Ulijifunza kuendesha gari ukiwa na umri gani?

Ulijifunza kuendesha gari ukiwa na umri gani?

Nikiwa na 24 nilikuwa naendesha, lakini mwanangu ana miaka 12 yuko kidato cha kwanza anaendesha vizuri tu anatupeleka kanisani na kurudi pia shuleni kwa wadogo zake, ila umri wa leseni bado hivyo mjini haendi
Hongera sana kwa kumfundisha kijana. Kuna watoto nawaona wana miaka 14 lakini tayari ni madreva wazuri.
 
Acha dharau na lori lenu nalidondosha maksudi 😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
😂😂😂😂😂
Ngoja nimalize kunywa chai ya maziwq nzito (ambayo umeanza kunywa juzi juzi) alafu nimuoneshe Dad comment yako.

😂😂😂
 
Kuna dogo nilikua namfundisha kuendesha gari mtaani mbona nilikoma.

Kuna sehemu tulipita mtaani kwao, njia haikua nzuri kwa mtu anaejifunza, hivyo nikamwambia twende tukazungukie mbele.

Kumbe pale kwenye njia mbovu kuna masela wake na yeye anataka awaonyeshe anajua gari, si akakunja kona ghafra palepale.(mmmk)

Sasa namuuliza unafanya nini na mie ticha nimekukataza usipite hapa tayari akaingia panic mode, akakanyaga wese mpaka kibati, gari yenyewe cresta gx 110 mpyaaa, alooooooo!!! Ni kama ilipaa mzee kuja kustuka tupo sebuleni kwa mtu.

Pua yooote ya gari ipo sebuleni, tumekuta jamaa anaangalia TV.

Sema katika moja na mbili jamaa alikua muelewa akasema nimjengee tu pale nilipovunja, nikaita mafundi tukalimaliza kiume, vijumba vyenyewe vile vya kota vimechakaa.
Duh pole mkuu Mnyenz ntakuja na mimi unifundishe
 
Hii kisheria imeakaaje mkuu? Hatuombei mabaya ila kwa nia njema je akipata ajali akiwa anaendesha utaziambiaje Mamlaka?

Mi dogo simruhusu kabisa kuendesha japo anang'ang'ania na ana miaka 13 yupo form 2 sasa.
Kisheria ni kosa ila tu tunajitoa ufahamu
 
Back
Top Bottom