Uliza ujibiwe kuhusu madini, gesi na mafuta


mwenye shamba
swali
1.ni vifaa gani vyenye bei nafuu ambavyo mchimbaji mdogo anaweza kuvitumia kugundua madini yaliyopo aridhini?
jibu

kunachangamoto hiyo mwenye shamba, kwa kuwa umeuliza kutoka geita nafikiri madini unayoamanisha ni dhahabu.
kwakifupi dhahabu huwa ni vitu vigodovidogo sana kulinganisha na ukubwa wa mwamba hivyo kwa dhahabu za kwenye mwamba hakuna kifaa moja kwa moja kinaweza kukwambia kuwa kunadhahabu nyingi kiasi gani au kina gani utazipata. ila kunanjia za kuweza kutafiti kwa garama kidogo kwa wachimbaji wadogowadogo. kwa dhahabu za mwamba uliooza na kusambaa juu ya aridhi(kanda ya ziwa wanaita dhahabu za sesa) kunakifaa kinaitwa gold detector ndiyo kinaweza kungundua zilipo na zenyewe ziwe kwa wingi kwerikweri vinginevyo hata zenyewe huwezi kuzigunduz. kifaa hivi vipo vya modeli tofauti tofati vinauzwa kuanzia 5milion hadi hata 40million. hiki kifaa hakiwezi kupima dhahabu ya kwenye mwamba japokuwa sasa kunatechnolojia nyingi zinzatengenezwa lakini hakuna kifaa kinachoweza kufanya kazi kwa ufanisi kwa kuonesha mwamba ulipo kwa usahihi.
njia zinazoaminika hadi sasa kutafiti dhahabu kwa wachimbaji wadogo wadogo ni hii hapa lakini kwa miamba iliyitokeza juu ya aridhi.
kupiga sample za sesa(dhahabu za mwamba ulioza na kusambaa aridhini). hivyo ukigundua zilipo dhahabu za namna hii ujue kunamwamba karibu hivyo unaweza kufatilia kwa kupiga sample kuelekea zinakokwenda hadi zinaweza kukufikisha zilikotokea




tanzama picha hapo ukiwa na kalai lako na maji nunaweza kuutafuta mwamba uliosambaza dhahabu kutoka bondeni kuelekea mlimani kwani hii inamaana kama umekuta kuna dhahabu bondeni jaribu kuangaria kuelekea juu mlimani


hebu tazama picha hapo juu rangi nyekundu inaonesha mwamba wa dhahabu ambapo kwa juu umeoza na kuanza kusambaa


hapo juu unaweza ona mwamba huo wa dhahabu ulivyooza na kusambaza dhahabu maeneo ya karibu. hivyo ukiwa makini na karai yako unaweza tafuta mwamba wa dhahabu ulipoanzia na kugundua. hivyo hii ndiyo njia yenye garama na fuu sana kwa mchimbaji mdogomdogo. Ila lazima pia uwe na uzoefu wa madini ya dhahabu na miamba yake. na hili kwa mchimbaji mdogo mdogo ni kitu cha kawaida.

SWALI
2.katika machimbo madogo madogo mule ndani ya mashimo kunawakati huwa kunazuka gas hatari ambayo huua na kukausha.je[a]gas hii husababishwa na nn? je kama watalaamu na watafiti hamuoni kuwa geita inapaswa kufanyiwa utafiti wa gesi kutokana na kiashiria hicho?[nipo tayari kuwapeleka ktk eneo husika]

JIBU
mwenye
shamba
gas unayoiona mashimoni ni gas ya ukaa (carbon monoxide) na siyo sawa na gasi inayozungumuziwa mtwara na lindi
kama umewahi kusikia kuwa usilale na jiko la mkaa ndani likiwa linawaka ni hatari litakusababishia kufa kiailensa( huuwa na kukausha). hii ndiyo gas ya carbon monoxide hiyo pia kutokea wakati mkaa unaungua kwenye jiko ila hautuasili katika mazingira nyenye hewa nyingi kila siku watu wakiwa wanapika .
mwenye shamba labda nikueleze husababishwa na nini shimoni( chazo cha gas hii machimoni ni nini?)

