Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Tuambie sasa ukweli ni upi?

Wewe wa kishua au choka mbaya??

Maana naonaga unatunywesha sana chai humu.

Mara utuambie una plan kufungua duka la vipodozi, mara una plan kuuza kitimoto na kufungua ki pub.
Hahahah mzee unahangaika mno halafu haitakusaidia 🤣 wanaonijua wanaelewa huu sio ubao wa matangazo
 
Duh ila ndugu wa mume jamani kuishi nao yataka moyo.nimekuja kugundua kwanini watu wengi wanaishi na ndugu zao kuliko ndugu wa mume.nikiishi na mdogo wangu namtuma nitakavyo hata nguo zangu nampa anifulie hutomsikia kunung'unika, ndugu wa mume mtume hata mara moja ukoo wao mzima watajua . Nako hapa naishi na wifi yangu kaachika kwa mume wake yaani ni kero jamani nyumba imekuwa kama na wanawake wawili mimi napanga kipikwe hiki yeye anapika kile mavyakula anapika mengi anaishia kumwaga yaani ilimradi fujo.hapa napanga na mimi niondoke niende kuishi kwa kakaangu
Mwambie mumeo ampangie chumba,
 
My story, mazingira ni kijijini.

Nilihamia kwa uncle nikiwa 9yrs old baada ya home kutokuwa hapasomeki kutokana na uhohehahe wa home. Ilikuwa rahisi kwenda kwa uncle sababu nilikuwa naishi huko kwa bibi(kabla hajafariki, baada ya kufariki nilipelekwa nyumbani) ambapo mji ulikuwa mmoja kama tunavyojua vijijini kaya huwa zipo pamoja kwa asilimia kubwa.

Lengo la kwenda uncle ilikuwa ni kupata unafuu wa maisha, bila hiyana nilipokelewa vizuri ila nilipoulizwa jinsi nilivyoondoka home nilidanganya kuwa nimeondoka kwa ruhusa ila home nilitoroka, kule kwa uncle nilisema nimekuja nitakuwa nawasaidia kuchunga ng'ombe. Bila hiyana wakakubali maana walikuwa wananifahamu tangu nikiwa naishi kipindi bibi yupo hai. Wao pia walikuwa wanajua hali halisi ya nyumbani kwetu

Nature ya uncle na mkewe ni uonevu, kunyanyasa mtu yeyote asiyekuwa mtoto wao wa rika lolote anayeishi hapo, tabia hiyo inajulikana na watu wote mtaani.

Maisha yakaanza bana, kwa kuwa nilisingizia nimekuja kuwasaidia kuchunga nikaianza hiyo kazi. Nikawa napigishwa kazi nyingi sana hapo nyumbani mbali na kuchunga, nikawa kila kazi ikitokea nalazima niitwe nikaifanye hata kama ni kazi ndogo ambayo watoto wao wanaweza kuifanya, kama sipo(nimeenda kucheza kwa majirani lazima nitafutwe niinde nikaifanye, ilifikia kipindi nikawa natoka bila wao kujua ili nikacheze kwa majirani kukwepa kazi ndogo ndogo ila na wao wakawa wananiambia nisitoke maana nilikuwa natoka baada ya lunch, kumbuka hapo nikiwa sijaenda kuchunga).

Nikawa natumwa kwenda kusaga unga mashineni ila mzigo ninaoupewa ni mkubwa hadi nasota, nikiwa najikongoja nao kichwani nakutana na watu hadi wanashangaa na kusema mama fulani hafanyi vizuri anampa mtoto mzigo mkubwa, endapo ikitokea anaandaa mzigo halafu majirani wakawa pale kwenye kupiga story na akaambiwa mbona unamfungia mzigo mkubwa sana anasema sio mkubwa na huyu ni mtoto mkubwa. Watu wanabaki kumuangalia tu.

Mwaka mmoja baadae nikiwa pale nikafundishwa kuendesha baiskeli, hapa palikuwa nafuu nikawa napiga kazi nyingi kwa baiskeli. Kusaga ikawa jambo nafuu, kuchota maji ikawa kazi yangu(watoto wao wanafanya kwa hiari, jla mimi ni shurti na siwezi kukataa)

Baada ya wao kuona napiga kazi vizuri wakaamua kunipeleka/kuniandikisha shule nikiwa umri ushaenda (10yrs) ingawa kwa kijijini ilikuwa kawaida. Mimi pia nilikuwa nataka shule nikafurahi bila hiyana, kwa umri huo tulikuwa wanafunzi wengi tukaenda kuanzishwa darasa la pili. Hapa kwenye kunipeleka shule walicheza kama The late Pele maana kwa miaka kadhaa hadi nimalize la saba lazima wanifaidi katika kazi, na kweli walinifaidi maana nilikuwa mtiifu sana.

