Uongo na Ukweli Kuhusu TANESCO Kuzuiwa Kufanya Maintenance

Uongo na Ukweli Kuhusu TANESCO Kuzuiwa Kufanya Maintenance

Kama ambavyo wadau mbalimbali wamekuwa wakisema mara kadhaa, Mkakati wa Taifa kuhusu uzalishaji wa umeme ulikuwa:-

View attachment 2015968
Yaani, malengo hadi kufikia June 2020, tulitakiwa tuwe tumezalisha 4,915 MW. Hiyo ni Performance Audit Report iliyotolewa na CAG March 2019.

Hata hivyo, ripoti ya wizara inasema hadi kufikia mwishoni mwa 2019, tulikuwa tunazalisha ONLY 1,565.72 MW... ni takribani 33% TU ya malengo!

View attachment 2015977
Kutofikiwa huko kwa malengo kulitokana na kuhamishia nguvu ZOTE kwenye Bwawa la Nyerere, na hata zile Kinyerezi III na Kinyerezi IV, zikatekelezwa!!!

Of course, labda waliamini kwamba 1,602.32 zingetosha kutufikisha hadi kuanza kutumia Bwawa la Nyerere!! Sasa sijui walizingatia kila siku kuna wateja wapya wa umeme, na kwamba kuna kuharibika kwa mitambo... only God knows!!!

Tuje kwenye Ubungo II ambayo tunaambiwa ni mbovu, huku wengine wakihoji ikiwa ubovu umeanza baada ya JPM kufariki!!! Au ni janja janja tu ya kutaka kuhujumu Mradi wa Bwawa la Nyerere!!!

Je, maintance ilikuwa inafanyika?! Jibu lipo kwenye ripoti kwamba:-
View attachment 2015999
Utaona hapo, Mashine #1 na #2 zilipitisha zaidi ya saa 10,000 tangu siku zilipotakiwa kufanyiwa maintanance!! Yaani Machine #1 iliendelea kuburuzwa kwa mwaka 1 na miezi tangu ilipotakiwa kufanyiwa ukarabati, huku Mashine #2 ikiburuzwa kwa zaidi ya miezi 18 bila kufanyiwa maintanance tangi siku ilipotakiwa kufanyika!!

Je, ikiwa hiyo ni ripoti iliyoandikwa kutoka kwenye takwimu za 2018, je maintance ilifanyika? Na kama ilifanyika, ilifanyika lini?

TANESCO wenyewe, hawa hapa chini:-
View attachment 2016022

Kumbe, hata baada ya miaka 3 baadae, bado Ubungo II ilikuwa haisomeki!!!

Sasa ikiwa tatizo lililopo miaka na miaka, ni mjinga tu ndie anaweza kuamini kwamba hivi sasa Ubungo II ipo operational, lakini sie wapiga deal za kuuza majenereta tunafahamu mambo bado si shwari!!!

Ina maana shida ni kukosekana kwa vifaa peke yake ndo maana haya mambo ya maintanance yanachelewa namna hii?!

Again, CAG's Performance Audit Report iliyotolewa March 2019 inasema:-

Kumbe, jamaa ilikuwa wakitaka kufanya maintanance, wanapigwa STOP, na matoke yake mitambo ikawa inaburuzwa tu hivyo hivyo!!!

View attachment 2016037

Wadau walipozungumzia hilo suala, wakaitwa majina yote ya ovyo ili mradi tu....!!

Ndipo tunarudi pale pale, mbona hilo tatizo la upungufu wa umeme halikuwepo wakati wa JPM!!!

Swali ambalo nimekuwa nikiwauliza wanaotoa hiyo hoja ni kwamba nyie wenzetu mlikuwa mnaishi Tanzania ipi ambayo haikuwa na matatizo ya umeme!!

Anyway, inawezekana wenzetu ni watoto wa kishua mnaoishi kwenye viunga vya Ikulu... lakini sie tulio huku Ushenzini, hususani kwenye miji na vitongoji vikongwe vyenye uchakavu wa miundombinu, kwetu tatizo liliendelea kuwepo muda wote!!

But on top of that, ripoti hapo inaonesha, TANESCO walikuwa wanapigwa STOP kufanya maintenance pale Ubungo II kwa sababu hatukuwa na hifadhi ya kutosha ya umeme kwenye Grid ya Taifa.

