Urusi kuwa na mji wa Bakhmut na Soledar, hasara ni kubwa kuliko faida

Urusi kuwa na mji wa Bakhmut na Soledar, hasara ni kubwa kuliko faida

Kushinda vita ingekuwa ni rahisi kama hii kauli yako, Urusi ingekuwa aliishaikamata Ukraine ndanibya masaa 72 kama alivyotamka Putin.
Unaweza kutuwekea hapa kauli ya Rais Putin kuwa atamaliza SMO ndani ya masaa 72
 
Madam umekiri kuondoka kwa bakhmut na soledar basi tulia uchumi wa urusi watu waliudharau tangu zamani tu lakin wanaona aibu leo wao kwahiyo na wewe huna tofauti na wao ambao wanapenda kufanya propaganda mwisho wanaumbuka jengine ukileta idadi ya warusi wanaokufa bila kuleta na wa ukraine ni sawa na uzombi tu maana utakua umelinganisha wapi ili kupata idadi iliyo pungua zaidi
Hii ndo aina ya watu tulionao. Na yeye hapo alipo anajiona katoa bonge la analysis ya hii vita.

Kwa hiyo baada ya Kuchukuliwa Soledar na Bakhmut vikapandisha uchumi wa Russia. Ama kweli vichwa vingi vimebeba urojo tu.
 
Hii ndo aina ya watu tulionao. Na yeye hapo alipo anajiona katoa bonge la analysis ya hii vita.

Kwa hiyo baada ya Kuchukuliwa Soledar na Bakhmut vikapandisha uchumi wa Russia. Ama kweli vichwa vingi vimebeba urojo tu.
Ona ulivyo kiazi ndio maana mnaitwa wapumbavu onesha sehemu nimesema kua urus kachuku bakhmut sasa uchumi wake umepanda?
Ukishindwa jipige kifuani jiite wew ni kiazi
 
Unaweza kutuwekea hapa kauli ya Rais Putin kuwa atamaliza SMO ndani ya masaa 72
Usiwe mvivu. Putin haongei kiswahili au English hata ukipewa usikilize hotuba yake hutaambulia kitu. Kama unakijua Ki Russia sikiliza hotuba yake ya kutangaza SMO. Tafuta mtu anayejua kirusi akutafasirie. Ndiyo maana kazi ya media ni kukuletea taarifa kwa lugha unayoijua
 
Youn have a point. Kwamba;
1. Bakhmut imetumika kama trapping position kwa Russia ndo maana akapeleka resources kubwa. Matokeo yake kapoteza wanajeshi wengi na vifaa vingi (Heavily inflicted) with small gain. Ni njia ya ku drain resources zake. Kwenye hilo kuna hoja.

2. USA, German and allies wana prolong vita kwa lengo la kumdhoofisha Russia na kujua uwezo wake unakoishia ili mwisho wa siku asiwe na madhara kwa nchi zingine. Hiyo ni hoja ya msingi ina mashiko.

3. Russia anazoofishwa kiuchumi. Uchumi wake unazidi kusinyaa. Vita ikiendelea atashindwa kui finance na hataweza kushinda hii vita.
Ulijificha kwenye uchambuzi usio na upande lakini naona umeshindwa kudumu kwa muda mrefu umerudi kwenye rangi yako.Tulikujua tangu zamani...
Unaposema Russia kapeleka resources nyingi unatumia criteria gani mpaka kufikia hitimisho hilo,Kama upande wa personal Ukraine ndo amefanya rotation ya reserve nyingi ya wanajeshi hapo Bukhamut kuliko Russia.
Kwa upande wa Urusi walioshiriki hapo kwa kiasi kikubwa ni Musician pmc na Russia regular army walikuwa kwenye atelar na aviation tu.
2: kama hoja ni vifaa nadhani unajua nani ambaye analilia vifaa kila kukicha.Hivi unajua kwanini kumeitwa meat grinder.
 
Wachangiaji na Pro Russia wengi wanashindwa kuelewa dhana hii kuhusu NATO na ushiriki wa nchi zilizojiunga NATO kuisaidia Ukraine.

NATO ni entity inayojitegema na ina resources zake (Financing, Military equipment na Human resources). Inachangiwa financing na wanachama wake tu. Inanunua vifaa vya kivita kwa mahitaji yake kwa technology inayoitaka kwa mazingira ua wakati husika. Siyo kwamba inapewa donation ya silaha kama nchi zinavyofanya kwa Ukraine la hasha.

