Ushauri: JWTZ/JKT wajikite kwenye tafiti za kisayansi na teknolojia. Wabuni silaha zao wenyewe

Ila kukamata watu kisa nguo zao ni ushamba mkubwa nenda Rwanda, uganda kenya na hata huko USA wananchi wanavaa nguo za jeshi bila shida
 
Hawawezi, unaenda kufundishwa kuvunja matofali kwa technolojia ya leo sijui utampigaje adui yupo umbali wa 800KM kwa tofali, pia wengi ni failure siyo rahisi kuwa na ubunifu
 
Jeshi la Misri linafanya biashara hadi ya mikate
 
jeshi la Rwanda ni mfanya biashara mkubwa nchini humo.
 
Hapa Africa jeshi linalo ongoza kwa kufanya biashara (mult billion dollars) ni Egypt wana makampuni makubwa ya ujenzi, viwanda vikubwa na vya kisasa. Alivianzisha Nasser na Baba wa Taifa alijaribu kuchukua ideas hizo kwa kuanzisha vitu kama Mzinga corporation na Nyumbu.
 
Kazi ya JKT ni pamoja na uzaliashaji mali
 
Kampuni mama ya Halotel, Vietel inamilikiwa na Jeshi la Vietnam.
 
Watu wengi hawajamuelewa mleta mada.

Yeye hapingi Jeshi kufanya biashara. Lakini siyo biashara za kiraia bhana!!

Hapa Tanzania tupo na makampuni zaidi ya 8 ya maji. Iweje na wewe unakuja kufanya biashara za uchuuzi?

Yani jeshi lijihusishe na upambaji kwenye maharusi. Aaaaaa!!! Hapana jamani.

Tanzania hatuna ngano. Kwanini wasilime ngano?
 
Hahahaha yaani baada ya kuona jeshi halina hata dalili ya kuunga mkono siasa za chadema na mnaanza kuliponda [emoji23][emoji23][emoji23]kabla ya dp world mbona mlikua mnalisifu
 
Dunia inabadilika unaijua viatel/halotel basi ni biashara ya jeshi.Sioni tatizo kwa jeshi kujikita katika biashara na uwekezaji kwani unasaidia kuziba pengo la vijana wavivu wavivu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…