Unajisikiaje kumuona binti chuoni hapati mahitaji kisa hana pesa?

Chuoni hakuna sababu ya kushindana GPA. Mimi nimesoma chuo ambacho hostel ni kama Almas, mwaka wa tatu niliuza kitanda nikawa nalala kwa kuvizia na kwenye majengo mabovu.

Ada ni Mungu alipita kati tu. Kula tumepika sana na washkaji hostel. Tulinunua rice cooker, hilo hilo tunapikia maharage, ugali, wali, uji 🤣

Hapo bado stress za kukataliwa kufanya papers kwasababu ya ADA. Field nimeenda mkoani nikiwa nina nauli tu ya Tsh 20,000 nimelala sana stand halafu baridi kaliii, asubuhi unaamka kama vile kila kitu kiko poa🤣

Miaka 3 unasota chuo, unamaliza kwa kudra za Mungu unakutana na utawala wa kibwengo Jiwe kila siku anahuburi madaraja tu huku pesa anahonga wapinzani na kurudia chaguzi.

Unaamia kupiga mishe yoyote, naamua kuwa mlinzi Jiwe anazuia fao la kujitoa kwahiyo anafikiri watu wanaweza kufanya hizi kazi mpaka miaka 55?

Unaweza kudhani ni ndoto sometimes.
 
Nimesoma chuo,nilikua na suruali nne tu! Viatu pea tatu,mashati hayazidi 5! Msimu wa maembe,nilikua nakula maembe mchana,then nakula msosi usiku! Pesa ya boom hiyo hiyo nakata,nalipa nusu ada na admin coast! Nyie acheni tu haya maisha
Pole sana!
 
Pole kaka!
 
Ni ya mpito tu, ndio maana yuko hapo, kuboresha maisha yake. Mimi sikuwahi kuwaona au pengine wote walikuwa na hali nzuri. Nilipambana na hali yangu.
 
Nimesoma chuo,nilikua na suruali nne tu! Viatu pea tatu,mashati hayazidi 5! Msimu wa maembe,nilikua nakula maembe mchana,then nakula msosi usiku! Pesa ya boom hiyo hiyo nakata,nalipa nusu ada na admin coast! Nyie acheni tu haya maisha
Viatu pea tatu 3??. Watu tuna savaivu na pea moja.
 
Nenda kituo chochote cha yatima ukatoe msaada. Kama hujui vilipo sema hapa tukutajie makumi ya vituo vya yatima na wazee.

Kama unataka kusaidia katika elimu ya chuo. Pitia kwa dean ana list ya wanafunzi wanaosuasua fedha hasa vyuo private
Unajua nimeshaenda vituo vingapi vya mayatima kutoa nilichonacho? Kumsaidia yatima aliyepo kwenye kituo cha kulea yatima na kumsaidia yatima aliyeko chuoni unaona kuna tofauti kwako?

Kwanini kila mtu mnamuona limbumeni wa mapenzi hivi?
 
Yupo chuo gani?
 
Hii ya mimba imetokea juzi tu kwa jirani yangu, kuna binti yake anamsomesha kwa hela ya kudunduliza lakini mwanafunzi kapachikwa mimba na wahuni, halafu cha kuumiza zaidi binti hana mkopo.
Classmate wangu alipewa mimba uko kanda ya ziwa ila akaendelea na masomo. Kamaliza diploma mwaka jana kapewa mimba nyingine within 2 years. Sikuamini hiki kitu nilipoambiwa, yani uzuri wake ndio basi tena. Alafu wazazi wawili tofauti na wote hawana uwezo wa kulea watoto. Huyo classmate mwenyewe mama yao aliwalea kwa shida ni mapacha. Sijui ni laana au ng'ombe wa maskini hazai
 
Yani unashindia jero afu ukirudi mtaa ajira hamna na elimu uliyonayo ni general knowledge huwezi kujiajiri labda uchukue boda kwa mdosi uzungushe au ufungue kibanda cha chips. dah mmmk walah [emoji3][emoji3]
 
Hii ya mimba imetokea juzi tu kwa jirani yangu, kuna binti yake anamsomesha kwa hela ya kudunduliza lakini mwanafunzi kapachikwa mimba na wahuni, halafu cha kuumiza zaidi binti hana mkopo.
Muhuni kaona safi, vuta mtoto geto pika pakua wanaenjoy life.
 
Nilimuona akiwa hana furaha, mavazi yake na viatu vyake vilimtofautisha na wanachuo wengine!

Huruma ilinijaa ya kugawana chochote nitachokula au kupata. Aliponitajia jina lake nikajifanya kumfananisha na dada yangu hadi jina ili tu asinifikieie kuwa msaada wangu ulilenga kitu kwake.

Kwakuwa nilikuwa nimepanga geto nje ya chuo, nikamweka karibu ili atapohitaji kitu anijulishe au afike kwa kaka yake bila hata hofu.

Sikuwahi kumtaka kwa lolote, japo alijua sijatulia ila tuliheshimiana.
Nilifurahi kumuona mwenye furaha, amani kiasi na mabadiliko ya kimavazi.

Muda mwingi yeye aliniombea tu kwa Mungu, masela wangu pia waliamini ni dada yangu.

Najua akipitia comment hii anaweza kumbuka, japo kwasasa sijui alipo na namba zake zilipigwa pini na NIDA hadi sasa.
 
Hongera kaka, ndio ubinadamu huo.
 
Niunganishe nao maana watanzania tunapendana na tunasadiana
 

Yupo chuo gani mkuu?
 
Hongera kaka, ndio ubinadamu huo.
Asante sana.

Nilikumbuka mambo mengi sana nilipomuona, maana hata mimi niliwahi kusaidiwa na mtu asiyenifahamu.

Moyo wangu uliniuma kuona kama ni mtu aliyetengwa. Na mwanzo nilifikiria labda ni mgonjwa.
 
Mkuu,ikiwa kweli ulifanya hivyo kwa nia njema,basi nikwambie tu kuwa hauko mbali na Ufalme wa Mungu.
 
SAUT SAUT... Dah,ndugu yangu kajazwa mimba pale. Ashakuwa single mother, Nani atamuoa? Mabinti someni.... Watoto wa nje ya ndoa hukutanq na changamoto nyingi kimalezi hususan kihisia na kiuchumi. Mabinti epukeni watoto wa zinaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…