Watu wengi wanafikiri USA, German, UK and allies kuisaidia kifedha, kujenga uwezo na vifaa vya kivita Ukraine kuwa ndo NATO anapigana na Russia. Hakuna kitu Russia anachokiogopa kama akiingia battle direct na NATO, hiyo mistake Russia hatakuja aifanye maana anajua hatachukia round. Russia anajua High precision equipment with high technology millitary equipments anazotumia NATO. Hakuna military equipment ambayo NATO anazitumie zimeenda Ukraine. Hata USA, German vifaa anavyotoa vina technology ya chini kuliko anavyotumia NATO.

Ushiriki wa NATO ni kutoa wataalam wa kuwafundisha Wanajeshi wa Ukraine kwenye vifaa vinavyotolewa kwa Ukraine maana yeye NATO amevitumia sana siku za nyuma ana uzoefu mkubwa sana kuhusu hivo vifaa. Pia kuwapa military tactical. Lakini siyo kwamba NATO anapeleka majeshi yake au vifaa vyake kwa Ukraine.
[emoji1019][emoji1019][emoji1019][emoji1019]
JamiiForums806342927.jpg
JamiiForums121665422.jpg
 
Usiwe mvivu. Putin haongei kiswahili au English hata ukipewa usikilize hotuba yake hutaambulia kitu. Kama unakijua Ki Russia sikiliza hotuba yake ya kutangaza SMO. Tafuta mtu anayejua kirusi akutafasirie. Ndiyo maana kazi ya media ni kukuletea taarifa kwa lugha unayoijua
Sasa kama hakuna anayejua wewe mwenzetu umejua Je kama alitangaza atamaliza vita ndani ya masaa 72.
Kila mmoja kwa wakati wake alipata kuiona ile hotuba ya Putin wkt anatangaza kuanza kwa SMO na aliweka malengo ya hii operation nini.Katika malengo hakuna sehemu alisema ana mpango wa kuitwaa kiev au kuikalia Ukraine kama unakataa leta kauli yake hapa.
Uzuri ile hotuba ili tafsiriwa kwa ki ingereza
 
Sasa kama hakuna anayejua wewe mwenzetu umejua Je kama alitangaza atamaliza vita ndani ya masaa 72.
Kila mmoja kwa wakati wake alipata kuiona ile hotuba ya Putin wkt anatangaza kuanza kwa SMO na aliweka malengo ya hii operation nini.Katika malengo hakuna sehemu alisema ana mpango wa kuitwaa kiev au kuikalia Ukraine kama unakataa leta kauli yake hapa.
Uzuri ile hotuba ili tafsiriwa kwa ki ingereza
1. Malengo ya SMO yalikuwa yapi. ? Na yalikuwa yakamilike lini? Tutajie.

2. Kama hakuwa na malengo ya kuitwaa Kiev majeshi yake yalienda Kiev kufanya nini?

3. Kwa nini mpaka leo wanahangaika kurusha missile Kwenda Kiev?
 
Alisikika mrusi moja wa kwa Tandele kwa mtogole akisema Urus imepata hasara
 
5. Putin amechezewa changa la macho why kiufupi wanamtaka mkuu wa wagnér na ili kumpata nikumpa tonge la nyama na kwa kuwa nimroho atalifakamia ila kichwa chake ndio hali yao while anafakamia nyama. Nyie tulieni Putin atalia kama ubwa alie acha yatima na mama yake while ana nyonya. Hii vita inapigwa kwa akili kubwa sana kiasi Kuna siri siwezi kuziandika hapa ila tulieni Mrusi atalia kiasi Dunia itasikia. Siku za Putin ni fupi sana kuliko kesho na anajuwa muda wake upo ukingoni. Huwezi pigana vita huna chakula huna pesa.
Wabongo bwana eti una siri huwezi kuziandika hapa! Daah! Acha kamba Mkuu.
 
