Umaskini ni laana; nimeamini pia maskini ana roho mbaya sana

Umaskini ni laana; nimeamini pia maskini ana roho mbaya sana

Hizo kazi unafanya mwenyewe? Hamjui humu ndani kuna wau wa aina gani na kazi tunazofanya, hiyo serikali unayoiba hivyo labda ya Congo, sisi tuna CPA zile za miaka ambayo wewe unasoma standard 3, na tunajua mifumo haswa, umetudharau sana wewe mjinga
Nimekwambia haina haja ya kujieleza nafanya nini mkuu. Amini unachoamini ila nilichoandika ndio ukweli wangu
 
Ha ha ha, serikalini? 3m kwa siku? Labda kama wewe ni waziri, Pima, Mkurugenzi wa Arusha yuko Magereza kwa sababu ya hela chini ya 120m, ambazo amezitoa kijanjanja kwa ukandarasi, wewe unaondoka na 3m kila siku, mi Tanzania mijinga sana
Kasema hayuko Serikalini
 
Hiki niandikacho ni kisa cha kweli na ndicho ninachopitia.

Nikiri kwamba nimezaliwa kwenye umaskini na nimesomeshwa kwenye umaskini mpaka namaliza elimu yangu

Nilisota kidogo tu kitaa baada ya kumaliza elimu nikapata kazi sehemu nikaajiriwa, baada ya mda kutokana na Tabia yangu ya ukimya na usiri mkuu wangu wa kazi akanihamishia idara ambayo baadae nilikuja kujua ni sehemu yenye michongo mingi ya pesa.

Nikafundishwa kazi, nikaiva. Hela zipo idara hii bwana, kwa Siku nilikuwa nikitoka kazini mfukoni kuna 3+m kama hamna hamna sana nina 1+m.

Ndani ya miezi 3 nikiwa pale nikawa niko vizuri nikanunua uwanja sehemu yenye hadhi kidogo heka 3 nikaweka mansion yangu ikiwa na uwanja wa basebal na netbal ikiwemo sehemu za kucheza watoto na mabwawa ya kuogelea.

Mpaka huu mjengo unakamilika nilitumia zaidi ya 400+m, siku nawapeleka wazazi na ndugu hawakuamini kutokana na mazingira niliyotoka na namna nilivo mkimya. Sikuishia hapo wadogo zangu tumbo moja wote nilianza mchakato wa kuwajengea nyumba kila mmoja yake na nikafanikisha nyumba nzuri za kisasa ambazo wastani nilitumia 120+m

Ndugu zangu wote nilitoa msaada kwao bila kubagua, watoto ambao walikuwa wamefeli shule niliwapa uchaguzi wanachotaka wanawafanyia, nimetoa mitaji nimepeleka vyuo vya ufundi natimiza mahitaji yao kila kitu maana hela ninayo na sioni fahari ya kuabudiwa.

Sasa baada ya miaka 6 kuona nazidi kuwekeza kwa kasi ileile tu, mashangazi wakaanza za chinichini huyu jamaa ni Freemason mimi nikiwa sijui chochote. Kuna kipindi msiba ulitokea, Mke wa mtoto wa shangazi alifariki kulingana na majukumu yangu ule msiba sikufika ila nilibeba gharama zote za msiba.

Bwana kama miezi 6 hivi za msiba kupita, napata habari k kumbe watu wanachukuzwa na mafanikio, mashangazi wanapanga mipango ya kunidhuru kwa mda mrefu na mmoja aliyepewa majukumu ya kuchukua baadhi ya vitu kwenye mwili ikawa mlopokaji akanipa mchongo wote, wala sikuvumilia nikawawashia Moto mashangazi kufatilia kumbe baba zangu baadhi wanazo habari za hii mipango na wakanyamaza. Imenitia hasira sana.

Wanasema nimemuua yule mke wa binamu yangu na moja ya masharti niliyopewa ni kuwa na roho nzuri ya kuwasadia kwa hiyo nao wanataka kulipa kisasi kwa kunidhuru. Nina hasira na hawa watu Moto niliowawashia nimejikuta nawatukana mpaka matusi ya nguoni.

