Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Umeshawahi kusaidiwa nini na mganga ukaona kabisa mganga wako fundi?

Waganga wazushi tu niliibiwa simu ktk mazingira ya kutatanisha simu kala na gharama sn.

Ss mm sio mtu wa ulozi kama mshana jr, akaja mwanangu mmoja na kuniambia anipeleke kwa mganga hiyo simu aliyeiba atarudisha.

Tumefka kwa sangoma baada ya kuelezea shida zetu mixer akasaga majanimajani si jui ni ya aina gani akasema nichemshe ninywe simu itarudi.

Sasa nipo njiani najiuliza simu aibe mwingine mijani ya dawa ninywe mie, halafu kuna uhusiano gani Kati ya kurudi kwa simu na mm kunywa Yale majani

Aahh kudadeki niliitupilia mbali ile mijani na mpaka ss siamini ulozi na hiyo simu nishasamehe[emoji3061]



Sent from my itel W4001P using JamiiForums mobile app
Umefanya vyema mm niliibiwa vitu vya gari. Stata na vitu vingien vya miklioni2 h ila nikatulia tu nilitaka kwenda lkn naaziawapi na mm sijui hbr hzo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Baada ya kuona biashara yangu imekwama nikaongea na wenyeji wa mji, nikapelekwa kwa mganga mwanamke,

Kwanza mganga huyo akikaa anaogea kama anapokea simu au anapokea maelekezo kutoka sehemu,

Nilikutana na watu wa hadhi tofauti wanamiliki mabasi mapya na magari mengine mapya wamepeleka yakafanyiwe uchawi,

Zoezi la kwanza baada ya kujieleza akanituma nikachote maji kwenye kisima chake, hiki kisima ni maalum kwa kazi hiyo ya kiganga, kipo umbali kama wa kilometer moja kutoka mji ulipo,

Hivyo nilipewa mashariti nisigeuke hadi nikifika nyumbani kwa mganga kupeleka maji na endapo nikigeuka napaswa kurudia zoezi upya.... ila nikajikuta nimegeuka nikiwa nakaribia kufika... niling'atwa na nyuki kwelikweli,

Nikaona uvivu kurudi tena kisimani nikaamua kwenda kwa mganga na maji yale yale .. nilipofika tu akaniamba usikae wewe umegeuka (umekosea mashariti) rudia zoezi, ikanibidi nirudie[emoji23]

Tulishindwana alipoanza kuniuliza
Kabila langu, Wazazi wangu kama wapo hai, idadi ya watoto na mke, pia nichague nani nataka afahamu ninachokifanya endapo nakufa ataendeleza mali.

Nikamwambia nimegailisha zoezi kwa leo ngoja nikajitafakari upya, akanigundua namkimbia akanipa adhabu kabla sijaondoka nikanunue jogoo mkubwa zaidi ya wote nitakaemkuta kwenye cage ya wauzaji sokoni nimpelekee,

Kufika sokoni nikakuta bei mbaya nika bargain nikachukua mdogo kati ya yule mkubwa zaidi, ile kurudi kwa mganga akasema sio huyo, kamlete yule mweupe uliyemuacha[emoji23] tulisumbuana zoezi hilo mara 3 ikabidi nikubali kumnunua na kumpelekea.

Nikatoka nduki hata nyuma sikutazama tena.
 
Baada ya kuona biashara yangu imekwama nikaongea na wenyeji wa mji, nikapelekwa kwa mganga mwanamke,

Kwanza mganga huyo akikaa anaogea kama anapokea simu au anapokea maelekezo kutoka sehemu,

Nilikutana na watu wa hadhi tofauti wanamiliki mabasi mapya na magari mengine mapya wamepeleka yakafanyiwe uchawi,

Zoezi la kwanza baada ya kujieleza akanituma nikachote maji kwenye kisima chake, hiki kisima ni maalum kwa kazi hiyo ya kiganga, kipo umbali kama wa kilometer moja kutoka mji ulipo,

