Umaskini ni laana; nimeamini pia maskini ana roho mbaya sana

Umaskini ni laana; nimeamini pia maskini ana roho mbaya sana

Hata kama hii hadithi siyo ya ukweli, lakini Themes zake zina ukweli. Jamii za watu masikini zina watu wenye roho mbaya mno mnooo.
Nakubali.

Kimahesabu kwa mwezi kwa 3+, anakunja 90M,kwa mwaka anaweka 1.08B. Nawaza hata kama ni michongo hii michongo gan.
 
Usidhani kama unaweza kujua kila kitu kwa wakati wote. Anyway ungejua tu hata mfagiaji wa sehemu ninapofanyia kazi ungekuja kufuta haya maandishi yako

Sijakataa kuwa unaweza kuwa unaweza kuona hizo Pesa. Tatizo linakuja kwenye Kanuni za wizi ndio wadau hapo wanaona Stori imepikwa.
Milioni tatu Kwa Siku sio mchezo sheikhe, tena uibe kila Siku hivyo ndani ya mwezi Una milioni 60.
Na hapo ofisini haupo pekeako, sijajua idadi ya wakubwa wako wapo wangapi, nao kila mmoja wachukue tuseme 100m+ Kwa mwezi.
Wizi WA kila Siku labda ufanyike kwenye miamala ya Pesa yaani iwe zaidi kieletroniki na Huko ni rahisi mfumo kushtukia.

Wizi salama ni ule wa kupiga mapigo ya kushtukiza hasa Kwa Watu walioajiriwa kama wewe na msio na mamlaka
 
Sijakataa kuwa unaweza kuwa unaweza kuona hizo Pesa. Tatizo linakuja kwenye Kanuni za wizi ndio wadau hapo wanaona Stori imepikwa.
Milioni tatu Kwa Siku sio mchezo sheikhe, tena uibe kila Siku hivyo ndani ya mwezi Una milioni 60.
Na hapo ofisini haupo pekeako, sijajua idadi ya wakubwa wako wapo wangapi, nao kila mmoja wachukue tuseme 100m+ Kwa mwezi.
Wizi WA kila Siku labda ufanyike kwenye miamala ya Pesa yaani iwe zaidi kieletroniki na Huko ni rahisi mfumo kushtukia.

Wizi salama ni ule wa kupiga mapigo ya kushtukiza hasa Kwa Watu walioajiriwa kama wewe na msio na mamlaka
Sijaandika kubishana, nimeandika ukweli wangu..Mimi wangu ndio huo kaka kama unaona ni uongo ni vema pia maana sipo hapa kukufanya uamini?

Na sidhani kama kuna sehemu nimezungumzia wizi? Nilichosema ni kwamba natoka na zaidi ya 1m kwa siku. Ishu napataje hiyo wewe hutakiwi kujua

Vinginevyo unaweza kuamini unavyoamini
 
Mkuu wewe una roho ya kipekee na ukifa hautooza, na wewe ni mbinguni moja kwa moja hebu achana na hao ndugu zako wewe nifanyie mpango elfu mbili ya ulanzi na msikaki wa buku hapa mwangata, usafiri sikusumbui nitatembea kwa mguu tu sio mbali kufika kilabuni
 
Usidhani kama unaweza kujua kila kitu kwa wakati wote. Anyway ungejua tu hata mfagiaji wa sehemu ninapofanyia kazi ungekuja kufuta haya maandishi yako
Mkuu nitafutie hata kufagia choo watu tunashida hatutakuangusha bhana tuna njaa hatujala tangu Jana jioni hii tena ugali sijui nitapata wapi sio wote hatuna shukrani ni neema Bado haijatushikia. Fanya mpango hata wa kamtaji mkuu
 
Pole sana mkuu, nimegundua wewe ni mtu mwema sana...[emoji41]
Sasa ebu fanya hivi.....
Kama itawezekana naomba ufanye mpango unitumie 20k ili walau nikanunue debe la mahindi na kilo moja ya dagaa, kuni nitajisumbukia...[emoji17]
Hutaki kujengewa nyumba na ww
 
Mpe na lipa namba kabisa ili iwe rahisi mkuu kuna mwenzio aliomba ya Smart Gin kimasihara tu akatumiwa kwenye namba yake kupitia NMB hapo hapo kwa hio changamkia fursa weka namba haraka sana uwekewe mpunga
Upo sahihi kabisa mkuu...
Tigo wakala ni 537797 Ashraf Abdallah...😊
M-pesa wakala ni 876134 Ashraf Abdallah....😋
 
Hiki niandikacho ni kisa cha kweli na ndicho ninachopitia.