Kuhusu sare za shule na daftari nilikuwa najinunulia mwenyewe kupitia kufanga vibarua vya kulima hasa msimu wa kulima, mara nyingine wao wananipa kibarua kwenye shamba lao napiga kazi wananipa hela naenda kununulia daftari, nikiwa shule endapo daftari ikiisha labda ya somo la hisabati nikiomba hela nitaambiwa kachanganye kuandika, yaani nikaandikie kwenye daftari ama la kiswahili au sayansi. Kwa hali hii nikawa nikipata hela naitunza ili ije inisaidie kununua daftari. Wakati mimi napambana na hali hii ila watoto wao hela zao wakipata kwenye vibarua wanaenda kununulia soda, biskuti, pipi hadi zinaisha maana madaftari yakiisha tu wananunuliwa mengine.

Kwenye msosi ikawa ni mwendo wa kupunjwa kama ni maziwa mimi nitaambulia nusu kikombe wengine wanapata kikombe full halafu mimi ndio kinara wa kwenda kuchunga, watoto wao wanaona hiyo hali ila hawasemi, mara nyingine uncle anajishtukia ananiongezea kutoka kwenye maziwa yake na endapo mkewe akiwa karibu na akiona anachukia kiaina. kitendo cha kupunjwa kila mtu aliyewahi kuishi pale asiye mtoto wao alikipitia. Pia unaweza kupewa mboga zilizoisha muda wa matumizi yaani mboga ya juzi unaweza kuipewa leo uitumie na usiweze kusema kitu, unaishia kugusa na kula tonge kavu kavu.

Ikiwa sijaenda kuchunga halafu ni weekend huwa tunafua nguo za shule, mimi nitaambiwa fua nguo zote hadi za wanawe hata kama wapo na hawana kazi maana suala la kufua wanamuachia mama yao na yeye ananipa huo msala. mara nyingine nilikuwa napewa nguo za mume wake naambiwa zifue, kama hamna maji hapo nyumbani naambiwa nenda kafulie mtoni.

Wakati wa kulima mimi nitaaamshwa alfajiri saa kumi na moja ila watoto wao wanaamka muda wowote wakipenda na mara nyingine wakisema hawaendi kulima waachwa, mimi siwezi kufanya hivyo maana mziki wake si wa kitoto nitakaoupata kuanzia kuchezea stick hadi kunyimwa msosi(binafsi sikufikia level ya kunyimwa msosi ila wapo waliowahi kunyimwa), stick ndio nimezichezea sana pamoja na kutukanwa kwa kosa dogo tu.

Life langu la primary likawa hivyo hadi nikamaliza la saba na sasa nishasahau hizo tabu zote na kupitia wao ndio inekuwa chachu ya kubadili maisha ya kwetu niliyoyakimbia enzi hizo ingali ni mdogo na endapo nisingekimbia sijui kama ningekuwa hapa nilipo sasa, hata kama ningekuwa hapa sasa labda sijui ningepitia njia gani maana mlango wa kutokea ulikuwa mgumu sana.

Jambo zuri walilokuwa nao hawa walezi walikuwa na exposure ya elimu japo kunipigisha kwata za kazi ila walikuwa wanafurahia maendeleo yangu mazuri kwenye masomo na walikuwa wanajidai mtaani kuhusu hasa wakiwa wanaambiwa sifa zangu na juhudi shuleni.

Nawapa MAUA yao hawa walezi walinitoa jalalani kama yule Prof wa awamu iliyopita.
Watoto wao wapo kwenye Hali gani sasa?
 
