Upinzani Tanzania una matatizo? Vyama havina Succession Plan hivyo vina Usultani! CHADEMA kuna Usultani? Usultani huu Utakiinua au Utakiangamiza?

Kila siku wapo na Mbowe tu, siku akiunga mkono juhudi za Mtukufu utasikia sifa zikimiminwa! Kama juzi kwa Calisty Lazaro au kwa Mtatiro au kipindi kile kwa Kafulila! Ccm kama ni wa umini wa demokrasia wasingekuwa wanapora ushindi wa Maalim Seif kule Zenji!
 
Benard Membe atarusiwa kuchukua fomu 2020 kugombea nafasi ya Urais?
Pascal Mayalla maswali yako ni vigumu kupata majibu. Majibu mengi utakayokutana nayo ni kama hili la huyu mchangiaji. Ni ushabiki unaokolezwa na uelewa finyu ndiyo unafanya watu wajibu hivi. Hawajua kuwa japo CCM inaweza kuwa inafanya makosa hayahaya lakini kwa vile imeshika dola haiathiriki. Sasa hawa wenzangu wao dola hawana halafu wanataka wafanye kama CCM inavyofanya. Ni majanga!
 
Tanzania bila Mikakati kisiasa vyama vyote vinauwawa ndani ya mwaka mmoja.

1. NCCR mageuzi iliuwawa kwa uzembe kidogo tu kupitia vibaraka wa CCM

2. CUF imeuwawa kupitia mbinu zilezile zilizoiangamiza NCCR mageuzi.....ccm

CCM Inajinadi hadharani kuuwa upinzani tena bila kificho kupitia njia zote haram

A) magoli ya mkono kupitia tume ya uchaguzi nk sio siri ipo wazi kabisa

B) Nguvu za dola, mahakama na bunge, msajili. hakuna siri tunaona

Mahakama
Viongozi wote muhimu vyama vya upinzani wanabambikiwa kesi au kufungwa au kusumbuliwa hovyohovyo kila siku kuripoti mahamani, mahakimu wameacha kutenda haki....... kiongozi awe teyari kubeba msalaba huu.

Dola
Mawaziri, wakuu wa mikowa, wilaya, idara na taasisi mbalimbali, Wanatoa adhabu na mapingamizi kwa wanasiasa mashuhuri wa upinzani kila siku.
- kukamatwa na polisi bila sababu za msingi
- kuwekwa mahabusu bila sababu za msingi
- kupigwa na kunyanyasana bila sababu za msingi -kutekwa ama kupotezwa..... kiongozi aweteyari kwa haya.

Bungeni
Bunge kimekuwa kikao cha ccm, wapinzani wasiongee, wasitoe hoja, nikuzomewa, kulazimishwa kufuta au kutolewa nje, kufungiwa kutokuhudhuria vikao bila sababu za msingi nk... .kiongozi aweteyari kupoteza haki zake ilikubakia mtiifu kwa wanachama na wapenzi wake.

Msajili
Yeye nikiranja wa CHADEMA na ACT hajishughulishi na ccm, wala matawi ya ccm
UDP
TLP
Kwa msajili makosa hufanywa na wafuatao na viongozi wake wanawindwa kuadabishwa popote muda wowote....
- CUF asili
- CHADEMA
- ACT
Katiba ya jamhuri haiwahusu CCM kabisa, ndio maana majuzi katibu mkuu ccm katishia hadharani kumfukuza kazi msajili ..... Msajili amenyamaza kimyaaa maana aliyesema sio zito, maalim wala mbowe.... wangeona cha mtema kuni.

Serikali,
Tunashudia maajabu sana viongozi wa kisiasa kutoka upinzani wakirejea kwa kasi ccm wengine wakipewa madaraka mfano kafulila, waitara, katamba nk

Hitimisho.
Vyama vya upinzani havihitaji kuonja sumu kwa kujipendekeza ilikuwafurahisha ccm ilikuweka viongozi wa kitaifa wasioeleweka vema.