Nikiri kwamba nimezaliwa kwenye umaskini na nimesomeshwa kwenye umaskini mpaka namaliza elimu yangu

Nilisota kidogo tu kitaa baada ya kumaliza elimu nikapata kazi sehemu nikaajiriwa, baada ya mda kutokana na Tabia yangu ya ukimya na usiri mkuu wangu wa kazi akanihamishia idara ambayo baadae nilikuja kujua ni sehemu yenye michongo mingi ya pesa.

Nikafundishwa kazi, nikaiva. Hela zipo idara hii bwana, kwa Siku nilikuwa nikitoka kazini mfukoni kuna 3+m kama hamna hamna sana nina 1+m.

Ndani ya miezi 3 nikiwa pale nikawa niko vizuri nikanunua uwanja sehemu yenye hadhi kidogo heka 3 nikaweka mansion yangu ikiwa na uwanja wa basebal na netbal ikiwemo sehemu za kucheza watoto na mabwawa ya kuogelea.

Mpaka huu mjengo unakamilika nilitumia zaidi ya 400+m, siku nawapeleka wazazi na ndugu hawakuamini kutokana na mazingira niliyotoka na namna nilivo mkimya. Sikuishia hapo wadogo zangu tumbo moja wote nilianza mchakato wa kuwajengea nyumba kila mmoja yake na nikafanikisha nyumba nzuri za kisasa ambazo wastani nilitumia 120+m

Ndugu zangu wote nilitoa msaada kwao bila kubagua, watoto ambao walikuwa wamefeli shule niliwapa uchaguzi wanachotaka wanawafanyia, nimetoa mitaji nimepeleka vyuo vya ufundi natimiza mahitaji yao kila kitu maana hela ninayo na sioni fahari ya kuabudiwa.

Sasa baada ya miaka 6 kuona nazidi kuwekeza kwa kasi ileile tu, mashangazi wakaanza za chinichini huyu jamaa ni Freemason mimi nikiwa sijui chochote. Kuna kipindi msiba ulitokea, Mke wa mtoto wa shangazi alifariki kulingana na majukumu yangu ule msiba sikufika ila nilibeba gharama zote za msiba.

Bwana kama miezi 6 hivi za msiba kupita, napata habari k kumbe watu wanachukuzwa na mafanikio, mashangazi wanapanga mipango ya kunidhuru kwa mda mrefu na mmoja aliyepewa majukumu ya kuchukua baadhi ya vitu kwenye mwili ikawa mlopokaji akanipa mchongo wote, wala sikuvumilia nikawawashia Moto mashangazi kufatilia kumbe baba zangu baadhi wanazo habari za hii mipango na wakanyamaza. Imenitia hasira sana.

Wanasema nimemuua yule mke wa binamu yangu na moja ya masharti niliyopewa ni kuwa na roho nzuri ya kuwasadia kwa hiyo nao wanataka kulipa kisasi kwa kunidhuru. Nina hasira na hawa watu Moto niliowawashia nimejikuta nawatukana mpaka matusi ya nguoni.

Natamani siku zirudi nyuma nisingefanya huu ujinga wa kusaidia hawa wanaoitwa ndugu, huku tunakoelekea naona kabisa kuna dalili mbaya kisa mafanikio yangu

Nimeongeza nguvu zaidi upande wa mama, huko nawajengea majumba ya maana.. Sasa naona wivu waziwazi mpaka watoto wao niliowasaidia kwa hali na mali.
Kitu kidogoo sana hicho.. endelea kula maisha. Una thawabu nyumbani.

Ila kawaombe msamaha hayo matusi nao wakuombe msamaha... Mpeane mikono muachane kwa amani.
 
Upo sahihi kabisa mkuu...
Tigo wakala ni 537797 Ashraf Abdallah...😊
M-pesa wakala ni 876134 Ashraf Abdallah....😋
Manzile fanya muamala hapo namba hizo ushapewa jamaa anataka umrushie 20,000/- tu akanunue mahindi ya ugali
 
Ndio naelewa sasa kwanini watu wengine hata wawe na pesa vp watakua radhi kuhudumia msiba na sio mgonjwa[emoji17] kweli umasikini ni laana. Kaa nao mbali lkn matusi yako hayawezi kuwafanya warudi nyuma kua makini bro
 
Manzile fanya muamala hapo namba hizo ushapewa jamaa anataka umrushie 20,000/- tu akanunue mahindi ya ugali
Hiyo inatosha na dagaa wa Mwanza kilo moja, huku mitaa yetu ya Ibologelo kuni zipo za kuokota tu..😊
 
Back
Top Bottom