1) huko kanda ya ziwa huwa kunamiamba inayoambatana na dhahabu huwa ina aina ya mawe ambayo yana carbonate hivyo huwa yanapata joto na kusababisha kutoa hewa ya carbon monoxide(gas ya ukaa) hasa wakati wa kulipua migodini kwani husababishia moto kutokea hata kama bila kulipua kama shimo limebana sana inaweza sumbua sana hiyo gas

2) pia kutumia mitambo inayotoa moshi humo shimoni nayo husababisha gas hiyo kujaa mgodini humo

njia ya kuepukana na tatizo hilo ili uendelea kula pesa ya dhahabu inayotoka kwenye shimo lako.

1) kuweka mashiyo ya hewa ya kutosha kwenye mgodi ili hewa iingie ya kutosha( good ventilation) hii njia hutibu kwa hewa hii kwa njia ya kikemia. yaani hewa ya ukaa +hewa ya oxjeni unapata hewa ya corbon dioxide ambayo sawasawa na hewa tunayopua binadamu.(Co + O = CO2)

2) Weka mtambo wa kuingiza hewa safi shimoni. mfano wengine wanatumia upepo wa copresa ili kuingiza hewa shimoni na pia kunamitambo mahususi kwa ajili ya kuingiza hewa shimoni.


swali
3.katika uchenjuaji wa dhahabu wa wachimbaji wadogo,kemikali ya zebaki/mecury hutumika kukamatisha dhahabu iliyopo katika mchanga ulioragwa karashani.kwa bahati mbaya kemikali hii imeonekana kuwa na madhara ya kiafya na pia kuacha dhahabu nyingi kwenye mcianga.je, hakuna njia nyingine nzuri ya kukamatisha dahabu?.

jibu


nikweri zebaki ni hatari kwa afya tena mbaya mno lakini ubaya wake hasa ni sawa na ugonjwa wa HIV kwani zebaki haiui papo kwa papo. ninaomba nikueleze kuwa zebaki hata kama ikiwagwa sehemu harafu ukapanda mchicha inaweza kuingia kwenye mchicha na ukiuchuma ukaula utaipata mwilini, pia ikiingia kwenye mkondo wa maji inaweza safiri hadi hata ziwani na samaki akiila nawe ukija kumula samaki utaipata mwilini mwako, pia ukiikamata ukiwa na kidonda inaweza kukuingia mwilini mwako. na wale wanoochoma dhahabu kwenye moto sehemu isiyo nahewa yakutosha mvuke wake utakuingia na unaharibu ubongo .
pia ni kweri mercury huacha dhahabu nyingi kwenye mchanga. lakini naomba nikukumbushe kuwa siyo mercury inayosambabisha dhahabu ibaki kwenye mchanga bali ni njia ya uoshaji wa mchanga wa dhahabu. kwani mwenye shaba mercury hutumika kukamatishia tu na hii ni hatua ya mwisho ambayo huwa umebaki na mchanga wa takilibani ndoo moja ya lita20 kutoka kwenye michanga wa viloba 300(kiloba ni mifuko ya kilo 50 iliyojazwa unga uliosangwa kalashani).





mwenye shamba huo ndio mtambo wa kuoshea dhahabu kwa wachimbai wadogowadogo (gold washing plant for small scale) kwa kingereza mtambo huu unaitwa sluice box

