Ushahidi: Delila hakumnyoa Samsoni bali alisingiziwa

Ushahidi: Delila hakumnyoa Samsoni bali alisingiziwa

Kama kwenye mafundisho huko kunapatikana picha hizi... napata walakini
 
kusema kwamba Samson alikuwa gaidi ni kukosea mana alikuwa mtetezi wa kuwakomboa wa Israel kutoka kwenye utumwa wa wafilisti japo serikali ya kifilisti ilimchukulia kama adui ndomana wakamtumia delilah kumwingiza mtegoni hivyo kama ni makosa delilah atashtakiwa na serekali ya Israel ila kwa wafilisti ni shujaa.
 
Penzi kitovu cha uzembe.

Mwamba alilala usingizi wa namna gani, alitudhalilisha sana.
Nasubiri ajichanganye Delila mwingine maishani mwangu,nimlipue kombora. Samsoni popote ulipo nimejifunza jambo kubwa na muhimu sana katika sakata lako.
 
Samsoni hakunyolewa na Delila bali Delila amekaa kusingiziwaView attachment 2040992
Imekuwa ikienea kuwa mwanamke kwa jina la Delila ndiye alimunyoa Samsoni kitu ambacho si kweli. Wengi hufikiri kuwa Samsoni alinyolewa na Delila.

Ushahidi unaonyesha katika biblia takatifu Delila yeye alihusika katika kumdanganya Samsoni na kujua siri zilizo zificha katika Nywele zake na Delila yeye alihusika pia wakati Samsoni ananyolewa lakini Delila binafsi yeye hakumunyoa Samsoni kitu ambacho Delila amekaa kusingiziwa.

Ushahidi katika biblia ukisoma Waamuzi 16:19
Imeandikwa "Waamuzi 16:19
[19]Naye akamlaza usingizi magotini pake. Kisha akamwita mtu akavinyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake; akaanza kumsumbua, nguvu zake zikamtoka.


Hivyo ukirejea ushahidi wa biblia Samsoni alinyolewa na mtu mwingine ambaye hakutajwa na wakati huo Samsoni alikuwa magotini mwa Delila.
Msichokijua nikuwa Delilah alikuwa ni mpelelezi wa jeshi la wafilisti
 
Hapo Samsoni alikuwa tayari kashanyolewa na pia picha hiyo ni picha ya kuchora hivyo ni ngumu kufanana na uhalisia.

Kwaiyo Baada Ya Kunyolewa Nywele Akawa Mzungu? Mkuu Picha Ya Simba Ni Lazima Iwe Ya Simba Hauwezi Ukachora Picha Ya Fisi Ukasema Ni Simba

Uyo Samsoni Aliyechorwa Hapo Siye Yeye Ni Tofauti Na Samsoni Wa Kwenye Biblia
 
Bado Delila ni mtuhumiwa namba 1.

Mashtaka ya Delila:
1.Kula njama za kumnyoa Samson
2.Kumlewesha Samson kwa nia ovu ya kumnyoa nywele zake.
3.Kushiriki kumnyoa samson.
4.Kutakatisha pesa(pesa alizolipwa baada kutekeleza huu uhalifu)
5.Uhujumu uchumi
Ongezea Kuunda genge la uhalifu(organized crime) na kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu
 
Bado Delila ni mtuhumiwa namba 1.

Mashtaka ya Delila:
1.Kula njama za kumnyoa Samson
2.Kumlewesha Samson kwa nia ovu ya kumnyoa nywele zake.
3.Kushiriki kumnyoa samson.
4.Kutakatisha pesa(pesa alizolipwa baada kutekeleza huu uhalifu)
5.Uhujumu uchumi
Hivi yule wakili msomi wa Kenya aliyefungua mashtaka dhidi ya Wayahudi kumuua Yesu kesi yake iliishiwa wapi?
Achangamkie na hili la Delila apige mpunga.
 
