US dola imejaa mpaka inamwagika, hongera sana Samia, hongera mwigulu

Na hakuna alowahi kuipandisha kw kasi hivyo bila sababu
 
Yaani mitanzania ambayo haijasoma ndo kama hili litoa mada jinga kabisa .
ELIMU
Mnamo september ili kuvutia wawekezaji usa iliamua kushusha intrest rate hadi 4% na ilitabiliwa kabisa kuwa mwezi huu dola itashuka imefanya hivo dunia nzima kwa pesa zote isipokuwa chache sana kama zambia(wanamatatizo yao)
.
Uganda na kenya nao mama anaupiga mwingi? Mama anafanya kazi nzuri ila acheni kumchezea akili .

Nikuongezee angalia kuanzia tarehe 20 dolla itaanzapanda na tutarudi 2600.sababu ni kuwq kumekuwa na exaggeration ya information east africa .kama unabisha ikifika 2200 nunua dola 100 tu kisha nipime kwa hilo.nakuapia december tunafunga ikiwa 2500 hadi 2600.
Sikunyingine usikurupuke wachumi tumo humu.
 
Dola yenyewe imeshuka wala sio kwamba thaman ya pesa yetu imepanda, sasa kushangilia na kujisifu kwenye hamna ni ujinga mkubwa sana huu mfumo wa uchawa huu ndio umekuja kuliua kabisa taifa hili
 
Wafuasi wa Mbowe watabisha Samia mitano tena CCM DAIMA
 
Usinitapishe bure kwa uchawa na uzwazwa uchwara mwanangu.
 
Currency value appreciation sio instrumental factor ya ukujaji wa uchumi, acha ushamba wewe... Kuna sababu nyingi sana zinazoweza kupelekea thamani ya sarafu kupanda ama kushuka ikiwemo uchumi wa nchi husika ya sarafu unayojilinganisha nao!

Kwanza unashingilia nini? Eti hakuna kama Samia, huyo Samia si alikuta $1 ni sawa na 2,370/=? Kwenye awamu yake hii ameipandisha mpaka 2,800/= haya leo hii imeshuka hadi 2,460/= halafu unaanza kumsifia?

Ndio Yale Yale ya kufuta bima ya toto Afya kisha kuirudisha halafu mnataka mpigiwe makofi.
 
Naona umekuja kulazimisha msifiwe. Hakuna wa kuwasifia boss, lipeni machawa wawasifie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…