Sijui kama umenielewa, huyu wifi yangu katoka kwa mume wake kaja hapa kwa kaka yake kuishi.ishu inayokuja kwa mfano hapa kwangu nina ratiba ya chakula asubuhi mchana na jioni,asa utakuta ratiba yangu jioni ni kupika hiki yeye atapika kile,hafu maagizo yote hela huwa namuachia binti wa kazi lakini ukirudi ulicho tegemea kukuta sicho kuuliza ooh aunt kasema tupike hiki. Kwahiyo ni kama anataka niishi apendavyo yeye.na sio kama hivyo vingine yeye hatumii hapana anatumia ila fujo tu.hapo bado atapika sufuria kubwa la chakula kesho unakikuta kwenye dustbin.haya asubuhi ataamka atapika chai ya rangi hapa kwangu kuna bili ya maziwa bado atapika na uji[emoji849] sio kama anamtoto wala hanyonyeshi siku mbili kilo ya sukari kwisha. hapo sijazungumzia mafuta,huwa nanunua viazi kwaajili ya chai lakini yeye kila siku asubuhi atapika chips anywe na chai,asa nakuta mafuta hayakai vile nlivyokusudia kumuuliza dada mnatumiaje mafuta aunt anapika chips kila mara asubuhi.na sio mjamzito .sawa kwake alikuwa yeye pekeyake na mume wake huenda alikuwa anaishi hivyo lakini mimi ninafamilia na sio kama tumetusua maisha jamani mimi na mume wangu wote ni wahanga wa ajira tuko mtaani tunaunga unga tu na tumepanga bado kwanini haelewi? Kila pesa tunayoipata tunaipangilia sana
Aisee,pole sana mawifi ni janga sana,kwani so aende kwao.
 
Yeah hili liko wazi. Mtoto atanyanyasika tu akikaa mahali ambako mwanamke sio ndugu yake. Hawezi kuwa huru lazma atasumbuliwa kihisia tu. Wanawake wengi wana roho za kishetani sana wakikaa na ndugu za waume zao. Tena hasa huyo ndugu awe na uchumi mzuri balaa huwa zito. Kwa niliyopitia staki kuja kuona mtoto wangu anakaa mahali ambapo sio kwao.

Bora tushindie mikate na chai ila sio kumpeleka kwa baba wadogo au baba wakubwa wake. Yani hata nikifa bora akae na shangazi yake tu. 🤣
Sahihi kabisa.
 
Dar watu wanaishi kwa bajeti finyu, wewe unataka ufungue mafriji na kuanza kula matunda au vyakula bila mpangilio, kwa hilo hata mimi sikusupport.

Halafu vyengine lazima ujiongeze mwenyewe, mfano sabuni, toothpaste na vile vidogo vidogo vya matumizi yako. Kumbuka hapo haupo wewe peke yako, umepewa pa kulala pengine ongezea maisha yaende mbele.
Mmmmh wewe ni balaaa
 
Chanzo Cha yote hayo ni njaa hukosefu wa chakula .

Mimi Nina kilo miatano za mchele na gunia mbili za maharage na Nina pesa za Mboga Sasa ukija kwangu kunitembelea huwezi kugombana na mtu .


Wanawake wana njaa Sana Mnabidi kulifahamu hilo Kama hauna chakula Cha kutosha usimlete ndugu ikiwa unakaa na Mwanamke ataishia kumnyanyasa Mimi nimejionea haya Mambo Nina ndugu yangu yeye anakaaga na vyakula magunia Mengi ya kutosha Sasa pale kwake ndugu wa mke na wa Mume wanakula na kusaza huwezi kuona ugomvi ukitokea Sasa njoo huku kwa Hawa sijui Mwalimu sijui nurse sijui nani huko pamoto Sana.
Baadhi ya wanawake hawana aibu kabisa yuko radhi afiche chakula hata kama kitaoza ndani.
 
Siku nshaondoka naanza life nikatoka kizungu kwa binamu.
Oven taka zote nnazo.
Dah siku wamekuja kusalimia kuna binti kalala mle ndani ana mimba.
Ikawa anhaa weh hivi tumekupa umeleta jeuri umekuja ukaoa.
Wakabeba tena vyoote[emoji1787][emoji1787][emoji1787].
Wakatimua navyo.
Demu nae anasema kumbe vitu sio vyako?
Katimua,
Nikaona afadhali sasa niko huru[emoji119]
Hahahhahahahhahahah
 
Bora nyie mlinyanyaswa na mashemeji zenu...
Miaka fulani ya nyuma nilimtembelea ndugu yangu maana alikuwa analalamika sifiki kwake.

