Unakumbuka nini wakati unafanya mtihani wa Kidato cha Nne

Unakumbuka nini wakati unafanya mtihani wa Kidato cha Nne

2012 Nilifanya pepa ya chemistry ya kupima uelewa mpaka nikawa nafurahi huku najibuu...!! matokeo kutoka ndalichakoo akatunyoosha balaaa shikamoo mama ndalii 😀 😀
Aisee kumbe mtoto wa juzi
 
Nimepiga awamu 2 .2004 nilipata channel Five masomo yote saba.Nikarudi kivingine 2007 nikapata C nne.Nachokumbuka kwenye paper la mathee nilikariri swali lolote la polynomial function likija jibu lake ni all real numbers except 4.Kwa sasa nadunda tuu.Asante Mama ,asante Mungu.
 
Sintosahau paper limevuja, tukafanya solving usiku mzima, kuingia kwenye mtihani kitu chenyewe kabisa, ile imefika nusu saa tukaambiwa tusimame wakakusanya makaratasi yao wakatugawia mtihani mwingine, nusu ya darasa tuliangua vilio
Chai
 
Nakumbuka ilikuaa paper la math, yani nilivyoona paper nikajua A uwakika si nikashangilia kwa nguvu kabla paper lijanza[emoji28].

Msimamizi akaja kunikagua kama nina chabo, lakini sikuwa na kitu nilikuwa kipanga kweli wa math japo nilisoma shule ya kata.

Na kweli matokeo yakivyotoka me ndio mwanafunzi wa kwanza kata ya chanika kupata A ya math, kutoka shule ya kata.[emoji1487]
Chai
 
Those days, mi nasolve maswali yangu kadhaa , rafiki wa karibu akawa amelala huku akisema " hayo hayatoki aisee, tulale tu" mi nikawa nafutilia vizuri sana yale maswali...kesho yeye alianza kupewa paper , naona mtu anageuka kuniangalia kwa huzuni...ile kufungua tu paaaaap, maswali kama yalivyo
Aisee
 
99 hiyo....naenda kupiga paper ya chemistry kesho yake....nikapiga konyagi nikawa top....asubuhi naingia kwenye mtihani sina habari niko wayuwayu....hangover kama India...Mzee mzima nikagonga nikasepa mchana tulikua sijui na paper ya kiswahili...nikapiga safari mbili...zile za mbuyu...! Ndio nikaenda kwenye paper la kiswahili

Matokeo..Chem C
...Kisw A

Mpaka leo konyagi sijaiacha....japo ladha yake imebadilika..!
Chai
 
Kipindi hicho, sie wahenga, ule mtiani uliofutwa! 1998,kwenye paper ya Physics practical, nikawa nachora kwa peni, zimebaki DK 10,muda uishe, ticha wangu akaja taratiiiibu akaninonngoneza, "ukichora kwa peni, unapigwa faini, hiyo paper ndio umeferi" Nilihisi nimemwagiwa maji,nikaona ndoto zangu za kuwa engineer ndio zimeisha, nilikuwa nachukua PCM, sie ndio wale tulikuwa tunajiita sayansi pure, staki combination nyingine, nikaweka nguvu kwenye PCM tu,!
Paper likaisha, jioni wakaja wadogo zetu na kaka zetu wa form 3,2,1,na five na, six, wanatuuliza paper vipi? Mi nilikuwa mmoja wa vipanga pale shuleni, form 4 yetu, ilikuwa inategemewa ifute machozi na Historia ya kufelisha, kabla yetu, shule ilikuwa haijawahi kupata div one au two, ya juu kabisa ilikuwa div 3,ya mwisho!
Ikafika jioni, taarifa ya habari,tukasikia paper imefutwa! (Mungu ananjia nyingi za kumfikisha mja wake apaatakapo) , nikasikia ahueni, tukrudi January 1999! Nikajipanga sawa sawa, piga paper vibaya Sana, nikaitoa kimasomaso shule na one ya point kadhaa, PCM ni Vibanda tu!
Fast forward, Leo na kula matunda ya uinjinia, nikiwaza, nimesoma shule haina umeme, nimetumia kibatari na TAA za chemli,maji mpaka mtoni au ziwani, hakuna smart phone, wala internet, techinolojia kubwa ilikuwa radio zenye FM!, harafu Leo, kuna mtoto hata kama upo st kayumba, material ya kusoma yapo kila Kona, harafu unafeli!
 
Nilipata dv four 😂🤣🤣🤣🤣🤣
Ila mindset ya kusoma Azania ilinisaidia sana chuo..
Maana nilianziaga certificate🤣🤣🤣 up to the top
Ndiyo SIASA hiyo BOSS wangu 🙏🏽🙏🏽
wee ngoma ya ndalichakoo ilikuwaa
Hapo utasikia kuna SPECIAL SCHOOLS kama MZUMBE, ILBORU, TABORA BOYS na KIBAHA SECONDARY. Lakini ukijaribu kuangalia TOP TEN YA MWAKA 2007 ya KIDATO CHA NNE, wote niliwaburuza m'maee...😂😂
 
Back
Top Bottom