Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Ana kitu Asipuuzwe!!lakini Tunaomba Sana usiwe Unatugombeza,,,alafu ukutute nae wa liwale anapambana kuja dar,,ni mifumo ya maisha ya kila siku ya wanadamu Kwa hiyo wala isikuudhi Sana,,,Utaghafilika bure na walimwengu na ya ulimwengu pia!!
 
Mimi niko Dar mwaka wa 8 sasa ni government employee . Sasa unataka niache kazi ya uhakika nikalime?
Nikitaka kulima huwa nalima mazao ya msimu Njombe viazi mviringo.

"Sasa unataka niache kazi ya uhakika nikalime"

Kwa hiyo mkuu kilimo ni cha second class citizens yani ukiona maisha yamekushinda ndio ukakimbilie kilimo

Ulichoongea ni kweli kwa asilimia kubwa lakini unatakiwa kujua kuwa, mtu maisha ya dar ya kimshinda haimaanishi akienda mkoa ndo atatoboa maana kuna wanaotoka mkoa na wanatobolea dar

Lastly, jiwekeze sana maana government officials wengi wakistaafu au kuondolewa kazini huchanganyikiwa kama si kufa kwa presha kwa sababu ya kuzoea comfortability.. Kwenye majibu yako nimeliona hilo kwa hiyo usidharau vipato vya watu na wakati ukitolewa kazini hata laki kuitafuta mtaani huwezi.. Kwa hiyo wekeza ili vya kutokea vikitokea, usije kuhadhirika
 
Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Mkuu,

Kwani ni lazima kila mtu atake unachotaka wewe?

Huelewi kwamba watu tofauti wana malengo tofauti katika maisha?

Unataka kulazimisha watu baki usiowajua waishi unavyopanga wewe?
 
Samsung na iphone zinamilikiwa na vijana wa dar tu? Mbona Tecno, infinix na Itel zinatumiwa na vijana wengi Dar es salaam..

Sasa kama wachumi wameligrade jiji la Dar kama jiji la kibiashara ambalo linaimpact kubwa kwenye uchumi wa Tanzania unaanza kudiss kwa kutumia maisha ya vijana wachache waliamua kuishi lifestyle zao.
Hakuna anaediss kuhusu Dar tunazungumzia wanaong'ang'ania dar na wakati wapo muda mrefu hawana cha maaana wanachofanya wakidhani maisha yapo hapo tu kumbe anaweza kujaribu sehemu zingine, we miaka 10+ bado unaoga kwenye bafu au choo hakina mlango inabidi mlangoni uweke shuka unalojifunika usiku sasa kwanini usiondoke hapo ukatafute maisha sehem nyingine?

Maana mikoani baadhi ya maeneo maendeleo na fursa zipo nyingi na watu wanaishi kwenye nyumba za hadhi ya kibinadam angalau haweki shuka kwenye mlango wa bafu
Nenda kahama,katoro,njombe na maeneo mengne katafute ukijiimarisha unaweza kurudi Dar ukiwa hata na mtaji
 
Hakuna anaediss kuhusu Dar tunazungumzia wanaong'ang'ania dar na wakati wapo muda mrefu hawana cha maaana wanachofanya wakidhani maisha yapo hapo tu kumbe anaweza kujaribu sehemu zingine, we miaka 10+ bado unaoga kwenye bafu au choo hakina mlango inabidi mlangoni uweke shuka unalojifunika usiku sasa kwanini usiondoke hapo ukatafute maisha sehem nyingine?

Maana mikoani baadhi ya maeneo maendeleo na fursa zipo nyingi na watu wanaishi kwenye nyumba za hadhi ya kibinadam angalau haweki shuka kwenye mlango wa bafu
Nenda kahama,katoro,njombe na maeneo mengne katafute ukijiimarisha unaweza kurudi Dar ukiwa hata na mtaji
Swali la msingi. Waliopo hizo sehemu wamefanikiwa kiasi kwamba ni guarantee asilimia 100 ukienda kahama utafanikiwa??

Jibu kama ndio basi mnachosema kipo sawa jibu kama ni hapana basi hamna hoja
 
Sahivi baadhi vijana wa daslam wameanzisha tabia ya kuwasifia wanaume wenzao wenye kipato tena wanawasifia kupita kiasi ili tu wapewe chochote wanajiita machawa mwisho nao wanalilia kuolewa
Machawa wote wamezaliwa na kukulia Kigoma labda na Kagera kidogo ila sio Dar.

Walikuja Dar kwa mbio za mwenge, Gari la mkaa au Gari Moshi Tena wakijificha chini ya viti.

Mwijaku-kigoma
Baba Level-Kigoma
Aristote-Kagera
 
Back
Top Bottom