Upinzani Tanzania una matatizo? Vyama havina Succession Plan hivyo vina Usultani! CHADEMA kuna Usultani? Usultani huu Utakiinua au Utakiangamiza?

Upinzani Tanzania una matatizo? Vyama havina Succession Plan hivyo vina Usultani! CHADEMA kuna Usultani? Usultani huu Utakiinua au Utakiangamiza?

Nitajie paskal successesion plan waliyonayo ccm
Ulikuja kutafuta plan au kumtuhumu mbowe hawez kuongoza cdm KWA mafanikio?
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko la maswali yenye facts
  1. Jee kuna ubishi kuwa Upinzani Tanzania Unamatatizo?. Ni matatizo gani na usaidiweje?.
  2. Vyama vingi vya Upinzani Havina Succession Plan, kwanini vyama hivyo havina succession plan na sio tuu kwenye uongozi wa ndani, hata kwenye ubunge na udiwani, mfano tunaelekea uchaguzi wa 2020, Chadema ina wabunge wa majimbo ambao wengine wame deliver na wengine hawaja deliver, hivyo uchaguzi wa 2020, wengi wanakwenda kupigwa chini na CCM!. Kwanini hakuna succession plan ya ndani kuwapima kukubalika na kuwapiga chini kabla kwa kusimamisha more able candidates wanaokubalika zaidi?.
  3. Vingi ya Vyama vya Upinzani, Vina Uongozi wa Kisultani, na sio Chadema pekee, Mzee Cheyo wa UDP, Mrema wa TLP, Lipumba wa CUF, etc. Kwanini hakuna grooming mechanism to groom their future leaders?.
  4. Hivyo jee hata uongozi wa Mhe. Freeman Mbowe ndani ya Chadema, ni kama Usultani fulani?.
  5. Jee Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema hiyo 18 Dec, ni uchaguzi kweli au ni uchaguzi kiini macho tuu?, kama utakavyokuwa Uchaguzi Mkuu wa 2020, tayari mshindi anajulikana!. Hivyo ni uchaguzi wa kukamilisha tuu taratibu kuonekane demokrasia amechukua mkondo wake? au ni uchaguzi kweli?.
  6. Kuna msemo, " no one is indispensable", no matter how good one is, huwa anafikia kiwango cha mwisho wa uwezo wake, ndio maana katiba unaweka ukomo wa uongozi, hata katiba ya Chadema ya 1992 ilikuwa na kipengele hicho, kwenye katiba ya 2006, kipengele hicho cha ukomo, kiliyeyuka, just vanish into thin air, bila kujadiliwa popote!. Jee kipengele hiki kiliyeyukaje?
  7. Waliokiweka kipengele hicho kwenye katiba ya Chadema, walikuwa na maana yao, kwa vile ile katiba ya 2006 kipengele hicho hakikuondolewa, bali kilijiondokea tuu chenyewe, kuondoka huku kwa kipengele hicho kuna maana gani kwa Chadema?.
  8. Je ni kwa kutokuwepo kwa kipengele hicho, cha ukomo ndiko kunatoa fursa ya usultani kwenye uongozi wa vyama vya siasa yenye Usultani, Jee Chadema nacho ni chama cha kisultani?, kuna Usultani?.
  9. Mkimfanyia Mhe. Mbowe a quick assessment tangu alipoitoa Chadema alipoingia kwenye uongozi mpaka hapa alipoifikisha Chadema, jee hakuna kweli wana Chadema wenye kuona mbali ambao wanao ona trends za Mhe. Mbowe kuwa japo amekifanyia mengi, makubwa na mazuri Chadema, lakini pia amefikia kiwango chake cha mwisho wa uwezo wake kwa Chadema kuhitaji kupata fresh blood?.
  10. Swali la mwisho na la msingi sana ni, jee kuendelea kwa Mhe. Mbowe kama Mwenyekiti wa Chadema, kwenye era hii ya changing political dynamism ya siasa za Tanzania chini ya JPM na CCM imara, Mwendelezo huu wa Uenyekiti wa Mhe. Mbowe, Jee Utakinua Zaidi Chadema kuliko hapo kilipofika, Au Utakiangamiza na sasa Chadema kinaelekea Kwishney?.
NB. Hili ni bandiko la maswali, kama una majibu ya maswali haya karibu, ukiwa huna, nakushauri jipitie tuu kimya kimya, sio lazima kuchangia kila thread.
Natanguliza shukrani.

