sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 3,344
- 9,066
Wafuasi wa Tundu Lissu wamekuwa wakimtetea huyu 'masia' wao kuwa ni mkweli, kanyooka, penye nyeusi anaita nyeusi, ni msafi.
Lakini siku zinavyozidi kwenda inajidhiilisha Tundu Lissu sio mkweli bali ni mropokaji.
Lissu anaropoka jambo lolote ambalo anahisi wafuasi wake watapenda kulisikia na litamuongezea political mileage.
Lissu sio mwanasiasa mwenye mipango madhubuti yeye anategemea mdomo, kuwatukana na kudhalilisha wengine ili yeye akue. Lakini hawezi kufanya mikakati ya kiuongozi na kisiasa.
Viongozi waropokaji kama Tundu Lissu ni hatari kwa usalama wa taifa. Ni wepesi sana kuchochea machafuko ili wapate upenyo wa kushika madaraka hawajui mbinu nyingine za ziada zaidi ya kuropoka na kuchochea vurugu.
Adolf Hitler aliingiza dunia kwenye vita ya dunia kwa sababu ya kuropoka sana na kuchochea ubaguzi. Alipata alichokitaka.
Nduli Iddi Amini nae alikuwa mropokaji mzuri sana ilifikia wakati aliichimba mkwara mpaka Uingereza na mashabiki wake walikuwa wanamshangilia sana. Lakini Nyerere alimpa kinachomstahili.
Hapa Tanzania tulikuwa na Mtikila alikuwa ni mropokaji kama Lissu na Lissu ni kama anaenda kuwa Mtikila mpya baada ya huu uchaguzi wa Chadema. Mtikila ilifikia wakati akaaminisha mashabiki wake kuwa wahindi ndio tatizo kwenye hii nchi yani uwepo wa wahindi ndio unasababisha waswahili wasiendelee. Mtikila mpaka anafariki alikuwa mwanasiasa wa hovyo kabisa sababu ya uropokaji.
Sasa huyu tulie nae anaitwa Tundu Lissu ni tatizo sio tu kwenye chama chake cha Chadema bali ni tatizo kwa taifa. Huyu jamaa anaropoka sana mpaka amepitiliza. Sijui hata wafuasi wake kama wanapata picha huyu jamaa ataenda kuongozaje chama kwa tabia za namna hiyo. Kwa uropokaji wa Lissu hawezi kuongoza chama kikawa kimoja hajui kuunganisha watu anachoweza ni kubomoa.
Ameshatoa kauli zinazoenda kuua chama anachotaka kukiongoza lakini kama haitoshi ametoa kauli nzito zinazoweza kuhatarisha umoja na amani ya taifa letu.
Kauli zake kuhusu kikao cha faragha na viongozi wa kidini zinatosha kabisa kusema huyu mropokaji hafai kuwa kiongozi na ni hatari na ikiwezekana akapimwe utimamu wa ubongo wake maana hii sio kawaida.
Shukrani Mbowe kwa maono yako, umechagua maslahi ya taifa over upepo wa mihemko.
Mkishammaliza uko CHADEMA kazi yake huku nje ni nyepesi. Maana hatopata tena platform ya kufanya uropokaji wake na akachukuliwa serious.
#KataaMropokaji
Lakini siku zinavyozidi kwenda inajidhiilisha Tundu Lissu sio mkweli bali ni mropokaji.
Lissu anaropoka jambo lolote ambalo anahisi wafuasi wake watapenda kulisikia na litamuongezea political mileage.
Lissu sio mwanasiasa mwenye mipango madhubuti yeye anategemea mdomo, kuwatukana na kudhalilisha wengine ili yeye akue. Lakini hawezi kufanya mikakati ya kiuongozi na kisiasa.
Viongozi waropokaji kama Tundu Lissu ni hatari kwa usalama wa taifa. Ni wepesi sana kuchochea machafuko ili wapate upenyo wa kushika madaraka hawajui mbinu nyingine za ziada zaidi ya kuropoka na kuchochea vurugu.
Adolf Hitler aliingiza dunia kwenye vita ya dunia kwa sababu ya kuropoka sana na kuchochea ubaguzi. Alipata alichokitaka.
Nduli Iddi Amini nae alikuwa mropokaji mzuri sana ilifikia wakati aliichimba mkwara mpaka Uingereza na mashabiki wake walikuwa wanamshangilia sana. Lakini Nyerere alimpa kinachomstahili.
Hapa Tanzania tulikuwa na Mtikila alikuwa ni mropokaji kama Lissu na Lissu ni kama anaenda kuwa Mtikila mpya baada ya huu uchaguzi wa Chadema. Mtikila ilifikia wakati akaaminisha mashabiki wake kuwa wahindi ndio tatizo kwenye hii nchi yani uwepo wa wahindi ndio unasababisha waswahili wasiendelee. Mtikila mpaka anafariki alikuwa mwanasiasa wa hovyo kabisa sababu ya uropokaji.
Sasa huyu tulie nae anaitwa Tundu Lissu ni tatizo sio tu kwenye chama chake cha Chadema bali ni tatizo kwa taifa. Huyu jamaa anaropoka sana mpaka amepitiliza. Sijui hata wafuasi wake kama wanapata picha huyu jamaa ataenda kuongozaje chama kwa tabia za namna hiyo. Kwa uropokaji wa Lissu hawezi kuongoza chama kikawa kimoja hajui kuunganisha watu anachoweza ni kubomoa.
Ameshatoa kauli zinazoenda kuua chama anachotaka kukiongoza lakini kama haitoshi ametoa kauli nzito zinazoweza kuhatarisha umoja na amani ya taifa letu.
Kauli zake kuhusu kikao cha faragha na viongozi wa kidini zinatosha kabisa kusema huyu mropokaji hafai kuwa kiongozi na ni hatari na ikiwezekana akapimwe utimamu wa ubongo wake maana hii sio kawaida.
Shukrani Mbowe kwa maono yako, umechagua maslahi ya taifa over upepo wa mihemko.
Mkishammaliza uko CHADEMA kazi yake huku nje ni nyepesi. Maana hatopata tena platform ya kufanya uropokaji wake na akachukuliwa serious.
#KataaMropokaji