Unaweza usiambiwe, ila sio vizuri kufanya mambo haya

Ukifika kwenye ukumbi wakati wa harusi acha ku"focus" na suti ya bwana harusi wala gauni la bibi harusi, wazia chakula tu. Hii inasaidia kukuepusha na umbea usio na maana 🤓
😅😅😅
 
Huku kwetu ambapo chakula ni chekwa,ukienda msibani na usipokula,unatafuta kesi ya jinai.Unawekwa kundi la wenye dharau sana.Jiandae kufanyiwa kisasi likitokea tukio kwako.
Ilishahawahi tokea mtaa fulani jijini yule Mzee alikuwa hana tabia ya kula kwenye misiba ya majirani kisa ni Mfanyakazi Wizara ya Afya kuna siku alifiwa kwake kapika misosi mingi tena ya maana. Watu hawakula mpaka vijana wa mtaani walikatazwa na Wazee ilikuwa aibu na fedheha sana
 
Kuishi na jamii kunahitaji akili zaidi kuliko ubwana mkubwa na ufahari.
 
ukienda kumuona mtu muone halafu ondoka usikae sana mpaka akushtue
Privacy muhimu ila wabongo wanapenda umbea tena aje alafu akukute upo na mgeni jinsia tofauti basi ndio atakaa wee..! Basi hadi athibitishe anachokiwaza!
 
...ukienda kwa mtu mda wa chakula, kama hamkuwa na miadi na unaona kabisa menu iliyopo haiwezi kukodhi wao na wewe, vunga tu, omba maji au juice.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…