Pre GE2025 Unawaongezea wananchi gharama za maisha halafu useme wakuchague ukaumize tena, CCM mmekuwaje?

Pre GE2025 Unawaongezea wananchi gharama za maisha halafu useme wakuchague ukaumize tena, CCM mmekuwaje?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kukatika katika hovyo kwa umeme

fukuza fukuza ya machinga

kuongeza nauli hovyo hovyo

ubovu wa miundombinu ya barabara

kukwama kwa miradi mbalimbali

mfumko wa kutisha wa bei

Rushwa iliyokithiri

mnataka mchaguliwe kwenda kuongeza tena gharama za maisha? yaani CCM mmepoteza mvuto na mmepoteza mwelekeo
Safi! Safi sana. Nakushauri yooote haya ingiza kwenye Ilani ya CHADEMA ya Mr Tundu 2025 bila shaka mtajishindia mkaifilisi TANESCO.
 
Tatizo wananchi wengi ni mazezeta ewala ewala kibao
 
Swali sio Watanzania tuko wangapi, swali ni kama sio CCM ni nani?.
P
Mbona jibu limeeleweka na hilo tena unataka kulipindisha??

Yaani ndani ya hao wananchi milionin60+ wanakosanikaje watu nje ya CCM wa kuongoza nchi hii??

Hao CCM wana ubora gani ambao unakufanya kuuliza wakitoka wao nani ataongoza nchi!!??
 
Ni lini hali hizi hazikuwepo na bado CCM imekuwa inachaguliwa!, what is the difference this time?

Lets suppose its true CCM imepoteza mvuto na imepoteza mwelekeo, hivyo CCM inapaswa ipumzishwe, aje nani?.
P
Kwa taarifa yako kama ccm imeweza kutawala nchi hii muda wote huu, hakuna chama kitashindwa. Nenda hapo Kenya kawaulize wale waliokuwa wanasema KANU tu ndio inaweza kuongoza Kenya, na utazame kinachoendelea Sasa baada ya KANU kuelekea kuzimu.

Watu wenye mitazamo ya kizee tu ndio Bado wamenasa kwenye hiyo propaganda ya ccm kuwa wao tu ndio wanaweza kuongoza nchi.
 
Upuuzi TU uliondika hapa. Ajuza anatafuta huruma apitishwe bila mchakato wakati MaRais wote waliopita walipitia michakato rasmi ya chama. Huo alionao ni wa kuokota.
Mchakato utafanyika na hakuna wa kumshinda huko ccm Kwa Sasa,kama yupo mtaje.

Mwisho Rais ni Samia Hadi 2035
 
Who are they? Where are they?
Na wanapitia chama kipi?
We start with Free and Fair Election 🗳
Bila mizengwe mizengwe ya aina yeyote ile !!
Likiwezekana hilo kila kitu kitawezekana !
Government of the people by the people for the people !!
 
Sio sisi, ndio kanuni ya dunia nzima, inatumia kanuni za Newton kilichopo kitaendelea kuwepo mpaka kitokee kingine cha kukisogeza, na kama kinatembea kitaendelea kutembea mpaka kitokee kingine cha kukisimamisha!.

Hata tukifanya uchaguzi huru kabisa na wa haki kabisa, katika hawa waliopo, nani anaweza kui replace CCM, tukaipa Ikulu yetu?.
P
Ingekuwa ccm inaweza kushinda kihalali, tusingekuwa tunaona uhayawani unaoendelea kwenye chaguzi zetu. Sio kwamba ccm inaogopa uchaguzi wa halali kwa bahati mbaya, inajua hiki sio kizazi Chao, na kitendo Cha kuruhusu uchaguzi huru tu ndio itakuwa mwisho wake. Na hii ni nature kuwa watu huchoka kitu baada ya muda fulani.
 
Sio sisi, ndio kanuni ya dunia nzima, inatumia kanuni za Newton kilichopo kitaendelea kuwepo mpaka kitokee kingine cha kukisogeza, na kama kinatembea kitaendelea kutembea mpaka kitokee kingine cha kukisimamisha!.

Hata tukifanya uchaguzi huru kabisa na wa haki kabisa, katika hawa waliopo, nani anaweza kui replace CCM, tukaipa Ikulu yetu?.
P

Ukiruhusu huru na haki katika chaguzi hicho kitakacho shinda ndo kitakuwa replaced
 
Back
Top Bottom