Ulishawahi kuona malaika?

Ulishawahi kuona malaika?

Hello natafuta majibu hasa kwa wenye uzoefu, hebu tupe story

Ilikuwaje

Anaonekanaje

Alisema nini

Na mimi nataka kuona nifanye nini nipo kwenye research nataka kuuona ulimwengu mwingine sasa sitaki kukaa kizembe hebu nipeni uzoefu na mimi niwe miongoni mwa watu wanaotafuta ukweli kwa macho yangu

Ikiwa na wewe mpenda story stay tunned tuwasikilize marafiki zetu
Hahahaha baada ya kusoma ule Uzi Wa Jamaa anazungumzia Mungu Wa walokole akagusia habari za malaika

Ili nipa hamasa sana ya kutaka kuona malaika

Sasa wakati nipo kwenye maombi ya jioni siku ya alhamisi wakati nimezama kwenye maombi ile story ya Jamaa ikanijia kichwani
Nikaona hapa hapa kwenye wingu la kuzama niombe Neema ya Mungu nione malaika

Ninapoanza kutamka tu nikajikuta nashukuru na kusema asante Mungu Kwa ajili ya uwepo Wa malaika wako mahali hapa

Gafla hali ya hewa ilibadirika kukawa na hali ya ukungu hivi aise ilishuka nguvu ya roho mtakatifu nijazama jumla hapo nikinena Kwa lugha

Kwa raha ya uwepo ule Wa nguvu za Mungu hata sikuwaza tena kuhusu malaika

So nikajua hata malaika niwaone haitakuwa na faida kwangu zaidi ya kujitafutia majivuno tu

Ninachohitaji nikudumisha ushirika wangu na Mungu wakati wote maana ushirika huo ndio unaosababisha malaika wanihudumie
 
Mzee kwa mujibu wa Biblia..
MALAIKA WANA MAUMBO YA KUTISHA SANA YAAANU KIFUPI MALAIKA WANATISHA SANA..

BORA HATA PICHA MNAZOMCHORA SHETANI...
WANATISHA SANA...
USITAKE KUWAONA
Mhhh
Hahahaha baada ya kusoma ule Uzi Wa Jamaa anazungumzia Mungu Wa walokole akagusia habari za malaika

Ili nipa hamasa sana ya kutaka kuona malaika

Sasa wakati nipo kwenye maombi ya jioni siku ya alhamisi wakati nimezama kwenye maombi ile story ya Jamaa ikanijia kichwani
Nikaona hapa hapa kwenye wingu la kuzama niombe Neema ya Mungu nione malaika

Ninapoanza kutamka tu nikajikuta nashukuru na kusema asante Mungu Kwa ajili ya uwepo Wa malaika wako mahali hapa

Gafla hali ya hewa ilibadirika kukawa na hali ya ukungu hivi aise ilishuka nguvu ya roho mtakatifu nijazama jumla hapo nikinena Kwa lugha

Kwa raha ya uwepo ule Wa nguvu za Mungu hata sikuwaza tena kuhusu malaika

So nikajua hata malaika niwaone haitakuwa na faida kwangu zaidi ya kujitafutia majivuno tu

Ninachohitaji nikudumisha ushirika wangu na Mungu wakati wote maana ushirika huo ndio unaosababisha malaika wanihudumie
Duuh point sana mimi sitaomba tena milele yote niwaone ila sasa nataka njia yake tu, hivi tofauti ya binadamu na malaika ni ipi?
Nani Mkuu nani anamtumikia mwenzie
 
Mkuu haya ndo maumbo na sura za malaika kwa mujibu wa Biblia..
Na kama utabahatika kusoma Angeology Utajua nachomaanisha..

kuna Makerubi ambao ndo malaika ngazi ya kwanza na Malaika wote ambao huitwa Arch Angel wote wapo kwenye group hili Kina Michael(Mikaeli) ,Gabriel, Raphael..
Hawa ndo huwa na uwezo wa kuongea na Mungu moja kwa moja na ukisikia malaika kaasi ujue ni Makerubi...

na kuna Seraphine (Maserafi)Hawa ndo wale walio Levo ya Pili baada ya Makerubi hawa hawana muda wa kuhoji wala Kuuliza maagizo ya Mungu wenye kutenda kama agizo lilivyo...

Na kamwe ukisikia Malaika wameasi au wameanguka Huwezi kuta mmojawapo akawa serafi wana utii wa hali ya juu sana... Kuna Malakh ambao hawa ni wajumbe na mara nyingi huweza kuchukua maumbo ya Vitu ,Wanyama au watu japo wenyewe hawana Umbo....kundi la nne ni Ophanim

Hivi ndivyo wanavyoonekana Kwa Pamoja..kwa Mujibu wa Biblia



View attachment 2825413


Ntafafanua baadae KIMOJA BAADA YA KINGINE
Mkuu! Hizi sura za mashetani wala sio malaika!
 
