Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Nithibitishe mara ngapi ?

Hivi unajua ya kuwa hakuna kitu chochote chenye ushahidi mkubwa na WA wazi kuzidi uwepo wa Allah ? Yaani hata uwepo wako wewe ushahidi wake sio mkubwa Wala wa wazi kuzidi ushahidi wa uwepo wa Allah.

Ndio maana hamjawahi kuthibitisha kutokuwepo kwake.

Ukiona mbingu, Ardhi, uwepo wako wewe vyote ni ushahidi wa kuwepo kwa Allah.

Niliweka andiko huko nyuma kuthibitisha uwepo wake.
Uwepo wangu mimi, unathibitisha vipi uwepo wa huyo Allah?

Mbona mimi simjui?

Ardhi ina thibitisha vipi uwepo wa huyo Allah?
 
Nimesoma maoni yako vzr rafiki yangu ...lakini kumbuka mambo mabaya yanayotupata msabibishi si mungu ...

Mungu anapenda watu wamwabudu kwa hiari yaani kwa kupenda ,alikuwa na uwezo kutuumba tuwe ka roboti ili kwamba tufanye atakacho yeye lakini yeye ametupa uhuru wa kuchagua tumtii au tusimtii

Pia mungu hakumuumba shetani ,aliumba malaika wakamilifu huko mbinguni ila malaika mmoja alitumia uhuru wake vibaya ,kwakutamani kuabudiwa awe ka mungu ndo huyo malaika mwovu anaitwa Shetani

Na matokeo yake huyo shetani alipinga enzi ya mungu kutawala akamwasi Mungu.Akaja duniani akanzisha uasi kwa wanadamu wasitii maagizo ya mungu.

Kumbuka pia mungu alimwambia mwanadamu matokeo yangekuwa nini ikiwa angekosa kutii maagizo hayo

Kwa hiyo Mungu ameacha muda upite kuthibitisha ikiwa wanadamu bila mungu wanaweza kujitegemea wenyewe? Mungu sio mtawala wa ulimwengu huu anayeoongoza ni shetani

Hivyo mambo yoote mabaya tunayopata sasa ni matokeo ya utawala wa shetani ..suluhisho ya matatizo haya ni kusubiri utawala wa mungu uje tena unaoitwa Ufame wa mungu ..


Kwa maongezi zaidi 0624009037/0717382740
Fatilia debate nzima...maana watu wamechoka kujibu hii hoja
 
Basi Akili unayosema tumepewa na huyo Mungu ya kupambana na mitihani ya kidunia ni DHAIFU sana na haina maana yeyote wala msaada wowote kwa binadamu.
Tuna akili ya kupambana hapa duniani ila hatuna uwezo wa kumzidi muumba .
 
Hapana huu si utawala wa mungu ..mtawala ulimwengu huu ni shetan na mungu kaacha ili athibitishe kuwa utawala wa shetan umeshindwa kuongoza wanadamu ndio maana tunasubiri utawala wake uje
🤣🤣🤣🤣Duu...so kaumba dunia kamweka nyoka atutese ili kuprove ye ana nguvu. It's lyk useme wazazi wako wakuzae afu wakutupe barabarani miaka na Miaka ili waone Kama utaweza kuishi afu baadae ndo wanarudi...🤣how is this not evil
 
kama Mungu hayupo, ni nani aliumba dunia na viumbe hai vyake.
Kwanza kwa nini unadhani Dunia ili umbwa?

Ume wezaje kuamini kwamba Mungu usiyemjua na haujawahi kumuona na kumthibitisha , kwamba hajaumbwa?

Ila Una shindwa kuamini dunia unayo iona na kuithibitishia ipo, kwamba na yenyewe haijaumbwa?

Kwa nini unashindwa kuamini dunia haija umbwa?

Ila una amini Mungu haja umbwa?
 
