Urusi kupeleka majeshi yake na silaha nzito nchini Cuba na Venezuela kama Marekani itaendelea na kujiingiza Ukraine

Yaani niache kuangalia takwimu niwasikilize mashabiki?sijajifunza tu walipokuwa wanabweka kudai us anaogopa kabla kuingia Iraq,afghanstan na libya? unashangaa kwamba hawa watu wana hamu na bloodshed nini?Hakuna nchi isiyoathirika na madhara ya vita au mnadhani bajeti kubwa ya kijeshi ya marekani ni kununua ma-parachute?!
 
Unafahamu kuwa Marekani yupo Syria tena anamiliki visima vya mafuta vya Syria sasa inakuwaje Mrusi ashindwe kumtoa Marekani Syria kwenye hayo maeneo ya visima vya mafuta?
Tofautisha kumiliki visima na kuimiliki nchi. Swali ni je, kwa nini US na washirika wake alishindwa kuiangusha serikali ya Syria kama walivyofanya Libya? Maana ndiyo ilikuwa lengo lao.

Ukweli usemwe tu uwepo wa Urusi, N. Korea, Iran na China unasaidia sana kupunguza baadhi ya ubabe ambao ungefanywa na hawa wanyonyaji.
 
649 billion dollars USA bajet ya usalama ambayo ni 3.1 percent ya GDP
Wakat Russia 61.6 billion dollar bajet ya usalama ambayo ni 4.1 percent ya GDP ya Russia
Ktk dunia ya sasa USA anaushawishi mkubwa sana kwa cuba tofauti na ilivyokua zaman ezi za kennedy 1970’s era
Russia kwa sasa anawakat mgumu sana kuishawishi Cuba
 
Swali kama hilo limekwisha jadiliwa sana humu miaka ya nyuma.

Ni kweli kulikuwa na mpango wa intervention ya kimataifa nchini Syria dhidi ya Assad lakini mpango huo haukuungwa mkono kikamilifu na nchi za NATO. Nchi kadhaa za NATO ziliukataa kwenye mabunge yao ikiwemo Uingereza. Na hii ni kabla ya Urusi kuingia Syria.
 
Tuwekee na budget ya ulinzi ya Taliban na Vietnam vs budget ya ulinzi ya USA.
 
Kafanye utafiti vizuri Ili ujue nchi pekee inayoweza kuipiga marekani ni Russia pekee.
Urusi haitoipiga Marekani kisha yenyewe [Urusi] ikabaki salama. Marekani itajibu mashambulizi na mwisho wake ni mutual assured destruction (MAD). Nenda kasome!
 
Nchi zote za NATO ziliunga na zinaunga mkono mipango ya kumtoa Assad madarakani, wanachotofautiana ni level of commitment baina ya nchi moja na nyingine kuhakikisha huo mpango unafanikiwa.

Nchi zilizokuwa mstari wa mbele kuhakikisha Assad anatoka ni Marekani, Britain, France, Turkey na Israel wakisaidiwa na Saudi Arabia, UAE na Qatar.

Kwa case ya Britain, serikali yao ilisema bungeni kuwa inafadhili na kufundisha vikundi vya kigaidi wenyewe wanaviita "moderate rebels" kwa ajili ya kupamba na ISIL na kuitoa serikali madarakani( kimsingi ndio lengo kuu).
https://questions-statements.parliament.uk/written-questions/detail/2018-04-13/135396
hili ni jibu la waziri bungeni. Pia kuna Case mshtumiwa wa ugaidi ilibidi waendesha mashtaka wa Uingereza waifute kwa kuwa mshutumiwa huyo wa Ugaidi alikuwa sehemu ya vikundi vinavyofadhiliwa na serikali ya Uingereza kumtoa Assad.

Nchi zote nilizotaja hapo juu zinafadhili hivi vikundi kwa ajili ya kumtoa Assad.

Pia unaweza kupitia hii "Operation Timber Sycamore" iliyoendeshwa na Marekani kumtoa Assad kwa kufadhili na kufundisha makundi ya kigaidi"moderate rebels".Timber Sycamore - Wikipedia


Kilichombakiza Assad madarakani kabla ya kuingia Mrusi ni jeshi la Syria, vikundi vya kikurdi na vikundi vinavyofadhiliwa na Iran.
 
Jibu jepesi tu ndugu.tuambie ni silaha gani ambayo Urusi alitumia kwenye ww2, aliyopewa msaada na Mmarekani.mfano tunajua Warusi walikuwa wantumia vifaru vyao ain ya T-34.
 
Kipindi Warusi wanaibaka Georgia, kuna mbwa yoyote ulimsikia kubweka?.au umesahau kuwa Rais alikuwa huyo huyo Bush kipindi icho
 
kama bajet kubwa wasingewakimbia taleban
 
Ukweli usemwe tu uwepo wa Urusi, N. Korea, Iran na China unasaidia sana kupunguza baadhi ya ubabe ambao ungefanywa na hawa wanyonyaji. ukweli mchungu huu kwawatakao taka kuusikia
 
endelea kujidanganya hvyo hvyo
 
hata german ilikataa kuingia IRAQ na IRAQ ikapigwa hata FRANCE ilikataa kuingia LIBYA na LIBYA ikanyooshwa
US walichemka no more
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…