Ulijificha kwenye uchambuzi usio na upande lakini naona umeshindwa kudumu kwa muda mrefu umerudi kwenye rangi yako.Tulikujua tangu zamani...
Unaposema Russia kapeleka resources nyingi unatumia criteria gani mpaka kufikia hitimisho hilo,Kama upande wa personal Ukraine ndo amefanya rotation ya reserve nyingi ya wanajeshi hapo Bukhamut kuliko Russia.
Kwa upande wa Urusi walioshiriki hapo kwa kiasi kikubwa ni Musician pmc na Russia regular army walikuwa kwenye atelar na aviation tu.
2: kama hoja ni vifaa nadhani unajua nani ambaye analilia vifaa kila kukicha.Hivi unajua kwanini kumeitwa meat grinder.
6 HOURS AGO

Russian mercenary fighters from the Wagner Group have been depleted after months of combat in the eastern Ukrainian city of Bakhmut, the Institute for the Study of War said in its latest assessment.

Source: Moscow Times.

Hiyo ni taarifa toka kwa Warusi wenyewe kuwa Wapiganaji wa Wagner group wameteketea huko Ukraine. Ndiyo maana wametangaza kuwa maeneo waliyokuwa wanayashikilia huko Ukraine, wanayakabidhi kwa wanajeshi wa Urusi, wao wanaenda 'kupumzika'. Kumbe ukweli ni kwamba hawaendi kupumzika bali ni njia ya kujiondoa kwenye mapigano kwa sababu hawana wapinaji wa kutosha, wengi wao wameteketezwa huko Ukraine.

Habari zaidi, tafuta kupitia vyombo vya habari vya huko huko Russia, vya Magharibi utasema ni propaganda.

 
Tangu Urusi aivamie Ukraine Feb 2022 ni miezi 15 sasa, kuna mengi tumeona na kusikia kwa kila upande katika uwanja wa vita.

Kuna maeneo matano (5) ambayo Urusi na Ukraine wameyafanya kuwa ni ngome za mapigano. Miji hii ni Bakhmut, Soledar, Avdiivka, Kreminna na Vuhledar.

Katika miji hii miwili tu ndo imekuwa maarufu zaidi ambayo ni Bakhmut na Soledar. Hii ni kwa sababu ina umuhimu wake katika medani za kivita. Miji hii ni millitary strategic positions.

Urusi iliwekeza nguvu kubwa sana Bakhmut na Soledar, kwa maana ya millitary equipments na personnel. Waliwekeza nguvu kubwa kwa sababu waliamini kuwa wakiiteka Soledar na Bakhmut basi itakuwa rahisi kwao kusonga mbele kwenye miji mingine muhimu kama Slovyansk, Kramatorsk, Sivers'k, na Kostyantynivka. Bakhmut ndio Center (Military Hub) ya kuifikia miji hii sababu ni makutano ya njia kuu kutoka Horlivka, Luhans'ke, Popasna na Lysychans'k.

Urusi Kuichukua Bakhmut na Soledar kajihakikishia kuwa supply logistic (kwa barabara na Reli) itakuwa imara kwenda frontline.

Ni kweli Bakhmut na Soledar ziko mikononi mwa Urusi kwa 100% hilo halina ubishi, akibisha mtu basi ujue tangu akiwa tumboni alikuwa mbishi. Lakini ukweli ni kwamba Hasara ni kubwa kuliko Faida aliyopata.

Nakiri kuwa pande zote mbili zimepoteza resources kubwa (military equipment and personel). Lakini zaidi Urusi imepoteza wanajeshi wake wengi zaidi ya 30,000 waliokufa achilia mbali majeruhi kwa eneo dogo lenye jumla ya SQKM 53.9. Bakhmut ina SQKM 41.6 na Soledar 12.3. Bado nasisitiza Hasara aliyopata Urusi ni kubwa kuliko Faida aliyopata.

Kuna maswali mengi ya kujiuliza. Mimi nitauliza maswali machache na mengine mtaongezea;

1. Nguvu kubwa na rasilimali aliyowekeza Urusi kwa miezi 15 kwa Bakhmut na Soledar zenye eneo la jumla ya SQKM 53.9 zimempa hasara au faida?

2. Kama anaweza kupigana kwa miezi 15 na kufanikiwa kuchukua eneo la SQKM 53.9 ambao ni wastani wa SQKM 3.6 kwa mwezi. Itamchukua muda gani kuichukua Ukraine yote kwa eneo ambalo hajalichukua zaidi ya SQKM 482,960 ?

