Upigaji Uyui: Waziri Mkuu ashangazwa kibanda cha Mlinzi VETA kujengwa kwa Tsh. milioni 11, aagiza waliyosimamia ujenzi kukamatwa

Waziri mkuu Majaliwa ameiagiza Takukuru kuwakamata wote waliosimamia ujenzi wa Chuo cha Veta Uyui

Majaliwa ameshangaa kuona kibanda cha mlinzi kimegharimu tsh 11 milioni

Source ITV habari
Hata na majaliwa ni mpigaji, sema yeye ana ulinzi. hata wewe ni mpigaji
 
Nyie mkipandisha bei za mafuta , Vifurushi na Transaction za benki tunawaelewa Ila nyie mkiongezewa Hela kidogo mwe ye miradi yenu mnaanza kulia lia
 
Na hapo fundi aliyefanya kazi unakuta hata laki 4 hazijafika na bado anasubiria mkandarasi alipwe ndio ampe chake
 
Waziri mkuu anahangaika na vijimilion 11 ili hali kuna mabilioni yanatafunwa kila kona
 
😅😂 acha ujinga wewe ktk miradi mingi wakat wa Magu hivyo vibanda vilijengwa kwa zaidi ya million 10, Magu alishindwa kugundua upigaji huo kwasabab ni ngumu unapokagua mradi kufuatilia kibanda badala ya mradi mkuu... Kilichotokea sasa hivi hivyo vibanda vinagundulika watu wedhurumiana pesa kwenye ukandarasi kwahio wanaunguza picha kwa kiongoz anaekuja kukagua mradi aangalie na vibanda bei yake...
 
Kwa hiyo Una shauri nini?
Tuendelee kufanya kazi bila ubadhirifu!! Sio kwamba eti kipindi kile walikuwa wanapiga sana kwahiyo sasa waendelee kupiga tu !! Tanzania bila upigaji inawezekana !! Mifano tulishaiona !!
 
Nilidhani wewe ni Mzalendo kumbe kweli wewe ni msaka fursa, na hapa nahisi umeamua kuonesha uhalisia wa sura yako baada ya kunusa kuwa lile jambo lako limeshabutuliwa.

Pascal naamini unajua vizuri muongozo wa "Force account" nilidhani maelezo yako yote yangezingatia muongozo huo ila tu kwa maksudi umeamua kupoza hasira zako dhidi ya jambo lako Ndiyo maana umeandika haya uliyo yaandika.

Tukirudi kwenye hoja ni kwamba.
1. BOQ za majengo ya serikali hazina chaguo la matakwa ya mtu binafsi, bali zimeainishwa kwa kuzingatia hali ya mahitaji ya kawaida na siyo anasa zaidi, hivyo ukiweka matamanio yako Ndiyo ubadhilifu wenyewe hata kama ni bora.

2. Mchakato wa ujenzi wa Force account ni wa bei huria kwa maana ya fundi na mzabuni wa vifaa kwa jumla ya ukamilifu wa kazi ya mradi, hivyo Basi hizo bei ulizoziandika ziwe za fundi au vifaa haziwezi kufikia huko kama kulikuwa na ushindani huria na sahihi wa zabuni.

3. Kwa Kila hatua ya mchakato wa mradi maofisa wa vifaa (pmu) hushirikishwa kukagua idadi ya vifaa na bei halisi kuona kuwa viko ndani ya bajeti au laa. Hivyohivyo ofisi ya mkandarasi naye hukagua Kila hatua kuona kuwa pamoja na ubora wa kazi lakini pia asiombe fedha zaidi ya mkataba wake kwa Kila hatua.

4. Veta kupata fursa hii ya kusimamia mradi ilikuwa ni fursa nzuri kwao kudhihirisha ubunifu wao katika kutumia fedha kidogo kupata kitu bora maana ufundi ndiyo taaluma yao. Serikali, Wananchi na wadau wa ujenzi walitarajia kuona wao wanatumia fedha kidogo kupata ubora stahiki na siyo fedha nyingi zaidi kama unavyotaka watu waamini.

5. Hivyo basi; pamoja na kusikika kwa mhusika mmoja katika ujenzi huu, ukweli ni kwamba, uzembe utakuwa umefanyika katika ofisi tatu ambazo ni Ofisi ya uhasibu (pmu), Ofisi ya mhandisi na Ofisi ya Mkuu wa chuo.

6. Pascal ktk hoja hii nakubaliana na waziri mkuu hicho chumba kimoja hakiwezi kugharimu milioni 11. Wewe una lako.
 
Je, ni lazima TAKUKURU waagizwe kufanya uchunguzi, wasipo agizwa maana yake ndio imetoka?

Sijajua hii taasisi inafanya vipi kazi ila ni mambo ya kushangaza sana. Daily utasikia waziri aagiza TAKUKURU ifanye uchunguzi, mara Mkuu wa Mkoa aagiza TAKUKURU. Sasa je, wao kama wao ni lipi wanachokifanya ofisini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…