Umoja wa Mataifa wapitisha azimio kutaka vita isitishwe, Israel yapinga na yaongeza mapigo Gaza

Umoja wa Mataifa wapitisha azimio kutaka vita isitishwe, Israel yapinga na yaongeza mapigo Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kwa sauti moja hapo jana baraza kuu la umoja wa mataifa lilipitisha azimia likitaka vita visitishwe kwa muda ili kutoa fursa ya majadiliano na kuwezesha misaada kuingia Gaza.

Kinyume chake taifa la Israel limepinga azimio hilo na katika kipindi cha masaa 24 wameongeza mapigo makali kuzidi ukali wa siku iliyopita.Katika tamko la kupinga azimio hilo Israel imeiambia UN haina uhalali wa kutoa azimio kama hilo.

Vikosi vya IDF vimeanza kuingia Gaza kwa wingi kwa kutumia vifaru ardhini na ndege za kijeshi angani zikisaidiwa na droni.

Hali ya Gaza imeelezwa na walio ndani kuwa sasa ni balaa tupu,hakuna matumaini tena na hata watu walioko huko ikiwemo waandishi wa habari hawawezi kufikiwa tena. Ndugu walioko nje na ndani kusini na kaskazini hawawezi kujuliana hali tena.
 
Israel kitakachomkuta ataomba msamaha yeye
Ndhivyo inavyokuwa.Binadamu akiona mipango yake inakwenda sawa huwa anapta kiburi sana.Israel kwa sasa amepanda hilo daraja mpaka juu.Kinachofuata ni kuporomoshwa kwa aibu ili ulimwengu wote ushuhudie kuwa ufalme wa dunia una mwenyewe aliyeumba mbingu na ardhi.
 
Mashambuizi ya ndege za kivita ndio hatari zaidi.Hamas hawana ndege hata moja wala kifaru.Kama wewe si mtu muovu basi huwezi kupigwa na mtu kama Hamas.

Mkuu embu fafanua kidogo hapa labda mm kilaza sijaelewa.
Ina maana Hamas wanawapiga tu waovu? Kama sio mwovu hawakupigi?
Kama ndivyo, wao mamlaka wameyapata wapi ya kupiga hao waovu? Na wanatumia factor gan kuamua huyu ni mwovu ama sio?
 
Mungu wa Israel na Isaka endelea kuijalia heri na fanaka Israel na wafuasi wake.
 
Mkuu embu fafanua kidogo hapa labda mm kilaza sijaelewa.
Ina maana Hamas wanawapiga tu waovu? Kama sio mwovu hawakupigi?
Kama ndivyo, wao mamlaka wameyapata wapi ya kupiga hao waovu? Na wanatumia factor gan kuamua huyu ni mwovu ama sio?
Ufafanuzi ni kuwa ukiona mtu ana nguvu sana lakini anapigwa na mtu dhaifu basi ujuwe huyo hakupigwa na huyo dhaifu bali aliyempiga ni Mwenyezi Mungu.Hamas wasingeweza kufanikiwa kuingia ndani ya Israel kivile kama wasingepata baraka zake.
Nataraji umefahamu
 
Sisi haituhusu, wapigane huko huko makwao sisi kama waafrica tunasubir tusikie mshindi BBC au DW
 
Back
Top Bottom