Unakumbuka nini kuanzia Mwaka 1998 hadi 2000?

Mwaka 1998
*World Cup ya France nikanunuliwa na bag ya dark blue iliyokuwa na ile nembo ya World Cup France
  • Bigi Jii za stika za Wachezaji wa mpira ukimpata Ronald Nazario De Lima wewe una bahati sana 😅😅🤣
  • Album ya Kofi Olomide Loi iliwika sana mwaka ule
*Mwaka 1999 ilikuwa saa 7 mchana narudi shule kikatangazwa kifo cha Nyerere, Marehemu John Komba alifyatua sana nyimbo za maombolezo
*Mwaka 2000 nilipata Kipaimara.
 
Shuleni kwetu tulikuwa na michango 3 maarufu,kama hujalipa hiyo husogei darasani!


1.UPE
2.ULINZI
3.UMITASHUMTA
 
Muhenga on flick!
 
year 1999, tumetoka fanya mazoezi ya graduation ya darasa la saba, mdogo mdogo tukapiga tz11 hadi home, umbali kama wa kilomita 4-5 toka shule hadi home, tunafika home saa 10 jioni, tunachungulia dirishani tunamuona mama na rafiki yake wanakodorea macho tv, huo haukuwahi kuwa muda wa mama kuangalia tv, kuingia ndani ndio tunagundua Nyerere hayupo tena.

Kesho yake Mwalimu Mkuu akatangaza hakutakuwa tena na graduation, shughuli ya primary ikaishia hapo, hata cheti cha leaving hatukupewa tena.
 
Kwa haraka haraka nakumbuka mwaka 1998 nilikua sebleni na baba tunaangalia tv tukasikia kishindo kikubwa nje....nikatoka kuangalia nguzo ya umeme tukijua ndio tatizo...baadae tunapata taarifa ni bomu limelipuka ubalozi wa Marekani pale opposite na ubalozi wa France...ilikua siku ya huzuni kwa taifa.
 
Basi mimi kipindi nasikiliza redioni natapata taarifa ya kifo cha Mwl Julius K Nyerere mwaka 1999 , niliona hapa Tanzania tumeisha...
 
1998 natoka Lusaka naelekea Cape Town kitongoji kimoja kinaitwa Gugulethu NY 21 House number 77 nilipofika Cape Town niliuliza hiace zinazoenda Gugulethu na nauli yake nilipanda Hiace mpaka Gugs nikashushwa mtaa wa NY 21 nikaanza kutafuta namba ya nyumba mpaka nikafika ndugu yangu aliponiona hakuamini kabisa maana alinipa Address nikiwa home Tanzania baadae mawasiliano nilipoteza ila Address yake niliandika nyuma ya Passport ndugu yangu alifurahi sana na hakuamini...ndio mwanzo wa Mapambano ya SA huko Cape stad The City of good hope au wenyewe wanaiita Mothercity nikasota mwaka mmoja kwa kazi za magari mara supermarkets ila mwaka 2000 nilipata kazi ya ndoto yangu Debeers Marine kama saidia fundi Engine room baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu na kupelekwa vyuo nikawa Fundi kamili Engine room kweli maisha tumetoka mbali sana...
 
1. I need a girl ya diddy inanikumbusha mara yangu ya kwanza kuingia club pale PAN AFRICA HOTEL MOSHI 2. mwaka 1998 gavoo ilifuta paper ya 4m4 baada ya kuvuja nchi nzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…