Unahitaji mtoto wa Kambo au Kumuasili?

Unahitaji mtoto wa Kambo au Kumuasili?

Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Kwa aliyebarikiwa neema ya Kulea watoto kwa malezi ya kambo au kumuasili kisheria awe wake;


UTARATIBU;

Baada ya kuwasilisha maombi Halmashauri;

1. Afisa Ustawi wa Jamii atakutembelea na kufanya tathmini.

2. Taarifa itawasilishwa kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii Wizarani.

3. Iwapo hakuna hoja pingamizi, Kamishna atatoa kibali kwa mwombaji kumtambua mtoto.

4. Afisa Ustawi wa Jamii ataendelea kufanya ufuatiliaji wa maendeleo ya familia iliyomtambua mtoto na kuanza kumlea malezi ya kambo.

5. Taarifa ya maendeleo ya malezi ya kambo baada ya mathalani miezi sita hivi itawasilishwa tena kwa Kamishna, kwa ajili ya kuthibitisha kuwa maendeleo ya malezi ya kambo ni mazuri, hakuna changamoto hivyo, kibali cha kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya Kuasili mtoto huyo kitatolewa.

Hakuna malipo yoyote epuka ulaghai wa wasio waadilifu.
Asante kwa huo muongozo kutoka serikalini,
Kuna maswali machache ningependa kukuuliza,
1. Ningependa kujua, je kisheria serikali inaruhusu ku adopt mtoto mwenye umri kuanzia miaka mingapi?
2. Endapo ume adopt mtoto kumbe mzazi wake yupo kimya tu, badae mtoto amekua mkubwa mzazi wa huyo mtoto akaja muhitaji Sheria inasemaje?
3. Kwa wale ambao wanatafuta watoto kwa njia ya In vitro fertilization (IVF) Sheria inasemaje endapo mhusika wa mtoto au watoto akatumia surrogate mother na kumlipa??
 
Aleikum Salaam, shukrani 🤲
Naomba jibu ya swali langu, mnapotoa taarifa au kuanzisha mijadala kwenye jamii ni vizuri muwe mmejiandaa kujibu maswali katika nyanja tofauti,
Kuna vitu vingi ambavyo jamii inahitaji kuelimishwa hasa jambo la In vitro fertilization (IVF) lakini hadi sasa hakuna muongozo wa kisera toka serikalini ili hali sasa Kuna hospital nyingi zinatoa hiyo huduma sasa hapa nchini
Maswali niliyouliza kwenye post # 45 ni
1. Ningependa kujua, je kisheria serikali inaruhusu ku adopt mtoto mwenye umri kuanzia miaka mingapi?
2. Endapo ume adopt mtoto kumbe mzazi wake yupo kimya tu, badae mtoto amekua mkubwa mzazi wa huyo mtoto akaja muhitaji Sheria inasemaje?
3. Kwa wale ambao wanatafuta watoto kwa njia ya In vitro fertilization (IVF) Sheria inasemaje endapo mhusika wa mtoto au watoto akatumia surrogate mother na kumlipa??
 
Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Kwa aliyebarikiwa neema ya Kulea watoto kwa malezi ya kambo au kumuasili kisheria awe wake;


UTARATIBU;

Baada ya kuwasilisha maombi Halmashauri;

1. Afisa Ustawi wa Jamii atakutembelea na kufanya tathmini.

2. Taarifa itawasilishwa kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii Wizarani.

3. Iwapo hakuna hoja pingamizi, Kamishna atatoa kibali kwa mwombaji kumtambua mtoto.

4. Afisa Ustawi wa Jamii ataendelea kufanya ufuatiliaji wa maendeleo ya familia iliyomtambua mtoto na kuanza kumlea malezi ya kambo.

5. Taarifa ya maendeleo ya malezi ya kambo baada ya mathalani miezi sita hivi itawasilishwa tena kwa Kamishna, kwa ajili ya kuthibitisha kuwa maendeleo ya malezi ya kambo ni mazuri, hakuna changamoto hivyo, kibali cha kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya Kuasili mtoto huyo kitatolewa.

Hakuna malipo yoyote epuka ulaghai wa wasio waadilifu.
Asante muheshimiwa, ila kuna urasimu mwingi sana. Kuna ndugu yangu aliambiwa lazima awe na milioni ishirini kwenye account ndio aweze kuasili. Yeye ni muajiriwa tu wa serikali kuipata hiyo hela ni ngumu, ila uwezo wa kutunza mtoto anao.
Tunaomba muheshimiwa toa tamko kwa idara zote husika, wasifanye mambo kuwa magumu. Wafanye due diligence yao na kufuata all the necessary procedures bila kumkatisha tamaa mtu mwenye nia njema ya kuasili.
 