Nikapewa chumba nyumba ndogo ya nje ambayo alikuwa anakaa bro na mke wake ila chumb changu kinajitegemea tofauti kabisa na jamaa, hata choo nilikuwa namtumia cha nje ila jamaa kwake ilikuwa ni master bedroom.

Sasa huo usiku mkojo umenibana, ile natok nje tu nakutana na 2 grown Dobermanns with cropped ears na mwingine hadi mkia amekatwa[emoji15][emoji15]. I was like hee kumbe humu ndani kuna mbwa tena wakubwa hivi na hawaniambii hawa si wauwaji kabisa kwa kweli sikupenda[emoji1787][emoji1787]. Ikabidi nirud geto, nikampigia simu bro akaja akawashika mbwa nikaenda msalani.

Ilikuwa kero maana karibia kila siku nampigia jamaa anisindikize chooni kama mtoto mpaka jau, jamaa akanipanga hawana shida hao wakishakuzoea. Kesho yake nikawa nipo nao karibu tunacheza nao mixa wanapewa maelekezo wanizoee, yule mmoja alinirukia yani over nilitupiwa kakiroba cha kilo 50!! Nilipata ka upenyo nilijikuta nasepa ka upepo, yule mbwa anakuja nyuma ananikimbiza, anadhani tunacheza kumbe mwenzie ndio nasevu hivo[emoji1787][emoji1787]. Ilifika wakati ikifika kuanzia saa 9 au kumi sinywi maji mpaka kesho yake!

Sasa huo usiku nataka kwenda chooni kama kawaida, ile nafungua mlango tu yakanyanyuka masikio yamewasimama kama antenna yani kama washajiandaa kwa kitu fulani so alerted, nikasema hapana nikarud ndani pigia sana bro simu haipatikani. Mkojo unazidi kubana na ndani hakuna hata chupa. Nikachungulia tena nikawaona wako mbali kidogo nikachomoka kama mkuki mpaka chooni, yalikuja kwa kasi yakaanza kuparua mlango. Wakat nataka nirudi nkayaona yamesimama kwa mbali kidogo yapo serious sio mchezo, nikayachekiii nikaanza kuambaa ambaa na fence kuutafuta mlango wa geto, nayo yakaanza ku move kunifata. Nikajisemea hapana hii sio ishara nzuri nikarudi mbio mpaka chooni, majamaa yakaja speed mpaka pale mlangoni yanaunguruma mixa kuparua mlango.Nilienda na simu chooni, piga sana simu ya jamaa haipatikani nikajisemea leo nimeisha[emoji16]. Nikavuta ndoo ya chooni nikakaa kuanzia saa 9 hivi kuelekea 10mpaka 12 hadi nikapitiwa na usingizi na ile baridi sio poa. Nashukuru Mungu choo kilikuwa kisafi.

.......hapo sijaelezea tukio lengine la kukimbizwa na hao mbwa kidogo ning'atwe hawakuwa wamefungwa vizuri plus kukojoa mlangoni.....

Asubuhi baada ya kuyafungia namimi ndio nikajifanya natoka chooni, yule mzee akaniuliza umeingia chooni saa ngap sijakuona?! I was pissed off sikutaka hata kumwambia yaliyonikuta maana mjadala ungekuwa mrefu na sikuwa n huo mda wa kuanza kuoneana huruma, kwanza nausingiz/kichwa kinauma na hapo nafikiria kama naweza pata bus la saa mbili au la[emoji1787]. Jioni yake nikaaga kesho narud kwetu, mzee akamaind sana akapiga simu nyumbani sikubadili maamuzi. Kesho yake asubuhi nikasepa!

Zile siku chache nilizokaa pale ndani zilikuwa ni mateso, wale mbwa walinikosesha raha kabisa hasa usiku. Maana mda wote ilibidi niangalie huku na huku nijue wako wapi kabla sijafanya movement kama vile navuka barabara maana wana eneo kubwa. Na hadi leo sijawahi kwenda tena!
Japo niliwapendea ile tough and aggressive looking yao lakini haiondoi ukweli kwamba mimi na mbwa bado haziivi kivileee.

iStock-1223511966-1024x711.jpg
 
Habari za muda huu, ni siku tulivu sana hapa. Jiji la Dar es Salaam kumekucha salama, ingawa kulikuwa na upepo wa baridi sana, poleni na natumaini kila mmoja wetu ni mzima kabisa. Nawatakia kila la kheri katika pilika za kuijenga Tanzania kuwa kubwa tena, yenye amani na upendo. Twende kwenye mada.

