USA hata kama akasimama pekeake dhidi ya dunia nzima kivita, bado tutapigwa tu

USA hata kama akasimama pekeake dhidi ya dunia nzima kivita, bado tutapigwa tu

🤣🤣
Alipovamia Vietnam hakufanya cost benefit analysis?
Wanajeshi wako wamekufa, na bado unalazimisha raia waingie vitani (Ref: Mohamed Ali), bado Hali inakuwa ngumu. Vifaa vita vyako vimechakazwa....../ Mwisho wa siku unasema hii vita Sina maslahi mayo, "ngoja niondoke" ../ really? Inamaana kabla ya vita hukujua faida na hasara za vita unayokwenda kupigana?
kwa wajinga kama nyiny mtachukua miaka 100 kuja kuwahelewa USA
 
Umejitahidi kufafanua vyema sana, lakini kuna sehemu unahitaji kusahihisha takwimu zako, ni kweli kabisa Usa ana uchumi mkubwa kuliko Russia, lakini kwenye upande nguvu za kijeshi mataifa hayo haya utofauti mkubwa, kuna baadhi ya vyanzo huonyesha Russia ana jeshi kubwa kulio Usa na vyanzo vingine huonyesha Usa ana jeshi kubwa kuliko Russia.
Lakini unapokuja kwenye swala la nguvu za Nuclear Russia ana siraha nyingi sana za Nuclear kuliko Usa tena mbali sana.
Lakini pia unaposema kwamba Usa anaweza kupigana na dunia nzima na akashinda hapo nadhani umeongea kwa kutanguliza mapenzi kwa nchi hiyo, hicho ni kitu ambacho hakiwezekani.
Kuna nchi kama china ambazo haziimbwi sana zina nguvu sana kijeshi hata Usa mwenyewe anajua.
 
😂😂😂Walikuwa wapi kujiokoa kabla Japan hajaanza kuwa bize kupigana na wakubwa?
Mwanajf unaweza kuwa na hoja ila kiukweli China ya WWII sio kama ya leo. Sipo katika mjadala wa mleta uzi, ila narekebisha hapo.
 
Acha ujinga haikuwa vita kamili! Ilikuwa vita ya kiitikadi kati ubepari na ukommunist!
Mwanajf "vita kamili" ni nini? Sijaelewa hapa. Vita kuu ya pili ya dunia haikuwa vita kamili? Na wala haikuwa ya kiitikadi?
Kwa takwimu USA ana nuclear warhead zaidi ya million 100 mpaka UN ikapiga kelele kuhusu wingi wa stocks za nukes.
Mwanajf naona hapa unatunywesha chai sasa. Namba ya Nuclear warheads sidhani kama iliwahi kuzidi Elfu 65. Labda utupe source. Kwa sasa inakadiriwa kuna Nuclear warheads 12500 na kiasi worldwide, U.S. akiwa anakadiriwa kuwa na nuclear warheads Elfu 5 na kiasi.

 
Hebu tuache porojo.. ni vita gani ambayo amewahi kupigana peke yake akaishinda.

Vita ya Vietnam alipigwa hadi akajiondoa, Afghanistani aliwakuta taliban na kawaacha yani sawa ameshindwa, pale Iraq alikuwa na collabo.

Sasa unaweza kusemaje akisimama na dunia nzima atashinda au movie zinakuchanganya mzee?

Hitler tu alishindwa na teknolojia aliyokuwa nayo kipindi kile. Hivi unajua wanasayansi wa Nazi ndio aliwachukua US wengi wakawa viongozi wa vitengo ikiwemo NASA, maana walikuwa ni wabobezi wa rocket propellant?
Bora wewe unajua mkuu hawa walamba soli wa USA hakuna wanachokifahamu mtu hajapitia OPERATION PAPER CLIP ambapo USA alichukua wanasayansi wa GERMANY zaidi ya 1600 akawapa na uraia .

