Una maoni gani kwa matokeo haya ya kidato cha pili Shule ya Diplomasia inayopatikana Dar?

sababu kubwa shule za Dar kufanya vibaya mfano zilizopo maeneo ya Temeke, kuna Msimbazi wanavaa blue bahari, kuna chanika na nyingine ipo bunju ni ya kata.

1. Utandawazi; hii ni sababu moja kubwa ya watoto wengi wa dar kufeli. Hili linasababishwa na usimamizi mbovu wa wazazi kwa watoto wao wakiwa busy kukimbizana na maisha, watoto kuingia kwenye starehe za mapema, kuangalia video za ngono.

2. Serikali; maisha ya dar ni magumu, kada hii ya ualimu imesahaulika, miundombinu Mibovu, hakuna Hamasa kwa kwa walimu kufanya kazi kwa asilimia zote wanafanya bora liende.

Nimeona mtaala mpya mambo mengi sana, lakini kama serikali haitajitahidi kuboresha maisha na masilahi ya walimu hatutaona mabadiliko.

Wizara husika waliangalie hili suala kwa kina, usitegemee ukafanya vitu kwa njia ile ile ukategemea matokeo tofauti.
 
Kufeli na kufaulu kupo zaidi katika mindset zaidi.

Wengi tumefika tulipo sio kwamba tulikuwa na IQ kubwa bali tulikuwa na positive attitude toward the studies.

Mtu kabla ya yeye kuanza kusoma anabidi kuipenda shule kwanza.


Hivyo nadhani walimu wa hiyo shule plus wanafunzi wameshapoteza winning mentality.

Kuhusu changamoto za usafiri sio sababu za MTU kupata four au zero
 

Unajua kuna nguvu kubwa katika peoples you hang out with.
 
Duuh noma sana hao watoto wa msimbazi sec ninaish maeneo ya karibu aseeee ni hatr hapo ni mimba, bangi bora umpe mtot mtaji auze maji kuliko kumpeleka hapo
 
Wanafunzi wa Dar wa day mpaka wamalize kusoma wamechoka sana, saa moja usiku unakuta wanafunzi bado wanazunguka vituo vya daladala... Asubuhi wanatakiwa kuwahi tena shule ni kasheshe sana.
 
Wanafunzi wa Dar wa day mpaka wamalize kusoma wamechoka sana, saa moja usiku unakuta wanafunzi bado wanazunguka vituo vya daladala... Asubuhi wanatakiwa kuwahi tena shule ni kasheshe sana.
sasa hili ndio chanzo kikubwa cha mimba haswa kwa jinsia KE.

bodaboda na bajaji ndio wanageuza hao watoto kuwa wake zao,
 
Huyu amemaliza kilakitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…