Ulikuta kitu gani kwa Watu ukajua "hapa pesa ipo"?

Ulikuta kitu gani kwa Watu ukajua "hapa pesa ipo"?

Dah kuna huyo mwanetu enzi tunasoma sekondari 2006 mwamba alikuwa mtu wa mbeya somebody Mwangoka nadhani, alifiwa na mzee wake ilikuwa ajali ya gari au alianguka na pikipiki akakanyagwa pande za Mwenge mataa.

Kituko ni ule msiba picha linaanza tunafika msibani wameweka mziki full buster zinapigwa zile kwaya za Mbeya.

Msiba haukusafirishwa kama wiki hivi anangojewa kaka wa marehemu kutoka Russia.

Wafiwa wote full matisheti ya picha za marehemu.

Mie na masela wangu tulikuwa tunatoka shule tunaenda kumfariji mwanetu msibani, msosi ni mwendo wa kujipakulia minyama kwenye bufee.

Yaani nyuso za wafiwa hakuna hata mwenye huzuni.

Upande wa kina baba ni watu smatsmat tu wamekaa kwa mafungu wanakunywa na kula taratibu taratibu.

Pale kulikuwa na hela sio mchezo..
Yote hayo lakini marehemu hakufufuka. Mimi ni Christian ila napenda waislam hawana tabia ya kuchosha marehemu.
 
Bakheresa mwenyewe tu utajiri wake tunaambiwa haufiki hata $2b.... Halafu leo hii eti awe anatenga $200k Kila mwezi anawapa watoto wake waende wakaitupe?, huo uwendowazimu hata watoto wake wenyewe tu hawawezi kuukubalia.

Hapo kwenye bold ndio familia nyingi za kitajiri zinafanya hivyo huwa wanaandaa budget ya maana kwa ajili ya kula Bata mahala popote duniani inapofika holiday season.

Afterall Hawa wanaoongelewa hapa ni upper middle class tu, yaani ni watu wenye hela za kuwakidhi mahitaji yao na familia zao tu basi labda na kufanya anasa za hapa na pale.

Mfano Sasa hivi nikiuliza kati ya hao matajiri(kwa mujibu wa hizi story hapa) walioongelewa hapa kwenye huu Uzi ni wangapi ambao angalau wamejenga hata barabara za mitaa yao kwa kiwango Cha Rami na wakaweka street lights, utakuta hakuna hata mmoja..

Au ni wangapi ambao angalau wamejenga hata vyuo vya ufundi kwenye mikoa yao waliotoka hili kuleta impact kwenye sector ya elimu kama alivyofanya bwana Patrice Motsepe huko kwao south Africa? obvious jibu ni hakuna.

Dar Kuna shida kubwa sana ya maji, najua watu wengi sana wanachimba visima...je, Kuna tajiri hata mmoja ambaye kwa gharama zake mwenyewe amevuta maji Moja kwa Moja kutoka mto ruvu ambapo maji hayo yananufaisha mamia ya watu..? Jibu ni hakuna

Hivi ndivyo vitu ambavyo matajiri wa kweli wanafanya na sio Hawa upper middle class citizens wanaoongelewa hapa.
Hili nalo neno kwako Extrovert
 
Fatuma ni nn?
Miaka ya 60's mpaka early 2000 kilikuaga na wizi /uvamizi kuvunja mlango na ndio kisa Cha watu kuanza kuweka milango ya ma grill

Iko ivi wezi watakuja na jiwe kubwaa ambalo liliitwa FATUMA....Wezi watakua na mbeleko na wanaweza kuhesabu mpaka tatu na kulirusha jiwe uelekeo ulipo mlango then mlango utavunjika ndipo watapata nafasi ya kuingia ndani na kuwaibia Mali mbali mbali..

Wengine watakuja kuongezea zaidi..
 
Tumekula usiku Vyakula mboga sio 7 ile ni Mboga 20 bufeee la kwenye maharusi nikalikuta pale. NIKAHISI kwasababu sisi wageni tunakaribishwa.

Day 2 same applies

Day 3 same applies

Day 4 asubuhi nikawa na hamu sana na Kunywa chai na kiporo, Nikamuomba dada kiporo..

Akaninyima akaniambia ntaumwa TUMBO kimeenda kumwagwa...

Nikaona enheee hapa Nimefika, Likizo irefushwe.
Hahaha
 
Miaka ya 60's mpaka early 2000 kilikuaga na wizi /uvamizi kuvunja mlango na ndio kisa Cha watu kuanza kuweka milango ya ma grill

Iko ivi wezi watakuja na jiwe kubwaa ambalo liliitwa FATUMA....Wezi watakua na mbeleko na wanaweza kuhesabu mpaka tatu na kulirusha jiwe uelekeo ulipo mlango then mlango utavunjika ndipo watapata nafasi ya kuingia ndani na kuwaibia Mali mbali mbali..

