Ulishawahi kununua asali kwenye duka la serikali? Uliwezaje?

Ulishawahi kununua asali kwenye duka la serikali? Uliwezaje?

Ni mara ya tatu sasa naenda kwenye duka la linalomilikiwa na serikali linalouza asali ila sijawahi kufanikiwa. Duka lipo karibia na mataa yaA Chang'ombe kama unaelekea mkuki house (dar es salaam).

Lile duka hawapokei cash malipo ni kwa control namba, lakini hata hiyo control namba mara zote husema network inasumbua....kila siku network ni shida??? sasa biashara wanafanya lini??? nakereka sana kufunga safari ndefu halafu nafika majibu ndio hayo, hivi wameshindwa hata kuuza kwa risiti??? Hadi nahisi labda huwa hawauzi je kuna mtu alishawahi kupata huduma pale???
Kama kweli unahitaji asali safi, agiza ya mzee Pinda Dom ni fresh na imepakiwa vizuri. Kama unaipenda niambie. Mimi sipo ila nina mwanangu yupo huko. Siyo Tapeli kama tulikotoka kwenye ule uzi.
 
sio cheap bei kawaida lita 1 tsh 10000 ila ni asali nzuri

tumeaminishwa vibaya.mtu hujawahi kununua hata mara moja tayali unasema ile itakuwa nzuri.Hata hiyo inaweza chakachuliwa na kwa kuwa ni serikali hakuna kwa kulalamika.

Unaenda pale kununua muuzaji anakutazama kama wewe ombaomba vile.mimi kuna mtu ananileteaga asali bora sana toka Tabora.Ila sema inabidi uwe unazijua asali kama hujuzijui ni bora ukaenda supermarket.
 
mmh ila mashelf muda wote huwa yamejaa asali sijawahi kuona pamepungua ila sijawahi kuuziwa vile vile
Kwa nini hujauziwa na Asali ipo? Tatizo mpo negative kwa kila kitu cha Serikali. System ya malipo ya serikali inajulikana, hakuna mahali watu wanapokea cash, na inaweza kutokea umefika system ipo chini, katika nchi hii hiyo kutokea ni kawaida, hata mabenki kuna wakati system inakuwa down. Mtumishi wa aliyepo hapo hawezi kupokea cash under any circumstances, kwa sababu hata kama atafanya hivyo kukusaidia ili kukupunguzia usumbufu in case system ipo chini utarudi hapa kusema pale hela zetu zinapigwa maana wanapokea cash! No one wants that! Mifumo ni ya Serikali na pesa ni za Serikali, mfumo ukigoma utaambiwa tu umegoma, hakuna namna, sababu no one wants to mess up with government money.
Suala la kitu kiddogo napinga, anayeuza namjua ni very decent lady. Kama ilitokea hukuuziwa na Asali ipo itakuwa ni sababu nyingine.
 
Kama kweli unahitaji asali safi, agiza ya mzee Pinda Dom ni fresh na imepakiwa vizuri. Kama unaipenda niambie. Mimi sipo ila nina mwanangu yupo huko. Siyo Tapeli kama tulikotoka kwenye ule uzi.
Yule mdada bonge ndiyo rafik yako??
 
Siku nyingine nenda na "shati lenye mikono mirefu"
 
Kila kitu Serikalini kinaenda kwa mtindo huo lakini hapa namba moja wa kulaumiwa ni wananchi wenye nchi ambao badala ya kutimiza wajibu wao wa kuiwajibisha serikali huwa wapo wapo tu na kushangaa shangaa kama mazombi yaliyofufuka kutoka kuzimu.
Tupe mwongozo, we unavyoiwajibisha ili tufate nyayo....mimi nilifanya kwenye sanduku la kura nikashindwa
 
Evelyn Salt kila siku napita hapo kesho ntapita kuchukua nione kama wataniletea habari za mtandao, maana mimi huwa navaa sura ya kazi ninapoingia ofisi za serikali kitu kinachonifanya nipate huduma bila ubabaishaji
 
Evelyn Salt kila siku napita hapo kesho ntapita kuchukua nione kama wataniletea habari za mtandao, maana mimi huwa navaa sura ya kazi ninapoingia ofisi za serikali kitu kinachonifanya nipate huduma bila ubabaishaji
utanijulisha....Mimi day 1 niliambiwa hatupokei cash, nikatoka nje kuweka pesa kwenye simu nilivorudi nikaambiwa network inasumbua, kero tupu
 
tumeaminishwa vibaya.mtu hujawahi kununua hata mara moja tayali unasema ile itakuwa nzuri.Hata hiyo inaweza chakachuliwa na kwa kuwa ni serikali hakuna kwa kulalamika.

Unaenda pale kununua muuzaji anakutazama kama wewe ombaomba vile.mimi kuna mtu ananileteaga asali bora sana toka Tabora.Ila sema inabidi uwe unazijua asali kama hujuzijui ni bora ukaenda supermarket.
mimi kutonunua haimaanishi sijatumia, kama niliionja mahali je??
 
Acha uongo, mbona watu wananunua kila siku? Ni kweli kuna wakati stock huisha kwa sababu Asali inayouzwa hapo ni ile iliyozalishwa na Serikali tu.
kwamba uongo hapa ni upi??? nimeuziwa nimesema sijauziwa??? au ni upi??
 
Bora hata wewe uliambiwa kuhusu kulipia kwa control no [emoji1787][emoji1787][emoji1787] mie kila nikienda naambiwa hakuna.
Hakuna mzigo umeisha.
Njoo wiki ijayo.
Nikienda tena naambiwa mzigo haujafika.
Nilishaacha kwa kweli.
Unataka lita ngapi nikuletee asali toka tabora!?
 
Kila kitu Serikalini kinaenda kwa mtindo huo lakini hapa namba moja wa kulaumiwa ni wananchi wenye nchi ambao badala ya kutimiza wajibu wao wa kuiwajibisha serikali huwa wapo wapo tu na kushangaa shangaa kama mazombi yaliyofufuka kutoka kuzimu.
Sisi watz ndio wananchi wapumbavu kuliko woote duniani.
 
Back
Top Bottom