Mungu ni mmoja hakuzaa wala hakuzaliwa na hakuna kinachofanana nae.
Ndg elimu ni pana sana. Kama unataka kumelewa zaidi soma hao Masheikh na Mapadre wamesoma ndugu acha masihara na mambo ya imani.
🤣Hao ma padre na mashehe Hadi Leo hawawezi kukubaliana kuhusu Mambo ya dini zao...Kama ingekuwa simple hivyo kungekuwa na dini moja na dhehebu moja ila Kuna dini nyingi ma madhehebu mwengi katika kila dini...which means hao wasomi wako nao hawaelewi
 
Uwepo wako wewe hapa duniani ndio unathibisha kama Mungu yupo

Na Ili upate uhakika katika hili nenda ukamulize baba yako shahawa zake zilizokuleta wewe hapa duniani yeye alizipata wapi atakuwambia alitunukiwa na Mungu

Kama atakupa jibu tofauti uje utuambie hapa hizo shahawa baba yako alizinunua katika super market gani?

Maana mbele ya Mungu wewe si chochote ila shahawa za baba yako
🥺Kwa hiyo tunatunukiwa shahawa duu...sijui Mimi nitatunukiwa lini maana mi sijawahi fatwa na Mungu anipe shahawa...au nyie wadau vipi huko
 
Tuna akili ya kupambana hapa duniani ila hatuna uwezo wa kumzidi muumba .
Kama tuna Akili ya kupambana
hapa hapa duniani, kwa nini tunashindwa kutumia Akili hiyo kuzuia majanga ya asili ya hapa hapa duniani?

Huoni akili hiyo unayo dai tumepewa na huyo Mungu ya kupambana na mitihani ya kidunia
(majanga ya asili yakiwemo) ina UDHAIFU mkubwa sana, hapa hapa duniani?
 
Mbinguni ni kule Roho huenda zikitoka kwenye miili yetu!!
Una ushahidi gani kwamba mwili una roho? Na roho ni nini? Na mbinguni ni wapi, ipo katika universe yetu...coz zamani ilikuwa mawinguni ila wamehama coz binadamu katengeneza ndege na rocket so wamehamia wapi jamani 🤣
 
Kama tuna Akili ya kupambana
hapa hapa duniani, kwa nini tunashindwa kutumia Akili hiyo kuzuia majanga ya asili ya hapa hapa duniani?

Huoni akili hiyo unayo dai tumepewa na huyo Mungu ya kupambana na mitihani ya kidunia
(majanga ya asili yakiwemo) ina UDHAIFU mkubwa sana, hapa hapa duniani?
Majanga ya asili sijui vifo ni mambo yapo nje ya uwezo wetu ...Sisi binadamu hata kuishi hatuna tumaini la kuishi milele ila Mungu ndio anajua .
 
Binadamu kapewa akili ndio maana anaweza kupambana dhidi ya mitihani pia ni kiumbe bora bora kabisa.

Hata shule mnapewa mitihanu kujua kutokana mmesoma.
Ila mtihani ni WA SoMo moja maswali sawa na mda wa masaa sawa Kwa watu wote, na watu wote mmepitia same syllabus. In lyf Kuna watu wa mazingira tofauti hence dini tofauti na pia akili na Mali tofauti so uwezo wa watu kuamini dini fulani as real unatofautiana accord to akili, ukuaji, mazingira na Mali. So how is it fair...afu wengine huu mtihani wanafanya miaka 3 wengine miaka 80
 
Kwanza, kwa nini unadhani ulimwengu uliumbwa

Nadhani hapa logic imekamilika.
Sawa ulimwengu haujaumbwa na umetokeza wenyewe tu. Lakini nani ana hakika kama ulimwengu umejitokeza tu hauna Mwanzo Wala mwisho??

Mantiki ni kujibu swali na si kushambulia wanaoamini kwamba Kuna Mungu.

Jee unaweza kusema ni kwa nini wewe ni binadamu na si Ng'ombe??
 
Tuna akili ya kupambana hapa duniani ila hatuna uwezo wa kumzidi muumba .
Kama tuna Akili ya kupambana
hapa hapa duniani, kwa nini tunashindwa kutumia Akili hiyo kuzuia majanga ya asili ya hapa hapa duniani?

