Unahitaji mtoto wa Kambo au Kumuasili?

Unahitaji mtoto wa Kambo au Kumuasili?

Hii inatumika kwa watu wasio na uwezo wa kupata mtoto, labda mwanaume hawezi kutungisha mimba au mwanamke hana uwezo wa kupata ujauzito kwa sababu kadhaa.
Hivyo wanakubaliana kupandikiza ujauzito kwa njia za kisayansi hiyo njia ndio inaitwa In vitro fertilization (IVF) sasa Kuna namna mwanaume anaweza kutumia mayai ya mwanamke mwingine na ujauzito ukabebwa na mwanamke mwingine.
Hili jambo linafanyika sana katika hospital nyingi hapa Tanzania sasa, ila hadi sasa hakuna sera au Sheria kuhusu hili jambo au kama hizo sera na Sheria zipo basi ni vyema wananchi wakajulishwa na kuelimishwa
Asante sana kwa hii elimu sikuwahi kujjua kama sayance imefika huko, vipi DNA itasoma takwimu za mwanamke yupi kati ya hao wawili
 
Asante sana kwa hii elimu sikuwahi kujjua kama sayance imefika huko, vipi DNA itasoma takwimu za mwanamke yupi kati ya hao wawili
DNA itasoma kwa mwanamke alietoa yai, ila wataalam wataelezea zaidi
 
Tunahofia wake zetu wakijua patatimka hapo nyumbani. Hakuna namna ya kumfunga mdomo bi mzuri?
Hukumuhofia wakati unamsaliti uje kumuhofia tayari ushaleta kiumbe duniani??
Chukua mtoto wako lea yy hata akinuna akipasuka haiwezi kubadili ukweli ww una mtoto na ulimsaliti.! Kingine unamnyima mtoto haki zake za msingi na yy hakukutuma umlete ni shobo zako.
 
Hii thread nilikua naisibiria kwa hamu sana, ngoja nimalize kibanda changu then nianze mchakato, plan ni ku adopt mmoja tuu na jukumu langu kubwa ni kimlea kama sehemu ya familia yangu, Mungu baba nipe nguvu kweny hili...asante....
 
Wasaalam Wana Jukwaa wote.

Kwa aliyebarikiwa neema ya Kulea watoto kwa malezi ya kambo au kumuasili kisheria awe wake;


UTARATIBU;

Baada ya kuwasilisha maombi Halmashauri;

1. Afisa Ustawi wa Jamii atakutembelea na kufanya tathmini.

2. Taarifa itawasilishwa kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii Wizarani.

3. Iwapo hakuna hoja pingamizi, Kamishna atatoa kibali kwa mwombaji kumtambua mtoto.

4. Afisa Ustawi wa Jamii ataendelea kufanya ufuatiliaji wa maendeleo ya familia iliyomtambua mtoto na kuanza kumlea malezi ya kambo.

5. Taarifa ya maendeleo ya malezi ya kambo baada ya mathalani miezi sita hivi itawasilishwa tena kwa Kamishna, kwa ajili ya kuthibitisha kuwa maendeleo ya malezi ya kambo ni mazuri, hakuna changamoto hivyo, kibali cha kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya Kuasili mtoto huyo kitatolewa.

Hakuna malipo yoyote epuka ulaghai wa wasio waadilifu.
Samahani dokta gwajima nipo nje ya mada nilikua nauliza hivi bado unajifukiza kama kipindi kile cha korona na je ina msaada gani na madhara ki afya
 
