Pre GE2025 Ushauri kwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS Kuhusu Kero Sugu ya Uhalifu wa Kiuchaguzi Unaofanywa na Wanasiasa Matapeli Wakati wa Chaguzi tangu 2010 hadi 2024

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nilitamani CCM iungane na CHADEMA kudai reforms; maana ni dhahiri marekebisho hayo yanafaida zaidi kwa CCM kuipa uhalalali kuliko kung'ang'ania mazoea ambayo yanao ukomo.

4R's zithibitike kivitendo!
 
Endeleeni tu kuishi kwenye fikra mfu za kijinga hizo.

Kwa hiyo tufuate siasa na mifumo mliyoianzisha ya uchawa? Kusifu na kuabudu?

Tuendelee na ujinga wenu wa kutengeneza kizazi kinachoishi kwenye uchawa na kusifu na kuabudu? Hizo ndo siasa za Tanzania na mfumo wa Tanzania mnataka tuendelee nao?

Kwa hiyo tuendelee na hali hii ya kuiba uchaguzi? Kuengua wagombea wa vyama vya upinzani? Kutanganza wagombea ambao hawajashinda kweli kwenye kura halali za wananchi?

Unafikiri hizo ndo zitalifanya Taifa letu kuwa imara? Kweli we kilaza
 
Majibu yana tija, nimependa.

Chadema tuna wabunge wangapi bungeni na nani anaweza kuwasilisha huu muswada wa hati ya dharura na kuhakikisha unapita?
 
Majibu yana tija, nimependa.

Chadema tuna wabunge wangapi bungeni na nani anaweza kuwasilisha huu muswada wa hati ya dharura na kuhakikisha unapita?

Nimependekeza kuwa TLS waandae miswada kwa kushirikiana na serikali. Then wizara ya sheria ndio iwasilishe bungeni kwa hati ya dharula. Ajenda yetu sio ajenda ya Chadema. Ni ajenda ya kitaifa.
 
Kinachoenda kufanyika kutakuwa na jipya zaidi ya 2020 uchaguz mkuu au 2024 serikali za mitaa?
Mashindano ya kujaza form, kuengua wapinzani kwa hoja nyepesi, wizi wa kura wa wazi kabisa,kuna haja gani ya uchaguzi?
Bora TAL na chadema wapaze sauti na Watz na ulimwengu uone jinsi nchi inavyotumia rasimali vibaya kabisa kwa kivuli cha uchaguzi ambao sio haki wala wazi kabisa!
 
Imagine kwa kweli
 
Nimependekeza kuwa TLS waandae miswada kwa kushirikiana na serikali. Then wizara ya sheria ndio iwasilishe bungeni kwa hati ya dharula. Ajenda yetu sio ajenda ya Chadema. Ni ajenda ya kitaifa.
Inawezekana kabisa na tukapata kitu Tangible kwa Maslahi ya Taifa.
 
Huko unakosema "kusifu na kuabudu" nako ni njia mnazotumia "as a leverage of tarnishing other people's image".

Huko kuitwako "kusifu na kuabudu" kumekuwa "overrated" sana kwani IBADA NA KUSIFU KIDINI kunafanyika katika nyumba za ibada tulizozizoea ikiwemo VILINGENI...ni wapi huko ambako tunakusanyika KIIBADA kusifu na kuabudu viongozi wetu ?!!

Laa ukisema huwa TUNASIFU tu kwa kawaida ya ADA yetu basi nitakwambia ni kweli huwa TUNASIFU viongozi wetu.....

Binafsi ninawasifu viongozi wangu si kwa ajili yao "personal gains" bali kwa lengo kuu la "kutoinajisi ardhi tukufu ya JMT" kwani kutowasifu viongozi ni kutomthamini Mwenyezi Mungu aliyetuweka hapa katika taifa tukufu la Tanzania.

Vijana werevu tunaamini katika imani kuu 2:
-Binadamu wote ni sawa ,
-Kila mtu anastahili HESHIMA* ya KUTAMBULIWA NA KUTHAMINIWA UTU WAKE....