Hivyo dhaahabu nyingi hubaki kwenye mchanga ( marudio, senate na kwa kimombo tunaita tailling) siyo kwa sababu ya zebaki(mercury) bali kwa sababu ya mtambo wetu huu wa kuoshea siyo mzuri na umepitwa na wakati.
kutokana na hili ndiyo maana kunanjia nyingine za kuweza kupata dhahabu iliyobaki kwenye mchanga huko kanda ya ziwa tunaita kuozesha (yaani kutumia asidi iitwayo cynide) na ndiyo maana mchanga uliooshwa unanunuliwa kwa bei kubwa sana na wanaenda kuozesha na kupata dhahabu iliyobaki na njia hii kwa kilataalamu tunaiita cynide leaching. migodi mikuwa ndiyo wanatumia njia hii ila inakuwa tofauti kidogo njinsi ya mitambo yao inavyofanya kazi ( na hiki kitendo cha kuosha mchanga ili kupata zahabu ndiyo tunaita kuchenjua)

mwenye shamba mchanga unaobaki wenye madini baada ya kuosha ndiyo unaenda kukamatishwa na mercury na mchang huu ni kidogo sana hivyo huwezi kusingizia mapato yako mgodini ni kidogo kutokana na mercury bali ni kidogo kutokana na mtambo wa kuoshea wa kizamani

MWENYE shamba mitambo ya kisasa ipo ila inahitai pesa
mfano ya plant iliyojengwa busolwa huko Geita







mwenye shamba nafikili utakuwa umenielewa hapo.


swali

4.OMBI:HUKU GEITA ndani ndani kata ya lwamgasa kunasehemu kunamawe yenye shaba nyingi sana.yaani nyingi kweli kweli.kama kunanamna ningependa kuwakaribisha ktk utafiti wa shaba.ahsanteni.

Ombi lako limepokelewa ninaratiba ya kutembela huko kwani huko mimi ni nyumbani nitakutafuta nikija GEITA ili niweze kuona eneo lako hilo la shaba.

ASANTE SANA KWA MASWALI KAMA HUJAELEWA UNAWEZA NIULIZA TENA.
 
mwenye shamba angalia video ya mtambo wa kuoshea wa uliofungwa busolwa geita. kwa wachimbaji wadogowadogo ndio tunatumia mtambo wa mbao kama huu hapa. unaweza ona tofauti na kwa nini tunapata dhahabu kidogo na nyingine kubaki kwenye mchanga




mwenye shamba mtambo huu ni matambo wa kuchenjulia dhahabu kwa wachimbaji wadogowadogo. na mtaombo uliopo kwenye video nao pia ni mtambo wa kuchenjulia dhahabu kwa wachimbaji wa kati.
 

Attachments

Kweli ruby garnet uko deep sana kwenye geology bravo sana. Mi nauliza kwa mkoa wa singida maeneo ya mlima sekenke nilikuwahi sikia kuna dhahabu na wachimbaji wadogo walianza kuchimba kabla ya serikali kuzuia, sasa ni kwanini serikali ilizuia na kwanini mpaka leo hatuoni uchimbaji ukiendelea? Na eneo lingine ni morogoro milima ya uruguru napo nilisikia uchimbaji ulianza mara ghafla serikali ikazuia,hili la serikali kuzuia uchimbaji ni nini sababu?
Asante
 
Wana JR uliza swali lako lolote kuhusu madini, mafuta na gas, kuanzia njisi yanavyojitengeneza ardhini, kufanyiwa utafiti, kuchibwa hadi kuuzwa nawe utajibiwa na mtaalamu wako hapo.
Mkuu naomba unijuze asili ya maeneo yanayopatikana Dhahabu.

Kwa hapa tanzani ni sehemu zipi zinasifika kwahiyo Dhahabu zinazoweza kuwa detected umbali usiozidI ft. 5
 
nina degree ya Bsc in geology from UDSM. toka nihitimu nafanya uchimbaji mdogomdogo wa madini. na pia huwa natoa ushauri kwa wachimbaji wadogowadogo wa madini.
 
nina degree ya Bsc in geology from UDSM. toka nihitimu nafanya uchimbaji mdogomdogo wa madini. na pia huwa natoa ushauri kwa wachimbaji wadogowadogo wa madini.
 