3. Kama imemchukua miezi 15 kuichukua Bakhmut na Soledar tu kwa direction ya Donetsk ni kweli ataweza kuichukua miji ya Slovyansk, Kramatorsk, Sivers'k, na Kostyantynivka, ukizingatia kuwa kila siku Ukraine wanazidi kuimarisha frontline na anga lao?

4. Urusi ataweza kuishikilia Bakhmut na Soledar kwa miezi 3 ijayo.? Au utakuwa ni ushindi wa muda kama ilivyokuwa Kwa Kherson city, Kharkiv na maeneo mengine?

5. Kwa kuwa Prigozhin amesema tarehe 25/05/2023 atawaachia Russian Regular troops ili wakapate mapumzika na mafunzo zaidi. Je, Russia regular troops watamudu peke yao kuushikilia mji wa Bakhmut bila Wagner?
Ukraine wanaendelea kuifundishwa Russia mbinu za kivita.
Wazivyo na akili wamekubali kujitangazia ushindi kwenye mji usi na raia hata mmoja na sasa wamebaki wenyewe wakishangilia 'Ushindi' huo.
Hata hawajiulizi yalipopotelea wale mgambo wa Ukraine waliokua wakiwawashia mtiti. Tena wamepotea gjafla baada ya Russia kuganikiwa kuingiza wanajeshi wengi zaidi.
kifutacho ni hekaheka Mtoni...simulizi ya vijito vya damu kutoka Bakhmut
 
Inaelekea hata hujui kinachoendelea ila na wewe unataka uonekane unajua kumbe unajiaibisha mbele za watu.
Punguza hasira Mkuu. Mpaka sasa hali halisi ya uwanja wa mapambano inajulikana. NATO wanaisaidia Ujkraine kwa silaha na kila kitu lakini hakuna cha maana walichofanikiwa zaidi ya kuharibu uchumi wa nchi za Magharibi.
 
Kwa mfuatiliaji mzuri wa vita hii, nadhani aliisikia ile kauli kuwa wataivuta vita hii kwa muda mrefu kadiri inavyowezekana mpaka watakapohakikisha Urusi siyo tishio tena kwa Taifa lolote.

Ushindi kwa nchi za Magharibi dhidi ya Urusi, wala siyo kuikomboa Bakhmut bali ni kuifanya Urusi imalize resources zake zote kwenye vita. Na baada ya hapo iwe Taifa dhaifu ambalo halitaweza kuwa tishio kwa usalama wa mataifa jirani, na wala asiwe na uwezo ya kusaidia tawala za kidikteta Duniani.

Hiyo ndiyo sababu ya kauli inayorudiwa mara kwa mara, 'tutaendelea kuisaidia na kuiunga mkono Ukraine bila ya kujali vita itachukua muda mrefu kiasi gani'.

Na sasa hivi, tayari uchumi wa Urusi umeanza kuyumba, sarafu inaanguka, mauzo ya mafuta na gas yanashuka, na India ambaye ni mnunuzi mkuu wa mafuta ya Russia amepewa onyo kuwa kama ataendelea kununua mafuta ya Russia, hataruhusiwa kuuza bidhaa yoyote inayotokana na mafuta kwa nchi za Magharibi. Vijana, hasa wataalam wa fani mbalimbali wanazidi kuikimbia Russia wakuenda nchi za Magharibi.
Kwa akili yako unadhani ni Urusi pekee inayopoteza rasilimali kwenye hii vita. Vipi Marekani na nchi nyingine za NATO hawapotezi rasilimali na kuharibu uchumi wao kwa kutuma mabilioni ya fedha na silaha Ukraine yaliyo nje ya bajeti zao?
 
Wachangiaji na Pro Russia wengi wanashindwa kuelewa dhana hii kuhusu NATO na ushiriki wa nchi zilizojiunga NATO kuisaidia Ukraine.

NATO ni entity inayojitegema na ina resources zake (Financing, Military equipment na Human resources). Inachangiwa financing na wanachama wake tu. Inanunua vifaa vya kivita kwa mahitaji yake kwa technology inayoitaka kwa mazingira ua wakati husika. Siyo kwamba inapewa donation ya silaha kama nchi zinavyofanya kwa Ukraine la hasha.