Kwa nini Delila alipokea rushwa ili kuifanya kazi hiyo?
Sio rushwa, waandishi ! Ndo wamejichanganya,, kipindi hicho waisrael wakiishi miongoni mwa wafilisti kama wahamiaji, kwani hawakuwa bado na serikali yao, delila alikua mfilisti, kusema alipokea rushwa ni sawa na kusema makachero wakilewa malipo kwa kazi ni rushwa
 
Duh sasa ahadi ya Mungu kuwakomboa kutoka misri utumwani kwenda nchi ya ahadi yenye maziwa na asali Kanani ina maana gani kama waliishia kuwa watumwa chini ya wafilisti.?
Ndo hivyo walipofika caanan,, waliishi tu kama wageni , king saul wamekuja kumchagua baadae sana , lakini wanahistory wanadai, kikundi kilichotoka misri ni handfull person, hivyo ili kujitawala iliwachukua miaka mingi,, vile vita alipigana joshua,, vimekua overated kidogo
 
kusema kwamba Samson alikuwa gaidi ni kukosea mana alikuwa mtetezi wa kuwakomboa wa Israel kutoka kwenye utumwa wa wafilisti japo serikali ya kifilisti ilimchukulia kama adui ndomana wakamtumia delilah kumwingiza mtegoni hivyo kama ni makosa delilah atashtakiwa na serekali ya Israel ila kwa wafilisti ni shujaa.
Samsoni alinyang'anywa dame wake sijui na nani, kwa hasira akaenda kuua watu 200,, baadae kapewa dame aoe kwa mahari ya magovi ikabidi tena aue watu na kuwakata magovi,, halafu akabet. Alipoliwa,, kwa hasira akachoma mashamba ya watu moto,, askari wakaanza kumsaka wamfikishe ? Mahakamani , delila alitumika tu kama honeytrap
 
Kama kwenye mafundisho huko kunapatikana picha hizi... napata walakini
Hiyo ni picha ya kuchora na mafundi wa kuchora kipindi hicho.
Ila huenda hali yenyewe ilikuwa hivyo ndio maana hata Samson hakuweza kuchomoa.
 
Kwaiyo Baada Ya Kunyolewa Nywele Akawa Mzungu? Mkuu Picha Ya Simba Ni Lazima Iwe Ya Simba Hauwezi Ukachora Picha Ya Fisi Ukasema Ni Simba

Uyo Samsoni Aliyechorwa Hapo Siye Yeye Ni Tofauti Na Samsoni Wa Kwenye Biblia
Utofauti wa Samson huyo kwenye mchoro na kwenye biblia ni nini tueleweshane.
 
Hivi yule wakili msomi wa Kenya aliyefungua mashtaka dhidi ya Wayahudi kumuua Yesu kesi yake iliishiwa wapi?
Achangamkie na hili la Delila apige mpunga.
Ulikosekana ushahidi.
Ila kwa hii pia watamshinda maana Delila alikuwa na makosa kibao.
 
Sio rushwa, waandishi ! Ndo wamejichanganya,, kipindi hicho waisrael wakiishi miongoni mwa wafilisti kama wahamiaji, kwani hawakuwa bado na serikali yao, delila alikua mfilisti, kusema alipokea rushwa ni sawa na kusema makachero wakilewa malipo kwa kazi ni rushwa
Kiasili hii ilikuwa kama rushwa rejea.

Waamuzi 16:5
[5]Nao wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, Mbembeleze, upate kujua asili ya nguvu zake nyingi, na jinsi tutakavyoweza kumshinda, tupate kumfunga na kumtesa; nasi tutakupa kila mtu fedha elfu na mia moja.
 
Utofauti wa Samson huyo kwenye mchoro na kwenye biblia ni nini tueleweshane.

Biblia Inasema Samsoni Alikuwa DredRock Rejea Huo Mstali Wa 13; Ni Black Man Pekee Ambae Nywele Zake Zinaweza Kujisokota, Sio Mzungu Wala Mwarabu Sasa Hiyo Picha Apo Ya Huyo Mzungu Ni Ya Nani?
Nazani Ni Mwendelezo Wa Dramma Zile Zile Za Kuuficha Ukweli;
 
Back
Top Bottom