Nawatakia Chadema maandalizi mema uchaguzi na wengine wote Jumapili Njema.

Paskali
Rejea


Uko sahihi kabisa zidumu fikira za mwenyekiti bado zipo sana
 
Tatizo CDM hawaaminiani kila mmoja anamuoneshea mwenzie kidole ndio maana wanaona bora abaki huyohuyo Muasisi awakokote mpaka pale watakapoaminiana
 
Paskali,
Usife moyo endelea huenda ukakumbukwa. Ila nasikitika kusema; Kama unataka kweli kujijenga mwambie wa kwetu asiogope kivuli. Weshamwambia CDM iko ICU hivyo asihofu anayepumulia mashine. Wala asiuondoe mpira wa pumzi bali ajiendee uwanjani aweke uchaguzi huru aone kama kuna taahira atakayekichagua chama kinachopumulia mashine.
Kinyume cha hapo, yu people are just living a wishful thinking life. Chama kongwe hivyo haklifai kuyaishi maisha hayo tena. Mwambiye aweke mpira kati na refa makini ajipime mwenyewe. Hamtakuwa na mithali hizi humu JF.
 
P. Naamini wewe ni mwachama hai wa ccm na usisahau kuwa ccm Ina wenyewe wewe ukiwa sio mmojawapo! Hii slogan ya " ccm Ina wenyewe" inatenda sambamba na cdm Ina wenyewe pia! Kwa maana nyingine acha kutumika kwa Mara nyingine kwa kuitumia kalamu yako kuwabomoa viongozi wa upinzani na vyama vyao Kama ulivyofanya mwaka 2015 kwani hukufaidika kwa lolote zaidi ya kubezwa na kuitwa kuhojiwa ulipotaka kujitambua! Njia hii unayopitia Sasa ili uteuliwe si sahihi hata kidogo kwani naamini hutakuwa tayari kuitwa mpumbavu mbele ya halaiki pale utakapofanya asiyotaka mteuaji!
 
Hii ni inconvenient truth!

Mbowe ni Kiongozi wa kimila, chadema ni zaidi ya Chama cha Siasa, hiyo iko kihistoria. Wachaga ( Machame + Marangu) wanasapoti chadema shauri ya Mbowe + Mtei ambao kwao ni Chief, Mbowe akitoka na chadema kwishney kwani Wachaga (karibia wote ) watatoka pia.

Ni kama ilivyokuwa CUF na Waislamu ndivyo ilivyo chadema na Wachaga, bila ya Waislamu hakuna CUF, huo ndio ukweli hata kama hamuutaki.
Poor observation! Hivi huwezi hata siku moja kujenga hoja bila kuongoza ukabila! Najua upo kwa special mission ya kuchochea vurugu za ukabila kwani vurugu zinaru kwenye veins zako wewe mrundi! Na utateseka Sana kuikamilisha hiyo kazi ya kuchochea ukabila na vurugu kwani hutoikamilisha!
 