Kuna kipindi kwenye Life cycle ya kimaisha ilinifanya nihamie kwa uncle wangu kuishi nae ili kuangalia uwezekano wa kufanya maisha. Enzi zile ndio nimemaliza masomo nipo home tu nikapata mchong huo, nilikuwa very excited sana na hili, maana nilikuwa ninavuta picha fulani hivi kabla ya kufika kwa uncle Dar.

Siku mbili baada ya kupewa taarifa ya safari nilijiandaa lakini ilikuwa ghafla sana kutokana na uchu wa safari ya kuja huku hata watu niliokuwa nawadai pesa zangu wengi niliwapotezea, kitu ninachojutia sana.

Siku ya safari ikawadia, panda nikapanda basi safari mpaka Dar, nifika mida ya saa moja hivi enzi za ubungo terminal pale, akaja mshakaji aliyekuwa anakaa kwa huyo uncle, wakanichukua freshi mpaka home.

Hapo nipo so excited na wishes nying sana how it's going to be in the up coming day's, nikachil, nikafika home. Yale mapokezi tuu yakanidropisha point. Yule mke wake alikuwa anagubu sana, nilivyofika nikaona hapa chakike.

Picha linaanza kulipokucha tunaamshwa saa kumi na moja tufanye usafi, duuhh nilichoka. Kumbe wanafuga mbwa, sehemu padogo mbwa wanajisaidia, morning ni kuzoa na kusafisha kumwaga maji, nilichoka. Ila nikajikaza kumbe bado kuna kuosha magari usiku unaamshwa uoshe, kibaya zaidi ni kila siku iwe mvua au jua.

Kibaya zaidi ni huyo mke wake alikuwa na visa na maneno ya shombo, mara hataki watu watoke nje ya geti anafunga, mara hataki watu wakae sebuleni, hata kunywa maji ya kwenye friji jau, akinunua matunda mpaka akupe yeye na atakupa wakati linaanza kuharibika ukila atakuja kuongea mpaka ujute.

Kwa kipindi kile ilikuwa ni mateso sana, sabuni ya kuogea unajinunilia, mafuta ya kujipaka pia, tulikuwa tunajitegemea kama tumepanga hata kipindi tunaenda K/Koo ilikuwa ni taabu sana.

Ilinipasa kuishi kama mtoto wa miaka kumi kushuka chini, maana ni kama sikuwa najielewa. Maana watu walikuwa wanakuja pale wanashangaa tunawezaje kuishi na hawa, hata wadogo zake na yule mama walishindwa kukaa nae, wengine walikimbia na kutoroka. Ila ndo changamoto tunazokutana nazo katika maisha ya wengi wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikiwa darasa la kwanza nilisingiziwa kusudi kuiba sh.400 au 200 lengo niondoke nimpunguzie mke wa mjomba mzigo wa kulea, Yule mbwa simpendi hadi Leo na anajua hata kwake sigusi napita road tu basi. Sana sana naenda nakaa kwenye kaburi la uncle kipenzi changu kama kumsamilia uncle basi nasepa
 
Bora nyie mlinyanyaswa na mashemeji zenu...
Miaka fulani ya nyuma nilimtembelea ndugu yangu maana alikuwa analalamika sifiki kwake.

Nikapewa chumba nyumba ndogo ya nje ambayo alikuwa anakaa bro na mke wake ila chumb changu kinajitegemea tofauti kabisa na jamaa, hata choo nilikuwa namtumia cha nje ila jamaa kwake ilikuwa ni master bedroom.

Sasa huo usiku mkojo umenibana, ile natok nje tu nakutana na 2 grown Dobermanns with cropped ears na mwingine hadi mkia amekatwa[emoji15][emoji15]. I was like hee kumbe humu ndani kuna mbwa tena wakubwa hivi na hawaniambii hawa si wauwaji kabisa kwa kweli sikupenda[emoji1787][emoji1787]. Ikabidi nirud geto, nikampigia simu bro akaja akawashika mbwa nikaenda msalani.

