Usafiri wa ndege Dar es Salaam - Mwanza kwa Tsh 120,000, unaanza Machi 13, 2023

Unaambiwa bus luxury ukiuliza kuna nn una aambiwa kuna ac na wanagawa pipi 😆
 
Ndege wakiondoa ukiritimba sio ghari kivile na abiria wa Mwanza,Mbeya,Dom, Arusha na Zanzibar wapo wengi sana ni vile wameweka password inaonekana ni usafiri wa anasa...

[emoji1787][emoji23][emoji23]bro unaelewa aviation vizuri lakini...ground charges za airport...bado ground handling charges za airport(swissport, dnata, celeb) ni kubwa sana mzee...bado kuna safety issues za kila siku kabla haijaondoka...very expensive kwiayo huo ukiritimba huujui vizuri
 
Acha uongo sio kwa Africa! Nchi gani Africa imefanikiwa kuweka bei ya chini?. Suala liko kwenye mazingira ya biashara hasa kutokuwa na uwezo wa uzalishaji wa vipuri na huduma za ndege na pia kodi zisizo rafiki na udogo wa soko kutokana na umasikini.
South africa ilikuwa na budget air line kama tatu hivi na zilikuwa cheap kuliko Saa
Kukula .com
Mango
Fly 540
Kulula wanakuja hadi zanzibar na ilikuwa cheap.
 
Budget airline au Low Cost Carrier (LCC) zilizoanzishwa Africa ngapi zinaendelea ku operate as LCC,? Yes cost structure ni tofauti kwa kuhakikisha hawatoi hizo inflight services, wanatumia special designed aircraft kupunguza uzito ili kutumia mafuta kidogo , discouraging mizigo mizito ili kupunguza mafuta otherwise you pay heavily, kutumia viwanja vyenye tozo za chini. Muhimu zaidi kuwa na passenger volume kubwa ili kubeba abiria wengi au kuuza tiketi nyingi to facilitate forward sales kubwa maana wanahitaji cash flow kubwa! Do we have these conditions in Afrika? Then utajua kwanini nimekuwanikipinga kuwa fastjet eti kahujumiwa. By the way, landing ambayo ita save mafuta ni procedure ya kila shirika kutokana kuwa item yenye gharama kubwa za uendeshaji
 
Wewe unajua unachoongea.
 
Mambo yako hayo....watu wanaona rahisi sana aviation business.
 
Mtaqlamu
unakosea sana unapolinganisha mazingira ya biashara ya aviation Ulaya na africa , na hili ni tatuzo letu, Tan road inanperate kwa kutumia sheria za uingereza yani ni copy and paste , Tra nao sheria ni za copy and paste vile vile .
Uiishakua na attitude kama hii hakuna biashara inaweza survive , ndio maana biashara nyingi nyingi haziwezi kuishi Africa .Lcc ni mojawapo

Lcc zilianzia ulaya na makampuni mengi pia yalikufa pia ila walitafuta njia ku adopt , ndi hiyo unaona Ryan air anadunda hadi leo. Sababu mazingira yanawa favour .

Lcc inagitaji cash flow kubwa , ukishakuwa na cash flow kubwa kwa mazingira yetu tayari umealika Tra, hapo survival yako inategemea kudura za Mungu, na rushwa n.k maana hakuna biashara inatoboa kwenye chujio la kodi kirahisi, ShopRite na Game wamefunga biashara katika mazingira kodi ,na hizi ni stores kubwa hazIkuwa na upinzani hapa kwetu, Fastjet alikua na mazingira magumu ya kodi , expesive swissport charges na serikali iliponunua ndege zake ikaanza figisu, ilikuwa lqzima ife.
 
Ground charges ni na handling ni kubwa kwetu na zililalamikiwa na mashirika makubwa ya ndege , na ndio sbabu ndege nyingi ziliamua kuishia Nairobi . Lakini hili lingeweza kujadilika kama tusinge binafsisha Dahaco

Dahaco haikuwa efficient , lakini ilikuwa na unafuu . Swissport ni mzungu yeye anachoangalia ni faida yake , kodi zikiwa kubwa jua mlaji ndo anaumia , ndio maana gharama za swissport ni juu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…