Binafsi si mwendawazimu wa kutotambua na kutothamini HESHIMA ya VIONGOZI wetu ambao wao wanatekeleza agizo la Muumba mbingu na nchi kwetu sote la kulinda AMANI NA UTULIVU WA MATAIFA YETU.....

#Hebu kurupuka na ulitupe hilo shuka kwani jua limeshachomoza na kumekucha muda mrefu!
 
Majibu: Labda ungeandika hivi, “There MAY be no reforms, na uchaguzi UNAWEZA fanyika!” That way, utakuwa umeongea kama learned fellow. Lakini wawe sio mwamuzi halafu unaandika kauli ya kimaamuzi. Umepotoka.
Ame quote usemi kutoka kwa mtu mwingine, the Said Words are npt entitled to the Thread Creator but for reference only.
 
Umejibu very logically!
Kudos!
 
Nimependekeza kuwa TLS waandae miswada kwa kushirikiana na serikali. Then wizara ya sheria ndio iwasilishe bungeni kwa hati ya dharula. Ajenda yetu sio ajenda ya Chadema. Ni ajenda ya kitaifa.
....si dharula ni "dharura"!!
 
Ikiwa wapinzani kama akina Lissu wanahisi uchaguzi nchini unachezewa katika nyanja mbalimbali, unawashauri wafanye nini?
 
Bado tuna imani Dr Samia ni Mwislam safi hatapenda kupata vitu visivyo halali hivyo anaweza kuufanyia kazi Ushauri wako Murua kwa manufaa ya Watanzania wote.

Ni jambo linalowezekana njenya hapo ni visingizio tu
 
Kukusaidia tu. Fanya utafiti wako namna Mobutu alivyoiongoza Congo kwa kutengeneza hicho kizazi cha kusifu na kuabudu ilivyoiathiri Congo unayoiona leo.

Nyie wajinga tusipokuwa makini na nyie ni dhahiri nchi yetu itaenda kuwa kama Congo siku si nyingi.

Hamtafuti maarifa ya kulisaidia kweli Taifa ila mnaishi kwa kusifu na kuabudu ili mkono uende kinywani hadi mnaliharibu Taifa hili na vijana wetu kuona uchawa ndo maisha.

Kama wewe ni mzalendo kweli lazima utaungana na mleta mada kuhimiza Reforms ambazo zinalijenga Taifa imara lililobase kwenye meritocracy ambalo litastawi na kuwa imara siku zote.

Watanzania hawatokuwa wajinga siku zote. Na sio kwamba hawajui namna mnavyoiba na kunajisi chaguzi. Sio kwamba hawajui mnavyoiba pesa za umma kwa mambo yenu ya Ufisadi.

Ni heri mkubali mabadiliko haya yafanyike sasa na sio wakati ambao Watanzania wataamua liwalo na liwe.
 
Bado unaendeleza "baseless allegations"...

Watanzania tulio wengi huko vijijini na humu mitaani tumeshaamka kwa kujifunza kilichotokea ETHIOPIA....

-Katiba yetu hatutaki iwe na vifungu vya tawala za KIMAJIMBO....zilipelekea vifo ,kupoteza mali na ulemavu wa viungo kwa waethiopia wengi huko kuliko na makao makuu ya AFRIKA.....leo "perpetrators" wanatafuta suluhu za kidiplomasia ,ni vipi wahanga wa vile vita ?!!
Wanasiasa wanatafuta REFORMS kwa maslahi yao ya kisiasa+ kiuchumi kupitia GHARAMA kubwa kwetu wananchi....taifa si la wanasiasa tu....nchi yetu haijasimama kwa ajili ya siasa na wanasiasa pekee(politicians & democracy).

Mobutu Seseseko alikuwa ni mtawala kwa kupitia mapinduzi ya kijeshi , mfano huu uko wapi hapa Tanzania ?!!
 
😲😲😲
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…