Watu wengi wanafikiri USA, German, UK and allies kuisaidia kifedha, kujenga uwezo na vifaa vya kivita Ukraine kuwa ndo NATO anapigana na Russia. Hakuna kitu Russia anachokiogopa kama akiingia battle direct na NATO, hiyo mistake Russia hatakuja aifanye maana anajua hatachukia round. Russia anajua High precision equipment with high technology millitary equipments anazotumia NATO. Hakuna military equipment ambayo NATO anazitumie zimeenda Ukraine. Hata USA, German vifaa anavyotoa vina technology ya chini kuliko anavyotumia NATO.

Ushiriki wa NATO ni kutoa wataalam wa kuwafundisha Wanajeshi wa Ukraine kwenye vifaa vinavyotolewa kwa Ukraine maana yeye NATO amevitumia sana siku za nyuma ana uzoefu mkubwa sana kuhusu hivo vifaa. Pia kuwapa military tactical. Lakini siyo kwamba NATO anapeleka majeshi yake au vifaa vyake kwa Ukraine.
Bro acha uongo! Hivi Leopard tanks siyo advanced weapon ya NATO? Patriot Missile System haimo kwenye NATO arsenal?
 
Kwahiyo wewe umeona kweli kuhakikisha usalama na kuwepo kwa Russia ni gharama ndogo kweli? Analysis yako ni ya layman militarily kuna sehemu ndogo 10km lakini ina umuhimu kuliko eneo lenye 10000 Square kilometer, nani kakwabia kwa 30.000 jeshi ndo walikufa Russia katimia macenary sio Red army......bado urusi inanguvu hata Nato inakubali kabisa.
Lini NATO uliwauliza wakakwambia Urusi ana nguvu? Natamani watu wawe wanakuja na reasoning kama hii ya jamaa aliyeweka mambo logically kwamba kama Urusi imetumia muda mwingi kwa eneo dogo kama hilo, je kwa eneo kubwa zaidi itakuwaje? Hiyo ndo logic. Siyo mtu anakuja na ushabiki tu ambao hatuwezi kupima physically wala logically!
 
Alisikika mrusi moja wa kwa Tandele kwa mtogole akisema Urus imepata hasara
Ukitaka kukimbiza Warusi wa kwa mtogole anzisha uzi wa kingereza hutawaona au waulize maswali magumu hutawaona kuyajibu.

Wanachungulia tu wanasepa. Maana porojo wanazoziongea hawataweza kuziandika kwa kwa kiingereza.
 
Kupitia uchangiaji kwenye jukwaa hili (jamiiforums) nimejifunza mambo yafuatayo;

1. Watu wengi wapiga propaganda na porojo (Both Pro Russia and Pro Ukraine) wanaojifanya wanaijua hii vita hawana military skills na hawajui hata uwanja wa vita huwa ukoje? Wanafikiri ni kama sinema za Rambo.

2. Hawajui kwa nini USA, German, UK & Allies waliamua kumuunga Ukraine na kumsaidia kwa kumpa silaha na maarifa (Skills) za kivita.

3. Hawajui lengo la Putin kuivamia Ukraine kuanzia Crimea na sasa Ukraine yote. Pro Russia wengi wamekalili Special Military Operation (SMO) na hawajui hata SMO ni nini kwa muktadha wa Kijeshi na malengo yake huwa ni nini hasa.

4. Pro Russia wengi wanaamini kuwa majeshi ya NATO yanapigana Ukraine, kumbe ni propaganda tu za Russia. NATO hajapeleka hata silaha moja ya NATO wala wanajeshi wa NATO zaidi ya kushiriki kwenye vikao vya maamuzi ya nchi washirika (joint coordination committee) kutengeneza strategies (strategic level)

5. PRO Russia wengi wanaamini kuwa USA imepeleka wanajeshi wake frontline kupigana. Wakisikia Raia wa marekani kafa wanaamini kuwa mwanajeshi ambaye yuko in service. Hawajui kuwa Ukraine naye ana wanajeshi wa kujitolea (waliostaafu) kwenye majeshi ya nchi mbali mbali na wameenda kuomba ajira ili wapigane. Hawajui kuwa Ukraine nao wana mercenaries kama walivyo wagner.

6. Hawajui kuwa USA, German & allies wanapeleka wanajeshi wao (in service) si kwa ajili ya kupigana la hasha ni kwa ajili ya kutoa technical support yaani knowlege transfer ili Ukraine wapate uzoefu kuanzia installation, maintenance and support.
 
Back
Top Bottom