Paskali,
Usife moyo endelea huenda ukakumbukwa. Ila nasikitika kusema; Kama unataka kweli kujijenga mwambie wa kwetu asiogope kivuli. Weshamwambia CDM iko ICU hivyo asihofu anayepumulia mashine. Wala asiuondoe mpira wa pumzi bali ajiendee uwanjani aweke uchaguzi huru aone kama kuna taahira atakayekichagua chama kinachopumulia mashine.
Kinyume cha hapo, yu people are just living a wishful thinking life. Chama kongwe hivyo haklifai kuyaishi maisha hayo tena. Mwambiye aweke mpira kati na refa makini ajipime mwenyewe. Hamtakuwa na mithali hizi humu JF.
Paskali unashangaza sana hivi kweli hujui vyama vya upinzani vinapitia nini?Mikutano vimezuiwa ila CCM inafanya,kesi ndio mikutano ya vyama vya upinzani kila Mkoa,wilaya wapinzani wako Mahakamani,wengine wamefungwa kwa kuonewa,polisi na wapinzani wanafukuzana,Tume Uchaguzi ,na Wakurugenzi ndio hao,watendaji kata wanakimbia na fomu yote hayo huyaoni?,
 
Kama issue ya msingi ni succession plan basi ni Tatizo kote hata CCM. Kwa maoni yangu ulitakiwa ulizungumzie zaidi ndani ya CCM kuliko upinzani kwa kuwa CCM wameng"ang'ania na kuhodhi madaraka hali ambayo imeadhiri mafanikio na maendeleo ya nchi kwa kila hali.

Mifano mdogo tu.... Kama CCM Wangekuwa na succession plan mtu kama Polepole asingekuwa hapo alipo, Bashiru asingekuwa Katibu Mkuu na huenda No. 1 wa sasa na aliyepata wasingetatanua kwenye lile jumba jeupe.
 
Kama kuna jambo ambalo cdm hawataki kulizungmzia ni kuhusu kubadil katiba kumruhusu Dj aendelee kutawala,

Ikiwa t hawajatawala wanabadil katiba je wakipewa Madaraka?
 
Sio kweli mkuu, wenyeviti wote wa CCM wanakuwepo katika uongozi kwa miaka isiyozidi kumi. CCM inao uwezo wa kwenda na wakati kwani inaheshimu taratibu inazojiwekea.

CHADEMA kuna mambo mengi ya kuzungukana, mnaongea mkicheka pamoja lakini ukiwapa mgongo watu wanaanza masengenyo ndani ya muda huo huo.
Taratibu za MTU kutoka upinzani kuamia ccm kupewa nafasi ya ubunge instantly plus uwaziri, chadema na ccm hakuna wa kumcheka mwenzake
 
Kama issue ya msingi ni succession plan basi ni Tatizo kote hata CCM. Kwa maoni yangu ulitakiwa ulizungumzie zaidi ndani ya CCM kuliko upinzani kwa kuwa CCM wameng"ang'ania na kuhodhi madaraka hali ambayo imeadhiri mafanikio na maendeleo ya nchi kwa kila hali.

Mifano mdogo tu.... Kama CCM Wangekuwa na succession plan mtu kama Polepole asingekuwa hapo alipo, Bashiru asingekuwa Katibu Mkuu na huenda No. 1 wa sasa na aliyepata wasingetatanua kwenye lile jumba jeupe.
Umeongea point bila ya kuegemea upande wowote, ukiangalia jinsi mpinzani anahamia ccm na kupewa nafas ya kugombea unagundua Luna tatizo mahali, Kwa hy ccm hawawez tupia chadema lawama wote wanafanana
 
Mkuu hawa jamaa wao wapo perfect kwa kila jambo awataki kukosolewa wala kushauriwa ila wao ndio wamejipa majukumu ya kukosoa na kushauri kwa wengine, nahisi ni chama cha MA GENIUS.


Angalizo subiria matusi na kejeri kutoka kwa wafuasi wao.

Mwisho Chadema ni zaidi ya KAOLE
 
Ushauri ni ku expand resources zenu...na mgawane equally mapato...watu hawatang'ang'ania madaraka..anyway this thread is useful kwa wao kufanya reflection...
 
Back
Top Bottom