Naomba jibu ya swali langu, mnapotoa taarifa au kuanzisha mijadala kwenye jamii ni vizuri muwe mmejiandaa kujibu maswali katika nyanja tofauti,
Kuna vitu vingi ambavyo jamii inahitaji kuelimishwa hasa jambo la In vitro fertilization (IVF) lakini hadi sasa hakuna muongozo wa kisera toka serikalini ili hali sasa Kuna hospital nyingi zinatoa hiyo huduma sasa hapa nchini
Maswali niliyouliza kwenye post # 45 ni
1. Ningependa kujua, je kisheria serikali inaruhusu ku adopt mtoto mwenye umri kuanzia miaka mingapi?
2. Endapo ume adopt mtoto kumbe mzazi wake yupo kimya tu, badae mtoto amekua mkubwa mzazi wa huyo mtoto akaja muhitaji Sheria inasemaje?
3. Kwa wale ambao wanatafuta watoto kwa njia ya In vitro fertilization (IVF) Sheria inasemaje endapo mhusika wa mtoto au watoto akatumia surrogate mother na kumlipa??
Ahsante Sana kufuatilia mjadala huu na kuchangia. Tumetoa namba hizo za call center za wizara Ili kama ikitokea tumechelewa kuona hapa basi fuatilieni kwenye namba hizo.

Ufafanuzi kwa ufupi;

1. Sheria imeruhusu kuasili mtoto wa umri wowote ila limitation ya umri imewekwa kwa waombaji/adoptive parents (mwombaji mwenye umri wa kuanzia miaka 50 ataruhusiwa kuasili mtoto wa kuanzia miaka 10 na mwisho wa kufanya applications ni miaka 65).

2. Ikitokea mzazi amejitokeza kwa ajili ya kuasili, Mahakama ndiyo imepewa mamlaka hivyo, atawasilisha kesi yake Mahakamani ambapo, Kamishna wa Ustawi wa Jamii atashirikishwa kwenye kufanya tathmini kwa sababu ndiye aliyetoa kibali cha kuwasilisha shauri Mahakamani baada ya kipindi cha malezi ya Kambo kwisha.

3. Ikumbukwe, kabla ya kuruhusu mtoto kuwekwa kwenye malezi ya Kambo Afisa Ustawi wa Halmashauri amepewa jukumu la kufanya uchunguzi wa kina kwa ushirikiano na Polisi ili kujidhirisha kwamba hakuna mzazi na kama Kuna mzazi ridhaa ya kisheria inatakiwa ya mzazi ila wakati mwingine kutegemeana na mazingira ya mzazi au mlezi Kamishna au Mahakama inaweza isihitaji ridhaa mfano, kama mzazi ana changamoto ya afya ya akili au amemtelekeza mtoto.

Kuhusu IVF; mpaka Sasa suala la IVF au surrogacy haijaingizwa kwenye Sheria ya Mtoto. Tutawasiliana na wizara husika.

Shukrani, 🙏🏽
 
Asante muheshimiwa, ila kuna urasimu mwingi sana. Kuna ndugu yangu aliambiwa lazima awe na milioni ishirini kwenye account ndio aweze kuasili. Yeye ni muajiriwa tu wa serikali kuipata hiyo hela ni ngumu, ila uwezo wa kutunza mtoto anao.
Tunaomba muheshimiwa toa tamko kwa idara zote husika, wasifanye mambo kuwa magumu. Wafanye due diligence yao na kufuata all the necessary procedures bila kumkatisha tamaa mtu mwenye nia njema ya kuasili.
Kifupi alidanganywa, angeibiwa, huo ni utapeli na ula rushwa. Hakuna malipo. Kama Yuko tayari anitumie ujumbe tuchunguze Ili aliyeomba hizo hela achukuliwe hatua. Hapa nahitaji ushirikiano wako tafadhali.
 
Hii ni solution Kwa Wanandoa wenye changamoto ya kupata watoto.

Mnaweza mkakubaliana na Mkeo, mkaenda kum-adopt mtoto wa miezi kadhaa then mkamlea na kumfanya wa kwenu.

Kama litafanyika Kwa upendo, inaweza kusaidia kupunguza watoto wa mitaani ambao wamekosa huduma na Walezi.

Wale ambao wataguswa kufanya hivyo vyema mkawahi mapema.

Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, "Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa"

Yakobo 1:27
Ahsante Sana kwa kujitoa kuelimisha, huu ndiyo ushirikiano wa wadau 🙏🏽
 
Back
Top Bottom