nae kwake milion kumi sio kitu10mil hapo sasa una kuwa umeshaingia uchumi wa daraja la kati chini π
Wenye mishahara hiyo ndio unasikia kafanya kazi 8yrs baada ya hapo ana kwambia kaacha kazi inamchosha ana taka sasa afanye mambo yake
Muajiriwa anaye pokea 10mil kwa mwezi huyu unakuta analipiwa nyumba mafuta ya gari etcHah sikumaliza kuandika Nika press enter,nilitaka Kusema anaelipwa milion kumi,nyumba anapanga suburban neighborhood,watoto shule za gharama,gari Cc2000,nae kwake milion kumi sio kitu
Maisha haya, mwenye mshaara mkubwa ndio analipiwa nyumba na gari,mwalimu analipwa laki 6 Kila kitu analipia,anakatwa Kodi,watunga sera mshaara mlima hakatwi hata Senti,.Muajiriwa anaye pokea 10mil kwa mwezi huyu unakuta analipiwa nyumba mafuta ya gari etc
Kibongobongo kwenye mshahara wake ana uwezo wa kuweka akiba kiasi cha kutosha tu kwa mwezi
Uza simu hio unayoingia mayo jamii forum alafu nunua unga na michele weka ndani na gas jaza kabisa utakuja kunishukuru badae alafu ingia mtaani au njoo hulu town pita kila ofisi omba kaz kila siku ndani ya wiki utakua ushapataUsiombe biashara ife au kazi iote mbawa, naishi maisha ya kuungaunga mwezi wa pili sasa baada ya kibarua kuota nyasi, poleni sana kwa mliowai kuishi maisha haya, maisha ya kula mlo mmoja na kutojua kesho yako, maisha ya kula leo saa saba mchana mpaka kesho saa saba mchana, hatari ogopa.
Jamaa unakonda ubaki kichwa tu, nimejiapiza hata home likitokea tatizo siwezi kwenda kwa muonekano huu.
Kama umewahi kupita nyakati kama hizi share hapa na wadau siku yako ilivyokua inapita kwa kuungaunga.
Hilo ni funzo ulipewa,usiache kazi kirahisi.Mungu ni mwema! Amini tu ipo siku atakufungulia milango!
Nakumbuka 2020 niliacha kazi mahali baada ya kuona kuna boya mmoja ananipelekea umbea kwa boss!
Nikapiga chini ile kazi nikiamini haitachkua mda ntapata nyingine, mzee hapo ndo nilikoma, nilikaa mwaka na nusu sina mbele wala nyuma, nikipiga mizinga marafiki wote nliokuwa nao, bado ndugu, hapo nna mke na mtoto wa mwaka mmoja,
Ilifika mahali mtoto akabaki kichwa na tumbo kubwaa, anakula ugali hata usio na mboga....tulikula dagaa mpaka tukanukia dagaa, inafika muda hakuna chakula ndani kabisa na huna hata sent na na na huna wa kumpiga kizinga tena.....hii hali sitakaa niisahau!
Ila Mungu alikuja kunikumbuka, angalau nikapata mahali angalau hata milo 3 inapatikana sasahivi, ila ile hali imenifunza, kila nikikumbuka najikuta naweka hakiba! Sasa hivi nimekusanya imefika mil 10 nataka nifungue biashara ya kuniboost maana hiz ajira hazitabirika asee!
Kama angeuza mwanzo, huu ushauri ungeutoa wapi? Anahitaji ushauri zaidi ya huu kwahiyo simu ni muhimu abaki nayoUza simu hio unayoingia mayo jamii forum alafu nunua unga na michele weka ndani na gas jaza kabisa utakuja kunishukuru badae alafu ingia mtaani au njoo hulu town pita kila ofisi omba kaz kila siku ndani ya wiki utakua ushapata
Pole sanaHatari sana hii hali. Nilichapika huku familia zinanitegemea. Ndugu michango watoto ada yani kama gwaride ukiambiwa nyuma geuka ni geuka mbele tembea ni tembea hakujulikani mbele wapi nyuma wapi...
Mzee wangu alinipiga tafu sana kipindi hiko plus mama watoto na bro. Sadly mzee akafariki mwezi kabla sijapata kazi.... Achana na hii hali. Yani ni kizungumkuti balaaa....
Ila piga moyo konde utatoboa tu tobo la aina yeyote.
AiseeBack in days
Hapo nimerudi chuo kwenda kufanya Supplimentary, nilikuwa na kama 500k mfukoni. Nimefika nikapambana nikapata pakulala,, doh , shetani la kamari likanipitia maana nilikuwa Mraibu wa kubet miaka hiyo,, nikaplace bet ya 100k,, inplay, ikaliwa.
Hasira ya kukimbiza hasara nikaweka 250k ikaliwa tena,
Hasira zikapanda huku najipa moyo ntairudisha labda , nikafanikiwa kula jumla nikawa na 130k kwenye Account ya bet.,, Shetani likanimbia weka yote upate zaidi, bwana bwana nikaweka Holaa,, nikaliwaa.
Hasira zikazidi kuwa kali Zaidi nikamalizia kudeposite tena 136k, nikala ikafika 200k, nikaanza kupata amani kwa mbali. Oooh mchezo ule usivyokuwa na baraka na ulivyolaaniwa ikaliwa yoote. Bare in your mind hapo mfukoni imebaki kama 14,000/= na Sup ratiba imekaa vibaya natakiwa nisubir mpk wiki ya tatu.
Nilianza kushindia muhogo mmoja kwa siku, na hapo ndio niliona picha halisi ya njaa, nikagundua pia ukiwa na Njaa haulali.
Wiki ya mwisho nilikaa siku 2 nakumbuka bila kula nakunywa maji na karanga tu.
Nauli ya kurudi nyumbani nilikuwa sina ikabid nikawaombe wale matrafic wa Pale Nane nane Dodoma waniombee lift alooh.
VIJANA KAMARI NI UMASIKINI.
We umemsaidia?Na hapa utatiwa moyo tuu hutapata msaada wa maana... Wanadamu ndivyo walivyo...