Mara ya pili ikatokea pale shuleni nilipoamua kuwa Atheist, nikasema kwa mdomo wangu Mungu hayupo na Yesu hayupo, Sayansi ndo imechukua nafasi ya Mungu.

Tena usiku wa manane nikaota ndoto, nilikuwa kwenye hatari ya watu waovu baada ya kujua siri zao , akatokea Malaika akanichukua na kunipeleka sehemu ya paradiso, nikakaa nje, sikuruhusiwa kuingia ndani, sasa mageti yakafunguliwa, nikamuona mtu akismile, akiwa na ndevu, Yesu ambaye nilisema hayupo. Aisee nilipigwa na butwaa.
Yesu uliyemuona anafanana na huyu wa kwenye movie???
 
Malaika ni wengi na hujitokeza katika maumbo ya wanadamu na kusema na watu mara nyingi bila watu hao kufahamu.

Utakutana na mtu usiyemjua akakuongoza katika jambo na baadaye akatoweka na utakuja kushangaa yule alikuwa nani mbona hata sikumuuliza jina au kumtizama sana usoni? Hao huwa malaika mara nyingine.

Kuna wachache hutokewa na malaika live inapokuwa lazima sana.

Pia wengine hukutana na malaika katika ndoto.

Jua pia kuwa mashetani huja kwa watu kwa njia hizo hizo.

Nikwenda Nairobi miaka mingi iliyopita kutafuta chuo. Nilifuatilia registration lakini sikupata. Wakati nipo jijini mle nilichujua hosteli kama kilometer 2 kutoka chuoni. Lakini ilinibidi kuhama hostel hizo baada ya kukosa usajili ili nikae nyumba ya wageni usiku ule kabla ya kurejea Tanzania.

Nilighadhbika sana mchana ule hadi kukaribia usiku. Nilisali sana kumwomba Mungu anisaidie niwe salama. Wakati natoka getini nilikuwa nimebeba shehena ya mabegi yangu kichwani narudi nyumba ya wageni na ilikuwa kuelekea saa 1 usiku.

Nairobi ya 2003 ilikuwa na uhalifu wa kutisha. Ghafla ilikuja tax nyuma yangu na mtu mmoja nisiyemfahamu alifungua mlango na kuniambia unafika wapi, nikupeleke? Unajua wakenya sio wakarimu kama watanzania tena ndani ya nairobi na tena kwa mtu asiyekujua ndio usiseme.

Bila kuwa na hofu nipanda tax na kumwambia nilikokuwa nakwenda. Mtu yule alinipeleka hadi hatelini na kuniacha pale huku akinipa namba ya simu na hakunichaji chochote! Kenya tena katikati ya Nairobi?!!! Alikuwa mkarimu ajabu!

Ajabu ni kwamba siku mark sura yake na hata ile namba ya simu sikujua niliiweka wapi!

Niliporudi Tanzania niliwaadithia ndugu zangu wanaojua Nairobi na walitetemeka sana kusikia nimepanda tax Nairobi ya mtu nisiyemjua!

Baadaye nilipata ufunuo kuwa hakuwa mtu wa kawaida ila malaika! Bwana Mungu asfiwe sana!
TOA hiyo hang over

Jitahidi uache ulevi

Alikuwa mtu WA kawaida tu
 
Unasema unataka ku experience mambo ya ulimwengu mwingine? Inawezekana kuwaona kama unavyotaka lakini inabidi kufanya tafiti jinsi na namna yakuwaona.

Kuna kitu kinaitwa invocation na evocation soma hivyo vitu viwili ndio utajua uwanzie wapi au unataka uwaonaje?
 
Humu kuna watu wana fikra za kipumbavu sijawahi ona. Kwa hiyo ukisaidiwa na mtu asiyekufahamu wala kumfahamu ugenini ni malaika huyo? Kuota unafanya jambo katika hali ya kustaajabisha unakuwa umetembelewa na malaika? Hivi unafahamu ukitaka milango yako ya fahamu iweze kudetect hatari mbele unaweza na sio kitu cha ajabu!? Hivi unafahamu kuwa nafsi yako inaweza kutangulia mbele ikaangalia hatari au uzuri ulioko mbele uendako ila usipoiheshimu unakuja kumbuka baadae na ndipo mnaanza kusema au ndio maana nilikuwa nasita kufanya jambo fulani.

Hakuna cha malaika wala nini, achaneni na masimulizi yenu ya kipumbavu mliyokaririshwa na wakoloni wa kimishionari. Shirikisha ubongo wako ipasavyo.
😂Mi nimewaacha...ililetwa thread ya story za uchawi nikaambiwa nimeharibu kisa nimesema uchawi haupo...wajinga ndo waliwao
 
Back
Top Bottom