Natamani siku zirudi nyuma nisingefanya huu ujinga wa kusaidia hawa wanaoitwa ndugu, huku tunakoelekea naona kabisa kuna dalili mbaya kisa mafanikio yangu

Nimeongeza nguvu zaidi upande wa mama, huko nawajengea majumba ya maana.. Sasa naona wivu waziwazi mpaka watoto wao niliowasaidia kwa hali na mali.
Laana hapana.
Roho mbaya ni kweli tunayo.
 
Kasema hayuko Serikalini

Ngoja nikupe facts:

- org yeyote au biashara ambayo mtu anaweza chukua 3m/day un noticed, baada ya kufanya kazi kwa miezi 3, ina maana anachukua about: 70m/month. Tupunguze tuweke 50m/month.

- Biashar ambayo mtu aliyefanya kazo kwa miezi 3 mwenye uwezo wa kuiba minimum of 50m a month, un noticed it is a mult milionear business, with billions of money.

- Biashara ya aina hiyo lazima imewekeza sana kwenye technology, mifumo na namna zozote za ku detect fraudy, na hii inaendana na kuajiri watu compent sana.

- Kama ana uwezo wa kutoka na 3m a day, hizo hela zinatoba bank? Ni petty cash? Ni sales au chanzo chake ni nino, ili ufanikiwe kuiba kiwango hicho, lazima ushirikiane na watu si chini ya wa 5, kama yeye ama miezi 3 anaondoka na 3m, hao wazamani wanaondoka na ngapi?
 
"Ndani ya miezi 3 nikiwa pale nikawa niko vizuri nikanunua uwanja sehemu yenye hadhi kidogo heka 3 nikaweka mansion yangu ikiwa na uwanja wa basebal na netbal ikiwemo sehemu za kucheza watoto na mabwawa ya kuogelea"

Hakuna office yenye books of account na excel uondoke na 3m cash kila siku kirahisi, labda kama wana bustani ya kulima noti na hiyo bustani wewe ndo unapalilia noti zikizingirwa na magugu
Hili usilibishie, inawezekana.
 
Sawa,wewe endelea kutekeleza majukumu yasiyo kuhusu. Naona hapo bandarini kitengo cha makasha kime kupa upofu.
Hiki niandikacho ni kisa cha kweli na ndicho ninachopitia.

Nikiri kwamba nimezaliwa kwenye umaskini na nimesomeshwa kwenye umaskini mpaka namaliza elimu yangu

Nilisota kidogo tu kitaa baada ya kumaliza elimu nikapata kazi sehemu nikaajiriwa, baada ya mda kutokana na Tabia yangu ya ukimya na usiri mkuu wangu wa kazi akanihamishia idara ambayo baadae nilikuja kujua ni sehemu yenye michongo mingi ya pesa.

Nikafundishwa kazi, nikaiva. Hela zipo idara hii bwana, kwa Siku nilikuwa nikitoka kazini mfukoni kuna 3+m kama hamna hamna sana nina 1+m.

Ndani ya miezi 3 nikiwa pale nikawa niko vizuri nikanunua uwanja sehemu yenye hadhi kidogo heka 3 nikaweka mansion yangu ikiwa na uwanja wa basebal na netbal ikiwemo sehemu za kucheza watoto na mabwawa ya kuogelea.

Mpaka huu mjengo unakamilika nilitumia zaidi ya 400+m, siku nawapeleka wazazi na ndugu hawakuamini kutokana na mazingira niliyotoka na namna nilivo mkimya. Sikuishia hapo wadogo zangu tumbo moja wote nilianza mchakato wa kuwajengea nyumba kila mmoja yake na nikafanikisha nyumba nzuri za kisasa ambazo wastani nilitumia 120+m

Ndugu zangu wote nilitoa msaada kwao bila kubagua, watoto ambao walikuwa wamefeli shule niliwapa uchaguzi wanachotaka wanawafanyia, nimetoa mitaji nimepeleka vyuo vya ufundi natimiza mahitaji yao kila kitu maana hela ninayo na sioni fahari ya kuabudiwa.