Hofu ikawa kwamba, kutokana na kutokuwa na hifadhi ya kutosha, kama mitambo ingezimwa kwa ajili ya maintenance, basi huenda tungelazimika kuingia kwenye mgao!!

Sasa kama tulikuwa tunaogopa kuzima Ubungo II ambayo umeme unaotoka pale is ONLY 105MW, nini kinaweza kutokea kukiwa na upungufu wa maji ambapo, total power generated from hydro, ni 574MW?!

View attachment 2016047

Kama unakataa nchi haipo kwenye ukame, basi tatizo hili la sasa ni la kutegenezwa na mafisadi na wapinzani wa Bwawa la Nyerere, huku sie vibaraka wao tukikesha kuwapanga watu!

Akili za kuambiwa, changanya na zako!

Lakini itoshe tu kusema kwamba, ushabikiwa kijinga unaliangamiza taifa!!!
Kwa hiyo JPM angekuwepo leo tungekuwa katika giza hili la mgao lingemuangukia jumba lake bovu? ceteris peribus?

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Pole sana Mheshimiwa....

Lakini hiyo ripoti haijaandikwa na Timu Msoga bali na CAG, na nyingine ni Ripoti ya Wizara ya Nishati!!

Narudia, pole sana!!
Ripoti ya cag iliandikwa upya baada ya kifo
 
I wish watu wangeacha ushabiki na kujiongeza ili wafahamu tunavyo underutilize gas resources wakati nchi bado ipo kwenye changamoto kubwa ya nishati ya uhakika!!
Tunachojua hatukuwa na Giza Wala ukosefu wa maji Wala ukame, hivyo vyote vilikuogopa JPM na vimeanza baada ya kifo chake ...
Porojo zenu mliziandaa kabla hamjamzika, baada ya kusema hizo propaganda zenu mtatujuza lini mnakodisha mitambo ili mjilipe na familia zenu maana miaka zaidi ya mitano ya wananchi kufurahia umeme na maji iliwatesa sana.
 
Kitaalam hayo matengenezo yanamaliza wiki ngapi?

2 kwa nini makamba anaingia mkataba wa mabilioni na wahindi kwa ajili ya ufaninsi wa kiutendaji wakati umeme hautoshi, hao wahindi watafanya ufanisi gani wakati umeme haupo wa kutosha?

Huoni huo ni uhalibisfu zaidi wa pesa za watanzania badala ya kupeleka hapo kinyerezi iii yeye anawapa ofa wahindi?

Je hapo mnamteteaje huyo wazili?

Kama maelezo yao ni mw 1606 na matumizi ni mw 1200 na mapungufu kwa ajili ya maji ni 370 je kwa nini pawe na uhaba?
Waongo tu Hawa wamerudisha hadithi zao za megawats ili waendelee kutumaliza tu waneemeke na familia zao
 
Zimetajwa at least 3 factors ambazo zinachangia kuchelewa kufanyika kwa matengenezo:-
1. Spare Parts
2. Wataalamu,
3. Kupigwa STOP kutokana na kutokuwa na hifadhi ya kutosha ya umeme kwenye gridi ya taifa!!

So, suala la muda gani inaweza kukamilisha matengenezo itagemeana na hizo factors!! Unaweza kusema "fine, zima mitambo hata kama itasababisha mgao, kisha jikiteni kwenye kazi moja tu: MATENGENEZO"

Well and good lakini je, kuna spare parts za kutosha! Je, yale matengenezo yanayohitaji some specialization, tunao hao mafundi walio-specialize au itabidi tu-contract?

Hapa umeniacha... unazungumzia mkataba upi?

Mosi, hizo 1606 MW ni TOTAL POWER Generated... uliopo kwenye grid ya taifa na ulio off-grid!!!

Kwa maenezo ambayo hayatumii umeme wa grid ya taifa, wao watakosa umeme kwa sababu nyingine tu lakini sio sababu inayohusu wale wanaotumia umeme wa grid!!

Pili, hizo aprox za kutumika units 1200 ni za almost 3 years ago, wakati kila siku wateja wapya wanaingia kwenye system wakati kiwango cha umeme kipo pale pale!!
Malizieni dili zenu watanzania malofa tu hawa nyie endeleeni
 
Hakuna cha miluzi mingi wala nini!

