Umoja wa wazalishaji wa sukari Tanzania (TSPA) Wajitetea kuhusu kupanda kwa Sukari. Hawajawahi kuficha Sukari, Si kazi yao kuagiza Sukari nje
Hujaona hayo mapapa yanavyohaha hapo? Bila Bashe ungeyajuwa hayo?

Wao wazalishe sukari, Bashe huko kishafunga mjadala, sasa hakuna cha kibali hakuna cha nini., NFRA wanahakikishsa wanaipata sukari popote ilipo mradi ghala lao la kuhifadhi lisipunguwe tani 200,000 za sukari.

Wananunuwa kwa nani kazi kwao.
Inabidi uwasikilize kwa makini wao wanajibu hoja tu ya kuitwa ‘cartel na maharamia’ na kuzushiwa kama chanzo cha uhaba wa sukari nchini.

Wakati si kweli wao ndio chanzo cha uhaba wa sukari, kwa sababu wanafanya risk assessment zao. If anything wao ndio waliona disruption inayofuata kwenye uzalishaji mara tu baada mamlaka ya hali hewa kutangaza El-Nino walianza kuomba vibali toka mwezi wa kumi na kutokupewa hadi January, ata hiyo tonne 4.5 walioleta ilkuwa gamble tu kufanya hivyo hawakuwa na kibali ila waliona madhara ya mbele kutokana na diminishing stock level zao.

They don’t care much nani ameingiza au akuagiza sukari kwa wakati ila hawataki wazushiwe wao kama chanzo cha uhaba.

NFRA wanapewa kibali cha kuagiza sukari wakati TSPA production capacity plan yao ya 2024~2025 kutakuwa hakuna na nakisi, na 2025~2026 wataanza kuwa na ziada ya tone 150K na kuweza kuuza nje ya nchi kwa uwekezaji waliofanya na unaoendelea kufanyika kwenye viwanda vyote nchini.

NFRA hiyo sukari yote wataipeleka wapi, ni sawa kuwa na three months buffer stock (incase inatokea unforeseen disruption) ila hizo tonne łąki mbili sijui łąki nne wanazotaka kuagiza watazipeleka wapi kama sio kujaza sukari sokoni (kwa kuchezea hela za walipa kodi) na kuleta madhara kwa wazalishaji wa ndani wenye high production costs na kwa umoja wao wana madeni ya karibu tsh 3.5 trillion ya uwekezaji waliofanya karibuni. Sasa ukishaleta hayo madhara na madeni waliyonayo si wanaenda pata hasara.

Shida ni Bashe hapo, sio tu kutoa vibali hovyo bali kuwatukana na kuwasingizia TSPA ni genge la wahuni lililosababisha tatizo wakati kuna fair competition regulator anaeangalia oligopoly kama ipo na kuchukua hatua, mbona sasa asiende report huko kama wana operate kama cartel.
 
ina maana hata yule dogo mlemavu (somebody matinyi if am not wrong) na yeye pia ni mtu nyeti???
Na washauri woote wa rais ni watu nyeti pia?

Au kuna kitu hutaki kuweka wazi au probably umezusha tu huo unyeti?
Unaelewa maana ya Washauri wa Rais?

Halafu Matinyi Siyo mlemavu ila alikuwa Msaidizi wa Rais kama Msemaji mkuu wa serikali 😀
 
Namheshimu sana Balozi Ammy Mpugwe, anadai amekuwa kwenye tasnia ya sukari akiwa na miaka 10 sasa ana miaka 76, kuna wakulima elfu 80 na elfu kumi wana mashamba, obvious elfu 70 ni manamba,

sasa, sasa miaka hamsini ya kilombero suger still we are importing suger? yet we are exporting suger on smaggling way based on economic osmosis!

anasema yeye hauzi vocha that means he is a gianty man. why are we still buying suger from brazil yet suger hii is cheaper than from his home land kilombero?

lakini, how is the man credible to our socity? ammy huyu wa tanzania one? huyu ammy wa capital mining? no no no, hapana kabisa.
Hujamuelewa ukiangalia hapo ni kwamba mabadiliko makubwa yamefanyika kuanzia 2015
 
Kwa mtazamo wangu, Bashe ameshinda hii Vita, amefanikisha kumtoa nyoka pangoni. Hii ni hofu ya financial bill, Mimi sijaona hoja yenye mashiko kwao, zaidi ya kujitetea kuwa wao sio maharamia Wala so mapapa. Ila kwangu Bashe amewashika pabaya. Amepiga kwenye mshono. Bashe anatakiwa kuungwa mkono na kupewa nguvu.
Ficha upumbavu wako
 
Kwa mtazamo wangu, Bashe ameshinda hii Vita, amefanikisha kumtoa nyoka pangoni. Hii ni hofu ya financial bill, Mimi sijaona hoja yenye mashiko kwao, zaidi ya kujitetea kuwa wao sio maharamia Wala so mapapa. Ila kwangu Bashe amewashika pabaya. Amepiga kwenye mshono. Bashe anatakiwa kuungwa mkono na kupewa nguvu.
Kuungwa mkono kwa lipi? Jiulize nini sera endelevu ya serekali ya CCM katika sector ya sukari? Miaka michache iliyopita JPM alihamasisha kwa nguvu kubwa Bakhresa anzishe kiwanda cha sukari Bagamoyo na wakati huo huo serekali ikawekeza kwenye kiwanda kipya. Leo hii waziri wa serekali ya CCM (Bashe) anajitokeza hadharani kwamba eti hatajali hata kama mashamba yote ya miwa nchini yatageuzwa kulima mpunga. Halafu mtu mwenye akili timamu anasema tumwunge mkono Bashe. Kweli TZ haitang'oa nanga.
 
Inaelekea wewe hukusikia vizuri ile habari ya "ukiwaona watoto wa simba wanachezacheza". Nakusihi usikilize tena hicho kipande, halafu uchanganye na zako!
Nimesikiliza tangia mwanzo na nikaelewa maana yake.

Isipokuwa nimetoa hiyo hoja kwa sababu muongeaji hakutoa maelezo toshelezi ni muda gani alihakikisha watoto wa simba wanaolialia wapo peke yao na kujihakikishia usalama wake ndiyo awasogelee?

Uoga wa aina hii husababisha haki nyingi za watu za msingi kudhulumiwa na genge la mibaka uchumi.

Ni heri angelinyamaza na kuiachia dunia iyapange mambo inavyotaka yenyewe!
 
Amesema cha kushangaza, hadi Desemba vibali vya kuagiza sukari vilikuwa havijatoka na Kampuni ya Sukari Kilombero ikalazimika kuizuia meli yake iliyokuwa inapeleka tani 45,000 ya sukari nchi nyingine na kuagiza iingizwe nchini kwa lengo la kufidia upungufu mkubwa uliojitokeza.
Hapa sijapaelewa vizuri.ina maana huwa tunauza sukari nje ya nchi?
 
Leo hii waziri wa serekali ya CCM (Bashe) anajitokeza hadharani kwamba eti hatajali hata kama mashamba yote ya miwa nchini yatageuzwa kulima mpunga. Halafu mtu mwenye akili timamu anasema tumwunge mkono Bashe. Kweli TZ haitang'oa nanga
kama alisema hivi ,siyo sahihi kabisa.hatuwezi kucha kulima miwa eti tutegemee sukari kutoa nje ya nchi.huku itakuwa ni kudhofisha uchumia wa nchi.tunatakiwa tulime miwe tuwe na sukari ya kutoshereza na inayozidi ili tuiuze nje ya nchi tupate dolla,euro,rupee etc.
 
Back
Top Bottom