Nimara 1000 bora kubakia na viongozi walewale wanaoleweka, wanajithamini nakuthamini mahitajio ya mioyo ya watanzania ilikuhakikisha vyama havipasuliwi na ccm kupitia
Dola
Bunge
Mahakama
Msajili

Upinzani unahita viongozi
1. shupavu
2. Wavumilivu
3. Wazalendo wa kweli
4. Wasio na tamaa kudukuliwa
5. Waliojitoa ....kufa, kupotezwa au mateso
6. Wanaona na kuthamini kiu na matarajio ya watanzania nyuma yao.

Vigezo vya kufakamia bora viongozi badala ya viongozi bora huu sio muda wake maana aliyepo juu lengo moja tu kuuwa upinzani.

Sumu haionjwi
 
kajishebedua wee kasahau hapa,

Membe ataruhusiwa kuchukua fomu 2020?

hau nafasi ya mwenyekiti wa fisiem ni ya kisultani?
Watu wa mbowe na myopia
Mada inahusu upinzani na haswa mbowe na chadema,badala ya kujibu maswali mnamrukia membe na ccm,huko ni kukosa majibu
Mbowe na genge lake ni wezi tu hawako kwa maslahi ya chama
Zaidi ya miaka 20,chamw kikuu kina ofisi ya makao makuu bandani
 
Naona Pascal Mayalla unapotosha watu. Kama Chadema ingekuwa haina succession plan au haina viongozi wanaofaa kupewa madaraka ni kutokana na ubora uliopo wa chama tofauti na CCM. Tumeona CCM ikirubuni wabunge na viongozi wa Chadema na wakienda CCM wanapewa nyadhifa mbalimbali ikiwepo kurudishiwa ubunge wao kwa njia ya wizi. Jee hapo mwenye mapungufu ya kupata viongozi ni nani kama sio CCM?
Najua were nawe unataka Ku base katika logic watumiayo CCM kuhusu mwenyekiti Mbowe!
Chadema inayo succession plan yake, ya nani anaweza kuwa nani baada ya nani kuondoka. Lakini suala ni muda, kama mwingine anastahili kuwepo kwa kipindi zaidi basis ataendelea kwa matakwa ya chama sio kwa matamanio ya CCM.
Wasichojuwa CCM ni kuwa wao ndio wanasababisha Chadema iendelee kulazimisha Mbowe abaki madarakani.
Kwa nini? Kwa sababu wao hawampendi, wanamuogopa na hawaishi kumtungia mabaya na kutamani angekufa kabisa. Unategemea kwa Mwanachadema mwenye mapenzi mema na chama afanyeje zaidi ya kumuhitaji na kumlinda Mbowe!
Ona Mwambe kasifiwa na Magufuli tuu Kule Masasi hata kura za uenyekiti kanda kapigwa.
Kwa hiyo labda vyama vingine, lakini niwaonavyo Chadema wako makini na hata wa kukaa pale zaidi ya Mbowe wapo wengi tuu na wameandaliwa. Hizo zingine ni mbwembwe zenu tuu.
 
Ki mtazamo pascal ni bwana mmoja mchokozi chokozi ktk mada.
Na mara nyingi kiuandishi anaonekana kukwepa kuonesha hisia yake ya mapenzi ya dhati aliyonayo kwa ccm ili tu apate wafuasi wa kusoma nyuzi zake,

lakini kiuhalisia huandika kupima hisia za wale anaodhani ni wapinzani nadhani lengo ni kupima mitazamo na lazima atakuwa ni mshauri huko kwa chama chake na huenda ushauri wake mwingi huutoa hapa.

Hii haifichi hisia zake kuwa anayo mapenzi yake ya dhati juu ya ccm.

Kaka inakupasa kujua wapo wachangiaji hapa sio wapinzani lakini kimichango wanaungana na upinzani kwa kuwa ni wahanga wa tawala dhalimu za chama chako.

Kilichopo wengi wangependa kuishi kwa uhuru na amani katika nchi yao hofu na vitisho vya watu nyuma ya ki bodi yako hawavipendi.

