Umoja wa wanawake CCM wasikitishwa na udhalilishaji wa Makonda, watoa tamko

Umoja wa wanawake CCM wasikitishwa na udhalilishaji wa Makonda, watoa tamko

Attachments

  • downloadfile-2.jpg
    downloadfile-2.jpg
    44.3 KB · Views: 1
Bashite awe Rais! Kama kosa lishatokea na tukajifunza kipindi cha Jiwe, Sukuma gang hawatakuja tena kupata nafasi ya Urais
 
Luka 13:32 - Akawaambia , "Nendeni mkamwambie yule mbweha , Tazama leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa , siku ya tatu nakamilisha ."

Yesu anamfananisha kiongozi mbinafsi, mdanganyifu na mwenye tabia ya uharibifu wa mali za umma na mbweha . Ingekuwa ni nyakati zetu, watu ambao hawana akili wangenong'ona na kusema Yesu amemdhalilisha kiongozi wa aina hii .
 
Mary Chatanda atakuwa ametumwa atoe tamko kama hilo [emoji872]

Sisi tuliosomea Cuba na USSR tumeshafahamu whats cooking [emoji872][emoji23]

Individually Mary Chatanda asingekuwa na courage hiyo !

After all mtu kusema mimi nina mke tena mzuri sioni kama ni udhalilishaji [emoji872][emoji849][emoji40]
Hahahahah eti mimi sioni, sasa kwani wewe lini ulikuwa unaona, au nipe tofauti ya wewe na Bashite
 
Hiki ni kikao cha kimetengenezwa,ili kimjengea makonda ajali ya kisiasa.

Kinana hamtaki makonda, na ccm ni ya wote.

Mkimgusa makonda sasa mtajua CCM Ina watu wachache.

Watu wanateseka na kero za kimaisha mnasema UWT?

WANAWAKE WANAOTESEKA NA WENYE KERO NI WENGI KULIKO WANAWAKE WALIOKO UWT.
Hii kweli ina chawa wengi sana, eti na wewe ni chawa, duh
 
Kwenye siasa vita moja ikiisha nyingine inaanza na kuama upande ni jambo la kawaida sana.

Ni kwa sababu hizo, ndio maana utakutana na kauli za hovyo walizopewa wanasiasa kama vile “tofauti ya dada poa na mwanasiasa; mwanasiasa bei yake ni kubwa zaidi” lakini wote wapo tayari kufanya kazi na yeyote mwenye dau.

Hakuna uadui wa kudumu kwenye siasa, kuna maslahi ya kudumu. Vita moja ikiisha nyingine inafuata na wachezaji wanabadili upande kwa maslahi yao mapana.

Ama ni utoto kinachoendelea huko CCM kila siku kumfanyia majungu Makonda, au wahuni wana mtu wao 2025 wanataka popular support ya ‘bi-tozo’ iendelee kubaki chini ili iwe rahisi kumvaa.

Vinginevyo hata dictatorship kama huko China serikali inajaribu kutafuta legitimacy ya uwepo wao kwa kuwafanyia kazi wananchi na kutatua shida zao. Hata wanapozuia wapinzani unakuta bado wana support ya wananchi walio wengi.

Uchaguzi mkuu sio kama chaguzi za ndani ya CCM wajumbe wananunulika kirahisi au wapiga kura wote ni watumishi wa serikali wanaopenda viongozi wazembe katika kuwasimamia wafanye yao. Wapiga kura waliowengi ni wananchi wa wakawaida na wengi ndio hao wanaojaa kwenye mikutano ya Makonda na huko anamtengenezea imani Samia anawajali.

Hata kama unajua unashinda chaguzi kwa hila, bado kuna umuhimu wa kutafuta legitimacy ya kuonekana unapendwa. Na mtu anaefanya hiyo kazi on the ground na kueleweka kwa sasa ni Makonda peke yake, wengine ni kuandaa makongamano ya kujitekenya na kucheka wenyewe hakuna wananchi wanaosikiliza upuuzi wao.

Bi Tozo aelewi somo au watu aliowaweka karibu ndio waliovuruga uraisi wake.

Ni upuuzi wa hali ya juu viongozi wa CCM kuwa na wivu na Makonda.

Ukiangalia clip wala akumdhalilisha yule dada, ye mwenyewe anaongea kwenye mkutano wa hadhara uku anatabasamu na kuchekacheka bila ya sababu za msing, ndio Makonda alipomwambia mbona unaongea kama tunatongozana mimi na wewe wakati wananchi wanataka majibu; mimi tayari nina mke mzuri (aina maana yule dada mmbaya).
Ulikuwa na hoja nzuri sana hapo mwanzo ila umemaliza vibaya sana kama Bashite mwenyewe
 
Mimi bila kupepesa macho nasema hivi lawama zote kwa mamlaka ya uteuzi. Makonda kauli yake ya kwanza alipofika Arusha alisema 'kuna watu wanasema Makonda amejifunza,sasa nawaambia kuwa sijajifunza kitu mimi ni yule yule.' Mwisho wa kunukuu.
 
Merry chatanda amepiga kelele kumhusu makonda ,lakini pia chini chini mahali anakopita huyu kiongozi watu wanapiga kelele ambazo hazisikiki, sauti zinazomsifia ni zile ambazo zimejaa hofu. Kuogopwa! Labda anawaongoza watu kwa kuwatisha!

Moyoni hata waliomteua hawajui chakufanya! Anaweza akafanya vizuri mambo matano akaharibu mambo 20! Akipewa maiki kuhutubia watu wanashika roho mkononi kwa sababu anaweza kuongea lolote wakati wowote!

Huyu mtu ana ulemavu wa ulimi tusimhukumu ,tumuombee mungu amponye ,popote ulipo ndugu Paulo christian makonda pokea uponyaji wa ulimi katika jina la YESU kristo ,Amina
Ulimi hutamka what the brain decides. He has low IQ for me.
 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) Marry Chatanda ameeleza kusikitishwa na kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda alichokiita unyanyasaji na udhalilishaji wa watendaji wanawake kwenye maeneo yao ya kazi.

Chatanda ameyasema hayo leo Jumamosi, Mei 25, 2024 jijini Dodoma wakati wa semina ya wabunge wa viti maalumu, manaibu waziri, mawaziri, makatibu wa jumuiya ya wazazi ngazi ya mkoa na wilaya ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania bara, Abdurahman Kinana

"Kuna 'clip' imezunguka kule Arusha, Longido haikuwa jambo jema wala sio zuri hata kidogo, kama wewe ni kiongozi mkuu wa Serikali na umemuona mtendaji wako amekosea ni vizuri ukakaa na kuzungumza nao, kwa suala la udhalilishaji wa wanawake siwezi kukubaliana nalo, tunaomba tuheshimiwe wanawake, tena sisi wanawake ni watendaji wazuri kuliko wanaume.

Chatanda amesema kuwa clip hiyo tayari ameshamtumia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Abdulrahmani Kinana.

Hatua hii ya UWT inafuatia matamshi ya Makonda katika kipande kifupi cha video kinachosambaa katika mitandao ya kijamii ambapo anasikika akisema, ...usiongee na mimi hivyo nina mke mzuri huongei na mchumba wako hapa...
Hawa UWT nao wajirekebishe waache kukurupuka
 
Siku Mhe. Gekul alipopata tuhuma tu ambazo hazijathibitishwa mpaka leo alivuliwa Uwaziri. Mbona hii ya Makonda ni special. Kwa nini Mamlaka ya uteuzi haujamvua Ukuu wa Mkoa?.
 
Back
Top Bottom