Hivyo nilipewa mashariti nisigeuke hadi nikifika nyumbani kwa mganga kupeleka maji na endapo nikigeuka napaswa kurudia zoezi upya.... ila nikajikuta nimegeuka nikiwa nakaribia kufika... niling'atwa na nyuki kwelikweli,

Nikaona uvivu kurudi tena kisimani nikaamua kwenda kwa mganga na maji yale yale .. nilipofika tu akaniamba usikae wewe umegeuka (umekosea mashariti) rudia zoezi, ikanibidi nirudie[emoji23]

Tulishindwana alipoanza kuniuliza
Kabila langu, Wazazi wangu kama wapo hai, idadi ya watoto na mke, pia nichague nani nataka afahamu ninachokifanya endapo nakufa ataendeleza mali.

Nikamwambia nimegailisha zoezi kwa leo ngoja nikajitafakari upya, akanigundua namkimbia akanipa adhabu kabla sijaondoka nikanunue jogoo mkubwa zaidi ya wote nitakaemkuta kwenye cage ya wauzaji sokoni nimpelekee,

Kufika sokoni nikakuta bei mbaya nika bargain nikachukua mdogo kati ya yule mkubwa zaidi, ile kurudi kwa mganga akasema sio huyo, kamlete yule mweupe uliyemuacha[emoji23] tulisumbuana zoezi hilo mara 3 ikabidi nikubali kumnunua na kumpelekea.

Nikatoka nduki hata nyuma sikutazama tena.
Na msadaa hukupata

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Ilikuwa Ujiji. Nimepigika kinyama mimi na mwanangu Q. Ghafla mbele yangu naona bango la Uganga, kwa maelekezo hakukuwa mbali na pale. Tunafika tunapisha na wateja ( kama sikosei ni mtu na wakeze ).
Yule Mganga alikuwa ni mwanamke! Basi baada ya salam akaanza makeke yake, shida zetu akazipatia Mule mule toka mwanzo wa Safari yetu mpaka ile siku tunafika kwake! Shida ikawa moja tu! Anataka 40000, sasa nikajiuliza yaani huyu Bazazi ameona yoote lakini kashindwa kujua kama hatuna ata mia? Nikamwambia fresh Mmama we tufanyie kazi sisi tutakupa 60000 sio hiyo 40000, basi ile kainuka tu kuingia ndani kuchukua madubwana yake, mimi nikakusanya pesa 45000 zilikuwa pale kwenye ungo na kinokia Obama nikamwambia Q mwanangu hii nauli tusepe. Tukatokomea hivyo yaani mpaka Mwaloni. Tukauza kale kanokia 15000 jumla tukawa na 60, tukala 7000, tukalipia boti 6000 kwa kila mmoja. Kufika mbele mbele huko kuna kijiji kipo ndani ya Gombe, mida ya saa 1:30 ile Boti inazama, tunatumbukia kwenye lile ziwa, maji naanza kuyaona meusi mwanangu hajui kuogelea anakaba shingoni anaogopa kufa, hali inazidi kuwa tete kila nikijitahid anishike japo ukosi wa shati yule maaluni kakaza kabali......sitosahau. yule mama alitupiga kitu kizoto. Siiendelezi naishia hapa.
Mmmh kuna harufu ya chai SAS uendelezi unataka kuombwaa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Nilikua machimboni pande za ishokera hela nikaenda kwa mganga Bariadi nikifika vzr bila kupotea kwakua ramani Nilikua nayo, nikapokewa na mjukuu wa mganga. mganga ni Bibi kizee kbsa, nikaambiwa utaaguliwa mda ukifika! Kweli saa9 ucku nikaitwa mganga kapandisha mizimu yake! Bandugu yule Bibi ni kwere alinipatia tangia Hustle zangu mpka kufika machimboni!, mganga akaniambia kua cku nikikuaga hpa kwangu utatembea kwa miguu utavuka vijiji vi2, kijiji cha3 utaitwa na wadada wawili watakufananisha lkn ww uwakubalie watakupikia kuku na wali pia watakukaribisha kulala nao kitanda ki1 LKN USIFANYE NAO MAPENZI KBSA! mtihani ulianzia hpo ndugu zangu kwa leo niishie hpo
oyaa letaa uzi huu...usitukatiri
 