Miluzi inaonekana mingi kwa sababu tunachukua kila kinachosemwa na yeyote ili mradi ana madaraka mahali, badala ya kutafuta chanzo kikuu cha taarifa husika!

Kwavile vyanzo vikuu taarifa zake zinakuwa in a written form, basi taarifa hiyo ikisomwa na hata watu 10M, bado ujumbe utabaki ule ule!!
Kwani serikali iliyopo ni ya CHAUMMA?
 
Hizo spea zinachukua mda gani kufika nchini?
Je tanesco hawana spea kwa jili ya dharula?
Spea za maintanance zinasubili kuagizwa kwenye shirika la umma linalotegemewa na nchi nzima wakati wakurekebisha?

Kwanini waziri wakati anaingia madalakani hakuona umuhimu wa kuongeza uzalishaji kwa hiyo kinyerezi 3 mpaka umeme ulete shida ndo aje kusema wanahakikisha watajenga lakini akaona aingie mkataba wa kuwalipa wahindi ambao watakuja kuweka mifumo ya uendeshaji kwa kitu ambacho sio stable?
Wizi mtupu hawana lolote timu wizi hawa
 
HAHAHAHA mkuu hongera kwa kumpambania Makamba watu wanahitaji umeme.... umeme ukiwa na shida watu watajua tuu na watasema wala tusijifiche kwenye visingizio hahahah yani hapa watu wanaona wazi kuna shida...... pamoja na hayo yote miaka hiyo yote hakukuwa na shida kubwa kama hii.... na kila mtu anajua na wala watu hawahitaji matakwimu hahaha
Wanahisi watu wanahitaji propaganda zao hizi
 
Kwanza tunashukuru umeelewa kuwa kilichokuwa kinaendelea wakati wa Magufuli sio utendaji bora,bali ni kusaka sifa za kijinga. Na sifa hizo za kijinga hazikuwa huko kwenye umeme tu, bali ni kwenye mambo mengi tena ya msingi.
Umeme ulikuwepo au alikuwa anatuwashia jua huyo mtaka sifa?
 
Huko kutokuwa na mgao mkubwa wakati huo,ndio kulikoleta hii cancer ya sasa. Sifa za kijinga mwisho chattle.
Na ule mgao wakati wa kikwete ni sifa za kijinga za Nani zilisababisha?
 
Huyu mwanzisha mada sijui alifanywa nini na JPM!

Kwa ufupi, hatukuwa na tatizo la umeme la kiwango hiki na hili wewe mtu mmoja huwezi kutufundisha! Wananchi wanajua!

Kama issue ni mitambo kutofanyiwa maintenance toeni schedule tuone toka mmeanza kufanya maintenance tuone improvements otherwise ni porojo.

Upungufu wa maji umesababishwa na nini? Mbona for 5 good yrs ilishafutika? Au JPM alifichaje yaani?
JPM aliipiga mkwara mitambo ikaacha kuzimika
 
Uliishi kwenye propaganda za kijinga, kiasi kwamba ukikutana na ukweli ndio unatamani iwe propaganda. Muda wote wa utawala wa Magufuli tulisema ni mtu mpika data na msaka sifa za kijinga. Kwa bahati mbaya hata hawa wanaojifanya kurekebisha mambo sasa ni waongo wenzake, tofauti ni kuwa yeye alikuwa muongo kuliko wao.
Kama propaganda za kijinga zinasababisha tupate huduma za jamii nadhani tunazihitaji sana hizo propaganda kuliko huu ushuzi wenu mnaoutetea hapa hauna hata suluhu nyie mnatetea deals zenu tu
 
Mmmh, upungufu wa maji umesababishwa na nini?! Ukweli una tabia ya kuumiza. Magufuli alikuwa ni tapeli mwenye roho mbaya, hawa wa sasa ni matapeli wenye tabia za ujanja ujanja.
Utapeli wake haukutuletea Giza, utapeli wake haukutuletea kiu na njaa Wala mfumuko wa Bei, tunahitaji zaidi huo utapeli kuliko huu ushuzi wenu mpaka mvua zimewagomea majini nyie
 
Hakuna na sijaona sababu ya wewe kuukataa ukweli ila kilichopo na ninachokiona kwako ni maradhi which entered into the minds of the majority of people has also entered your mind.
Maradhi kwenye uhalisia?
Kwani tulikuwa tunawashiwa jua au umeme huo wa uongo?
 
Back
Top Bottom