Huoni akili hiyo unayo dai tumepewa na huyo Mungu ya kupambana na mitihani ya kidunia
(majanga ya asili yakiwemo) ina UDHAIFU mkubwa sana, hapa hapa duniani?
Majanga ya asili sijui vifo ni mambo yapo nje ya uwezo wetu ...Sisi binadamu hata kuishi hatuna tumaini la kuishi milele ila Mungu ndio anajua .
Kama majanga ya asili yaliyopo
hapa hapa duniani yapo nje ya uwezo wetu,

Na wewe ulisema na unadai, Mungu huyo alitupa "Akili" ya kupambana na mitihani ya kidunia ni UONGO.

Na kama alitupa hiyo Akili , Basi Akili hiyo ni DHAIFU sana.
 
Sawa ulimwengu haujaumbwa na umetokeza wenyewe tu. Lakini nani ana hakika kama ulimwengu umejitokeza tu hauna Mwanzo Wala mwisho??

Mantiki ni kujibu swali na si kushambulia wanaoamini kwamba Kuna Mungu.

Jee unaweza kusema ni kwa nini wewe ni binadamu na si Ng'ombe??
Huyo Mungu nae kajitokeza tu...🤣Afu maswali gani unauliza... niambie kwa Nini ghorofa sio gari?
 
Kuonekana kukoje. Kama kuonekana ni kizingiti kwa upeo wa macho kwa kweli Mungu haonekani.

Lakini kama Mungu kuonekana kwake kunatokana na fikira ya binadamu kuhusu maumbile ya ulimwengu na jinsi ulimwengu unavyotenda kazi, basi Mungu anaonekana.

Kwa nini umewaza kuwa Ili Mungu awepo ni lazima awe anashikika? Kwa ivo Kwa kuwa Mungu hashikiki basi ndiyo kwamba hayupo.

Unataka kuiona Mbingu Ili ufanyaje wakati unaambiwa kuwa Mbingu ni suala la kiroho??
🤣Kiroho ni Chaka la kujifichia Kama mi niseme I have an invisible dragon in my garage hamuwezi muona
 
Ila mtihani ni WA SoMo moja maswali sawa na mda wa masaa sawa Kwa watu wote, na watu wote mmepitia same syllabus. In lyf Kuna watu wa mazingira tofauti hence dini tofauti na pia akili na Mali tofauti so uwezo wa watu kuamini dini fulani as real unatofautiana accord to akili, ukuaji, mazingira na Mali. So how is it fair...afu wengine huu mtihani wanafanya miaka 3 wengine miaka 80
Hapa sio dini maana ni mfumo wa maisha ila tunaongelea Mungu huyu ambaye anatoa riziki kwa wote ,hata yule anadhulumu watu bado atapata riziki.

Kuna hekima kubwa na jinsi dunia inavyoenda na mfumo wa duniani kuwa na matabak ya kiuchumi ,jinsia, elimu ,nguvu na mengine.

Haya yote yapo yana makusudio yake na wala sio kwmba pamekosewa ..

Inawezekana ikawa sio fair ila inafanyiwa hivi ili dunia kubalance ...

Duniani kuna equity ila ulikta equality lazima pawe na matatizo , mfano ukiweka equality kweny ndoa basi hap matatizo.

Equity ipoje hata kama wewe utakuwa labda una uchumi mkubwa basi utapata matatizo accordingly yaani utapata matatizo makubwa na utapewa mitihani labda kusaidia jamii na mandatory yaani mali zako ila unatakiwa kusaidia watu...Kwa maskini anapata mitihani midogo ya kimaisha naye atakuwa kweny level fulani atajiona kapanda au kashuka ,atakuwa na furaha na huzuni ila ataridhika na maisha yake .

Mtihani wa maskini inaweza kuwa mdogo hata kushindwa kulipa ada ya shlling laki moja ,ila yupi tajri anapambana kumlipia mwanae ada ya million 10.
 
Back
Top Bottom