Wengine watakuja kuongezea zaidi..
Shukran nimeelewa
 
Tuko ndani ya uwanja unaenda kule na kule, unakula upepo tuu..

Nikataka kwenda kuzurura zangu, nafika getini MLINZI kanikazia.

Kaniambia siruhusiwi kutoka kwa miguu, Akapgiwa simu DREVA nikaambiwa niende nae kapewa funguo kuingia kwa gari DEREVA ananiuliza nataka kwenda wapi?

Nmamwambia mi sijui nilitaka kwenda kutembea tu, Basi jamaa akaichukua hiyo ndo fursa akaenda mishe zake namimi ndani ya gari, akipgiwa simu kuulizwa tulipo anasema ananitembeza.

Wajomba IST zilikua hazijaingia enzi hiyo tuko na PRADO SAFARI lile limebenjuka flani ndo hiloo tunazurura nalo. LINAMKONGA kwa mbeleee.

Oyaaa wajombaa hiyo ndo life ya watu.
Duuh
 
Miaka ya 89's nyumbani tulikuaga na Tv, fridge, washing machine,choo Cha kukaa, nyumbani Kuna umeme, mashine ya kunyolewa, jiko la umeme , oven , pressure cooker N.K
Kumiliki ivyo vitu enzi izo yaani mnaonekana matajir wakubwa Sanaa 😊

Maisha yamebadilika Sanaa Sanaa sikuizi hivyo vitu sio big deal tenaa...
Kwa wakati ule mlikuwa matajiri wakubwa sana
 
Miaka ya 60's mpaka early 2000 kilikuaga na wizi /uvamizi kuvunja mlango na ndio kisa Cha watu kuanza kuweka milango ya ma grill

Iko ivi wezi watakuja na jiwe kubwaa ambalo liliitwa FATUMA....Wezi watakua na mbeleko na wanaweza kuhesabu mpaka tatu na kulirusha jiwe uelekeo ulipo mlango then mlango utavunjika ndipo watapata nafasi ya kuingia ndani na kuwaibia Mali mbali mbali..

Wengine watakuja kuongezea zaidi..
Kuna wezi waliendaga kuvamia nyumba ya kibibi na jiwe fatuma.

Wakati wanaliset set bibi akaamka akawasikia mipango yoote,

Bibi alichofanya alienda akasimama nyuma ya mlango, wale jamaa wakaanza moja, mbili...... ile kufika tatu, bibi akaufungua ule mlango ghafra, jiwe likapita mazima bila kugusa mlango mpaka ndani kisha kwa haraka akaufunga.

Jamaa wakakosa means ya kuvunja mlango wakaanza kumuomba bibi awafungulie walau wachukue jiwe lao
 
Huyo alikudanganya mkuu, kwanza EWURA hawawezi kutoa kibali na pia OSHA hawawezi wakatoa kibali cha kuweka fuel station kwenye makazi ya mtu.
Inawezekana

Makampuni mengi ya usafirishaji wana pump kwenye yard

So mtu anakuwa na yard pembeni ntumba yake

Hii kuna jamaa angu kwao wanakarakana kabisa ya magari ya familia

Tembea uone
 
epuka matapeli mil 500 kwa watu wawili tu ni bill moja hiyo!..
ndio ni tajiri lkn mh! matajiri nao huwa wana kanuni zao tena zaidi kwa watoto wao huwa hawapendi wawe na matumizi yakufuja mali maana ndio kesho ya utajiri wa mzazi wake.
Kwa magawio ya faida kwenye biashara inawezekana kabisa

Maana wanatengeneza hela ndefu
 
Kuna wezi waliendaga kuvamia nyumba ya kibibi na jiwe fatuma.

Wakati wanaliset set bibi akaamka akawasikia mipango yoote,

Bibi alichofanya alienda akasimama nyuma ya mlango, wale jamaa wakaanza moja, mbili...... ile kufika tatu, bibi akaufungua ule mlango ghafra, jiwe likapita mazima bila kugusa mlango mpaka ndani kisha kwa haraka akaufunga.

Jamaa wakakosa means ya kuvunja mlango wakaanza kumuomba bibi awafungulie walau wachukue jiwe lao
Duh. Kama ni kweli huyu bibi ni jasiri kama magaidi wa kujitoa mhanga.
 
Back
Top Bottom