Ilikuwa kero maana karibia kila siku nampigia jamaa anisindikize chooni kama mtoto mpaka jau, jamaa akanipanga hawana shida hao wakishakuzoea. Kesho yake nikawa nipo nao karibu tunacheza nao mixa wanapewa maelekezo wanizoee, yule mmoja alinirukia yani over nilitupiwa kakiroba cha kilo 50!! Nilipata ka upenyo nilijikuta nasepa ka upepo, yule mbwa anakuja nyuma ananikimbiza, anadhani tunacheza kumbe mwenzie ndio nasevu hivo[emoji1787][emoji1787]. Ilifika wakati ikifika kuanzia saa 9 au kumi sinywi maji mpaka kesho yake!

Sasa huo usiku nataka kwenda chooni kama kawaida, ile nafungua mlango tu yakanyanyuka masikio yamewasimama kama antenna yani kama washajiandaa kwa kitu fulani so alerted, nikasema hapana nikarud ndani pigia sana bro simu haipatikani. Mkojo unazidi kubana na ndani hakuna hata chupa. Nikachungulia tena nikawaona wako mbali kidogo nikachomoka kama mkuki mpaka chooni, yalikuja kwa kasi yakaanza kuparua mlango. Wakat nataka nirudi nkayaona yamesimama kwa mbali kidogo yapo serious sio mchezo, nikayachekiii nikaanza kuambaa ambaa na fence kuutafuta mlango wa geto, nayo yakaanza ku move kunifata. Nikajisemea hapana hii sio ishara nzuri nikarudi mbio mpaka chooni, majamaa yakaja speed mpaka pale mlangoni yanaunguruma mixa kuparua mlango.Nilienda na simu chooni, piga sana simu ya jamaa haipatikani nikajisemea leo nimeisha[emoji16]. Nikavuta ndoo ya chooni nikakaa kuanzia saa 9 hivi kuelekea 10mpaka 12 hadi nikapitiwa na usingizi na ile baridi sio poa. Nashukuru Mungu choo kilikuwa kisafi.

.......hapo sijaelezea tukio lengine la kukimbizwa na hao mbwa kidogo ning'atwe hawakuwa wamefungwa vizuri plus kukojoa mlangoni.....

Asubuhi baada ya kuyafungia namimi ndio nikajifanya natoka chooni, yule mzee akaniuliza umeingia chooni saa ngap sijakuona?! I was pissed off sikutaka hata kumwambia yaliyonikuta maana mjadala ungekuwa mrefu na sikuwa n huo mda wa kuanza kuoneana huruma, kwanza nausingiz/kichwa kinauma na hapo nafikiria kama naweza pata bus la saa mbili au la[emoji1787]. Jioni yake nikaaga kesho narud kwetu, mzee akamaind sana akapiga simu nyumbani sikubadili maamuzi. Kesho yake asubuhi nikasepa!

Zile siku chache nilizokaa pale ndani zilikuwa ni mateso, wale mbwa walinikosesha raha kabisa hasa usiku. Maana mda wote ilibidi niangalie huku na huku nijue wako wapi kabla sijafanya movement kama vile navuka barabara maana wana eneo kubwa. Na hadi leo sijawahi kwenda tena!
Japo niliwapendea ile tough and aggressive looking yao lakini haiondoi ukweli kwamba mimi na mbwa bado haziivi kivileee.

View attachment 2693982
Sasa mkuu ulishindwa nn hata kutayarisha chupa Usiku kabla yakulala napo ulikua unazembea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh ila ndugu wa mume jamani kuishi nao yataka moyo.nimekuja kugundua kwanini watu wengi wanaishi na ndugu zao kuliko ndugu wa mume.nikiishi na mdogo wangu namtuma nitakavyo hata nguo zangu nampa anifulie hutomsikia kunung'unika, ndugu wa mume mtume hata mara moja ukoo wao mzima watajua . Nako hapa naishi na wifi yangu kaachika kwa mume wake yaani ni kero jamani nyumba imekuwa kama na wanawake wawili mimi napanga kipikwe hiki yeye anapika kile mavyakula anapika mengi anaishia kumwaga yaani ilimradi fujo.hapa napanga na mimi niondoke niende kuishi kwa kakaangu
Ili nawewe ukavuruge ratiba ya msosi ya wifi yako hahahahaha
 
Mume anayefanya hayo sio bure atakuwa na matatizo. Au ndugu wa mke hawana nidhamu.
Hapana ni uchoyo tu, kuna ile mke akipata shida ni atajua mwenyewe yeye kaoa mke mmoja si ukoo, hivi mke anajiskia vipi kuhudumia ndugu wa mme!
 
Back
Top Bottom