Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Niliandika juzi nikajibiwa kashfa, hata wale waliouwawa wakasema ni Panya road hawakua panyaroad
 
hahahaaa nmependa hiyo aya ya mwisho
 
wewe pia panyaroad mwingine , unafananishaj mtu aliyesababisha ajali kwa ulevi na anaevunja mlango kisha anavunja vitu vyako vya ndani akiwa timamu anakupiga mapanga na anakupora vinavyobebeka , unaezaj msapoti mtu wa hv km ww sio mmoja wao
 
Uelewa wa watu wengi humu jf au Tanzania una walakini.
Sasa sheria zilitungwa ili zifanye kazi gani kama kuwa tu mtuhumiwa unauliwa?
Hawa wanaotafuna mabilioni ambayo yangejenga health center na kununua dawa si wauaji?
fuatilia acha mawenge ,au ww ni mmoja wao , unakimbia nn ? kama ww sio mtuhumiwa mf huko chamaz washaambiwa kila kitu , saa 7 usk unakuwa unaenda wp wkt waliambiwa doria kuanzia saa 3 usk ukiitwa usikimbie nami nmefanya hivyo mara tano wala sijawai kuzurika
 
acha kuchanganya mafaili , akili kisoda hata mm ni mpinzan ila usalama , kawafuate walibyia wenzio ambao kila kitu mnaona ni fursa ya kuleta siasa
 
Wasubiri wakishauliwa ndugu zao kimakosa kwa kuhusishwa na panya road ndio watakapoona umuhimu wa haki za binaadamu.

Mhukumu mtuhumiwa baada ya kumpa nafasi ya kijitetea na kujiridhisha kwamba huyu ni kweli mhalifu.
unaish wap ?
 
Kwa hiyo bw Robert, ukikutwa na na panya road, adhabu yako ni kifo?
Huwa nasoma makala zako nakuona kama ni mtu mbobevu,
Kumbe unashabikikia uuwaji wa watuhumiwa,?
Mahakama zifutwe ili police watoe hukumu kwa watuhumiwa,
saa 7 usk upo na panya road unafany nae nn , hlf msijitie uchiz kama hamjui tunazungumzia kuwa wanashikwa usiku , doria ni usiku , au kwenu doria ni mchana , NYINYI MTAKUW WAHALIFU NDIO MAANA MPO HAPA KUTETEA UHALIFU
 
Kiswahili cha ndani sana umetumia mku eti 'majambawazi' haa haa.
 
Bro unakaa wp
Mm sisi wa yombo tandika ndo tunajua tabu tunayopata kwa hawa panya road
 
umewai kutana nao au unahis ww una akili kuliko polisi ? mm nmeona wanawatishia polis huku polis wanawataka wajisalimishe , bahat yao siku ile polis walikuwa waoga , watoto walikimbia
 
Bila Shaka walikupa bapa za panga za kutosha mkuu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Maana nasikia vitoto vinabonda hivyo ni laana ,usiombe kukutana navyo
hahaaaa hao wanatoto hawapig bapa siku hz ni mapanga ya uso , jana imenibid niingie hasara nihamie mbez beach kutafuta usalama
 
Wanafki tu hawa, Kuna suki nilienda Amana hospitali usiku aisee nilikuta watu wamekula mapanga ya hao panya road aisee huwezi waangalia mara mbili, kuna miwatu humu nafikiri inanufaika na hawa panya road.
pale yombo vituka hospotal ( malawi ) xmas mwaka jana , new yr 2022 na pasaka zilitembezwa panga yombo vituka ile si chini ya watu 10 mahututi kweny hiko kituo cha afya , hlf ipo ng'ombe inachoma wez ila inatetea hawa wauaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…