3. Kwa wale ambao wanatafuta watoto kwa njia ya In vitro fertilization (IVF) Sheria inasemaje endapo mhusika wa mtoto au watoto akatumia surrogate mother na kumlipa??
Hii kitu mpya tusaidie kuielewa vizuri mkuu
 
Hii ni solution Kwa Wanandoa wenye changamoto ya kupata watoto.

Mnaweza mkakubaliana na Mkeo, mkaenda kum-adopt mtoto wa miezi kadhaa then mkamlea na kumfanya wa kwenu.

Kama litafanyika Kwa upendo, inaweza kusaidia kupunguza watoto wa mitaani ambao wamekosa huduma na Walezi.

Wale ambao wataguswa kufanya hivyo vyema mkawahi mapema.

Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, "Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa"

Yakobo 1:27
 
Hii kitu mpya tusaidie kuielewa vizuri mkuu
Hii inatumika kwa watu wasio na uwezo wa kupata mtoto, labda mwanaume hawezi kutungisha mimba au mwanamke hana uwezo wa kupata ujauzito kwa sababu kadhaa.
Hivyo wanakubaliana kupandikiza ujauzito kwa njia za kisayansi hiyo njia ndio inaitwa In vitro fertilization (IVF) sasa Kuna namna mwanaume anaweza kutumia mayai ya mwanamke mwingine na ujauzito ukabebwa na mwanamke mwingine.
Hili jambo linafanyika sana katika hospital nyingi hapa Tanzania sasa, ila hadi sasa hakuna sera au Sheria kuhusu hili jambo au kama hizo sera na Sheria zipo basi ni vyema wananchi wakajulishwa na kuelimishwa
 
Ninaye mtoto ambaye nimekuwa nikimlea kwa hiari yapata miaka 6 sasa, wazazi wake wote wapo ila walitengana mapema sana.... baba wa mtoto ndiye alikuwa rafiki yangu.

Baada ya kutengana kwao, baba hakutaka kuhusika na malezi kwa namna yoyote licha ya ushauri wangu kama rafiki..... mwisho mama mtoto akaniomba mimi nimsaidie malezi kwa kuishi na mtoto na kumsomesha.

Kuna nyakati kadhaa nimeshuhudia majina ya mtoto kwenye daftari zake akibadili na kuandika jina langu, ile kuulizia kumbe mama mtoto pia anajua na ameridhia.... kitu ambacho nimekipinga kwa kuwa nilihisi pengine itakuja kuleta shida mbeleni.

Kuna nyakati natamani kufanya hivyo ili kumwezesha mtoto kuwa mnufaika wa BIMA ya AFYA, ushauri niliopewa ni huu wa kumuasili ila bado sijafikia maamuzi..... sababu sijakubali kupora haki ya mzazi wake ambaye ni rafiki yangu japo hajali lolote ila huwezi kujua ya kesho.

Je, naweza kumuasili mtoto kisheria ili aweze kupata hizi 'benefits' lakini akabakia na majina yake?
Hongera sana una karama ya kipekee, nahisi umelelewa na wazazi wenye kumjua Mungu vilivyo, itapendeza ukiwa balozi wa kuwawezesha watu wengine kuwa na moyo wa upendo wa kiasi hicho

Ubarikiwe sana mkuu
 
Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Kwa aliyebarikiwa neema ya Kulea watoto kwa malezi ya kambo au kumuasili kisheria awe wake;


UTARATIBU;

Baada ya kuwasilisha maombi Halmashauri;

1. Afisa Ustawi wa Jamii atakutembelea na kufanya tathmini.

2. Taarifa itawasilishwa kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii Wizarani.

3. Iwapo hakuna hoja pingamizi, Kamishna atatoa kibali kwa mwombaji kumtambua mtoto.

4. Afisa Ustawi wa Jamii ataendelea kufanya ufuatiliaji wa maendeleo ya familia iliyomtambua mtoto na kuanza kumlea malezi ya kambo.

5. Taarifa ya maendeleo ya malezi ya kambo baada ya mathalani miezi sita hivi itawasilishwa tena kwa Kamishna, kwa ajili ya kuthibitisha kuwa maendeleo ya malezi ya kambo ni mazuri, hakuna changamoto hivyo, kibali cha kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya Kuasili mtoto huyo kitatolewa.

Hakuna malipo yoyote epuka ulaghai wa wasio waadilifu.
Asante sana Mheshimiwa na sisi tuliozaa nje ya ndoa Ila wake zetu hawajui utaratibu upoje?
 
Back
Top Bottom