Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

Mzee
Mambo sasa yanaanza kujianika kwenye mkeka wa uhakika. Ukweli unauzidi nguvu uongo kama mbegu inapochomoza kwenye udongo. Ukweli unaanza kutamalaki kama mashabiki kindakindaki au mwalimu na chaki. Tumedanganywa sana na kwa muda mrefu.

CAG amemwambia Mhe. Rais kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara ya mabilioni ya shilingi za kitanzania kwa miaka mitano sasa. Lakini Mwendazake na wenzake wamekuwa wakituamisha kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa faida. Katika kuchagiza hilo, ATCL imekuwa ikitoa hadi gawio kwa Serikali. Tulikuwa tukidanganywa.

Serikali ya Mwendazake ilijaa propaganda na uongo mkubwa. Tumeanza kuona upande wa pili wa tulichokuwa tukiambiwa. Ukweli unaupiga kumbo uongo uliotaka kudumu kwa muongo mzima. Amini nawaambia, hilo ni tone tu kwenye bahari ya propaganda zilizokuwa zikiendelea wakati wa uongozi wa Mwendazake. Mengi yanafuata baada ya tuta.

Ndugu yangu Kichere, angekuwepo Mwendazake ungeiwasilisha Ripoti ile inayoanika ATCL na hasara zake?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Mzee tupatupa kama ripoti ya CAG inasema ATCL imejiendesha kwa hasara ya miaka mitano, je hiyo miaka mitano kulikuwa na ndege ngapi?
Ninachojua ndege hizi kama zimefanya kazi zina miaka miwili na ushee, na ATCL imekuwa ikijiendesha kawa hasara toka ndege zife na ilibaki na madeni amabayo serikari ilikuwa inayabeba,

Kama kulipa wafanyakazi wakiobaki,
Kulipa ghalama za kimataifa na mengine wakati haina ndege.
Sasa hii miaka miwili na kitu hizo ndege zitalipa hayo madeni na kuanza kujiendesha kwa faida?
Kama mnataka kuchambua hiyo taarifa ya CAG Basi leteni hapa taarifa kabla ya ndege ununuliwa kulikuwa na deni la sh ngapi na sasa shirika lina deni la sh ngapi,
Na bado mjue hizo ndege bado shirika linailipa serikari mtaji wake.
 
Sasa kwa maigizo hayo mpaka ya kuleta gawio, hapo tunakuwa na mashaka na mambo mengi tuliyoambiwa. Kama mtu anaweza stage mpaka kawio huyo ni mwanaproganda hatari. Swali ni kwanini afanye hivyo? Motive haiwezi kuwa na jema. Hiki ni kipande cha barafu inayoelea. Sifa ya marafu inayoelea baharini eneo linaloonekana uwa ni dogo kuliko lililozama kweye maji.
Muda utasema mengi

acha CAG afanye kazi yake, he wasnt that bad tunaweza kusema ni mapungufu kuna vitu vingine vingi alifanya sawa tu kwahio mwache CAG afanye kazi yake
 
acha CAG afanye kazi yake, he wasnt that bad tunaweza kusema ni mapungufu kuna vitu vingine vingi alifanya sawa tu kwahio mwache CAG afanye kazi yake
Bila transparency kuna mengi kama mtu anaweza kustage gawio, 😂😂😂 basi kuna propaganda nyingi zilikuwa staged. Mojawapo ni tunajenga kwa pesa zetu
 
Ninatumaini Waziri wa Fedha atakuja na majibu ya kuridhisha kuhusu the real state of affairs za mashirika yote ambayo yako chini ya registrar. Je walipokea gawio (yeye alipokea on behalf of govt) kweli au ilikuwa mambo ya red carpet 😷😷😭😭? He should go
 
anaweza kujibu hayo maswali ni yeye mwenyewe but mm i think airlines ni muhimu sana, serikali inaweza kuikumbatia ATCL mpaka ikapata faida
Kwa hasara hii bado unataka serikali endelee kuikumbatia ATCL,

Mkuu haupo serious,kama upo serious basi utakuwa na matatizo ya akili sio bure
JamiiForums-1643154238.jpg
 
Ninatumaini Waziri wa Fedha atakuja na majibu ya kuridhisha kuhusu the real state of affairs za mashirika yote ambayo yako chini ya registrar. Je walipokea gawio (yeye alipokea on behalf of govt) kweli au ilikuwa mambo ya red carpet 😷😷😭😭? He should go
Ni rahisi tu, si ataonesha gawio hilo lilitumika kwa ajili ya nini, na kila mtu ataridhika na kulifurahia gawio hilo! Labda kama matumizi hayakuidhinishwa kwa kufuata utaratibu.
 