Sasa baada ya miaka 6 kuona nazidi kuwekeza kwa kasi ileile tu, mashangazi wakaanza za chinichini huyu jamaa ni Freemason mimi nikiwa sijui chochote. Kuna kipindi msiba ulitokea, Mke wa mtoto wa shangazi alifariki kulingana na majukumu yangu ule msiba sikufika ila nilibeba gharama zote za msiba.

Bwana kama miezi 6 hivi za msiba kupita, napata habari k kumbe watu wanachukuzwa na mafanikio, mashangazi wanapanga mipango ya kunidhuru kwa mda mrefu na mmoja aliyepewa majukumu ya kuchukua baadhi ya vitu kwenye mwili ikawa mlopokaji akanipa mchongo wote, wala sikuvumilia nikawawashia Moto mashangazi kufatilia kumbe baba zangu baadhi wanazo habari za hii mipango na wakanyamaza. Imenitia hasira sana.

Wanasema nimemuua yule mke wa binamu yangu na moja ya masharti niliyopewa ni kuwa na roho nzuri ya kuwasadia kwa hiyo nao wanataka kulipa kisasi kwa kunidhuru. Nina hasira na hawa watu Moto niliowawashia nimejikuta nawatukana mpaka matusi ya nguoni.

Natamani siku zirudi nyuma nisingefanya huu ujinga wa kusaidia hawa wanaoitwa ndugu, huku tunakoelekea naona kabisa kuna dalili mbaya kisa mafanikio yangu

Nimeongeza nguvu zaidi upande wa mama, huko nawajengea majumba ya maana.. Sasa naona wivu waziwazi mpaka watoto wao niliowasaidia kwa hali na mali.
 
Ngoja nikupe facts:

- org yeyote au biashara ambayo mtu anaweza chukua 3m/day un noticed, baada ya kufanya kazi kwa miezi 3, ina maana anachukua about: 70m/month. Tupunguze tuweke 50m/month.

- Biashar ambayo mtu aliyefanya kazo kwa miezi 3 mwenye uwezo wa kuiba minimum of 50m a month, un noticed it is a mult milionear business, with billions of money.

- Biashara ya aina hiyo lazima imewekeza sana kwenye technology, mifumo na namna zozote za ku detect fraudy, na hii inaendana na kuajiri watu compent sana.

- Kama ana uwezo wa kutoka na 3m a day, hizo hela zinatoba bank? Ni petty cash? Ni sales au chanzo chake ni nino, ili ufanikiwe kuiba kiwango hicho, lazima ushirikiane na watu si chini ya wa 5, kama yeye ama miezi 3 anaondoka na 3m, hao wazamani wanaondoka na ngapi?
Ungeamini unachoamini ingekuwa vizuri zaidi lakini nikuambie tu bado huelewi mambo mengi. Tufanye kwamba nilichoandika hapa ni uongo ili tuufunge huu mjadala wako
 
Ngoja nikupe facts:

- org yeyote au biashara ambayo mtu anaweza chukua 3m/day un noticed, baada ya kufanya kazi kwa miezi 3, ina maana anachukua about: 70m/month. Tupunguze tuweke 50m/month.

- Biashar ambayo mtu aliyefanya kazo kwa miezi 3 mwenye uwezo wa kuiba minimum of 50m a month, un noticed it is a mult milionear business, with billions of money.

- Biashara ya aina hiyo lazima imewekeza sana kwenye technology, mifumo na namna zozote za ku detect fraudy, na hii inaendana na kuajiri watu compent sana.

- Kama ana uwezo wa kutoka na 3m a day, hizo hela zinatoba bank? Ni petty cash? Ni sales au chanzo chake ni nino, ili ufanikiwe kuiba kiwango hicho, lazima ushirikiane na watu si chini ya wa 5, kama yeye ama miezi 3 anaondoka na 3m, hao wazamani wanaondoka na ngapi?
Haina haja kubishania hayo.

Ukienda kampuni za madini ndio utajua watu wanapiga hela
 
Back
Top Bottom