Kuna wakina Wernher von Braun ambaye aliwekwa nasa , Albert Einstein, Hans Bethe, John von Neumann, Leo Szilard, James Franck, Edward Teller, Rudolf Peierls, na Klaus Fuchs ambao wamehusika kwenye secret projects nyingi sana na wamefanya vumbuzi ambazo zilifichwa kwa muda mrefu na USA na nyengine nadhani hadi leo hazijatolewa.

Kuna wakina oppenheimer ambaye wazazi wake walikuwa wahamiaji kutoka ujerumani angalia jamaa alichounda mpaka leo hii japan wamebaki na kumbukumbu mbaya sana kutoka USA.

GERMANS NI HATARI SANA TUKIJA KWENYR ISHU ZA TECHNOLOGY SIJAJU KWANINI KWA SASA HAKUNA VICHWA VINAVYOTOKEA KULE.
 
Kuna watu wana uelewa mdogo sana kuhusu uwezo wa USA kiichumi, kivita, silaha, technology. Ukweli unabaki pale pale kwamba hakuna taifa lolote linalomsogelea MAREKANI kwenye:

a) Uchumi
b) technology
c) silaha
d) Vita
e) Biashara

Uwezo wa Marekani ni mkubwa mno kwenye hizo nyanja.

Kama ingetokea kwamba dunia nzima tukapigana na USA, bado jamaa watashinda hiyo Vita.

USA kwenye full scale war, hana mpinzani. Jeshi lake liko kila Kona ya dunia. Wana silaha za kisasa na wako vizuri Sana kwenye innovation

Uchumi wao ni mkubwa mno, USA anaweza kupigana full scale war kwa muda mrefu bila kuteteleka.

Nawashangaa Sana watu wanaosema Russia Ina uwezo mkubwa kuliko USA. Najiuliza ni mahaba au kweli wanamaanisha.

Uwezo wa USA dhidi ya Russia ni mkubwa mno.

Mfano mmoja ni huu, uchumi wa California ni mkubwa kuliko uchumi wa Russia Kama taifa. Uchumi wa Russia ni 2 trillion USA GDP. Uchumi wa USA ni almost 29 trillion USD. Russia anawezaji kupigana na taifa lenye nguvu kiasi hicho?

Wengine wanasema Russia ana nuclear bombs, Swali, Nani aligundua nuclear. Nani amewahi kutumia nuclear weapons?

Putin anajuwa Sana uwezo wa ki nuclear wa USA. Anajua vizuri kwamba akitumia nuclear tu, utakuwa ndio mwisho wake

Vitu vingine tuache mahaba. Tujifunze ya mwaka Jana ya Nancy Pelosi. Tulipata jibu sahihi
Ngoja nikuelezew kwa mfano ambao utaweza kuelewa maana huu mfano ndiyo unaendana na akili yako

Chukulia kuna mtu mmoja ana misuli kweli kweli na anajua kupigana halafu akapambanishwa na watu 100 kwa pamoja waje kumvamia unadhani ngumi zake na misuli vitamsaidia?
 
Marekani ina mashirika zaidi ya 10 ya Intellejensia, Wizara yao nishati yenyewe ina Shirika lake la Ujasusi.

Mtu anayedhani shit holes countries zinaweza kupigana na Marekani ni mjinga sana na hana strategic understanding ya mambo ya Dunia.

Hadi sasa only Russia na USA ndio wana Nuclear TRIAD, vita kubwa kuliko zote na ya hatari ni Marekani na Russia. Na hiyo vita atakaye pigwa in coventional war ni Russia.

Sababu kubwa Russia hataki Ukraine wawe NATO ni kuogopa Jeshi kubwa kama la Marekani liwe mpakani mwake
stormryder punguza kuangalia movie za kina Rambo.USA ana uchumi mkubwa kuliko Russia haina ubishi lakini kwenye Vita baina ya mataifa haya mawili hakuna mshindi.Wote wana silaha za kuangamiza dunia nzima,hakuna mwenye akili timamu anayetamani kuona mpambano wa hawa miamba wawili kwani hakuna atakayebakia kuhadithia yaliyotokea.
Napenda kukushauri ujaribu kuchuja source zako za habari.Hawa wenzetu wa magharibi wamebobea kwenye propaganda kiasi ambacho taarifa zao zimekuwa zinapuuzwa na watu makini.Kama unakumbuka kabla ya SMO ya Russia kwa Ukraine tulibebeshwa uongo mwingi juu ya ubora mkubwa wa silaha za USA dhidi ya za Russia,matokeo kwenye battle field ni tofauti kabisa.
 