Niachojua uchumi ni kama Nyuki. Hakumbatiwi wala hapigwi Busu. Dawa ni kuacha tu ajipambanue mwenyewe. Tulifikia mahali mpaka kunguru wanakata umeme Dar, tukafikia mahali mpaka vijana wa CCM wakatuambia wanataka kuwatia mimba wake zetu bila kujali wengine ni mama zao. Walifika mahali mpaka wakaanza kusema kama huoni ndege zinavyoleta hela wewe sio mzalendo.

Mungu tu anajua hawa watu na hii nchi.
Ulevi wa madaraka ni mbaya kuliko kulewa vilevi!! Leo ati "chumu asema 'kama' walikosea anaomba radhi... maneno meeengi sasa akamtie mimba mamaake"
 
siwezi jua alikua na lengo gan but an airline is very important hasa iki kipindi ambapo covid ni tatizo na watanzania wamezuiwa kusafiri mfano kurudi nyumbani
Kama amendanganya hapa je nimangapi atakuwa ametudanganya?
 
Bado ile miradi ya Chato ina wizi wa kutisha.
umeona eee! Binafsi naomba ukaguzi maalum wa miradi ya Chato, Ofisi ya RC Dar es Salaam enzi za Bashite na zile fedha zilizokuwa zikigawiwa barabarani na kwenye ziada za mwendazake
 
Kwa hasara hii bado unataka serikali endelee kuikumbatia ATCL,

Mkuu haupo serious,kama upo serious basi utakuwa na matatizo ya akili sio bureView attachment 1737744
Mkuu kuna akili na akiliccm ambazo hazijawahi kuwa akili ndio maana wenye akili wakikosoa au kushauri "huwa si wenzao au wametumwa na mabeberu"
Mungu atunusuru...
 
Naomba ukaguzi wa matumizi ya Bunge chini ya Job Ndugai
 
Hapa sasa ni kama msiba umeletwa kupisha uchunguzi - wacha tuone nyuso za waimba mapambio zitakavyosoma!!
 
Nakumbuka CAG Assad alipogusia tu kwamba kuna 1.5T hazijulikani zilipo alipingwa na kuhojiwa hadi bungeni na kufutwa kazi kisa tu eti serikali chini ya jemadari yule haziwezi kupotea fedha hata sent moja. Sasa hiki tukichosomewa jana ni ubadhirifu chini ya serikali ya kiongozi gani?
 
Chini ya fisadi na mbadhilifu Ndungai
Huyu babu mi namchukia sana, yani nikimuona kwenye t.v naona kama nimeona kinyesi, anatakiwa akimaliza muda wake wa Uspeaker, afutiwe kinga ya kushtakiwa aliopewa na marehemu. Halafu anyongwe kwa kuendekeza tumbo lake huku nchi ikiharibiwa.

Hasa kwa ushenzi wa;

1) kujifanya ana msimamo wa kukataa Report Ya CAG aliopita, kisa CAG aligoma kupelekeshwa na Marehemu ili atudanganye ATCL na TCCL zinaendeshwa kwa faida. CAG aliona mbali, akaona bora afukuzwe kazi kuliko kuungana na Marehemu na Speaker kudanganya watanzania. Sasa mungu amewaumbua na atawaumbua zaidi.

2) Kuapisha wabunge hewa bila uchaguzi na kuwaapisha hao Covid 19.
 
1617022021785.jpeg

'… Nampongeza Mh.Rais kwa ununuzi wa Ndege ambao tumeambiwa zimeanza kuingiza Faida bdani ya muda mfupi…tehe tehe (cheko la kebehi) maana kwny hili lazima tukiri sie tulishindwa…'-Jk


Pia CAG atuambie nani anachomekea figure za deni la Taifa hadi linakuwa kwa kasi wakati Hayati alikuwa anatumia fedha za ndani kujenga miradi yote
 
Whether it makes profit or not, ndege lazima ziwepo na wale wanaosomea urubani wapate pia ajira
kwani lazima uhalalishe uwepo wa ndege kwa kudanganya kwamba tunapata faida tu? kwani ukisema ukweli ili turekebishe na ndege ziwepo zile tu tunazoweza kuziendesha shida iko wapi?
 
Back
Top Bottom