Mimi ndo nasomea sasa hivi hapo hapo UDSM ila ninachukua shahada wa uhandisi uchenjuaji na metali (bsc in metallurgy and mineral processing engineering) umenikosha sana kwa jinsi unavyojibu maswali
nina degree ya Bsc in geology from UDSM. toka nihitimu nafanya uchimbaji mdogomdogo wa madini. na pia huwa natoa ushauri kwa wachimbaji wadogowadogo wa madini.
 
OK. sawa. kunabaazi ya kozi tulikuwa tunachangia nao watu wa mineral processing na mining kama GY100. PIA MT161, MT271 NA ZINGINE NYINGI. KAZA buti. but mtaani ajira zimekuwa ngumu. kwa hiyo wakati unasoma uwe unajiuliza swali kuwa yale unayoyasoma utaenda kuyafanyia kazi gani na wapi?
 
Nimefurahi sana kwa hii thread ruby garnet, binafsi ni mchimbaji mdogo wa dhahabu tumechimba bila mafanikio kwa muda mrefu na gharama kubwa. Ningeombaa ushauri kwako kama mtaaramu nikutumie pictures za mwamba turiopo kwa sasa iweze kutoa msaada kama ikiwezekana. Nipe green light nizipost Sir
 
mkuu serikali huzuia maeneo kwa sababu kuu mbili
1. kunaleseni ya mtu mwingine mahali hapo. hasa hizi leseni kubwa za utafiti huwa zinachukua eneo kubwa sana na wakati mwingine mhusika anaweza akaiomba na akapewa but asianze kuifanyia kazi mapema hivyo watu wengine huona labda eneo hilo halina mmiliki. mfano jaribu kutazama picha hii


unaweza ona picha rangi ya njano ni alama ambapo kuna leseni za utafiti (Pl). tazama zilivyojaa singida. hivyo wewe unaweza enda chimba mahala unafikri pako wazi. hii picha ni ya tarehe 31/08/2017. hivyo hadi sasa lesni zimejaa sana

2. kunasehemu za hifazi na vyazo vya maji huwa hapajimbwi mpaka vibali maalumu hivyo hata kama madini yakitokea munafukuzwa.
hizo sababu mbili ndiyo zinaifanya serikali iwafukuze wachimbaji wadogo wadogo. hasa kwenye sababu ya kwanza ndiyo mara nyingi huwa sababu ya kuwafukuza

KWA NINI HUONI WAKIYACHIMBA HAYO MAENEO?
Unahitaji kati ya 2-7 years utafiti tu. tena mkuu inahitaji millions of dollar kukamilisha hizo tafiti.
 
pole sana mkuu hii biashara ina risk kubwa sana. na hivyo usikate tamaa. ipo siku utatoka tu. but unahitaji uzoefu wa kazi hii.
 
Mkuu naomba unijuze asili ya maeneo yanayopatikana Dhahabu.

Kwa hapa tanzani ni sehemu zipi zinasifika kwahiyo Dhahabu zinazoweza kuwa detected umbali usiozidI ft. 5
mkuu zahabu zinapatikana hasa maeneo ya kanda ya ziwa pamoja mbeya bila kusahahu mkoa wa mpanda. sehemu hizi ndiyo zinafaa kwa uchimbaji mkubwa. but kwa mdogomdogo ni sehemu zote za tanzania unaweza pata na kuchimba

ni vigumu kukuambia zinapatikana wapi kwenye kina cha ft5.
mkuu dhahabu ni pesa na pesa popote pale ikipatikana imemwagwa ni vita kuichota. hautakaa usikie unaambiwa nenda sehemu fulani utakuta dhahabu ft5. kama unataka gold katafute mkuu kwa kutumia pesa, muda bila kusahau utaalamu wako.
 
madini ni utajili mkubwa ukiyafahamu na kuyafanyia kazi vizuri
 

Sasa nimekuelewa mkuu,, ila ulipotea sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…