Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Umewahi tembea umbali gani mrefu kwa miguu ndani ya jiji la Dar es Salaam?

Kutoka Temeke Mikiroshini ~Kariakoo ~Ubungo ~Temeke Mikiroshini
 
Posta kile kituo wanapaita baridi mpaka Jay Mall, Siku hiyo ndo mara ya kwanza nimepanda daladala sijui kuwa bus haziendi shusha posta mpya zinazunguka pale. Nilaani sana aliyeanzisha ule utaratibu..... Sina hamu mpaka leo.
 
Mawasiliano hadi muhimbili.
Sema tulikua wawili, ila nilichoka ile siku khaaah.
 
Watu wanadhani hizi ni kamba ila kiukweli laiti Bongo kungekuwa na mashindano ya kutembea kama Ulaya naamini ningeng'oka na medani.

Picha linaanza umesomea primary & sekondari vijijinini kwa zaidi ya miaka kadhaa ukitafuta shule kwa km 23 × 2 = km 46 (kwenda na kurudi), sasa utashindwaje kutembea km 59 kwa masaa 10 tena huenda ukazidi hapo ukiweka bidii tokana na maisha uliuokulia.

Kukimbia ndiyo huwa najilazimisha kwa dakika 75 na mazoezi ya viungo dakika 10/15, bado ujana unalipa.

Kinachonihasishaga haswa ni vipi ikiwa Mungu atanijalia neema ya maisha marefu, nitafika miaka 70 nikiwa na afya njema au nitakuwa napambana na BP, KISUKARI, SONONA n.k?

NB:

Kesho huandaliwa na leo.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Uko vizuri kamanda, lakini mwendo si huwa unapungua kadri unavyokata distance? namaanisha masaa mawili ya mwanzo speed yako haiwezi lingana na baada ya masaa ma5
 
Kuna rafiki zangu wakati tunasoma shule ya msini, ile likizo ya mwezi wa 6 walishatembea kwa mguu zaidi ya km 70 kutoka sehemu inaitwa Mlangali hadi Ludewa wilayani. Safari walianza jioni saa kumi na moja wakati tunatoka shule na wakafika asubuhi muda wa chai.
Mzee umesoma Ludewa?
Japo pale ni parefu sana na mapori mengi.
 
Mawasiliano hadi muhimbili.
Sema tulikua wawili, ila nilichoka ile siku khaaah.
Mbona pafupi tu hapo! Mimi nilikuwa nasoma Urafiki na mwamba mmoja. Huyo alikuwa anatoka Kimara go and return kila siku.
Alikuwa anafika darasani ameshajichokea kabisa.
 
Morocco- kimara baruti
Kimara baruti - mnazi mmoja (go & return).
 
Nakumbuka siku moja nikiwa Msasani alitokea kijana mmoja akaniomba nimtembeze kwenye mtumbwi.

Ila kwa bahati nzuri kukawa na boti linaenda Kigamboni siku hiyo, basi bhana nikamuunganisha akaniambia tuende wote mpaka taifa tukaangalie na Mpira kati ya Yanga na Mbeya city.

Alifurahi sana tulipofika Kigamboni tukapanda panton tukavuka posts tukaenda kupanda magari ya rangi tatu, basi bhana tulipofika akaenda kukata ticket kwenye gari akakata ya kwake tu akaniambia nimsubiri, anaenda kutoa hela kwenye simu, nikamuamini poa tu japo nilishashtuka ila nikawa najipa moyo.

Mpaka Mpira unaanza hakutokda ila bidi nianze kupiga ado ado na mguu mpaka msasani.
Upanga to Mwenge, Mlimani City, Ubungo, Manzese, Magomeni, Kariakoo to Upanga, ni mazoeI tu.
 
Nakumbuka siku moja nikiwa Msasani alitokea kijana mmoja akaniomba nimtembeze kwenye mtumbwi.

Ila kwa bahati nzuri kukawa na boti linaenda Kigamboni siku hiyo, basi bhana nikamuunganisha akaniambia tuende wote mpaka taifa tukaangalie na Mpira kati ya Yanga na Mbeya city.

Alifurahi sana tulipofika Kigamboni tukapanda panton tukavuka posts tukaenda kupanda magari ya rangi tatu, basi bhana tulipofika akaenda kukata ticket kwenye gari akakata ya kwake tu akaniambia nimsubiri, anaenda kutoa hela kwenye simu, nikamuamini poa tu japo nilishashtuka ila nikawa najipa moyo.

Mpaka Mpira unaanza hakutokda ila bidi nianze kupiga ado ado na mguu mpaka msasani.
Mwaka 1980 nilisindikiza mdundiko toka Kiwalani mpaka Tegeta,
Mwaka 1988 nilitembea toka Chang'ombe hadi Terminal One Ukonga
Mwaka 1995 nilitembea toka Ukonga mpaka corner Bar Ubungo External
 
Nakumbuka siku moja nikiwa Msasani alitokea kijana mmoja akaniomba nimtembeze kwenye mtumbwi.

Ila kwa bahati nzuri kukawa na boti linaenda Kigamboni siku hiyo, basi bhana nikamuunganisha akaniambia tuende wote mpaka taifa tukaangalie na Mpira kati ya Yanga na Mbeya city.

Alifurahi sana tulipofika Kigamboni tukapanda panton tukavuka posts tukaenda kupanda magari ya rangi tatu, basi bhana tulipofika akaenda kukata ticket kwenye gari akakata ya kwake tu akaniambia nimsubiri, anaenda kutoa hela kwenye simu, nikamuamini poa tu japo nilishashtuka ila nikawa najipa moyo.

Mpaka Mpira unaanza hakutokda ila bidi nianze kupiga ado ado na mguu mpaka msasani.
Segerea to Mwenge hili lilikua ni funzo la kuheshimu pesa........

Nilianza safari saa 11 jioni Nikafika saa 4 na nusu usiku.......
Nilipo fika tabata relini niliwaza nirud nilipo Toka au niendelee na safari ☺️😊😊 turufu ikanambia niendelee na safari......

Mbande/ kisewe to ubungo yaan boda to boda.....kanyaga sana sorry saivi nimekua Bonge mvivu sana kutembea....☺️☺️😊😊

Mikocheni to ubungo tembea mpaka Unapoteza Nuru ☺️☺️☺️😊😊😊

Kariakoo to mbagala kawaida sana yaan ni Tish tashi...muda Sasa miaka mitano Sasa sijawai Rudia kutembea umbali mrefu.....

Maisha yametufundisha MENGI ☺️☺️☺️😊😊😊😊
 
Tulitembea kutoka Titegemee(Mgulani) hadi msasani kisa mwanetu mmoja hakuwa na nauli so tukawa tunampa kampani, yeye aliendelea hadi victorial
 
Tabata to coco beach 2003 hiyo ni go and return kwa mguu
Ila Kwa maisha yangu ya saiv ya kukimbia km 42 marathon etc jiji la dar nalivuruga Sana .....mfano one route nilitoka ubungo to mbezi mwisho ,goba, madale to Tegeta to mbezi beach to mikocheni to sinza.
. etc ...
 
Back
Top Bottom