Kama mtaendelea, mtadhani mnauua upinzani kumbe mnajenga mioyo mibaya zaidi huko mbeleni itakayowatafuna na ninyi.

Watanzania wa leo hahitaji kutishwa, kunyanyaswa, kusababishiwa maisha magumu wanahitaji uhuru na dira ya maisha yenye furaha, mfikishieni huyo aliye nyuma ya ki bodi yako.

Upinzani wa leo sio vyama wala hauko katika vyama, upinzani uko kwenye mioyo ya watu hasa kwa maisha ya kishetani anayowasababishia wananchi na majibu yake yanayochochea hasira miongoni mwao.
Na siku wakizidiwa na hasira hakika mtayaona ya Bashiri. Maana alishushwa kwa bei ya mkate
 
Hili nalo ni jibu linawafanya wapinzani waendelee kudumaa. Kama unangojea kitu kinachoitwa ''mazingira sawa ya kisiasa'' kutoka kwenye utalawa wa CCM basi andika utasubiri mpaka kiama. Ukweli ni kwamba hata kama ingekuwa Chadema ndiyo iko madarakani isingefanya ''kosa'' la kujimaliza kama hilo. Kazi ya kuweka mazingira sawa inatakiwa ifanywe na wapinzani na siyo CCM! Hata Mbowe analijua hili ndiyo maana hawezi kuweka mazingira ya kugombea uenyekiti yawe sawa katika chama anachoongoza! Wewe enedelea kujidanganya.
 
Vyama havina succession plan kwa sababu wanajifunza kutoka ccm, vyama havina demokrasia kwa sababu ccm haina demokrasia ndani yake.

Haya ni matatizo yaliyetwa na ccm.
Kwa hiyo unatuambia kwamba mbadala wa CCM bado hamna??
Ok basi vema tutaendelea kuichagua CCM mpaka tutakapopata vyama mbadala ambavyo kwa dhati kabisa vitaweza kuepuka mapungufu ya CCM na kuenzi mazuri machache ya CCM..
Msilalamike kwamba mmeibiwa wakati mmeshindwa kujitofautisha na CCM sasa tuwachague kwa tumaini lip
Period
 
wenye uelewa mpana zaidi tunajua kuwa chama chetu CCM ndicho chenye matatizo makubwa zaidi kwani bila ya kutumia dola na intimidating politics hakiwezi kusimama chenyewe kama chama.

kaka Pascal Mayalla, ninyi watu wa media ni watu muhimu sana katika mustakabali wa amani ya nchi yetu. mnaona kabisa kinachoendelea lakini cha ajabu mmeamua kutokuushugulisha ubongo wenu kwa kutoyasema yaliyo wazi.

endeleeni tu kuwasaidia watawala ku marginalize upinzani. push the opposition from the overt politics, when they opt for a covert strategy sijui watoto na wajukuu wako umewaandalia nchi gani ya kuwaficha.

sawa endeleeni tu, but critical thinkers know all too well how/where all this is going to end.
 
kajishebedua wee kasahau hapa,

Membe ataruhusiwa kuchukua fomu 2020?

hau nafasi ya mwenyekiti wa fisiem ni ya kisultani?
Huu ujinga upo tz pekee! Mtu anakupa ushauri wa jinsi ya kutoka hapo ulipo wewe unaleta ngonjera eti mbona kule kuko hivi.
Kwahiyo tofauti yenu na ccm iko wapi sasa kama kila Mkiambiwa mnajilinganisha ccm?
 
Sina hakika kama una akili timamu!
Hivi mtu kama waitara mnaweza kumpa uongozi wa juu ktk chama chako?
Chama changu unakijua wewe Nyumbu? Mimi sio mwanachama wa chama chochote ila ni mwana mapinduzi na ningependa kuona mageuzi chanya kwenye vyama vyote vya siasa. Wakati mwingine huwa ninasikitika jinsi baadhi ya watu walivyoshikwa akili hata wakati mwingine hawawezi kufikiria nje ya box.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…