Bora wewe unajua mkuu hawa walamba soli wa USA hakuna wanachokifahamu mtu hajapitoa OPERATION PAPER CLIP ambapi USA alichukua wanasayansi wa GERMANY zaidi ya 1600 akawapa na uraia .

Kuna wakina Wernher von Braun ambaye aliwekwa nasa , Albert Einstein, Hans Bethe, John von Neumann, Leo Szilard, James Franck, Edward Teller, Rudolf Peierls, na Klaus Fuchs ambao wamehusika kwenye secret projects nyingi sana na wamefanya vumbuzi ambazo zilifichwa kwa muda mrefu na USA na nyengine nadhani hadi leo hazijatolewa.

Kuna wakina oppenheimer ambaye wazazi wake walikuwa wahamiaji kutoka ujerumani angalia jamaa alichounda mpaka leo hii japan wamebaki na kumbukumbu mbaya sana kutoka USA.

GERMANS NI HATARI SANA TUKIJA KWENYR ISHU ZA TECHNOLOGY SIJAJU KWANINI KWA SASA HAKUNA VICHWA VINAVYOTOKEA KULE.
Germany na Japan [emoji557] baada ya WWII, walipigwa Pini juu ya masuala ya kijeshi, badala yake USA ndo anebaki kuwa mlinzi wao. Uwekezaji wao katika jeshi, pamoja na enrollment iko very limited kutokana na mikataba waliosainiana na USA.
 
Kitendo cha marekani kuweka military base kila kona ya dunia maana yake hakuna wa kupigana naye akamshinda
Ujinga mtupu, watu wakiamua hizo base wanazichapa vizuri tu na hakuna kitu atafanya huyo Mmarekani. Vita ya Nako 2 Nako hao Marekani hawatoboi hata kwa majeshi ya kiafrika
 
Germany na Japan [emoji557] baada ya WWII, walipigwa Pini juu ya masuala ya kijeshi, badala yake USA ndo anebaki kuwa mlinzi wao. Uwekezaji wao katika jeshi, pamoja na enrollment iko very limited kutokana na mikataba waliosainiana na USA.
Na wao wakakubali kabisa😁
 
Unajichanganya mzee,hapo inaongelewa millitary operation aliyoefanya USA ndani ya Vietnam ilifeli.
Na haikufeli hiyo tu,hata vita ya Jangsari USA akiisaidia Korea Kusini aliingiza jeshi lake kamili na kila aina ya vifaa ili aisapoti Korea kusini dhidi ya Korea kaskazini,ila alikumbana na kibano cha jeshi la China likitumia silaha za kisoviet.
Mbona alirudi na kutaka yaishe na wakakaa mezani!?
Na hata world war 2 kama USA asingepiga nukes pale Hiroshima basi ile vita alikua anapigwa na Japan.
Japan alishaanza kulidhibiti kimapigano jeshi la USA ila zile nukes ziliwanyong'onyesha.
Wajapan walikuwa na roho za kikatili zaidi ya Wakurya 😁 ila Nuclear ziliamua ugomvi!
 
Kuna watu wana uelewa mdogo sana kuhusu uwezo wa USA kiichumi, kivita, silaha, technology. Ukweli unabaki pale pale kwamba hakuna taifa lolote linalomsogelea MAREKANI kwenye:

a) Uchumi
b) technology
c) silaha
d) Vita
e) Biashara

Uwezo wa Marekani ni mkubwa mno kwenye hizo nyanja.