Nilikua machimboni pande za ishokera hela nikaenda kwa mganga Bariadi nikifika vzr bila kupotea kwakua ramani Nilikua nayo, nikapokewa na mjukuu wa mganga. mganga ni Bibi kizee kbsa, nikaambiwa utaaguliwa mda ukifika! Kweli saa9 ucku nikaitwa mganga kapandisha mizimu yake! Bandugu yule Bibi ni kwere alinipatia tangia Hustle zangu mpka kufika machimboni!, mganga akaniambia kua cku nikikuaga hpa kwangu utatembea kwa miguu utavuka vijiji vi2, kijiji cha3 utaitwa na wadada wawili watakufananisha lkn ww uwakubalie watakupikia kuku na wali pia watakukaribisha kulala nao kitanda ki1 LKN USIFANYE NAO MAPENZI KBSA! mtihani ulianzia hpo ndugu zangu kwa leo niishie hpo
Noma sana!
 
zipo zenye faida mkuu mfano bibi yangu kijijin anapoishi ikitokea mtu amepotea au mifugo hasa Ng'ombe akipotea huko malishoni
Wanakuja kwake kumwomba msaada na akifanya dawa zake withn 2days kilichoptea kinapatkana na huwa haomb hela ya mtu ni wanarudi wenyew kutoa shukrani
Hao ndio wa kweli. Ukiona lina taka hela mapema lipe kisogo usepe kabla hajakupa msiba wa pili.
 
sijawai kusikia ana mizimu wala majini
Yeye hutuambia ni dawa za asili alifundishwa akiwa mdogo kusaidia kupata mifungo iliopotea , kuikinga mifugo dhidi ya wanyama wakali
na kujua mtu aliekwenda safari ya mbali kama bado yupo hai ama alishakufa

Dawa hizo pia hutumika kuwaita watoto waliokwenda mjini kutafta maisha na kusahau kurudi kijijn kusalmia wazee ,unambiwa ukifanyiwa hizo dawa utatafta kila njia urudi kwenu hata kwa mkopo ama kutembea kwa mguu

Na kuna ingine alinambia ikitokea hataki mtoto wake aende kutafuta maisha mbali na nyumban anachota unyayo wake anamix dawa na kwenda kuufunika na chungu
kuanzia hapo aliefunikwa hawez hata kufikiria kusafiri wala kwenda kuishi mbali na nyumbani.
Hiyo ni mizimu. Ila siku hiz haina tena nguv mana mambo mengi yamebadilika. Mifugo inavishwa hereni watoto wanasoma mbali nk..
 
Miaka hiyo ndio bodaboda zinaingia ingia kuna mwanangu wa haswa haswa,alipewa moja awe analeta hesabu.Shida ya mwanangu mtu wa kilaji sana na kamti pombe.Kwa kifupi alipoteza boda ya watu.Mwenyewe hakukubali akadai chombo yake haipotei kifala so sijui digala alienda kwa mtaaalamu.Mwana akawa analalamika anahisi ametwishwa boda mabegani hawezi kuamka wala kutembea ilikua ni kamzozo.Kila nikikumbuka haingii akilini nahisi kama kulikua mipango mingi hapo kati ambayo hatukuijua.
 
Nyingine kuna jamaa yetu anajikuta mtu wa mifugo sana,kila mtu na mambo anayoyapenda bwana.Siku hiyo kaniambia nimsindikize sehemu eti anafata dawa ya kupata njiwa weusi kwani ni deal sana.Kufika kwa mtaalamu akapewa kimjiti awe anaweka kwenye maji ,aisee njiwa walitotoa watoto weusi balaaa kila wakitotoa ni black tu mpaka akakatupa.
 
Back
Top Bottom