Dr am 4 real PhD
JF-Expert Member
- Jun 30, 2016
- 11,640
- 24,066
Kaiba mashuka ya government ππMimi nilikuta shuka la Msd Kwa jamaa nilicheka sana nikamuuliza lilifikaje jamaa akaniambia tulia wewe hujui maisha. Msela Wala hakuwaza. Kuhusu kwamba kujua pesa ipo ama haipo siyo jukumu langu.
Kawaida tuFriji limejaa ma yogurt, masamaki, manyama...
Chaii sio ya kuchapisha ni ya kuhesabu helaMashine ya kuchapisha hela daa nikajua jamaa yangu anakopesha nchi za jirani
Mzee ulienda nyumbani kwa Mama kizimkazi ?Nilikua naendesha gari ya mizigo nikapata kazi kupeleka mavyuma fulani hivi mbweni, sikwenda na mtu ila nilipewa namba ya simu nikaambiwa ukifika maeneo fulani piga simu kuna mtu atakufuata.
Mie huyoooo nilipofika eneo la tukio nikapiga simu full kufoka nimeshafika muda mrefu hapa, dk 0 ikaja V8 nyeusi tiiii. Ikaja kuni block kwa pembeni, jamaa akashusha kioo akasema nifuate.
Asee kila kona tunayokunja ni mijengo ya maana, mitaa mizuriii halafu pako kimyaaa, tukafika mpaka nje ya mjengo mmoja geti kuubwa, lile lango likafunguliwa kwa rimoti tukazama ndani.
Asee ile kuingia ndani nikawa nashangaa shangaa tu hata sielewi, lilikua bonge la jumba, swimming za maana halafu juu ya paa kuna parking ya helicopter, mataa ya barabarani yapo ndani.
Kuna jamaa nahisi aliona shauku yangu, akaniambia "zunguka zunguka uone nyumba ya rais wako ili uende ukasimulie na wenzio" nilizunguka kidogo tu ila maeneo mengi yalikua na makatazo kupita.(nyumba ilikua haijaisha ila ilikua inatisha aseee)
Unachokataa mkuu ukijui mm babu yangu alikuwa na fuel pump hadi Leo bado ipo. Ilikuwa wa mafuta ya taa na diesel na watu walikuwa wanakuja kununua mafuta kwa babu pale , pia kulikuwa na jengo la posta office hadi sasa bado lipo pale nafikili ni kutokana na umaarufu na pesa ya hahaha pamoja na chai . Miaka hiyo vitu viliwezekanahivyoHuyo alikudanganya mkuu, kwanza EWURA hawawezi kutoa kibali na pia OSHA hawawezi wakatoa kibali cha kuweka fuel station kwenye makazi ya mtu.
Mmmh....!!! Huyo Bakheresa mwenyewe ana utajiri kiasi gani mpaka Kila mwezi awe anawapa watoto wake Kila mtu $200k za kwenda kutupa tu?unashanga mil 5. baresa kila mwez pesa ya matumiz kila mtoto analamba m 500
Na wewe kweli umeikubali kwamba Kila mwezi Bakheresa anampa Kila mtoto wake Tsh.500m za kwenda kuchezea tu?kwa familia ya mzee bakhresa hapo sawa
Mkuu Kuna vitu vya kufikirisha sana unabaki kucheka tu. Unajiuliza huyu jamaa shuka la wagonjwa alipata wapi ujasiri wa kulibeba na kuanza kulalia kabisa bila wasiwasi!Kaiba mashuka ya government ππ
Huwezi elewa hiyo imeandikwa kitaalam sanaSasa babu kwani matajiri nguo zao zinakauka vipi
Na sikujua nipo nyumba ya nani mpaka mlinzi aliponiambia.Mzee ulienda nyumbani kwa Mama kizimkazi ?
ππili jina la mkuu kalagha bao nongwa hadi mimi huwa linanichekesha sanaWe jamaa kwanza before ujacomment na jina lako hilo huwa nacheka tuu...πππ
Mkuu nimeznguana nae baada ya kuanza kutangaza kwa kila mtu kmmk zake yule
Hizo nguo unaanikaje? Au unaweka ngazi?Ndio mkuu, mlingoti chuma mirefu balaa. Nikirudi nimelewa namwambia dreva boda unaona ile milingoti imechomoza kulee, ifate.
Endelea kujitafuta, uko nyuma mno.Friji limejaa ma yogurt, masamaki, manyama...
Una biashara gan sahiviTulihama mkoa na huko tulipoenda tukapata jirani,,, wenyewe walikua hawaendi shule kusoma wanasomea nyumbani tuu walimu wanakuja kuwafundishaπ shule wanaenda kipindi cha mitihani yenye maana tuu.. Tulivomaliza form 4 kila mtu alikabidhiwa biashara yake rasmi na mtaji wa kutosha, πππ kipindi iko sisi wengine ndo tunapambana kusoma vile vikozi vya kompyuta sijui nini tukisubiri matokeoππ. Sikuhizi nawaona huko tiktok wakifanya challenge na products zaoππ.
Mbona watoto wa Bakhresa wakubwa kabisa au unasema wajukuu zakeunashanga mil 5. baresa kila mwez pesa ya matumiz kila mtoto analamba m 500
Wifi yako ni mrefu mno, mtaani wanamuita TOLU.Hizo nguo unaanikaje? Au unaweka ngazi?