Kama ingetokea kwamba dunia nzima tukapigana na USA, bado jamaa watashinda hiyo Vita.

USA kwenye full scale war, hana mpinzani. Jeshi lake liko kila Kona ya dunia. Wana silaha za kisasa na wako vizuri Sana kwenye innovation

Uchumi wao ni mkubwa mno, USA anaweza kupigana full scale war kwa muda mrefu bila kuteteleka.

Nawashangaa Sana watu wanaosema Russia Ina uwezo mkubwa kuliko USA. Najiuliza ni mahaba au kweli wanamaanisha.

Uwezo wa USA dhidi ya Russia ni mkubwa mno.

Mfano mmoja ni huu, uchumi wa California ni mkubwa kuliko uchumi wa Russia Kama taifa. Uchumi wa Russia ni 2 trillion USA GDP. Uchumi wa USA ni almost 29 trillion USD. Russia anawezaji kupigana na taifa lenye nguvu kiasi hicho?

Wengine wanasema Russia ana nuclear bombs, Swali, Nani aligundua nuclear. Nani amewahi kutumia nuclear weapons?

Putin anajuwa Sana uwezo wa ki nuclear wa USA. Anajua vizuri kwamba akitumia nuclear tu, utakuwa ndio mwisho wake

Vitu vingine tuache mahaba. Tujifunze ya mwaka Jana ya Nancy Pelosi. Tulipata jibu sahihi
We jamaa ni mjinga kiasi chake kwa sababu unaleta hoja ila wakati huo huo unajichanganya. Uchumi wa dunia ni zaidi ya $100 Trillion wakati wa US ni $25T, sasa hizi pande 2 zikiingia vitani unasemaje upande wenye 25 utaushinda upande wenye 70+

Pili kijeshi mfano mdogo US ana siraha za nuclear karibu 5400 wakati siraha zote zilozoko duniani ni zaidi 13000 sasa unasemaje upande wenye siraha 5000 unaweza kuushinda upande wenye siraha 6000 plus.

Hapo huajaongelea vifaa kama vifaru vya vifaru, drones, artillery nk ambazo kila siku tunaona zina flop battlefield.

Tusiwaabudu sana US huenda tukawashangaa siku likitokea la kutokea.
 
September 11 ilitosha kusema Marekani inaweza kupigwa kabisa! Shukuru tu katika tukio hilo moja ya ndege zilizotekwa na Magaidi haikuangukia Pentagon huenda mifumo yake ya Ulinzi inge collapse kabisa.
Afghanstan,Vietnam,Somalia kote huko alipigwa akakimbia!
Ambacho nakubaliana na wewe kwa uchumi wake anaouwezo wa kuhimili vita kwa muda mrefu tu lakini siyo Vita!
Kila teknolojia yake aliyonayo imeshaibiwa!
 
Wajapan walikuwa na roho za kikatili zaidi ya Wakurya 😁 ila Nuclear ziliamua ugomvi!
Kuna movie inaitwa "HACK SAW RIDGE" nadhani mkuu unaifaham.
Aliigiza yule kijana aliyeigiza "Amazing spider man".
Ile movie ilikua dedicated kwaajili ya kusifia mchango wa mwanajeshi mmoja ambaye alipigana WW2 ila alifanikiwa kuokoa zaidi ya 70+ US soldiers ambao walioumia na hakushika bunduki wala kufyatua risasi.
Yule mzee sasa hivi anakaa katika wheel chair ana zaidi ya 80+ years,mwishoni mwa ile movie walimrekodi na alikiri akisema" kama haikuwa ile nuke iliyopigwa Nagasaki na Hiroshima,tusingewaweza Japan hata kama tumewazunguka".
Maana wale askari wa Japan walikua wanafanya hadi SUICIDE BOMBING.
Halafu kuna mpuuzi anakwambia eti Japan ilishindwa kabla.
Na kuna mjinga mwingine anakwambia USA inaweza kusimama hata na dunia nzima.
Aiseeeeee!
 
Back
Top Bottom