Unywaji wa vinywaji hivi nini matokeo yake miaka 10 ijayo?

Unywaji wa vinywaji hivi nini matokeo yake miaka 10 ijayo?

Inaweza kuwa ni kweli!...lakini ni chakula gani sasa iv kiko salama?matunda na mboga za majani zinapigwa sumu mpaka zinachanganyikiwa,nafaka zinahifadhiwa kwa sumu,sasa wapi tutaponea?tunakunywa soda kwa sababu ni afordable+upatikanaji wake hauna kona kona!...MBELE KWA MBELE DEREVE KANYAGA WESE
 
Sababu kubwa ni ufinyu wa uelewa elimu lishe. Miaka ya nyuma nikiwa kijana mdogo na mwenye uelewa finyu juu ya elimu lishe nilikuwa nawashangaa sana marafiki zangu wazungu ambao mkienda kugonga bia jamaa zangu hao unakuta wanakunywa bia moja au ikizidi sana mbili. Wakikuona unakunywa redbull ya kopo miaka hiyo wanakushangaa. Baadae ndiyo nikagundua umuhimu wa kuwa makini kwa kila unachotia tumboni, kama unataka kupunguza safari za kwenda hospitalini. Jamii zetu kiukweli zina shida kubwa sana kwenye kudhibiti ulaji na unywaji. Unakuta kijana anapiga MO energy 4 tena anapiga mix na konyagi au vile vi smart gin daaah...
 
Za kijiweni eti yule mkata umeme wa hospitali kubwa hali chochote zaidi ya matunda na mboga. huu ni unyama sana ila mimi ningeweza mana napenda sana mboga mboga
Decoded CEO wa MNH, Janabi
 
Soda nimekunywa toka nikiwa na miaka 2 hadi leo.

Spirits ndo mbaya, soda hazina tatizo
 
Mwaka jana nilienda home kusalimia nikakuta bi mkubwa anajenga banda la nguruwe basi nikasimamia kidogo mafundi wakawa wamemaliza katika kusafisha mazingira niliokota kopo za energy drink za azam na mo extra zaidi ya 70 na hizo ni zile wanazokunywa wakifika kazini kulikua na mafundi wanne tu kwenye kazi kile kitu kilinishangaza na muda wa kazi ilikua kama wiki mbili na kidogo nikaja kumuuliza fundi mkuu vipi mbona energy nyingi? Akanijibu asee siwezi anza kazi bila chupa moja mchana akila anakunywa au apige soda alafu jioni akifunga kazi lazima apitie dukani anunue moja kwa siku anasukuma 2 mpka 3 asee ni hatari
Wenye viwanda wanaweka kemikali za kujenga dependency
 
Miaka 10 ijayo madaktari watakuwa bize sana. Nna kiduka mtaani kwetu nauza na vileo, kuna mteja mmoja kwa siku anaweza kunywa Ambiance 5 kwa siku na kila akinunua Ambiance ananunua na Energy. Just imagine nini hatima yake? Kwa wasioijua Ambiance ni sawa na Kitoko/Double Kiki huko Daslam
Mteja mtarajiwa wa Mloganzila huyo, juzi juzi tuu nimeuguza ndugu yangu kwa matatizo ya ini na Figo, akafanyiwa dialysis kwa gharama kubwa sana but still Mungu akampenda zaidi. Nikapata muda wa kujifunza kuhusu hili tatizo la Figo aiseeee kumbe mgonjwa kabla ya kufanyiwa hiyo dialysis anachanganyikiwa na kuongea kama amedata kabisa, baadae jinsi wanavyomsafisha Figo hiyo hali inapotea.
 
Hao madokta wenu wa kisabato watawaua kwa hofu

Binadamu wa zamani walishindia matunda na nyama mbichi lakini wako wapi? wamekufa wote

We achana na sisi kufa kupo tu
As long as tunaenjoy
Tusitishane.

Niko napata coka,supu ya makongoro na chapati nne hapa . Alaaah
Inaitwa...wajaze hofu na mwisho wauzie suluhisho
 
Hao madokta wenu wa kisabato watawaua kwa hofu

Binadamu wa zamani walishindia matunda na nyama mbichi lakini wako wapi? wamekufa wote

We achana na sisi kufa kupo tu
As long as tunaenjoy
Tusitishane.

Niko napata coka,supu ya makongoro na chapati nne hapa . Alaaah
iyo coca ya mililita 350, ina sukari zaidi ya vijiko 7(suger) samr time unakula chapati nne (sugar) ilipikiwa mafuta ambayo hayajasafishwa(saturated fatty,fat=^sugar unakunya supu ya kongoro ngo'mbe amekuwa kwa booster, huyo msopo wote ni uchafu plus supu ime ongezwa maji machafu ya duwasa muda si mrefu unakunywa wadudu, wajitaidi waweka chlorine nayo inaharibu pinel gland
 
Back
Top Bottom